Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • “Mitume na Wazee Wakakusanyika Pamoja”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
    • Sila na Yuda wanasomea kutaniko katika Antiokia ya Siria kitabu ya kukunjwa.

      SEHEMU YA 5 • MATENDO 15:1-35

      “Mitume Na Wazee Wakakusanyika Pamoja”

      MATENDO 15:6

      Kulitokea tatizo yenye ingeweza kuvuruga amani na umoja wa kutaniko. Makutaniko ilitafuta wapi muongozo ili kumaliza ile tatizo? Mu hii sehemu, tutaelewa muzuri namna kutaniko ya mu karne ya kwanza ilikuwa inapangwa na namna inaachia mufano watu wa Mungu leo.

      Mwangalizi wa muzunguko iko natoa hotuba mbele ya kutaniko.
  • “Kisha . . . Kukosa Kupatana”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
    • MAFUNDISHO YA WALE WENYE WALISHIKILIA SANA DESTURI ZA KIYAHUDI

      Hata kama baraza yenye kuongoza ya karne ya kwanza ilikuwa ilishashugulikia tatizo ya kutahiriwa, watu fulani wenye walijiita kuwa Wakristo waliendelea kuikazia. Mutume Paulo aliwaita “ndugu wa uongo” wenye walipenda “kupotosha habari njema juu ya Kristo.”​—Gal. 1:7; 2:4; Tit. 1:10.

      Kusudi yao ilikuwa kufurahisha Wayahudi juu wasiwatese. (Gal. 6:12, 13) Wale Wakristo wa uongo walisema kama juu mutu akuwe mwenye haki alipaswa kushika Sheria ya Musa mu mambo sawa vile chakula, kutahiriwa, na sikukuu za Wayahudi.​—Kol. 2:16.

      Haishangaze kuona kama wale wenye waliamini ile mawazo ya uongo hawakujisikia muzuri kuwa pamoya na Wakristo wenye hawakukuwa Wayahudi. Jambo ya kuhuzunisha ni kwamba, hata Wakristo Wayahudi wenye walikuwa wanaongoza makutaniko walifikia kuchochewa na ile mawazo. Kwa mufano, wakati wajumbe kutoka kutaniko ya Yerusalemu walitembelea Antiokia hawakujiunga na ndugu na dada wa mataifa. Na hata Petro, mwenye alikuwa anajiunga na Watu wa Mataifa bila tatizo, alijiepusha nao na hakukula hata pamoja nao. Kwa kweli, alienda kinyume na kanuni yenye yeye mwenyewe alitetea mbele ya pale. Njo maana Paulo alimupatia mashauri makali.​—Gal. 2:11-14.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine