Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Kutoa Ushahidi Katika Eneo la Biashara
Sababu Gani Ni Lazima Kufanya Hivyo: Watu wengi wanapitisha muda wao mwingi kwenye kazi, kwa hiyo ili wapate ujumbe wa Ufalme ni lazima tuwafuate mahali kwenye wanafanyia kazi. Kutoa ushahidi katika eneo la biashara kunaweza kuleta matokeo mazuri, kwa sababu watu hawakose kuwa kwenye kazi yao na tena wanaheshimia kila mutu mwenye anakuja kwenye kazi yao kwa kuwa wanafikiri kwamba anakuja kununua vitu. Ili wapate matokeo mazuri, wahubiri wanapaswa kuwa na utambuzi, kuvaa muzuri na kujipamba kwa kiasi. (2 Kor. 6:3) Kwa hiyo, mwangalizi wa utumishi anapaswa kujua kama eneo za biashara zimehubiriwa mara ngapi, na wahubiri gani.
Tumikisha Shauri Hili Katika Mwezi:
Katika Ibada ya Familia ya mangaribi, mufanye mazoezi kuhusu namna ya kutoa ujumbe mufupi wakati mutu anahubiri katika eneo la biashara.