Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha
TAREHE 5-11/06
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | YEREMIA 51-52
“Neno la Yehova Linatimia Hata Katika Mambo Madogo-madogo”
it-2 uku. 243 fu. 5-6
Wamede, Inchi ya Mede
Pamoja na Waperse wanashambulia Babiloni. Katika miaka ya 700 M.K.Y., nabii Isaya alisema kama Yehova atachochea ushambulizi wa Babiloni kupitia ‘Wamede, ambao hawaione feza kuwa kitu na ambao, kwa habari ya zahabu, hawapendezwe nayo. Na pinde zao zitawavunja vipande-vipande hata vijana’ (Isa 13:17-19; 21:2) Hapa, inawezekana neno ‘Wamede’ linamaanisha pia Waperse, kwa sababu wanahistoria Wagiriki wa zamani walitumia mara nyingi neno hilo ili kumaanisha Wamede na Waperse. Kwa sababu hawakupendezwa na feza na zahabu, inaonekana kama wakati Wababiloni walishambulia, hawakukuwa na kusudi la kutafuta mali, walitaka tu kukamata muji; kwa hiyo, wala rushwa (kata-midomo) wala malipo yoyote haingewafanya waachane na mupango wao. Kama vile Waperse, silaha ya kwanza ya Wamede ilikuwa upinde. Upinde huo wa muti, wenye wakati fulani ulichanganywa na shaba nyeusi ao shaba nyekundu (linganisha na Zab 18:34), ‘ulivunja vipande-vipande vijana’ wa Babiloni pengine kwa kuwatoboa-toboa na mishale yenye walinoa sana ili iingie mupaka ndani sana.—Yer 51:11.
Kati ya maadui wa Babiloni, Yeremia (51:11, 28) inataja ‘wafalme wa Wamede;’ inawataja kwa uwingi kwa sababu, pengine wakati wa utawala wa Cyrus, kulikuwa pia mufalme moja ao wawili wa Waperse mwenye alikuwa anatawala; ilikuwa hivyo wakati wa zamani. (Linganisha na Yer. 25:25.) Tena, tunaona kama, wakati Babiloni ilikamatwa na majeshi yenye kuchangana ya Wamede, Waperse, Waelamu, na makabila mengine jirani, ni Mumede mwenye kuitwa Darius, ndiye ‘alifanywa kuwa mufalme juu ya ufalme wa Wakaldayo,’ pengine Mufalme Cyrus le Perse ndiye alimuweka hapo.—Dan 5:31; 9:1
it-2 uku. 365 fu. 6
Nabonide
Jambo la kushangaza, wanahistoria wanasema hivi juu ya kuanguka kwa Babiloni: “Askari wa Cyrus waliingia katika Babiloni pasipo kupigana vita.” Pengine hilo linamaanisha kama hakukukuwa vita kubwa na kwa hiyo inapatana kabisa na unabii wa Yeremia wenye ulisema kama ‘wanaume wenye nguvu wa Babiloni wangeacha kupigana.’—Yer 51:30.
it-1 uku. 252 fu. 2
Babiloni
Kuanzia mwaka huu wa maana sana, 539 M.K.Y., utukufu wa Babiloni ukaanza kufifia kulingana na namna muji ulirudia nyuma. Watu wa muji walitomboka ili kumupinga Darius I (Hystaspe), mufalme wa Waperse na wakati walifanya hivyo mara ya pili, muji ulibomolewa. Kisha kujengwa kwa sehemu, watu wa muji walitomboka mara ingine ili kumupinga Xerxès I na vitu vyote vya muji vikanyanganywa. Alexandre le Grand alipanga kufanya Babiloni kuwa muji wake mukubwa lakini alikufa haraka katika mwaka wa 323 M.K.Y. Nicator alikamata muji huo katika mwaka wa 312 M.K.Y. na akabeba sehemu kubwa ya vitu vya muji na kuvipeleka pembeni ya muto Tigre ili kujenga muji wake mukubwa mupya Séleucie. Lakini, wakati wa mitume, muji wa Babiloni ulikuwa bado ungali na Wayahudi fulani; ndiyo sababu mutume Petro alitembelea muji huo, namna anaonyesha mwenyewe katika barua yake. (1Pet 5:13) Maandishi ya Babiloni inaonyesha kama hekalu la Bel liliendelea kuwa huko mupaka mwaka wa 75 K.K.Y. Inaonekana kama, katika miaka ya 300 hivi muji huo haukukuwa tena. Uligeuka kuwa “marundo ya mawe.”—Yer 51:37.
Chimba Ili Kutapata Mali ya Kiroho
it-2 uku. 340 fu. 8
Mulima, Milima
Zinafananisha guvernema. Katika Biblia, mara nyingi milima inaweza kufananisha ufalme ao guvernema zenye kutawala. (Dan 2:35, 44, 45; linganisha na Isa 41:15; Ufu 17:9-11, 18.) Babiloni inaitwa ‘mulima wenye kuharibu’ kwa sababu majeshi yake yalishambulia mataifa mengi na kuyaharibu. (Yer 51:24, 25) Zaburi moja yenye kuzungumuzia matendo ya Yehova juu ya wanaume wapiganaji vita inamutaja hivi: “Umefunikwa na nuru, una utukufu kuliko milima ya mawindo.” (Zab 76:4) Pengine “milima ya mawindo” inafananisha falme zenye kupenda vita (Linganisha na Nah 2:11-13.) Daudi alisema hivi juu ya Yehova: ‘Umeusimamisha mulima wangu katika nguvu.’ Pengine Daudi alitaka kusema kama Yehova alisimanisha ufalme wake na kuufanya ukuwe nguvu. (Zab 30:7; linganisha na 2Sam 5:12.) Kuona kama milima inaweza kufananisha ufalme kunatusaidia tuelewe andiko la Ufunuo 8:8 lenye kuzungumuzia ‘kitu fulani kama mulima mukubwa unaowaka moto.’ Kufananisha “kitu fulani” hicho na mulima wenye kuwaka moto kunatuchochea tufikiri kama, pengine kitu fulani hicho ni utawala fulani wenye kuharibu kama moto.
it-2 uku. 258 fu. 2
Bahari
Majeshi yenye kujaa. Yeremia anasema kama sauti ya watu wenye kushambulia Babiloni inafanana na mungurumo wa “bahari.” (Yer 50:42) Kwa hiyo, wakati anasema kama “bahari” itakuja juu ya Babiloni, ni wazi kama alitaka kuzungumuzia kujaa kwa majeshi yenye kushambulia ya Wamede na Waperse.—Yer 51:42; linganisha na Dan 9:26.
TAREHE 12-18/06
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MAOMBOLEZO 1-5
“Kuendelea Kungojea Kunatusaidia Tuvumilie”
“Nafsi Yako Itainama juu Yangu”
Hata kama watu wengi walikuwa na huzuni, Yeremia alikuwa na tumaini kubwa. Alimulilia Yehova hivi: “Hakika nafsi yako [Yehova mwenyewe] itakumbuka na kuinama juu yangu.” (Mustari wa 20) Yeremia alikuwa na tumaini kabisa. Alijua kama Yehova hangemusahau yeye na Waisraeli wengine wenye walitubu. Basi, Mungu mweza-yote angefanya nini kwa ajili yao?—Ufunuo 15:3.
Yeremia alikuwa hakika kama Yehova ‘atainama’ ao kujishusha kuelekea wale wenye walitubu kwelikweli. Tafsiri ingine inasema hivi: ‘Kumbuka, na uniinamie.’ Maneno hayo yanatusaidia tumuone Yehova kuwa mutu mwenye kutuhangaikia kwa upendo. Yehova, ‘Aliye Juu Zaidi ya dunia yote,’ atainama ao kujishusha ili kuwainua tena waabudu wake watoke katika hali mubaya, na kuwafanya tena wakuwe na tumaini. (Zaburi 83:18) Hata kama Yeremia alikuwa na huzuni sana, tumaini hilo lilimutegemeza na kumufariji. Kwa hiyo, nabii huyo muaminifu aliamua kuvumilia mupaka wakati Yehova angewakomboa watu Wake wenye walitubu.—Mustari wa 21.
Yehova ni Fungu Langu
Yehova angekuwa fungu la kabila lote la Walawi. Hata hivyo, ni muzuri kuona kama Walawi wakiwa mutu moja-moja walitumia maneno “Yehova ni fungu langu” ili kuonyesha kama walijitoa kwa Mungu na kumutegemea yeye. (Omb. 3:24) Mulawi mwenye alisema hivyo alikuwa mwimbaji na mutungaji wa nyimbo. Tutamuita Asafu, hata kama, pengine alikuwa mutu wa familia ya Asafu, ule Mulawi mwenye aliongoza waimbaji katika siku za Mufalme Daudi. (1 Nya. 6:31-43) Zaburi ya 73 inasema kama Asafu (ao mumoja wa wazao wake) alishangaa. Aliwaonea wivu watu waovu wenye walikuwa na maisha ya muzuri na akafikia hatua ya kusema hivi: “Hakika nimeusafisha moyo wangu bure na kuiosha mikono yangu katika kutokuwa na hatia.” Inaonekana kama hakuchukua kwa uzito pendeleo lake la utumishi; hakuona kama Yehova alikuwa fungu lake. Aliteseka kiroho ‘mupaka alipoingia katika patakatifu pakuu pa Mungu.’—Zab. 73:2, 3, 12, 13, 17.
w07 1/6 uku. 11 fu. 4-5
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Maombolezo
3:21-26, 28-33. Namna gani tunaweza kuvumilia hata mateso makali sana? Yeremia anatufundisha. Hatupaswe kusahau hata kidogo kama Yehova amejaa matendo ya fazili zenye upendo na kama rehema zake ni nyingi. Tunapaswa pia kukumbuka kama kuwa hai kunatupatia sababu nzuri ya kuendelea kuwa na tumaini na kama tunapaswa kuwa wenye subira na kungojea wokovu wa Yehova, kimya-kimya na bila kulalamika. Zaidi ya hayo, tunapaswa ‘kutia kinywa chetu mavumbini,’ ni kusema, kukubali majaribu kwa unyenyekevu, tukijua kama Mungu iko na sababu nzuri ya kuacha majaribu hayo yatokee.
3:27. Kwa vijana fulani, kupambana na majaribu ya imani kunaweza kunamaanisha kupambana na hali ngumu na zihaka. Lakini ni ‘jambo njema kwa mwanaume kuchukua nira wakati wa ujana wake.’ Sababu gani? Kujifunza kuchukua nira ya mateso wakati wa ujana kunamutayarisha mutu kupambana na matatizo yake ya wakati wenye kuja.
Chimba Ili Kupata Mali ya Kiroho
w07 1/6 uku. 9 fu. 4
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Maombolezo
2:17—Ni “neno” gani lenye Yehova alitimiza kuhusiana na Yerusalemu? Inawezekana neno hilo linahusu andiko la Mambo ya Walawi 26:17 lenye kusema: ‘Hakika mimi nitauweka uso wangu juu yenu, nanyi hakika mutashindwa mbele ya adui zenu; nao wale wanaowachukia ninyi watawakanyangia chini, nanyi kwa kweli mutakimbia wakati ambapo hakuna mutu yeyote anayewafuatilia.’
w07 1/6 uku. 11 fu. 1
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Maombolezo
5:7—Je, Yehova anawaomba watu hesabu kwa sababu ya makosa ya mababu zao? Hapana, Yehova hapatie watu malipizi kwa sababu ya zambi za mababu zao. Biblia inasema: ‘Kila mumoja wetu atatoa hesabu kwa Mungu kwa ajili yake mwenyewe.’ (Waroma 14:12) Hata hivyo, matokeo ya makosa yanaweza kuendelea katika vizazi vya kufuata. Kwa mufano, wakati Waisraeli wa zamani walimuacha Yehova ili kuabudu sanamu, walifanya ikuwe vigumu hata kwa Waisraeli waaminifu wenye waliishi nyuma yao washikamane na njia ya haki.—Kutoka 20:5.
TAREHE 19-25/06
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | EZEKIELI 1-5
“Ezekieli Alifurahia Kutangaza Ujumbe wa Mungu”
w08 15/7 uku. 8 fu. 6-7
Namna ya Kushinda Magumu ya Mahubiri ya Nyumba kwa Nyumba
Kitabu cha Ezekieli kinafunua jambo lingine lenye linaweza kutusaidia kusema kwa ujasiri. Katika maono, Yehova alimupa Ezekieli kitabu cha kukunjwa chenye kimeandikwa pande zote mbili “nyimbo za huzuni na maombolezo na vilio” na Yehova akamuambia akikule, akasema: “Mwana wa binadamu, unapaswa kulisha tumbo lako, ili ujaze matumbo yako kwa kitabu hiki ninachokupa wewe.” Maono hayo yalifananisha nini? Ezekieli alipaswa kula kabisa ujumbe wenye angetangaza. Ni kama vile ujumbe huo ulipaswa kuwa sehemu yake, ni kusema, ulipaswa kumugusa moyo kabisa. Nabii huyo anaendelea kusema hivi: “Nami nikaanza kukila, nacho kikawa kitamu kama asali kinywani mwangu.” Ezekieli aliona kutangaza ujumbe wa Mungu mbele ya watu kuwa jambo la kufurahisha, kama kuonja asali. Aliona kama ni pendeleo la pekee kwake kutumwa na Yehova na kutimiza mugawo wenye Mungu alimupatia, hata kama alipaswa kuwatangazia watu ujumbe muzito wenye haukuwafuranisha.—Soma Ezekieli 2:8–3:4, 7-9.
Maono hayo yanafundisha watumishi wa Mungu wa leo somo la maana. Sisi pia tuko na ujumbe muzito wa kuwatangazia watu wenye wakati fulani hawafurahie kujikaza kwetu. Tunapaswa kujilisha muzuri kiroho ili tuendelee kuona huduma ya Kikristo kuwa pendeleo kutoka kwa Mungu. Hatuwezi kuelewa Neno la Mungu muzuri kabisa kama tunajifunza kijuujuu tu ao mara fulani tu. Je, unaweza kufanya maendeleo ili kusoma Biblia na kufanya funzo la pekee kwa ukawaida? Je, unaweza kuchukua wakati zaidi ili kufikiri juu ya mambo yenye unasoma?—Zab. 1:2, 3.
it-1 uku. 1203
Matumbo
Chakula kinaenda ndani ya matumbo ili kisagwe. Jambo hilo lilifananisha kusagwa kwa chakula cha kiroho katika maono ya Ezekieli wakati aliambiwa akule kitabu cha kukunjwa na kijae katika matumbo (Kiebrania, me·ʽimʹ) yake. Ezekieli alipaswa kupata nguvu ya kiroho kwa kufikiri sana juu ya mambo yenye kuandikwa katika kitabu hicho na kuweka mambo hayo katika akili yake. Katika njia hiyo alilishwa kiroho na alikuwa na ujumbe wa kutolea watu.—Eze 3:1-6; linganisha na Ufu 10:8-10.
w07 1/7 uku. 12 fu. 3
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Ezekieli—I
2:9–3:3—Sababu gani kitabu cha kukunjwa chenye nyimbo za huzuni na maombolezo kilikuwa kitamu kwa Ezekieli? Namna Ezekieli aliona kazi yake ndiyo ilifanya kitabu hicho cha kukunjwa kikuwe kitamu kwake. Ezekieli aliona kazi yake ya kuwa nabii Yehova kuwa pendeleo kubwa sana.
Chimba Ili Kupata Mali ya Kiroho
w07 1/7 uku. 11 fu. 6
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Ezekieli—I
1:4-28—Gari la mbinguni linafananisha nini? Gari hilo linafananisha sehemu ya mbinguni ya tengenezo la Yehova yenye kufanyizwa na viumbe waaminifu wa roho. Roho takatifu ya Yehova ndiyo inaongoza gari hilo. Mutembezaji wa gari hilo, mwenye kufananisha Yehova, ana utukufu mwingi sana. Upinde muzuri sana wa mvua unaonyesha utulivu wenye iko nao.
w07 1/7 uku. 12 fu. 4
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Ezekieli—I
4:1-17—Je, kweli Ezekieli alifanya kabisa mambo yenye kutajwa katika andiko hili ili kuonyesha kama kuzingirwa kwa Yerusalemu kulikuwa kumekaribia? Kwa sababu Ezekieli aliomumba Yehova abadilishe kile chombo angetumia ili kupika keki, na Yehova akakubali ombi lake, inaonekana kama kwa kweli nabii huyo alicheza kabisa-kabisa kuzungukwa kwa Yerusalemu. Alilalia upande wake wa kushoto kwa ajili ya kipindi cha miaka 390 cha makosa ya ufalme wa makabila kumi, ni kusema, kuanzia mwaka wa 997 M.K.Y. mupaka uharibifu wa Yerusalemu katika mwaka wa 607 M.K.Y. Alilalia upande wake wa kuume kwa ajili ya kipindi cha miaka 40 cha zambi za Yuda, chenye kilianza wakati Yeremia aliwekwa kuwa nabii katika mwaka wa 647 M.K.Y. mupaka mwaka wa 607 M.K.Y. Katika siku hizo zote 430, Ezekieli alikuwa na chakula na maji kidogo sana, ili kuonyesha kwa njia ya unabii kama kungekuwa njaa kali wakati Yerusalemu ingezungukwa.
TAREHE 26/06–2/07
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | EZEKIELI 6-10
“Utatiwa Alama ya Wokovu?”
Maulizo ya Wasomaji Wetu
Katika maono ya Ezekieli, mwanaume mwenye kuwa na kidau (chupa) cha wino na wanaume sita wenye kuwa na silaha za kuponda wanafananisha nani?
Wanafananisha majeshi ya mbinguni yenye yalitumikishwa ili kuharibu Yerusalemu na yenye yatatumikishwa ili kuharibu ulimwengu muovu wa Shetani kwenye vita ya Har-magedoni. Hayo ni mafasirio ya mupya. Sababu gani tulikuwa na lazima mafasirio hayo?
Mbele ya mwaka wa 607 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, Yehova alimuonyesha Ezekieli mambo yenye yangefanyika katika muji wa Yerusalemu mbele uharibiwe. Katika maono hayo, Ezekieli aliona mambo mengi ya mubaya yenye yalikuwa yanafanyika katika muji huo. Kisha aliona wanaume sita, kila mumoja wao alikuwa na ‘silaha yake ya kuponda mukononi mwake.’ Kulikuwa pia mwanaume fulani pamoja nao mwenye alikuwa ‘anavaa kitani’ na alikuwa na “kidau cha wino.”(Eze 8:6-12; 9:2, 3) Mwanaume huyo aliambiwa apite katikati ya muji ‘na kutia alama kwenye mapaji ya uso ya watu wanaougua na kulia kwa sababu ya machukizo yote yanayofanywa katikati yake.’ Kisha, wanaume sita wenye kuwa na silaha waliambiwa waue watu wote katika muji wenye hawakukuwa na alama hiyo. (Eze 9:4-7) Maono hayo yanaweza kutufundisha nini, na mwanaume mwenye kuwa na kidau cha wino ni nani?
Ezekieli alipata maono hayo katika mwaka wa 612 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu. Unabii huo ulitimizwa kwanza miaka tano kisha hapo, wakati Yehova aliacha jeshi la Babiloni liharibu Yerusalemu. Kwa kufanya hivyo, Yehova alitumikisha Wababiloni ili kupatia malipizi watu wake wenye walikosa utii. (Yer 25:9, 15-18) Lakini ni nini ilifikia Wayahudi waaminifu wenye walichukia mambo yote ya mubaya yenye yalikuwa yanafanyika katika muji huo? Yehova alikamata mipango ili waokolewe.
Katika maono hayo, Ezekieli hakutia mutu yeyote alama ya kwelikweli na hakuchangia katika uharibifu wa muji. Lakini, malaika ndio waliongoza uharibifu wa Yerusalemu. Kwa hiyo, unabii huo unatusaidia kuelewa mambo yenye kufanyika mbinguni. Yehova aliambia malaika zake wafanye mipango ya kuharibu watu waovu na kuhakikisha kama watu wenye haki waliokolewa.
Unabii huo utatimia pia wakati unaokuja. Zamani tulikuwa tunasema kama ule mutu mwenye kuwa na kidau cha wino anafananisha Wakristo watiwa-mafuta wenye wangali katika dunia. Pia, tulikuwa tunasema kama watu walikuwa wanatiwa alama ya wokovu wakati walikuwa wanasikiliza na kukubali habari njema yenye tunahubiri. Lakini, hivi karibuni ilionekana wazi kama ilikuwa lazima tubadilishe namna tunafasiria unabii huo. Tumejifunza katika andiko la Mathayo 25:31-33 kama Yesu ndiye anahukumu watu. Atafanya hivyo wakati unaokuja wakati wa ziki kubwa (taabu kubwa). Wakati huo, wale wenye watahukumiwa kuwa kondoo wataokolewa, na wale wenye watahukumiwa kuwa mbuzi wataharibiwa.
Kwa hiyo, maono ya Ezekieli yanatufundisha nini? Yanatufundisha mambo tano haya:
(1) Mbele ya uharibifu wa Yerusalemu, Ezekieli, Yeremia, na Isaya, walionya watu juu ya mambo yenye yangefanyika katika muji huo. Walikuwa kama vile walinzi. Leo, Yehova anatumikisha kikundi kidogo cha watiwa-mafuta ili kufundisha watu wake na kuonya wengine mbele ziki kubwa ianze. Kwa kweli, watu wote wa Mungu, ni kusema, watumishi wa nyumbani wa Kristo, wanafanya kazi hiyo ya kuonya.—Mt 24:45-47.
(2) Ezekieli hakutia alama wale wenye wangeokolewa. Vilevile watumishi wa Mungu hawafanye hivyo leo. Wanahubiria tu wengine habari njema na kuwaonya juu ya mambo yenye yatatokea wakati unaokuja. Kazi hiyo ya kuhubiri katika dunia yote inafanyika kwa musaada wa malaika.—Ufu 14:6.
(3) Wale wenye waliokolewa katika siku za Ezekieli, hawakukuwa na alama ya kwelikweli juu ya uso wao. Leo, wale wenye wataokolewa hawatakuwa na alama ya kwelikweli. Watu wanapaswa kufanya nini ili waokoke ziki kubwa? Wakati wanasikia onyo hilo, wanapaswa kujifunza kumuiga Yesu, kujitoa kwa Mungu, na kuunga mukono ndugu za Kristo kwa kuhubiri habari njema. (Mt 25: 35-40) Wakati wa ziki kubwa, watu hao watapata alama, ni kusema, watachaguliwa ili waokoke.
(4) Mwanaume mwenye kuwa na kidau cha wino anafananisha Yesu. Wakati wa ziki kubwa, Yesu atatia mukutano mukubwa wa watu alama wakati anawahukumu kuwa kondoo. Kisha wataishi milele hapa duniani.—Mt 25:34, 46.
(5) Leo, wale wanaume sita wenye kuwa na silaha za kuponda wanafananisha majeshi ya mbinguni yenye kuongozwa na Yesu. Wataharibu hivi karibuni mataifa na kumaliza uovu wote.—Eze 9:2, 6, 7; Ufu 19:11-21
Mambo yenye tunajifunza katika maono haya yanatusaidia tukuwe hakika kama Yehova hataharibu watu wenye haki pamoja na watu wabaya. (2 Pet 2:9; 3:9) Pia, yanatukumbusha kama kazi ya kuhubiri ni ya maana sana wakati wetu. Kila mutu anapaswa kusikia onyo mbele mwisho ufike!—Mt 24:14.
Chimba Ili Kupata Mali ya Kiroho
w09 15/9 uku. 23 fu. 10
Elimu ya Kutoka Kwa Mungu ni ya Maana Sana
Yehova peke yake ndiye anaweza kutusaidia tujitayarishe kwa ajili ya wakati wenye kuja kwa sababu anajua mambo yenye yatatokea wakati wenye kuja. Anajua namna maisha ya wanadamu yatakuwa wakati wenye kuja. (Isa. 46:9, 10) Unabii wa Biblia unasema kama “siku kuu ya Yehova iko karibu.” (Sef. 1:14) Kuhusu siku hiyo, maneno haya ya Methali 11:4 yatakuwa ya kweli kabisa: ‘Vitu vyenye samani havitakuwa na faida yoyote siku ya gazabu [hasira], lakini uadilifu utakomboa kutoka katika kifo.’ Wakati muda utafika ili Yehova ahukumu ulimwengu wa Shetani, jambo la maana zaidi litakuwa urafiki wetu pamoja na Mungu. Feza hazitakuwa na maana yoyote. Kwa kweli, andiko la Ezekieli 7:19 linasema hivi: ‘Katika barabara watatupa feza yao wenyewe, na zahabu yao wenyewe itakuwa chukizo.’ Kujua jambo hilo mbele ya wakati, kunaweza kutusaidia kutenda kwa hekima sasa.
Je, Unaruhusu Roho ya Mungu Ikuongoze?
Imani inamaanisha kwanza kumuona Yehova Mungu kuwa Mutu wa kweli kabisa. Ikiwa Mungu haiko mutu wa kweli kabisa kwetu, hilo linaweza kuongoza haraka kwenye mwenendo mubaya. Fikiria jambo lenye liliwapata watu wa Mungu wa zamani. Yehova alimuambia nabii Ezekieli kama mambo yenye kuchukiza yalikuwa yakifanywa wazi, alisema: “Je, umeona, Ee mwana wa binadamu, mambo ambayo wazee wa nyumba ya Israeli wanafanya katika giza, kila mumoja katika vyumba vya ndani vya sanamu yake ya kuchongwa? Kwa maana wanasema, ‘Yehova hatuoni. Yehova ameiacha Inchi hii.’” (Eze. 8:12) Umeona jambo lenye lilifanya tatizo hilo litokee? Hawakuamini kama Yehova alijua mambo yenye walikuwa wanafanya. Yehova hakuwa mutu wa kweli kabisa kwao.