-
Ulizo la 13: Biblia inasema nini juu ya kazi?Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
ULIZO LA 13
Biblia inasema nini juu ya kazi?
“Je, umemuona mutu mwenye ufundi katika kazi yake? Atasimama mbele ya wafalme; hatasimama mbele ya watu wa kawaida.”
“Ule mwenye kuiba asiibe tena; lakini afanye kazi kwa bidii, akifanya kazi ya muzuri kwa mikono yake, ili akuwe na kitu cha kumupatia mutu mwenye kuwa katika uhitaji.”
“Kila mutu anapaswa kula na kunywa na kufurahia kazi yake yote ya nguvu. Ni zawadi ya Mungu.”
-
-
Ulizo la 14: Namna gani unaweza kutumia mali yako?Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
ULIZO LA 14
Namna gani unaweza kutumia mali yako?
“Mwenye anapenda kujifurahisha atakuwa maskini; mwenye anapenda divai na mafuta hatakuwa tajiri.”
“Mukopaji ni mutumwa wa mukopeshaji.”
“Ni nani kati yenu mwenye akitaka kujenga munara hakae kwanza na kuhesabia garama, ili aone kama iko na vitu vya kutosha ili kuumaliza? Kama hafanye vile, anaweza kuweka musingi lakini anashindwa kumaliza munara, na wale wenye kumuangalia wataanza kumuchekelea, na kusema: ‘Mutu huyu alianza kujenga lakini hakuweza kumaliza.’”
“Wakati walikuwa wamekula na kushiba, akaambia wanafunzi wake: ‘Mukusanye pamoja vipande vyenye vilibakia, ili kitu chochote kisipotee.’”
-
-
Ulizo la 15: Unaweza kufanya nini ili upate furaha?Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
ULIZO LA 15
Unaweza kufanya nini ili upate furaha?
“Ni muzuri zaidi kula mboga za majani mahali kwenye kuko upendo kuliko kula ngombe-dume mwenye kunenepa mahali kwenye kuko chuki.”
“Mimi, Yehova, niko Mungu wako, Mwenye anakufundisha ili ujipatie faida, Mwenye anakuongoza katika njia yenye unapaswa kutembea ndani yake.”
“Wenye furaha ni wale wenye wanatambua uhitaji wao wa kiroho, kwa sababu Ufalme wa mbinguni ni wao.”
“Unapaswa kumupenda jirani yako kama wewe mwenyewe.”
“Kama vile munataka watu wawatendee ninyi, muwatendee kwa njia ileile.”
“Wenye furaha ni wale wenye wanasikia neno la Mungu na kulishika!”
“Wakati mutu iko na vitu vingi, uzima wake hautokane na vitu vyenye iko navyo.”
“Basi, kama tuko na chakula na nguo, tutatosheka na vitu hivyo.”
“Kuko furaha zaidi katika kutoa kuliko katika kupokea.”
-
-
Ulizo la 16: Namna gani unaweza kupiganisha mahangaiko?Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
ULIZO LA 16
Namna gani unaweza kupiganisha mahangaiko?
“Umutupie Yehova muzigo wako, naye atakutegemeza. Hataruhusu hata kidogo mwenye haki aanguke.”
“Mipango ya wenye bidii hakika inaleta mafanikio, lakini wale wote wenye kutenda haraka-haraka hakika watakuwa maskini.”
“Usiogope, kwa maana niko pamoja na wewe. Usihangaike, kwa maana niko Mungu wako. Nitakutia nguvu, ndiyo, nitakusaidia, nitakushika kwelikweli kwa mukono wangu wa kuume wa haki.”
“Ni nani kati yenu mwenye kwa kuhangaika anaweza kuongeza kipimo cha mukono mumoja kwenye urefu wa uzima wake?”
“Basi, musihangaike hata kidogo juu ya kesho, kwa maana kesho itakuwa na mahangaiko yake yenyewe. Kila siku iko na matatizo yake yenye yanaeneana na siku hiyo.”
“Muhakikishe mambo ya maana zaidi.”
“Musihangaike juu ya jambo lolote, lakini katika kila jambo kwa sala na sala ya kumulilia Mungu pamoja na kutoa shukrani, maombi yenu yajulishwe Mungu; na amani ya Mungu yenye kupita uelewaji wote italinda mioyo yenu na nguvu zenu za akili kupitia Kristo Yesu.”
-
-
Ulizo la 17: Namna gani Biblia inaweza kusaidia familia yako?Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
ULIZO LA 17
Namna gani Biblia inaweza kusaidia familia yako?
BWANA/BABA
“Kwa njia ileile, bwana wanapaswa kupenda bibi zao kama miili yao wenyewe. Mwanaume mwenye anamupenda bibi yake anajipenda yeye mwenyewe, kwa maana hakuna mutu mwenye anachukia mwili wake; lakini anaukulisha na kuutunza kwa upendo . . . Kila mumoja wenu anapaswa kumupenda bibi yake kama vile anajipenda mwenyewe.”
“Ninyi baba, musikuwe munakasirisha watoto wenu, lakini muendelee kuwalea katika nizamu na maonyo ya Yehova.”
BIBI
“Bibi anapaswa kumuheshimia sana bwana yake.”
“Ninyi bibi, mujitiishe kwa bwana zenu, kwa kuwa inafaa katika Bwana.”
WATOTO
“Watoto, mutii wazazi wenu katika umoja na Bwana, kwa maana hilo ni jambo la haki. ‘Heshimia baba yako na mama yako,’ hiyo ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi: ‘Ili mambo yakuendee muzuri na ukae wakati murefu katika dunia.’”
“Ninyi watoto, mutii wazazi wenu katika kila jambo, kwa maana hilo linamupendeza Bwana.”
-