Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w15 1/3 uku. 3
  • Sababu Gani Tuko na Lazima ya Kuokolewa?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Sababu Gani Tuko na Lazima ya Kuokolewa?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Namna Gani Adui Wetu Kifo Ataharibiwa?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2019
  • Inawezekana Kuishi Milele
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Watu Waliokufa Wako Wapi?
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Unaweza Kuishi Miaka Ngapi?
    Amuka!—2013
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 1/3 uku. 3
Fungu ndogo la maua yenye itakauka baadaye

HABARI KUBWA | YESU ANATUOKOA—NAMNA GANI?

Sababu Gani Tuko na Lazima ya Kuokolewa?

‘Mwanadamu, aliyezaliwa na mwanamuke, ana maisha mafupi na yenye kujaa musukosuko [taabu]. Amechanuka kama ua na kukatiliwa mbali, naye anakimbia kama kivuli wala haendelee kuwako.’—Ayubu 14:1, 2.

Tangu zamani watu wamewaza juu ya namna ingekuwa muzuri sana kuishi milele katika afya ya muzuri na bila kuzeeka. Lakini jambo la kuhuzunisha ni kwamba sisi wanadamu tunakufa. Ayubu alisema maneno yenye kuwa hapo juu kumepita miaka zaidi ya elfu tatu, lakini maneno hayo yangali ya kweli leo.

Tamaa ya kuishi milele ni yenye nguvu sana, na kila mutu iko na tamaa hiyo. Biblia inatuonyesha kuwa Mungu ametia tamaa ya kuishi milele katika mioyo yetu na pia tamaa ya kuelewa maana ya kuishi milele. (Mhubiri 3:11) Kwa hiyo, unaona kuwa ni jambo lenye kueleweka Mungu mwenye upendo aweke ndani yetu tamaa yenye haiwezekane kutimiza? Ikiwa unajibu hapana, haukosee. Neno la Mungu linasema kuwa kifo ni adui na linaahidi kuwa ‘kitaangamizwa.’—1 Wakorintho 15:26.

Bila shaka, kifo ni adui. Hakuna mutu mwenye akili sawa anayefurahia kifo. Wakati hatari inakaribia, tunaiepuka, tunajificha, ao kukimbia. Wakati tunagonjwa, tunatafuta namna ya kupona. Tunafanya kila jambo lenye tunaweza ili kuepuka mambo yenye yanaweza kutuletea kifo.

Kuna sababu yoyote ya kuamini kuwa adui huyo wa tangu zamani ataangamizwa kabisa? Ndiyo. Yehova Mungu, Muumbaji, hakuumba watu ili waishi tu miaka kidogo na kisha wakufe. Katika kusudi lake la mwanzoni, Mungu hakupenda watu wakufe. Alitaka watu waishi milele kwenye dunia, na anatimiza kila jambo lenye anakusudia.—Isaya 55:11.

Basi, namna gani kifo kitamalizwa? Tangu zamani, watu wamejikaza kumaliza kifo, lakini hawajaweza. Mupaka leo, watu wanaendelea kupiganisha kifo. Wanasayansi wamefanya chanjo (vaccin) na madawa yenye yamezuia magonjwa fulani. Wamechunguza kwa uangalifu muundo wa chembe za uriti za viumbe vyenye uzima. Katika maeneo mengi, inakadiriwa kuwa leo watu wanaishi miaka mingi kuliko katika miaka mia moja iliyopita. Lakini, kifo hakijamalizwa. Kama vile Biblia inasema, watu “wote wanarudi mavumbini.”—Mhubiri 3:20.

Habari ya muzuri ni hii: Hatupaswe kutegemea akili ya watu ili kumaliza tatizo hilo la muda murefu. Tayari Yehova Mungu amefanya mupango ili kutuokoa ao kutukomboa kutoka katika kifo, na mutu wa maana katika mupango huo ni Yesu Kristo.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine