-
Mapenzi ya Mungu Ni Nini?Ni Nani Wanafanya Mapenzi ya Yehova Leo?
-
-
Mapenzi ya Mungu Ni Nini?
Mungu anapenda tuishi milele katika amani na furaha mu paradiso ku dunia!
Lakini, unaweza kujiuliza hivi: ‘Hilo litawezekana namna gani?’ Biblia inasema kama ni Ufalme wa Mungu njo utafanya vile. Tena, Mungu anapenda watu wote wajifunze juu ya Ufalme huo, na wajue kusudi lake juu ya wanadamu.—Zaburi 37:11, 29; Isaya 9:7.
Mungu anapenda tukuwe na maisha ya muzuri.
Kama vile baba muzuri anapenda watoto wake wakuwe na maisha ya muzuri, Baba yetu wa mbinguni anapenda tuishi milele katika furaha. (Isaya 48:17, 18) Ametoa ahadi (ao malako) kama “ule mwenye anafanya mapenzi ya Mungu anadumu milele.”—1 Yohana 2:17.
Mungu anapenda tutembee katika njia zake.
Biblia inasema kama Muumbaji wetu anapenda ‘kutufundisha njia zake’ ili ‘tutembee katika mapito yake.’ (Isaya 2:2, 3) Amepanga muzuri “watu kwa ajili ya jina lake” ili wajulishe wengine mapenzi yake mu dunia yote.—Matendo 15:14.
Mungu anapenda tumuabudu katika umoja.
Ibada safi ya Yehova hailete mugawanyiko kati ya watu, lakini inawafanya wakuwe na umoja, na wapendane kabisa. (Yohana 13:35) Leo, ni nani wako wanafundisha watu mu dunia yote namna ya kumutumikia Mungu katika umoja? Tunakuomba usome broshua hii ili upate jibu.
-
-
Mashahidi wa Yehova Ni Watu wa Namna Gani?Ni Nani Wanafanya Mapenzi ya Yehova Leo?
-
-
SOMO LA 1
Mashahidi wa Yehova Ni Watu wa Namna Gani?
Denmaki
Taiwan
Venezuela
India
Unajua Mashahidi wa Yehova ngapi? Pengine wamoja kati yetu ni majirani wako, wafanyakazi wenzako, ao wanafunzi wenzako. Ao pengine tumekwisha kuzungumuza na wewe juu ya Biblia. Kwa kweli, sisi ni nani, na juu ya nini tunazungumuzaka na wengine juu ya mambo yenye tunaamini?
Tuko kama watu wengine. Tunatoka mu desturi mbalimbali, na tuko na hali mbalimbali za maisha. Wamoja kati yetu walikuwa mu dini ingine zamani, na wengine hawakukuwa wanamuamini Mungu. Lakini, mbele ya kuwa Mashahidi, sisi wote tulikamata wakati wa kuchunguza muzuri mafundisho ya Biblia. (Matendo 17:11) Tuliona kama mambo yenye tulijifunza ni ya kweli, na kwa hiyo kila mumoja wetu aliamua yeye mwenyewe kumuabudu Yehova Mungu.
Kujifunza Biblia kunatuletea faida. Sisi pia tuko na magumu na uzaifu kama watu wengine. Lakini, juu tunajikaza kutumia kanuni za Biblia mu maisha yetu ya kila siku, maisha yetu imebadilika na imekuwa muzuri zaidi. (Zaburi 128:1, 2) Ile ni sababu moja kati ya sababu zenye zinatuchochea tuambie wengine juu ya mambo ya muzuri yenye tumejifunza mu Biblia.
Tunafuata kanuni za Mungu mu maisha yetu. Kanuni hizo zenye zinapatikana mu Biblia, zinatusaidia kuwa na hali ya muzuri, kuheshimia watu wengine, na kuonyesha sifa mbalimbali kama vile unyoofu ao uaminifu na wema. Kanuni hizo zinatusaidia ili tukuwe na afya ya muzuri na tukuwe wanainchi wazuri, na zinasaidia familia zetu zikuwe na umoja na mwenendo muzuri. Juu tunaamini kabisa kama “Mungu hana ubaguzi,” tunajiona kuwa familia moja ya ndugu na dada mu dunia yote, hatuna ubaguzi wa rangi ya ngozi, na hatuache mambo ya politike itugawanye. Hata kama tuko kama watu wengine, familia yetu ya ndugu na dada mu dunia yote ni ya pekee.—Matendo 4:13; 10:34, 35.
Juu ya nini Mashahidi wa Yehova wako kama watu wengine?
Mashahidi wamejifunza kanuni gani mu Biblia?
-
-
Juu ya Nini Tunaitwa Mashahidi wa Yehova?Ni Nani Wanafanya Mapenzi ya Yehova Leo?
-
-
SOMO LA 2
Juu ya Nini Tunaitwa Mashahidi wa Yehova?
Noa
Abrahamu na Sara
Musa
Yesu Kristo
Watu wengi wanawaza kama Mashahidi wa Yehova ni jina la dini ya mupya. Lakini, miaka zaidi ya 2 700 yenye imepita, Mungu wa kweli aliita watumishi wake kuwa “mashahidi” wake. (Isaya 43:10-12) Mbele ya mwaka wa 1931, tulikuwa tunaitwa Wanafunzi wa Biblia. Juu ya nini tulikamata jina Mashahidi wa Yehova?
Jina hilo linaonyesha Mungu wetu ni nani. Jina la Mungu, Yehova, linapatikana mara 7 000 hivi katika maandishi ya zamani ya Biblia. Mu tafsiri za mingi za Biblia wameondoa jina hilo, na nafasi ya jina hilo wametia majina ya cheo ao ya heshima, kama vile Bwana ao Mungu. Lakini Mungu wa kweli yeye mwenyewe njo alimuambia Musa kama jina lake ni Yehova. Alimuambia Musa hivi: “Hilo ndilo jina langu milele.” (Kutoka 3:15) Jina hilo linaonyesha kama iko tofauti na miungu yote ya uongo. Tuko wenye furaha sana juu tunaitwa kwa jina takatifu la Mungu.
Jina hilo linaonyesha kazi yetu. Watu wengi wa zamani, kuanzia Abeli mutu mwenye haki, walimuamini Yehova na walitoa ushahidi juu yake. Noa, Abrahamu, Sara, Musa, Daudi, na wengine walijiunga na “wingu [hilo] kubwa la mashahidi.” (Waebrania 11:4–12:1) Kama vile tu mutu anaweza kutoa ushahidi kwenye tribinali ili kutetea mutu fulani mwenye hana kosa, sisi pia hatutaacha kuelezea wengine kweli juu ya Mungu wetu.
Tunafuata mufano wa Yesu. Biblia inaita Yesu “shahidi muaminifu na wa kweli.” (Ufunuo 3:14) Yesu mwenyewe alisema kama ‘alijulisha jina la Mungu’ na aliendelea ‘kutoa ushahidi juu ya ile kweli’ kuhusu Mungu. (Yohana 17:26; 18:37) Kwa hiyo, wanafunzi wa kweli wa Kristo wanapaswa kuitwa kwa jina la Yehova na kujulisha watu wengine jina hilo. Mashahidi wa Yehova wanajikaza kufanya vile.
Juu ya nini Wanafunzi wa Biblia walikamata jina Mashahidi wa Yehova?
Yehova amekuwa na mashahidi hapa ku dunia kuanzia wakati gani?
Ni nani mwenye kuwa Shahidi mukubwa zaidi wa Yehova?
-