Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Namna Gani Unaweza Kusaidia Kutia Nguvu Umoja Wetu wa Kikristo?
    Munara wa Mulinzi (Gazeti la Funzo)—2016 | Mwezi wa 3
    • sababu bibi na bwana wenye kuwa Mashahidi wa Yehova wanapaswa kuungana mukono. Hata kama umekuwa katika ndoa tangu miaka mingi ao umeoa ao kuolewa hivi karibuni, ufikirie mambo yenye unaweza kusema ao kufanya ili ndoa yako ikuwe nguvu. Ikiwa mumekuwa katika ndoa tangu miaka mingi, munaweza kuwa mufano muzuri kwa wale wenye wameoana hivi karibuni. Pengine munaweza kuwaalika kwenye ibada yenu ya familia. Wataona kwamba bibi na bwana wanapaswa kupendana na kuwa na umoja hata kama wamefanya miaka mingi katika ndoa ao wameoana hivi karibuni.—Tito 2:3-7.

      ‘TUENDE JUU KWENYE MULIMA WA YEHOVA’

      16, 17. Watumishi wa Mungu wenye kuwa na umoja wanangojea nini?

      16 Wakati Waisraeli walikuwa wanaenda kwenye sikukuu zao huko Yerusalemu, waliungana mukono. Walikuwa wanatayarisha vitu vyote vyenye walikuwa navyo lazima kwa ajili ya safari. Kisha, walisafiri pamoja na kusaidiana. Wote walimusifu Yehova na kumuabudu pamoja kwenye hekalu. (Luka 2:41-44) Kwa sababu tunajitayarisha leo ili kuishi katika dunia mupya, tunapaswa kuwa na umoja na kujikaza sana ili tuungane mukono. Unaweza kufikiria njia fulani zenye unaweza kutumia ili uendelee kufanya hivyo zaidi?

      17 Watu wa ulimwengu huu hawasikilizane na wanapigana. Lakini sisi tunamushukuru Yehova kwa sababu ametusaidia tukuwe na amani na tuelewe kweli! Katika dunia yote, watumishi wake wanamuabudu katika njia yenye kumupendeza. Pia, kuliko wakati mwingine wowote, katika siku hizi za mwisho, watumishi wa Yehova wanaishi katika umoja. Kama vile tu nabii Isaya na Mika walitabiri, tunaenda pamoja kwenye ‘mulima wa Yehova.’ (Isaya 2:2-4; soma Mika 4:2-4.) Wakati unaokuja, tutafurahi sana wakati watu katika dunia yote ‘wataunganishwa pamoja kwa upatano’ ili kumuabudu Yehova pamoja!

  • Yehova Anaongoza Watu Wake Katika Njia ya Uzima
    Munara wa Mulinzi (Gazeti la Funzo)—2016 | Mwezi wa 3
    • Bibi na bwana wako katika motokari, mbele ya alama zenye kuonyesha mahali njia ya treni inakutana na barabara

      Yehova Anaongoza Watu Wake Katika Njia ya Uzima

      ‘Hii ndiyo njia. Mutembee ndani yake.’—ISAYA 30:21.

      NYIMBO: 65, 48

      UTAJIBU NAMNA GANI?

      • Yehova alitoa muongozo gani wakati wa Noa na wakati wa Musa?

      • Ni muongozo gani mupya wenye Mungu aliwapatia Wakristo?

      • Namna gani tunaweza kuonyesha kwamba tunategemea muongozo wa Mungu?

      1, 2. (a) Ni onyo gani lenye limeokoa uzima wa watu wengi? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.) (b) Watu wa Mungu wako na muongozo gani wenye unaweza kuokoa uzima wao?

      “SIMAMA, TAZAMA, SIKILIZA.” Maneno hayo yalionekana kwenye pankarte kubwa zenye zilipatikana nafasi barabara zinakutana na njia za treni katika Amerika ya Kaskazini. Maneno hayo yalitumiwa zaidi ya miaka 100. Sababu gani? Kwa sababu treni zenye kukimbia sana zingegonga motokari zenye kuvuka njia hizo. Watu wengi waliokoa uzima wao kwa sababu ya kutii maneno hayo ya kuonya.

      2 Yehova hatuandikie kwenye pankarte maneno ya kutuonya; lakini anatufanyia jambo fulani la maana zaidi. Anaongoza watu wake ili waepuke hatari na wapate uzima wa milele. Yehova ni kama muchungaji mwenye upendo mwenye anaongoza na kuonya kondoo zake ili wasipite katika njia zenye kuwa na hatari.—Soma Isaya 30:20, 21.

      YEHOVA AMEONGOZA WATU WAKE TANGU ZAMANI

      3. Namna gani wanadamu wote waliingia katika njia yenye kuongoza kwenye kifo?

      3 Tangu wakati aliumba mwanadamu, Yehova amewapatia maagizo ao miongozo yenye kuwa wazi. Kwa mufano, katika shamba la Edeni, Yehova alitoa maagizo yenye kuwa wazi yenye ingeongoza wanadamu kwenye uzima wa milele na kuwaletea furaha. (Mwanzo 2:15-17) Lakini Adamu na Eva hawakufuata muongozo wa Baba yao mwenye upendo. Eva alisikiliza mashauri yenye Shetani alimutolea kupitia nyoka, na kisha Adamu alimusikiliza Eva, bibi yake. Ni nini iliwapata? Wote wawili walipata mateso, na walikufa bila kuwa na tumaini lolote. Pia, kwa sababu walishindwa kutii, waliongoza wanadamu wote katika njia yenye kuongoza kwenye kifo.

      4. (a) Sababu gani wanadamu walikuwa na lazima ya maagizo mengine kisha Garika? (b) Namna gani hali mupya ya wanadamu ilionyesha mawazo ya Mungu?

      4 Mungu alimupatia Noa maagizo yenye iliokoa uzima. Kisha Garika, Yehova aliwapatia wanadamu amri yenye kuwakataza kula ao kunywa damu. Sababu gani? Kwa sababu Yehova alikuwa tayari kuwaruhusu waanze kula nyama. Hali hiyo mupya ilifanya wakuwe na lazima ya maagizo haya mapya: ‘Isipokuwa tu nyama pamoja na nafsi [uzima] yake—damu yake—musikule.’ (Mwanzo 9:1-4) Amri hiyo inatusaidia kujua mawazo ya Mungu juu ya uzima, kwa sababu ulitoka kwake. Yeye ni Muumbaji na anatupatia uzima; kwa hiyo, iko na haki ya kutupatia maagizo juu ya uzima. Kwa mufano, alitolea wanadamu amri yenye kuwakataza kuuana. Mungu anaona uzima na damu kuwa vitakatifu; kwa hiyo, atawapatia malipizi watu wenye kutumia mubaya mambo hayo.—Mwanzo 9:5, 6.

      5. Tutazungumuzia nini, na sababu gani?

      5 Kisha wakati wa Noa, Mungu hakuacha kuongoza watu wake. Katika habari hii, tutazungumuzia mifano fulani yenye kuonyesha namna aliwaongoza. Kuzungumuzia tena mifano hiyo kutatusaidia tuamue kufuata kabisa maagizo yenye Yehova atatupatia katika dunia mupya.

      TAIFA MUPYA LINAPEWA MUONGOZO MUPYA

      6. Sababu gani watu wa Mungu walipaswa kutii sheria zenye aliwapatia kupitia Musa, na Waisraeli walipaswa kuziona namna gani?

      6 Wakati wa Musa, Yehova alipatia watu wake muongozo wenye kuonyesha namna walipaswa kujiendesha na namna ya kumuabudu. Sababu gani? Kwa sababu hali ya watu wake ilikuwa imebadilika tena. Waisraeli walikuwa watumwa katika inchi ya Misri kwa muda wa miaka zaidi ya 200. Waliishi kati ya watu wenye waliabudu wafu, wenye kutumia sanamu, na wenye kufanya mambo mengine mengi yenye kumukosea Mungu heshima. Wakati watu wa Mungu walikombolewa kutoka Misri, walikuwa na lazima ya maagizo mapya. Walipaswa kuwa taifa lenye kufuata Sheria ya Yehova tu. Vitabu fulani vinasema kwamba neno la Kiebrania lenye kutafsiriwa “sheria” linapatana na neno lenye kumaanisha “muongozo, kiongozi, ao mwalimu.” Sheria iliwalinda Waisraeli ili wasikuwe na mwenendo muchafu na waepuke dini ya uongo ya mataifa yenye yaliwazunguka. Wakati Waisraeli walitii Sheria hiyo, Mungu aliwabariki. Wakati walishindwa kutii, walipatwa na mambo mabaya sana.—Soma Kumbukumbu la Torati 28:1, 2, 15.

      7. (a) Eleza sababu gani Yehova aliwapatia watu wake muongozo. (b) Namna gani Sheria ilikuwa mutunzaji wa Waisraeli?

      7 Kulikuwa sababu ingine yenye ilifanya Waisraeli wapewe muongozo mupya. Sheria iliwatayarisha kwa ajili ya tukio la maana sana katika mupango wa Yehova, ni kusema,

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine