Hata kama baraza yenye kuongoza ya karne ya kwanza ilikuwa ilishashugulikia tatizo ya kutahiriwa, watu fulani wenye walijiita kuwa Wakristo waliendelea kuikazia. Mutume Paulo aliwaita “ndugu wa uongo” wenye walipenda “kupotosha habari njema juu ya Kristo.”—Gal. 1:7; 2:4; Tit. 1:10.
Kusudi yao ilikuwa kufurahisha Wayahudi juu wasiwatese. (Gal. 6:12, 13) Wale Wakristo wa uongo walisema kama juu mutu akuwe mwenye haki alipaswa kushika Sheria ya Musa mu mambo sawa vile chakula, kutahiriwa, na sikukuu za Wayahudi.—Kol. 2:16.
Haishangaze kuona kama wale wenye waliamini ile mawazo ya uongo hawakujisikia muzuri kuwa pamoya na Wakristo wenye hawakukuwa Wayahudi. Jambo ya kuhuzunisha ni kwamba, hata Wakristo Wayahudi wenye walikuwa wanaongoza makutaniko walifikia kuchochewa na ile mawazo. Kwa mufano, wakati wajumbe kutoka kutaniko ya Yerusalemu walitembelea Antiokia hawakujiunga na ndugu na dada wa mataifa. Na hata Petro, mwenye alikuwa anajiunga na Watu wa Mataifa bila tatizo, alijiepusha nao na hakukula hata pamoja nao. Kwa kweli, alienda kinyume na kanuni yenye yeye mwenyewe alitetea mbele ya pale. Njo maana Paulo alimupatia mashauri makali.—Gal. 2:11-14.