Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • bt sura 19 uku. 148-155
  • “Uendelee Kusema na Usinyamaze”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Uendelee Kusema na Usinyamaze”
  • “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • “Kazi Yao Ilikuwa Kutengeneza Mahema” (Mdo. 18:1-4)
  • “Wakorinto Wengi . . . Wakaanza Kuamini” (Mdo. 18:5-8)
  • “Niko na Watu Wengi Katika Muji Huu” (Mdo. 18:9-17)
  • “Kama Yehova Anapenda” (Mdo. 18:18-22)
  • “Niko Safi Kutokana Na Damu ya Watu Wote”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
“Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
bt sura 19 uku. 148-155

SURA YA 19

“Uendelee Kusema na Usinyamaze”

Paulo anajitegemeza kimwili lakini anatia kazi ya kuhubiri pa nafasi ya kwanza

Inategemea Matendo 18:1-22

1-3. Juu ya nini Paulo alienda Korinto, na ni mambo gani ilikuwa namuhangaisha?

NI KU mwisho wa mwaka wa 50 K.K.Y. Paulo iko Korinto, muji tajiri wa wafanyabiashara, wenye kuwa na watu wengi. Mu ule muji muko Wagiriki, Waroma na Wayahudi.a Paulo hakukuya Korinto ili kuuza ao kuuzisha vitu ao ili kutafuta kazi. Kuko sababu ya maana sana yenye imefanya akuye Korinto. Alikuya kutoa ushahidi kuhusu Ufalme wa Mungu. Iko na lazima ya fasi ya kuishi na hapendi kuwa muzigo kwa wengine. Hapendi wengine wawaze kama wanapaswa kumutimizia mahitaji yake ya kimwili juu tu iko nahubiri habari njema. Atafanya nini?

2 Paulo anajua kazi ya kutengeneza mahema. Haiko mwepesi kutengeneza mahema, lakini iko tayari kufanya ile kazi ili kujitegemeza. Atapata kazi mu ile muji yenye kuwa na mambo mingi? Atapata fasi ya muzuri ya kuishi? Hata kama ile mambo yote inamuhangaisha, Paulo hasahau mambo ya maana sana yenye ilimuleta kule: kazi ya kuhubiri.

3 Inaonekana kama Paulo alibakia Korinto kwa wakati fulani na kazi yake ya kuhubiri ilikuwa na matokeo ya muzuri. Mambo yenye Paulo alifanya Korinto inaweza kutufundisha nini yenye itatusaidia tutoe ushahidi kwa ukamili kuhusu Ufalme wa Mungu mu eneo yetu?

KORINTO​—MUJI WENYE ULIKUWA KATIKATI YA BAHARI MBILI

Korinto ya zamani ilikuwa sehemu ndogo ya inchi kavu yenye iliunganisha Ugiriki ya kusini yenye iliitwa Peloponisia na sehemu ingine ya inchi ya Ugiriki. Sehemu ya mwembamba zaidi ya Korinto ilikuwa na upana wa kilometre 6. Njo maana Korinto ilikuwa na bandari mbili. Bandari ya mangaribi, ni kusema bandari ya Lekayo, ilikuwa kwa ajili ya mashua zenye kutoka na kuenda Italia, Sisili, na Uhispania. Na bandari ya mashariki, ni kusema bandari ya Kenkrea, ilikuwa kwa ajili ya mashua zenye kuenda na kutoka katika visiwa vya Aegea, Asia Ndogo, Siria, na Misri.

Juu kulikuwa upepo sana mu eneo ya ku mwisho-mwisho ya Peloponisia, ilikuwa hatari sana kwa mashua kupita kule. Njo maana watu wenye kuendesha mashua walipendelea kusimama ku bandari moya kati ya bandari mbili za Korinto. Walikuwa wanashusha mizigo yao ku inchi kavu na kisha walikuwa wanaipeleka ku bandari ingine ya Korinto ili kuitia tena mu mashua. Kama mashua haikukuwa kilo, wangeweza hata kuikokota ku inchi kavu na kuifikisha ku bandari ingine. Juu Korinto ilikuwa katikati, wafanyabiashara wengi walikuya mu ule muji kupitia inchi kavu ao kupitia bahari ili kuuza na kuuzisha vitu. Walileta makuta mu muji, lakini pia walikuwa na mwenendo muchafu sana; kwa hiyo Korinto ikafikia kuwa muji wenye mwenendo mubaya sana.

Wakati wa mutume Paulo, Korinto ilikuwa muji mukubwa wa jimbo ya Waroma ya Akaya, na mambo mingi ya serikali ilikuwa nafanywa pale. Watu wa Korinto waliamini mambo mingi tofauti-tofauti. Kwa mufano kulikuwa hekalu kwenye walikuwa wanaabudu mutawala wa Roma, kulikuwa fasi mingi kwenye walikuwa wanaabudu miungu ya Wagiriki na Wamisri, na kulikuwa sinagogi ya Wayahudi.​—Mdo. 18:4.

Kila miaka mbili watu walikuwa wanafanya michezo karibu na Korinto. Ile michezo ilikuwa ya maana sana sawa tu Michezo ya Olimpiki. Inawezekana Paulo alikuwa Korinto wakati wa michezo ya mwaka 51 K.K.Y. Kamusi moya yenye kufasiria Biblia inasema kama “Haishangaze kuona kama wakati Paulo aliandika barua yake ya kwanza kwa Wakorinto, alitumia mufano kuhusu watu wenye kufanya michezo.”​—1 Ko. 9:24-27.

“Kazi Yao Ilikuwa Kutengeneza Mahema” (Mdo. 18:1-4)

4, 5. (a) Paulo alikuwa naishi wapi wakati alikuwa Korinto, na alifanya kazi gani? (b) Pengine ni namna gani Paulo alifikia kuwa mutengenezaji wa mahema?

4 Wakati fulani kisha Paulo kufika Korinto, alikutana na bibi na bwana Wayahudi wenye walikuwa wakaribishaji-wageni; mwanaume aliitwa Akila na bibi yake aliitwa Prisila ao Priska. Akila na Prisila walihamia Korinto wakati Mutawala Klaudio aliagiza “Wayahudi wote watoke Roma.” (Mdo. 18:1, 2) Akila na Prisila walimukaribisha Paulo ili aishi nao na atumike pamoya nao. Kitabu ya Matendo inasema hivi: “Kwa sababu walifanya kazi ileile, akakaa katika nyumba yao na kufanya kazi pamoja nao, kwa maana kazi yao ilikuwa kutengeneza mahema.” (Mdo. 18:3) Wakati wote wenye Paulo alikuwa nahubiri Korinto, aliishi na wale bibi na bwana wenye walikuwa wakaribishaji-wageni na wenye walikuwa na moyo muzuri. Pengine ni wakati alikuwa anaishi na Akila na Prisila njo aliandika barua fulani zenye zilifikia kuwa kati ya vitabu vya Biblia.b

5 Paulo alikuwa mutu mwenye alisoma sana, juu alifundishwa “kwenye miguu ya Gamalieli.” Sasa namna gani alifikia kuwa mutengenezaji wa mahema? (Mdo. 22:3) Inaonekana kuwa Wayahudi wa karne ya kwanza hawakuona kama ni jambo ya kujizaraulisha kufundisha watoto wao kazi fulani ya mikono, hata kama watoto wao walikuwa nasoma masomo ingine. Juu Paulo alitoka Tarso katika Kilikia, eneo yenye ilijulikana sana kwa sababu ya nguo fulani yenye kuitwa ciliciume yenye ilitumiwa ili kutengeneza mahema, inawezekana Paulo alijifunza ile kazi ya kutengeneza mahema wakati alikuwa kijana. Kazi ya kutengeneza mahema ilikuwa nafanywa namna gani? Mutu alipaswa kukata nguo ya kufanya nayo hema na kisha alipaswa kuishona. Haikukuwa mwepesi kufanya vile juu nguo zenye walikuwa natumia zilikuwa za nguvu-nguvu. Ikuwe ile kazi ilikuwa nafanywa namna gani, ilikuwa tu kazi ya nguvu.

6, 7. (a) Paulo aliona namna gani kazi ya kutengeneza mahema, na nini inaonyesha kama Akila na Prisila walikuwa na mawazo kama yake? (b) Namna gani Wakristo leo wanafuata mufano wa Paulo, Akila, na Prisila?

6 Paulo hakufanya kazi ya kutengeneza mahema ikuwe ya maana zaidi mu maisha yake. Aliifanya juu tu imutegemeze mu kazi yake ya kuhubiri, na ili atangaze habari njema ‘bila kuomba kitu.’ (2 Ko. 11:7) Akila na Prisila nao waliona kazi yao namna gani? Juu walikuwa Wakristo, bila shaka walikuwa na mawazo kama ya Paulo kuhusu kazi ya kimwili. Wakati Paulo aliondoka Korinto mu mwaka wa 52 K.K.Y., Akila na Prisila waliacha kazi yao na wakamufuata Efeso Kule nyumba yao ilitumiwa kuwa fasi ya kufanyia mikutano ya kutaniko. (1 Ko. 16:19) Kisha wakati fulani, walirudia Roma na kisha wakarudia tena Efeso. Wale bibi na bwana wenye bidii, walitia faida za Ufalme pa nafasi ya kwanza na walikuwa tayari kujitoa ili kusaidia wengine. Ile ilifanya “makutaniko yote ya mataifa” iwaonyeshe shukrani​—Ro. 16:3-5; 2 Ti. 4:19.

7 Wakristo wa leo wanafuata mufano wa Paulo, Akila, na Prisila. Leo wahubiri wenye bidii wanatumika sana ili ‘wasiweke muzigo muzito’ kwa wengine. (1 Te. 2:9) Mapainia wengi wanatumikaka siku fulani tu katika juma, ao kipindi fulani tu katika mwaka ili kutimiza mahitaji yao. Lakini kazi ya upainia njo ya maana zaidi mu maisha yao. Kama Akila na Prisila, watumishi wengi wa Yehova wenye kuwa wakaribishaji-wageni wanakaribishaka waangalizi wa muzunguuko ku nyumba zao. Kwa hiyo, wale wenye ‘kufuata njia ya ukaribishaji-wageni’ wanajua kama kufanya vile kunajenga na kunatia moyo sana.​—Ro. 12:13.

BARUA ZENYE KUONGOZWA NA ROHO YA MUNGU ZENYE ZILITIA MOYO

Mu kipindi ya miezi 18 yenye Paulo alikuwa anaishi Korinto mu mwaka wa 50-52 hivi K.K.Y., mutume Paulo aliandika karibu barua mbili zenye zilifikia kuwa sehemu ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo ni kusema Watesalonike wa Kwanza na wa Pili. Aliandika pia barua kwa Wagalatia pengine mu ile kipindi ao wakati kidogo kisha pale.

Watesalonike wa Kwanza njo barua ya kwanza yenye Paulo aliandika yenye ilifikia kuwa kati ya vitabu vya Biblia. Paulo alitembelea Tesalonike mu mwaka wa 50 hivi K.K.Y., wakati alikuwa mu safari yake ya pili ya umisionere. Bila kukawia kutaniko yenye ilianzishwa Tesalonike ilianza kupambana na upinzani wenye ulifanya Paulo na Sila watoke mu ile muji. (Mdo. 17:1-10, 13) Juu Paulo alikuwa na wasiwasi kuhusu hali ya ndugu na dada wenye walikuwa mu ile kutaniko ya mupya alijaribu kurudia kule mara mbili, lakini “Shetani alizuia njia [yake].” Kwa hiyo, Paulo alituma kule Timoteo ili afariji na kutia moyo wale ndugu na dada. Inawezekana ku mwisho-mwisho wa mwaka wa 50 K.K.Y., Timoteo alimukuta Paulo Korinto na alileta ripoti ya muzuri kuhusu kutaniko ya Tesalonike. Kisha pale njo Paulo aliandika barua yake ya kwanza kwa Watesalonike.​—1 Te. 2:17–3:7.

Inawezekana Watesalonike wa Pili iliandikwa muda mufupi kisha Watesalonike wa Kwanza, pengine mu mwaka wa 51 K.K.Y. Mu barua zote mbili Timoteo na Silvano (mwenye anaitwa pia Sila mu kitabu ya Matendo) wanatuma pia salamu pamoya na Paulo. Lakini hakuna kwenye Maandiko inaonyesha kama wale ndugu watatu walikutanaka tena pamoya kisha Paulo kutoka Korinto. (Mdo. 18:5, 18; 1 Te. 1:1; 2 Te. 1:1) Juu ya nini Paulo aliandika ile barua ya Pili? Inaonekana Paulo alikuwa amepata habari zaidi kuhusu kutaniko ya Tesalonike. Pengine mutu mwenye alipeleka barua yake ya kwanza njo alileta ile habari. Habari zenye Paulo alipata zilimuchochea asifu ndugu na dada kwa sababu ya upendo wao na uvumilivu wao, lakini pia arekebishe mawazo ya Watesalonike fulani wenye walikuwa wanasema kama kuwapo kwa Bwana kulikuwa karibu.​—2 Te. 1:3-12; 2:1, 2.

Kulingana na mambo yenye Paulo aliandika mu barua yake kwa Wagalatia inaonekana alikuwa amewatembelea karibu mara mbili mbele awaandikie. Mu mwaka wa 47-48 K.K.Y., Paulo na Barnaba walitembelea Antiokia ya Pisidia, Ikoniamu, Listra, na Derbe; ile miji yote inapatikana mu jimbo ya Waroma ya Galatia. Mu mwaka wa 49 K.K.Y. Paulo alirudia tena mu ile maeneo pamoya na Sila. (Mdo. 13:1–14:23; 16:1-6) Paulo aliandika ile barua juu wale wenye kukazia desturi za Wayahudi walifika Galatia kisha tu Paulo kuondoka, na walikuwa nafundisha kama Wakristo walipaswa kutahiriwa na kufuata Sheria ya Musa. Bila shaka Paulo aliandikia Wagalatia kisha tu kupata habari kuhusu ile mafundisho ya uongo. Pengine aliandika ile barua wakati alikuwa Korinto, lakini inawezekana pia aliiandika wakati alikuwa Efeso kwenye alibakia kwa muda mufupi mu safari yake ya kurudia Antiokia ya Siria ao pia aliiandika wakati alikuwa kule Antiokia.​—Mdo. 18:18-23.

“Wakorinto Wengi . . . Wakaanza Kuamini” (Mdo. 18:5-8)

8, 9. Paulo alifanya nini wakati Wayahudi walimupinga, na alienda kuhubiri wapi?

8 Paulo alifanya kazi ya kimwili ili tu kutegemeza utumishi wake. Ile ilionekana wazi wakati Sila na Timoteo walikuya na zawadi za mingi kutoka Makedonia. (2 Ko. 11:9) Mara moya, Paulo ‘alianza kuhangaikia sana lile neno [“kutumia wakati wake wote kwa ajili ya kuhubiri,” Biblia Habari Njema].” (Mdo. 18:5) Lakini, wakati Paulo alikuwa nahubiri kwa bidii sana, Wayahudi waliendelea kumupinga. Juu walikatala habari kuhusu Kristo yenye ingeweza kuwaokoa, Paulo alikunguta manguo yake na akaambia hivi wale Wayahudi wapinzani: “Damu yenu ikuwe juu ya vichwa vyenu. Mimi niko safi. Kuanzia sasa na kuendelea nitaenda kwa watu wa mataifa.”​—Mdo. 18:6; Eze. 3:18, 19.

9 Paulo angeenda sasa kuhubiri wapi? Mwanaume mwenye kuitwa Titio Yusto, pengine Muyahudi mugeuzwa-imani, mwenye nyumba yake ilikuwa nakamatana na sinagogi, alikaribisha Paulo mu nyumba yake. Kwa hiyo Paulo akaacha kuhubiri mu sinagogi na akaanza kuhubiri mu nyumba ya Yusto. (Mdo. 18:7) Wakati wote wenye alikuwa Korinto, aliendelea kuishi mu nyumba ya Akila na Prisila, lakini nyumba ya Yusto njo ikakuwa fasi ya mahubiri.

10. Nini inaonyesha kama Paulo hakuazimia kuhubiria tu Watu wa Mataifa?

10 Wakati Paulo alisema kama ataenda kwa watu wa mataifa, hakumaanisha kama ataacha kuhubiria Wayahudi ao wageuzwa-imani wenye walikuwa tayari kusikiliza. Kwa mufano, “Krispo, ofisa-musimamizi wa sinagogi akakuwa muamini katika Bwana, yeye pamoja na nyumba yake yote.” Ni wazi kama watu wengine wenye walikuwa naenda mu sinagogi, walijiunga na Krispo, juu Biblia inasema hivi: “Wakorinto wengi wenye walisikia wakaanza kuamini na kubatizwa.” (Mdo. 18:8) Kwa hiyo, nyumba ya Titio Yusto ikakuwa fasi yenye ile kutaniko ya mupya yenye ilianzishwa Korinto ilikuwa nakutana. Ikiwa Luka aliandika matukio namna ilifuatana sawa vile alizoea kufanya, ni kusema wale Wayahudi ao wageuzwa-imani walifikia kuwa Wakristo kisha Paulo kukunguta manguo yake. Kama ni vile ile inaonyesha kama Paulo alikuwa tayari kubadilisha mawazo yake na kuhubiria kila mutu mwenye alipendezwa.

11. Namna gani Mashahidi wa Yehova leo wanaiga mufano wa Paulo wakati wanahubiria watu wenye wanajiita kuwa Wakristo?

11 Leo mu inchi za mingi, makanisa yenye kujiita kuwa ya Kikristo imechochea maisha ya watu wengi. Mu inchi fulani na mu visiwa fulani, wamisionere wa zile makanisa wanajikaza sana ili kufanya watu wengi wakuwe wafuasi wao. Sawa vile Wayahudi wenye walikuwa Korinto mu karne ya kwanza, watu wengi wenye kujiita kuwa Wakristo wanakazia sana desturi za dini yao kuliko uhusiano wao pamoya na Mungu. Lakini, sawa vile Paulo, Mashahidi wa Yehova wanahubiria kwa bidii wale watu na kuwasaidia waelewe mambo yenye wanasoma katika Maandiko. Hata kama wanatupinga ao viongozi wao wa dini wanatutesa, hatupoteze tumaini. Kati ya wale wenye “wako na bidii kwa ajili ya Mungu, lakini haiko kulingana na ujuzi wenye hauna makosa,” kuko wenye wanapenda kujua kweli juu ya Mungu. Kwa hiyo tunapaswa kuwatafuta.​—Ro. 10:2.

“Niko na Watu Wengi Katika Muji Huu” (Mdo. 18:9-17)

12. Yesu alihakikishia Paulo nini katika maono?

12 Ikiwa Paulo alikuwa najiuliza kama ataendelea kuhubiri katika Korinto ao hapana, kisha Yesu kumutokea katika maono usiku, alijua jambo ya kufanya. Yesu alimuambia hivi: “Hakuna mutu mwenye atakushambulia ili kukuumiza; kwa maana niko na watu wengi katika muji huu.” (Mdo. 18:9, 10) Ile ilikuwa maono yenye kutia moyo kabisa! Yesu yeye mwenyewe anamuhakikishia Paulo kama atamulinda juu asitendewe mubaya, na kama mu ile muji muko watu wengi wenye watakubali kweli. Paulo alitenda namna gani kisha kupata ile maono? Biblia inasema hivi: “Akakaa kule kwa mwaka mumoja na miezi sita (6), akifundisha neno la Mungu kati yao.”​—Mdo. 18:11.

13. Inawezekana Paulo alikuwa nafikiria nini wakati alikuwa nakaribia ile kiti ya hukumu, lakini juu ya nini alijua kama ile haitamufikia?

13 Kisha kupitisha karibu mwaka moya mu Korinto, Paulo alijionea jambo ingine yenye ilihakikisha kama Yesu alikuwa anamutegemeza. ‘Wayahudi waliungana na kumushambulia Paulo na wakamupeleka kwenye kiti cha hukumu,’ chenye kiliitwa beʹma. (Mdo. 18:12) Watu fulani wanasema kama ile kiti ya hukumu ilikuwa fasi tambarare yenye kuinuka, yenye ilipatikana karibu na katikati ya soko ya Korinto; ile kiti ilifanyizwa kwa majiwe ya mweupe na ya bleu na ilikuwa na michoro yenye kupendeza. Mbele ya ile kiti ya hukumu kulikuwa fasi ya kutosha kwenye watu wengi wangeweza kukusanyika. Wanahistoria fulani wanasema kama inawezekana ile kiti ya hukumu haikukuwa mbali na sinagogi, na kwa hiyo ilikuwa karibu ya nyumba ya Yusto. Pengine wakati Paulo alikaribia ile kiti ya hukumu, alifikiria namna Stefano alipigwa majiwe kwa sababu alikuwa natoa ushahidi juu ya Kristo. Paulo mwenye ile wakati aliitwa Sauli “alikubaliana na kuuawa kwa Stefano.” (Mdo. 8:1) Jambo ya vile ingefikia Paulo naye? Hapana, juu Yesu alikuwa amemuahidi hivi: ‘Hakuna mutu mwenye . . . atakuumiza.’​—Mdo. 18:10.

Galio anafukuza watu wenye kasirani wenye walimushitaki Paulo. Maaskari waroma wanajaribu kutia mustari wanaume wenye kasirani.

“Halafu akawafukuza kutoka mbele ya kiti cha hukumu.”​—Matendo 18:16

14, 15. (a) Wayahudi walimushitaki Paulo nini na juu ya nini Galio hakukubali ile mashitaka? (b) Nini njo ilimufikia Sostene, na pengine ile ilikuwa na matokeo gani?

14 Nini ilitokea wakati Paulo alifika ku kiti ya hukumu? Muamuzi mwenye alikuwa ku ile kiti, alikuwa gavana wa jimbo ya Akaya, mwenye aliitwa Galio. Alikuwa ndugu mukubwa ya mwanafilozofia Muroma Seneca. Wayahudi wakaanza kumushitaki Paulo hivi: “Mutu huyu anashawishi watu wamuabudu Mungu kwa njia yenye kuwa kinyume cha sheria.” (Mdo. 18:13) Wale Wayahudi walipenda kusema kama Paulo alikuwa anageuza watu kuwa Wakristo kwa kuvunja sheria. Lakini, Galio aliona kama Paulo hakufanya “kosa” na hakukuwa na hatia ya “uvunjaji mukubwa wa sheria.” (Mdo. 18:14) Galio hakupenda kujiingiza mu mabishano ya Wayahudi. Juu hata mbele Paulo aseme neno moya ili kujitetea, Galio alisema uamuzi wake! Watu wenye walimushitaki Paulo walikasirika sana. Na kasirani yao yote waliimwangia Sostene, mwenye pengine alikamata nafasi ya Krispo ya kuwa ofisa musimamizi wa sinagogi. Walikamata Sostene “na wakaanza kumupiga mbele ya kiti cha hukumu.”​—Mdo. 18:17.

15 Juu ya nini Galio hakuzuia watu wasimupige Sostene? Pengine Galio aliwaza kama Sostene njo alikuwa naongoza ile kikundi yenye ilimushitaki Paulo na kwa hiyo alistahili kupigwa. Ikuwe mambo ilikuwa vile ao hapana, inawezekana ile ilileta matokeo ya muzuri. Miaka mingi kisha pale, wakati Paulo aliandikia kutaniko ya Korinto barua ya kwanza, alizungumuzia ndugu fulani mwenye kuitwa Sostene. (1 Ko. 1:1, 2) Alikuwa uleule Sostene mwenye walipigaka Korinto? Kama ni yeye, pengine ile hali ya kuumiza yenye ilimufikiaka ilimusaidiaka afikie kuwa Mukristo.

16. Juu ya nini hii maneno ya Yesu, “Usiogope, lakini uendelee kusema na usinyamaze,” inatuchochea tuendelee kuhubiri?

16 Kumbuka kama ni kisha Wayahudi kukatala mahubiri ya Paulo njo Yesu alimuhakikishia hivi: “Usiogope, lakini uendelee kusema na usinyamaze.” (Mdo. 18:9, 10) Ni muzuri tuendelee kukumbuka ile maneno ya Yesu, zaidi sana wakati watu wanakatala ujumbe wetu. Tusisahau hata siku moya kama Yehova anasoma mioyo ya watu na anavuta kwake watu wenye mioyo mizuri. (1 Sa. 16:7; Yoh. 6:44) Kujua vile kunatuchochea tuendelee kuhubiri kwa bidii! Kila mwaka mamia ya maelfu ya watu wanabatizwa, ni kusema mamia ya watu kila siku. Yesu anawahakikishia hivi wale wenye kufuata amri ya ‘kufanya wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote’: “Niko pamoja na ninyi sikuzote mupaka umalizio wa mupangilio wa mambo.”​—Mt. 28:19, 20.

“Kama Yehova Anapenda” (Mdo. 18:18-22)

17, 18. Pengine Paulo iko nafikiria nini wakati iko mu safari ya kuenda Efeso?

17 Hatujue ikiwa uamuzi wa Galio kuhusu watu wenye walimushitaki Paulo ulifanya kutaniko ya mupya katika Korinto ifurahie kipindi fulani ya amani. Lakini, Paulo alibakia Korinto kwa “siku fulani” mbele ya kulaga ndugu zake wa Korinto. Mu mwaka wa 52 K.K.Y. alifanya mipango ya kuenda Siria. Alienda ku bandari ya Kenkrea, yenye ilikuwa ku kilometre 11 mashariki mwa Korinto ili kukamata mashua. Lakini mbele ya kuondoka Kenkrea, Paulo ‘alikatisha nywele zake . . . , kwa sababu alikuwa amefanya naziri.’c (Mdo. 18:18) Kisha akachukua Akila na Prisila na wakasafiri pamoya katika Bahari ya Aegea ili kuenda Efeso katika Asia Ndogo.

18 Wakati Paulo alikuwa nasafiri mu mashua ya kutoka Kenkrea, inawezekana alikuwa nafikiria wakati wenye alipitisha Korinto. Kuko mambo mingi yenye ilipitikana kule yenye kufurahisha. Mahubiri yake ya miezi 18 mu ile muji, ilikuwa na matokeo ya muzuri. Kutaniko ya kwanza ilianzishwa katika Korinto, na walikuwa wanakutana mu nyumba ya Yusto. Kati ya wale wenye walifikia kuwa waamini, kulikuwa Yusto, Krispo na watu wa nyumba yake, na watu wengine wengi. Paulo alipenda sana wale waamini wapya, kwa sababu aliwasaidia kuwa Wakristo. Kisha wakati fulani, wakati aliwaandikia alisema kama walikuwa barua ya kupendekezwa yenye iliandikwa ku moyo wake. Siye pia tunapendaka sana watu wenye tumesaidia ili waanze kumutumikia Yehova. Tunafurahiaka sana kuona wale ndugu na dada wenye kuwa kama “barua za mapendekezo”!​—2 Ko. 3:1-3.

19, 20. Paulo alifanya nini kisha tu kufika Efeso, na mufano wake unatufundisha nini kuhusu kufuatia miradi ya kiroho?

19 Wakati tu Paulo alifika Efeso, mara moya alianza kazi ya kuhubiri. “Aliingia katika sinagogi na kufikiri na Wayahudi.” (Mdo. 18:19) Lakini mara hii Paulo alibakia Efeso wakati kidogo tu. Hata kama walimuomba abakie kwa wakati murefu, “hakukubali.” Wakati alikuwa nalaga ndugu wa Efeso, aliwaambia hivi: “Nitarudia kwenu tena, kama Yehova anapenda.” (Mdo. 18:20, 21) Bila shaka Paulo alijua kama kulikuwa kungali kazi kubwa ya kuhubiri katika Efeso. Kwa hiyo Paulo alipanga kurudia tena Efeso, lakini aliacha Yehova aamue. Hauone kama ile ni mufano muzuri kwetu? Wakati tuko nafuatia miradi ya kiroho, ni muzuri kukamata hatua fulani. Lakini, siku zote tunapaswa kumutegemea Yehova ili atuongoze, na tunapaswa kutenda kulingana na mapenzi yake.​—Yak. 4:15.

20 Paulo anaacha Akila na Prisila katika Efeso, kisha anakamata mashua ya kuenda Kaisaria. Inaonekana “alipanda” Yerusalemu ili kusalimia ndugu wenye walikuwa mu kutaniko ya Yerusalemu. Kisha akaenda Antiokia ya Siria kwenye alikuwa naishi wakati hakukuwa mu safari. Ni vile safari yake ya pili ya umisionere ilifikia mwisho, na ilikuwa na matokeo mingi ya muzuri. Ni mambo gani itatokea mu safari yake ya mwisho ya umisionere?

NAZIRI YA PAULO

Matendo 18:18 inasema kama wakati Paulo alikuwa Kenkrea, ‘alikatisha nywele zake . . . , kwa sababu alikuwa amefanya naziri.’ Ilikuwa naziri ya namna gani?

Kwa kawaida, naziri ni ahadi ya kujipendea yenye mutu anafanya kwa Mungu juu ya kufanya jambo fulani, kutoa kitu fulani, ao kujiweka mu hali fulani. Watu fulani wanasema kama Paulo alikata nywele zake juu ya kutimiza naziri ya Unaziri. Lakini tukumbuke kama kulingana na Maandiko kisha kipindi ya utumishi wa pekee kwa Mungu, Munaziri alipaswa kukata nywele zake “kwenye muingilio wa hema ya mukutano.” Juu ile ilipaswa kufanyika tu Yerusalemu lakini Paulo alikuwa Kenkrea ile inaonyesha kama haikukuwa naziri ya Unaziri.​—Hes. 6:5, 18.

Habari yenye kuwa mu kitabu ya Matendo haiseme jambo yoyote juu ya naziri yenye Paulo alifanya. Pengine Paulo alifanyaka ile naziri mbele hata akuwe Mukristo. Tena Biblia haiseme ikiwa Paulo alimuomba Yehova jambo fulani ya pekee. Kitabu fulani kinasema kama juu Paulo alikata nywele zake, pengine ilikuwa ili kuonyesha shukrani kwa Mungu juu alimusaidia amalize utumishi wake katika Korinto.

a Ona kisanduku “Korinto​—Muji Wenye Ulikuwa Katikati ya Bahari Mbili.”

b Ona kisanduku “Barua Zenye Kuongozwa na Roho ya Mungu Zenye Zilitia Moyo.”

c Ona kisanduku “Naziri ya Paulo.”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine