Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • gf somo 1 uku. 3
  • Mungu Anataka Uwe Rafiki Yake

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mungu Anataka Uwe Rafiki Yake
  • Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu!
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Unaweza Kuwa Rafiki ya Yehova
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Unawaza Namna Gani?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2018
  • Rafiki Muzuri Ni Nani?
    Amuka!—2014
  • Tunawezaje Kuchagua Marafiki Wazuri?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Ona Habari Zaidi
Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu!
gf somo 1 uku. 3

Somo 1

Mungu Anataka Uwe Rafiki Yake

Mungu anataka uwe rafiki yake. Je, umewahi kuwazia kwamba unaweza kuwa rafiki ya Mtu mkuu zaidi katika ulimwengu wote? Abrahamu, aliyeishi zamani za kale, aliitwa rafiki ya Mungu. (Yakobo 2:23) Watu wengine pia wanaotajwa katika Biblia walikuwa marafiki wa Mungu, nao walibarikiwa sana. Leo, watu kutoka sehemu zote za dunia wamekuwa marafiki wa Mungu. Wewe pia unaweza kuwa rafiki ya Mungu.

Kuwa rafiki ya Mungu ni bora kuliko kuwa rafiki ya binadamu yeyote. Mungu hawavunji moyo kamwe marafiki wake wenye uaminifu-mshikamanifu. (Zaburi 18:25) Kuwa rafiki ya Mungu ni bora kuliko kuwa na mali. Tajiri anapokufa, fedha zake huchukuliwa na watu wengine. Lakini, wale wanaofurahia urafiki pamoja na Mungu wana kitu fulani chenye thamani ambacho hakuna mtu anayeweza kuwanyang’anya.​—⁠Mathayo 6:⁠19.

Huenda watu fulani wakajaribu kukuzuia usijifunze juu ya Mungu. Hata huenda wengine kati ya marafiki wako na familia yako wakajaribu kukuzuia. (Mathayo 10:​36, 37) Watu wengine wakikucheka au kukutisha, jiulize hivi, ‘Je, mimi ninataka kumpendeza nani​—⁠binadamu au Mungu?’ Fikiria jambo hili: Ikiwa mtu fulani angekuambia uache kula chakula, je, ungemtii? Bila shaka hapana! Unahitaji chakula ili uishi. Mungu anaweza kukufanya uishi milele! Kwa hiyo, usiache kamwe mtu yeyote akuzuie usijifunze jinsi ya kuwa rafiki ya Mungu.​—⁠Yohana 17:⁠3.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine