Neno la Mungu Linafundisha Nini?
Sababu Gani Tunapaswa Kulitumia Jina la Mungu?
Habari hii inazungumuzia maulizo fulani ambayo labda umejiuliza na inaonyesha mahali ambapo unaweza kupata majibu katika Biblia. Mashahidi wa Yehova watafurahi kukusaidia upate majibu ya maulizo hayo.
1. Sababu gani Mungu amejipatia jina?
Kwa kweli, unapenda watu wakuite kwa jina lako kuliko kukuita kwa majina ya heshima kama vile “mutu,” “bwana,” “bibi,” ao “mwanamuke.” Jina lako linakutofautisha na watu wengine. Mungu anaitwa kwa majina ya cheo ao ya heshima kama vile ‘Bwana Mwenye Enzi Kubwa,’ “Mungu Mweza-Yote,” na ‘Muumbaji Mukubwa.’ (Mwanzo 15:2; 17:1; Mhubiri 12:1) Lakini amejipatia pia jina ili kutusaidia tufanye uhusiano pamoja naye. Katika Kiswahili, jina la pekee la Mungu ni Yehova.—Soma Isaya 42:8.
Katika Biblia nyingi, watafsiri wameliondoa jina la Mungu, na mahali pa jina hilo wametia majina ya cheo ao ya heshima kama vile “Mungu” na “Bwana,” lakini jua kama jina hilo linapatikana karibu mara 7 000 katika maandishi ya kwanza-kwanza ya Biblia katika luga ya Kiebrania. Hilo linaonyesha wazi kama Mungu anapenda watu walijue jina lake.—Soma Isaya 12:4.
2. Sababu gani ni jambo la lazima kujua jina la Mungu?
Kujua jina la Mungu hakumaanishi tu kujua kama anaitwa Yehova, lakini kunamaanisha mambo mengi. Kujua jina la Mungu kunamaanisha kujua maana ya jina hilo na kuwa na uhusiano muzuri pamoja naye. Jina Yehova linamaanisha “Yeye Anajifanya Kuwa.” Jina hilo linatuhakikishia kama Mungu atajifanya chochote kinachohitajika ili atimize kusudi lake. Kwa hiyo, kujua jina la Mungu kunamaanisha tena kuamini kama Mungu atatimiza ahadi zake. (Zaburi 9:10) Imani ya watu ambao wanajua jina la Mungu na kulitumia inawachochea wamutumainie na kumutia pa nafasi ya kwanza katika maisha yao. Yehova Mungu atalinda watu kama hao.—Soma Zaburi 91:14.
3. Sababu gani Mungu anataka watu walijue jina lake?
Mungu anataka watu walijue jina lake kwa sababu kujua jina hilo kunawaletea faida nyingi. Tena, kujua jina la Mungu kunawafanya wawe marafiki wake na kunawapatia tumaini la kuishi milele. Hakika, si jambo la kushangaza ikiwa Yehova anataka tuwasaidie wengine walijue jina lake!—Soma Yohana 17:3; Waroma 10:13, 14.
Yesu aliwajulisha watu jina la Mungu alipowafundisha njia za Mungu, sheria Zake na ahadi Zake. Leo, wafuasi wa Yesu wanaendelea kujulisha jina la Mungu katika mataifa yote. Wanatumika kwa umoja ili kujulisha watu jina la Mungu, wao ni “watu kwa ajili ya jina lake.”—Soma Matendo 15:14; Yohana 17:26.
4. Namna gani Mungu atalitakasa jina lake?
Yehova Mungu atalitakasa jina lake kwa sababu limechafuliwa. Kwa mufano, watu fulani wanasema kama watu hawakuumbwa na Mungu na kwa hiyo si lazima tumutii. Wengine wanasema kama Mungu hatuhangaikie na kama ni yeye ndiye anayetuletea mateso. Watu kama hao wanalichafua jina la Mungu. Lakini Mungu hatawaacha waendelee kulichafua milele. Mungu ataharibu wale wote wanaolichafua jina lake.—Soma Zaburi 83:17, 18.
Yehova atalitakasa jina lake wakati Ufalme wake utaharibu serikali ao guvernema zote za wanadamu na kuletea watu amani na usalama. (Danieli 2:44) Hivi karibuni, kila mutu atajua kama Yehova ndiye Mungu wa kweli.—Soma Ezekieli 36:23; Mathayo 6:9.
Sasa wewe, unapaswa kufanya nini? Umukaribie Mungu kwa kujifunza Neno lake na ujiunge na watu wanaomupenda. Wakati Yehova atalitakasa jina lake, atawakumbuka watumishi wake waaminifu.—Malaki 3:16.
Ili kupata habari zingine, usome sura ya 1 ya kitabu hiki, Biblia Inafundisha nini Hasa?, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.
[Picha katika ukurasa wa 16]
Jina la Mungu katika maandishi ya kwanza-kwanza ya Kiebrania