Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha
TAREHE 1-7/01
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATHAYO 1-3
“Ufalme wa Mbinguni Umekaribia”
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 3:1, 2
Akihubiri: Neno la Kigiriki lenye lilitumiwa hapa linamaanisha “kutangaza ujumbe kwa watu wote.” Linakazia namna ya kutangaza: zaidi sana mazungumuzo na watu, kuliko kutolea hotuba kikundi cha watu.
Ufalme: Ni hapa neno la Kigiriki ba·si·leiʹa linaonekana kwa mara ya kwanza, neno lenye linamaanisha serikali ya mufalme, na pia eneo na raia wenye kutawaliwa na mufalme. Neno hilo linapatikana mara 162 katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo; tunaweza kulipata mara 55 katika Injili ya Mathayo na mara nyingi linamaanisha utawala wa Mungu wa mbinguni. Mathayo anatumia neno hilo mara nyingi sana; kwa hiyo, Injili yake inaweza kuitwa Injili ya Ufalme.
Ufalme wa mbinguni: Katika Injili ya Mathayo tu, maneno hayo yanapatikana mara 30 hivi. Lakini, katika Injili zao, Marko na Luka wanatumia maneno “Ufalme wa Mungu;” hilo linaonyesha kama “Ufalme wa Mungu” uko katika mbingu za kiroho na unatawala kutoka huko.—Mt 21:43; Mk 1:15; Lu 4:43; Dan 2:44; 2Tim 4:18.
umekaribia: Hapa ni kusema Mutawala wa ufalme wa mbinguni alikuwa karibu kutokea.
nwtsty picha na video
Nguo za Yohana Mubatizaji na Namna Alionekana
Yohana alikuwa anavaa nguo yenye kushonwa na manyoya ya ngamia yenye ilibanwa kwenye kiuno na mukaba wa ngozi, ao mukaba wenye ungesaidia kubeba vitu vidogo-vidogo. Nabii Elisha pia alivaa nguo kama hiyo. (2Fal 1:8) Nguo yenye kushonwa na manyoya ya ngamia ilikuwa nguvu-nguvu na mara nyingi ni masikini ndio waliivaa. Lakini, matajiri walivaa nguo laini (za teke-teke) za hariri (soie) ao za kitani (laine). (Mt 11:7-9) Kwa sababu Yohana alikuwa munaziri tangu kuzaliwa kwake, pengine nywele zake hazikukatwa. Pengine namna alivaa na namna alionekana ilionyesha wazi kama aliishi maisha mepesi, alijitoa kabisa kufanya mapenzi ya Mungu.
Nzige
Katika Biblia, neno “nzige” linaweza kumaanisha kila aina ya mapanzi wenye kuwa na antene za mufupi, zaidi sana mapanzi wenye wanahama-hama pamoja katika vikundi. Kulingana na uchunguzi wenye ulifanywa Yerusalemu, nzige wenye kuwa katika jangwa wako na 75 % ya proteine. Leo, mbele zikuliwe, zinaondolewa vichwa, miguu, mabawa na tumbo. Sehemu yenye kubakia, ni kusema kifua, kinakuliwa kibichi ao chenye kupigiwa. Watu wanasema kama vidudu hao wako na utamu moja na uduvi (crevette) ao kaa (crabe).
Asali ya Pori
Huu ni muzinga (ruche) wenye ulijengwa na nyuki wa pori (1) na sega lenye kujaa asali (2). Pengine asali yenye Yohana alikuwa anakula ilitengenezwa na aina ya nyuki wa pori wenye kuitwa Apis mellifera syriaca, wenye kupatikana katika eneo hilo. Nyuki hao wakali wanaishi muzuri katika maeneo ya joto na yenye haina mvua katika jangwa la Yuda, lakini mwanadamu hawezi kuwafuga. Kuanzia miaka ya 800 M.K.Y., watu wenye waliishi katika Israeli walifuga nyuki ndani ya machupa ya udongo. Sehemu kubwa ya machupa hayo ilivumbuliwa katikati ya eneo moja la zamani (lenye kuitwa leo Tel Rehov), lenye kupatikana katika Bonde la Yordani. Asali yenye ilivumbuliwa katika machupa hayo ilitengenezwa na aina fulani ya nyuki wenye pengine walitoka katika Turquie ya leo.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 1:3
Tamari: Mwanamuke wa kwanza kati ya wanamuke tano wenye Mathayo anataja katika kizazi cha Masiya. Wengine ine ni Rahabu na Ruthu, wote haiko wanamuke Waisraeli (mustari wa 5); Bath-sheba, “bibi wa Uriya” (mustari wa 6); na Maria (mustari wa 16). Mathayo anataja wanamuke hao katika kizazi cha Yesu, katikati ya wanaume, pengine kwa sababu ya jambo la maana sana lenye kila mumoja wao alifanya ili kufikia kuwa tate ao nkambo ya Yesu.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 3:11
ninawabatiza ninyi: Ao “ninawatumbukiza ndani ya maji.” Neno la Kigiriki ba·ptiʹzo linamaanisha “kuzamisha; kutumbukiza.” Vitabu vingine vyenye kufasiria Biblia vinasema kama ubatizo ni kuzamisha kabisa. Wakati fulani, Yohana alikuwa anabatiza watu mahali fulani katika Bonde la Yordani karibu na Salimu ‘kwa sababu kulikuwa kiasi kikubwa cha maji.’ (Yoh 3:23) Wakati Filipo alibatiza toashi Muetiopia, wote wawili walishuka na “kuingia ndani ya maji.” (Mdo 8:38) Tafsiri ya Septante inatumia neno hilo-hilo la Kigiriki katika 2Fal 5:14 wakati inazungumuzia namna Naamani ‘alijitumbukiza katika Yordani mara saba.’
TAREHE 8-14/01
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATHAYO 4-5
“Mambo Yenye Mahubiri ya Yesu ya Mulimani Inatufundisha”
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 5:3
Wenye furaha: Haiko tu hali ya kujisikia muzuri, kama vile wakati mutu anajifurahisha. Lakini, wakati neno hilo linatumiwa juu ya wanadamu, linamaanisha hali ya mutu mwenye Mungu amebariki mwenye anafurahi kwa sababu Mungu anamukubali. Neno hilo linatumiwa pia juu ya Mungu na Yesu katika utukufu wao huko mbinguni.—1Tim 1:11; 6:15.
wale wenye wanatambua uhitaji wao wa kiroho: Neno la Kigiriki lenye kutafsiriwa “wale wenye wanatambua,” neno kwa neno, “wale wenye kuwa masikini (wenye kukosewa kila kitu; masikini wenye kuomba-omba),” hapa linamaanisha watu wenye kuwa na uhitaji na wanatambua kabisa jambo hilo. Neno hilo linatumiwa pia katika Luka 16:20, 22 ili kumaanisha Lazaro, ‘masikini mwenye kuomba-omba’. Maneno ya Kigiriki yenye Biblia fulani zinatafsiri wale wenye kuwa “masikini wa roho” inaleta wazo la watu wenye wanakubali kwa shida kama wao ni masikini wa kiroho na wako na lazima ya Mungu.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 5:7
wenye rehema: Maneno ya Biblia yenye kutafsiriwa “wenye rehema” ao “rehema” haimaanishe tu kusamehe ao kuhurumia wakati wa hukumu kwenye tribinali. Mara nyingi inamaanisha hali ya kusikilia huruma yenye inachochea mutu kufanya jambo fulani ili kusaidia.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 5:9
wenye kufanya amani: Wenye hawaendeleze tu amani, lakini wanaleta pia amani mahali haiko.
w07 1/12 uku. 17
Umufundishe Mutoto Wako Akuwe Mwenye Kufanya Amani
Wazazi Wakristo wanajikaza kuwafundisha watoto wao namna ya ‘kutafuta amani na kuifuatilia.’ (1 Petro 3:11) Kwa sababu mutu mwenye kufanya amani anapata furaha nyingi, tunapaswa kufanya yetu yote ili kushinda hali ya kujisikia kuwa na mashaka, kuvunjika moyo, na chuki.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 4:9
kunifanyia tendo la ibada: Neno ao kitenzi cha Kigiriki chenye kinaweza kutafsiriwa “kuabudu” kinaonyesha hali ya aoristi, ni kusema, jambo lenye kutendeka kwa muda tu. Kwa sababu neno hilo linatafsiriwa “kunifanyia tendo la ibada,” hilo linamaanisha kama Shetani hakumuomba Yesu aendelee kumuabudu; alimuomba “tendo” moja tu “la ibada.”
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 4:23
akifundisha . . . kuhubiri: Kufundisha ni tofauti na kuhubiri, kwa sababu mwenye kufundisha hahubiri tu; anafasiria, anazoeza, anasadikisha, na kutoa ushuhuda.
TAREHE 15-21/01
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATHAYO 6-7
“Muendelee Kuutafuta Kwanza Ufalme”
Namna ya Kumukaribia Mungu Katika Sala
Katika sala zetu, mambo ya Yehova Mungu ndiyo inapaswa kutiwa pa nafasi ya kwanza. Tunapaswa kumusifu na kumushukuru kutoka moyoni kwa sababu ya wema wake wote. (1 Mambo ya Nyakati 29:10-13) Katika sala ya mufano, inayopatikana katika andiko la Mathayo 6:9-13, Yesu alitufundisha tusali jina la Mungu litakaswe, yaani, tulione kuwa kitu kitakatifu. (Soma.) Kisha alitufundisha tusali Ufalme wa Mungu ukuje na mapenzi yake yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni. Ni kisha kuzungumuzia mambo hayo ya lazima ya Yehova ndipo Yesu alitaja mambo ya kipekee ya mutu. Wakati sisi pia tunamutanguliza Mungu katika sala zetu, tunaonyesha kama hatuhangaikie tu mambo yetu wenyewe.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 6:24
kutumikia: Neno la Kigiriki linamaanisha kutumika kama mutumwa, ni kusema, kuwa mali ya bwana mumoja tu. Hapa Yesu alikuwa anamaanisha kama haiwezekane Mukristo ajitoe kabisa kwa Mungu na wakati uleule ajitoe kabisa ili kutafuta vitu vya kimwili.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 6:33
Muendelee . . . kuutafuta: Neno ao kitenzi cha Kigiriki kinaonyesha tendo lenye kuendelea na kinaweza kutafsiriwa “kuendelea kutafuta.” Wanafunzi wa kweli wa Yesu hawapaswe kutafuta Ufalme kwa muda tu na kisha wanaenda kutafuta vitu vingine. Lakini wanapaswa kutia Ufalme pa nafasi ya kwanza katika maisha yao.
Ufalme: Vitabu fulani vya Kigiriki vya zamani vinasema “Ufalme wa Mungu.”
yake: Ni kusema ya Mungu, “Baba yetu wa mbinguni” mwenye kutajwa katika Mt 6:32.
mambo yenye kuwa sawa: Wale wenye kutafuta mambo yenye kuwa sawa ao haki ya Mungu wako tayari kufanya mapenzi yake na wanafuata kanuni zake kuhusu m ya muzuri na mambo ya mubaya. Fundisho hilo lilikuwa tofauti kabisa na mafundisho ya Mafarisayo wenye walitafuta kuweka haki yao wenyewe.—Mt 5:20.
Tafuta Ufalme, Usitafute Vitu vya Kimwili
Soma Mathayo 6:33. Wanafunzi wa Yesu wanapaswa sikuzote kutia Ufalme pa nafasi ya kwanza katika maisha yao. Tukifanya hivyo, kama vile Yesu alisema, ‘tutaongezewa hivi vitu vingine vyote.’ Sababu gani tunaweza kusema vile? Yesu alieleza katika mustari wenye kutangulia: ‘Baba yenu wa mbinguni anajua munahitaji vitu hivi vyote,’ ni kusema, mambo yenye tuko nayo lazima ili kuishi. Yehova anaweza kujua mbele ya wakati vitu vyenye kila mumoja wetu iko navyo lazima, kama vile, chakula, manguo, na nafasi ya kuishi, hata mbele sisi wenyewe tukuwe navyo lazima. (Flp 4:19) Anajua manguo yenye tutakuwa nayo lazima. Anajua tutakuwa na lazima ya chakula gani. Na anajua kama wewe na watu wa familia yako muko na lazima ya nafasi ya kuishi. Yehova atahakikisha kama umepata mambo yenye uko nayo lazima kabisa.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
Namna ya Kuwatendea Wengine Katika Mahubiri
Tuseme kwamba mutu fulani mwenye hautambue sauti yake anakuita kwenye telefone. Haumujue, lakini anakuuliza ni chakula gani chenye unafurahia. Utajiuliza mutu huyo ni nani na anataka kabisa nini. Pengine kwa sababu ya adabu, unaweza kuongea naye kidogo, kisha unakata mazungumuzo. Kwa upande mwingine, wazia kama mutu mwenye anakuita anajieleza kwanza, kisha anasema kama yeye ana elimu ya mambo ya chakula, na anakuambia kwa upole kama ana habari fulani yenye inaweza kukusaidia. Pengine unaweza kuwa tayari kumusikiliza. Zaidi ya hilo, unafurahi wakati watu wanazungumuza na weye waziwazi na kwa heshima. Namna gani tunaweza kuonyesha heshima kama hiyo kwa wale tunahubiria?
Katika maeneo mengi, tunahitaji kumuelezea musikilizaji wetu sababu gani tunamutembelea. Ni kweli kwamba tunajua mambo mengi kuliko musikilizaji. Lakini, wazia kama tunafika kwa mutu na mbele hata ya kumuambia sisi ni nani na tunakuja kufanya nini, mara moja tunamuuliza hivi: “Ikiwa ungekuwa na uwezo wa kumaliza matatizo yote katika dunia, ungemaliza tatizo gani kwanza?” Tunajua kama kusudi la ulizo hilo ni kutaka kujua mawazo ya mutu na kisha kumuonyesha mambo yenye Biblia inasema. Lakini musikilizaji wetu, anaweza kujiuliza katika moyo wake hivi: ‘Mutu huyu anatoka wapi, na sababu gani ananiuliza ulizo hili? Sababu gani ananisumbua hivi?’ Kwa hiyo, tunapaswa kujaribu kumufanya musikilizaji wetu asikuwe na mashaka juu yetu. (Flp 2:3, 4) Namna gani tunaweza kufanya hivyo?
Mwangalizi moja mwenye kusafiri ameona ufundi huu kuwa wenye matokeo mazuri. Kisha kumusalimia musikilizaji, anamutolea trakte yenye kichwa; Je, Ungependa Kujua Kweli? na anasema hivi: “Leo, tunawatolea watu trakte hii katika eneo hili. Inazungumuzia maulizo sita yenye watu wengi wanajiuliza. Yako hii.” Ndugu huyo anasema kama watu wengi wanaonekana kuwa wenye kutulia wakati tunawaelezea sababu gani tunawatembelea. Mara nyingi, kisha kufanya hivyo inakuwa rahisi kuanzisha mazungumuzo. Kisha mwangalizi anamuuliza hivi mutu huyo: “Umekwisha kujiuliza ulizo gani kati ya maulizo haya?” Ikiwa musikilizaji anachagua ulizo moja, ndugu anafungua trakte hiyo na anaanza kumuonyesha mawazo ya Biblia kuhusu ulizo hilo. Ao, ndugu anachagua ulizo moja na kuanza kuzungumuza na musikilizaji wake bila kumuuliza-uliza maulizo. Njia hizo mbili ni kati ya njia nyingi zenye tunatumia ili kuanzisha mazungumuzo. Katika maeneo fulani, tunapaswa kufuata desturi fulani wakati tunasalimia watu mbele ya kuwaambia sababu gani tunawatembelea. Jambo la maana ni kuanzisha mazungumuzo kulingana na namna watu wa eneo letu wanataka.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 7:28, 29
wakashangazwa: Neno la kigiriki lenye lilitumiwa hapa linaweza kumaanisha “kushangaa sana mupaka mutu anakosa la kusema.” Neno ao kitenzi hicho kiko katika hali ya kuendelea, hilo linaonyesha kama maneno ya Yesu ilikuwa na matokeo yenye kuendelea juu ya watu.
namna yake ya kufundisha: Maneno haya yanahusu namna Yesu alikuwa anafundisha, ufundi wake wa kufundisha, ni kusema, mambo yote yenye alifundisha katika Mahubiri yake ya Mulimani.
hapana kama waandishi wao: Kuliko kuiga waandishi kwa kutaja maneno ya marabi wenye kujulikana sana, Yesu alikuwa musemaji wa Yehova, alifundisha kama mutu mwenye mamlaka. Mafundisho yake ilitegemea Neno la Mungu.—Yoh 7:16.
TAREHE 22-28/01
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATHAYO 8-9
“Yesu Alipenda Watu”
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 8:3
akamugusa: Sheria ya Musa iliomba watu wenye ukoma watenganishwe na wengine ili wasiwaambukize. (Law 13:45, 46; Hes 5:1-4) Lakini, viongozi wa dini ya Kiyahudi waliongezea watu sheria nyingi. Kwa mufano, hakuna mutu aliruhusiwa kukaribia sana mutu mwenye ukoma, ni kusema, kumukaribia metre 1.80 hivi, lakini wakati wa upepo watu walipaswa kusimama mbali sana na mutu mwenye ukoma, ni kusema, kwenye metre 45 hivi. Sheria kama hizo zilifanya watu wenye ukoma watendewe bila huruma. Sheria zao zilisifu rabi moja mwenye alifichama watu wenye ukoma na mwengine mwenye aliwatupia majiwe ili wasimukaribie. Lakini, Yesu aliguswa moyo sana wakati mutu mwenye ukoma alimuomba amuponyeshe, na hilo lilimuchochea afikie hata kugusa mwanaume huyo mwenye ukoma, jambo lenye Wayahudi wengine hawangefanya hata kidogo. Alikuwa na uwezo wa kuponyesha mwanaume huyo kwa kumuambia tu neno moja; lakini alimugusa.—Mt 8:5-12.
Ninataka: Yesu hakukubali tu ombi la mwanaume huyo, lakini alionyesha kama alipenda kabisa kumusaidia; hakufanya hivyo kwa sababu tu alilazimishwa.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 9:10
anakula chakula: Ao “kukaa kwenye meza.” Kukaa pamoja kwenye meza kulionyesha kama watu walikuwa marafiki sana. Ndiyo maana Wayahudi wa wakati wa Yesu hawangeweza hata kidogo kukaa kwenye meza, ao kula chakula, na watu wenye hawakuwa Wayahudi.
wakusanya-kodi: Wayahudi wengi walikusanya kodi kwa ajili ya wenye mamlaka Waroma. Watu walichukia Wayahudi hao kwa sababu walitumika pamoja na mamlaka ya inchi ingine, lakini pia waliomba kodi nyingi kuliko kawaida. Kwa kawaida wakusanya-kodi walichukiwa na Wayahudi wenzao, wenye waliwaona sawa-sawa na watenda-zambi na makahaba.—Mt 11:19; 21:32.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 9:36
akawasikilia huruma: Neno ao kitenzi cha Kigiriki splag·khniʹzo·mai chenye kilitumiwa kinalingana na neno “matumbo” (splagʹkhna), lenye kuonyesha namna mutu anajisikia ndani sana ya mwili, hisia kubwa sana. Ni moja kati ya maneno yenye nguvu sana ya Kigiriki yenye kuonyesha namna mutu anajisikia kabisa wakati anajitia pa nafasi ya wengine.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
w02 15/8 uku. 13 fu. 16
Niliwaachia Mufano
Vilevile, wakati mukubwa moja wa jeshi, pengine Muroma ao mutu mwenye haiko Muyahudi, alimukaribia Yesu na kumuomba aponyeshe mutumwa wake mugonjwa, Yesu alijua kama askari huyo alikuwa na uzaifu mbalimbali. Wakati huo, pengine mukubwa wa jeshi kama huyo angekuwa ametenda mambo ya mubaya sana, kuua watu, na kuunga mukono ibada ya uongo. Lakini, Yesu alikazia jambo lingine la muzuri, imani yake kubwa. (Mathayo 8:5-13) Kisha, wakati Yesu alizungumuza na mutenda-maovu mwenye alikuwa pembeni yake kwenye muti wa mateso, hakumulaumu kwa sababu ya matendo yake ya zamani, lakini alimutia moyo kwa kumupatia tumaini kwa ajili ya wakati wenye kuja. (Luka 23:43) Yesu alijua kama kuwa na maoni yenye haifae na kuwalaumu wengine kungewavunja moyo kabisa. Ni wazi kama alijikaza kutafuta sifa za muzuri za wengine; hilo liliwachochea watu wengi wafanye maendeleo.
Sababu Gani Wanafunzi wa Yesu Hawafunge?
Yesu anasaidia wanafunzi wa Yohana Mubatizaji waelewe kwamba hawapaswe kutazamia kama wafuasi wa Yesu watafuata tabia za zamani za dini ya Kiyahudi, kama vile desturi ya kufunga. Hakuja kutia viraka na kuendeleza aina fulani ya ibada yenye kuzeeka, yenye ilikuwa karibu kuachwa. Ibada yenye Yesu anatia watu moyo kufuata haitegemee dini ya Kiyahudi na desturi zake za wanadamu. Wala, haiko anajaribu kutia kipande cha nguo mupya juu ya nguo yenye kuzeeka ao kutia divai ya mupya ndani ya chupa ya ngozi yenye kuzeeka.
TAREHE 29/01–4/02
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATHAYO 10-11
“Yesu Alitolea Watu Kitulizo”
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 10:29, 30
ndege shomoro: Neno la Kigiriki strou·thiʹon linamaanisha ndege wote wadogo-wadogo, lakini linatumiwa sana ili kutaja shomoro, ndege wa bei chini zaidi kati ya wote wenye wanauzishwa ili kuliwa.
kwa feza moja ya kichele ya samani kidogo: Neno kwa neno “kwa sarafu moja ya asarioni (assarion),” ilikuwa mushahara wenye mutu angepokea kisha kutumika dakika 45. (Angalia Nyongeza B14.) Hapa, wakati alitembelea Galilaya mara ya tatu, Yesu alisema kama shomoro wawili walikuwa na bei ya sarafu moja ya asarioni. Wakati mwingine, pengine mwaka moja hivi kisha kazi yake ya kuhubiri katika Yudea, Yesu anasema kama mutu angenunua shomoro watano kwa sarafu mbili za asarioni. (Lu 12:6) Hesabu hizo zinatusaidia kuelewa kama wafanyabiashara waliona kuwa shomoro hawakuwa na maana yoyote; kwa hiyo, wakati mutu alinunua shomoro waine, aliongezewa matabishi ya shomoro moja.
hata nywele zote za vichwa vyenu zimehesabiwa: Inakadiriwa kama mutu ana nywele zaidi ya 100 000. Kujua hata mambo madogo-madogo juu yetu kunaonyesha kama Yehova anapendezwa sana na kila mwanafunzi wa Kristo.
nwtsty picha na video
Ndege shomoro
Ndege shomoro walikuwa wa bei chini zaidi kati ya wote wenye waliuzishwa ili kuliwa. Shomoro wawili wangeuzwa kwa mushahara wenye mutu angepokea kisha kutumika dakika 45. Neno la Kigiriki linamaanisha ndege wote wadogo-wadogo, na pia shomoro wa nyumbani (Passer domesticus biblicus) na shomoro wa inchi ya Espagne (Passer hispaniolensis), wenye kupatikana wengi sana huko Israeli.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 11:28
wenye kubeba mizigo mizito: Wale wenye Yesu alialika wamufuate walikuwa ‘wamelemewa na mizigo’ kwa sababu ya mahangaiko ya maisha. Ibada yao kwa Yehova ilikuwa imekuwa muzigo kwa sababu ya sheria za wanadamu zenye ziliongezwa juu ya Sheria ya Musa. (Mt 23:4) Hata siku ya Sabato, yenye watu walipaswa kupumuzika, ilikuwa muzigo wenye kulemea.—Kut 23:12; Mk 2:23-28; Lu 6:1-11.
nitawapumuzisha: Neno la Kigiriki lenye kutafsiriwa “kupumuzisha” linaweza kumaanisha kupata kitulizo (Mt 26:45; Mk 6:31) na kupumuzika ili kupata tena nguvu kisha kufanya kazi ngumu (2Kor 7:13; Flm 7). Hapa, kubeba “nira” ya Yesu (Mt 11:29) kunamaanisha kutumika, hapana kupumuzika. Neno ao kitenzi hicho cha Kigiriki kinaleta wazo la kutuliza na kupatia nguvu watu wenye kuchoka ili wafurahie kubeba muzigo wa Yesu wenye kuwa laini na mwepesi.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 11:29
Mubebe nira yangu: Yesu alitumia neno “nira” kwa njia ya mufano ili kumaanisha kujitiisha kwa mamlaka na kufuata muongozo. Kama alikuwa anafikiria nira mbili, yenye Mungu alimubebesha, kwa hiyo, alipenda kualika wanafunzi wake wabebe nira pamoja naye na kama angewasaidia kuibeba. Katika hali hiyo, maneno hayo ingetafsiriwa hivi: “Mubebe nira pamoja na mimi.” Kama nira hiyo ni ile yenye Yesu mwenyewe anabebesha wanafunzi wake, kwa hiyo, wanapaswa kujitiisha kwa mamlaka yake na muongozo wake.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
Yohana Anapenda Kupata Habari juu ya Yesu
Je, hilo linaonekana kuwa ulizo lenye kushangaza? Yohana ni mwanaume mwaminifu mwenye, wakati alibatiza Yesu kumepita karibu miaka mbili, aliona roho ya Mungu inashuka juu ya Yesu na alisikia sauti ya Mungu yenye kutangaza kuwa amemukubali Yesu. Hatuna sababu za kufikiri kuwa imani ya Yohana imekuwa zaifu. Kama ilikuwa hivyo, Yesu hangemusifu Yohana, kama vile anamusifu wakati huu. Lakini ikiwa Yohana angali na imani, sababu gani anauliza ulizo hilo juu ya Yesu?
Pengine Yohana anapenda tu Yesu mwenyewe amuhakikishie kuwa yeye ndiye Masiya. Hilo lingemutia Yohana nguvu wakati anaendelea kuteseka katika gereza. Na ulizo la Yohana linaonekana kuwa na maana ingine. Anajua muzuri unabii mbalimbali wa Biblia wenye kuonyesha kuwa Mutiwa-Mafuta wa Mungu anapaswa kuwa mufalme na mukombozi. Lakini, Yohana iko katika gereza kumepita miezi mingi kisha yeye kumubatiza Yesu. Kwa hiyo, Yohana iko anauliza ikiwa kuko mwingine mwenye iko nakuja, mwenye atachukua nafasi ya Yesu na kutimiza mambo yote yenye yalitabiriwa kuwa Masiya atatimiza.
Ole kwa Kizazi Chenye Kukataa Kusikiliza
Yesu anamuona Yohana Mubatizaji kuwa mutu wa maana sana, lakini watu wengi wanamuona Yohana namna gani? Yesu anasema hivi: “Kizazi hiki ni kama watoto wadogo wenye kukaa katika masoko na kuita wachezaji wenzao wakisema: ‘Tuliwapigia filimbi, lakini hamukucheza; tuliomboleza, lakini hamukujipiga-piga kwa huzuni.’”—Mathayo 11:16, 17.
Yesu anapenda kusema nini? Anafasiria wazi-wazi maneno yake. Anasema hivi: “Wakati Yohana alikuja hakukuwa anakula na hakukuwa anakunywa, lakini watu wanasema, ‘Iko na pepo muchafu.’ Wakati Mwana wa binadamu alikuja alikuwa anakula na kunywa, lakini watu wanasema, ‘Angalia, mutu mulafi na mwenye anazoea kunywa divai, rafiki ya wakusanya-kodi na watenda-zambi.’” (Mathayo 11:18, 19) Kwa upande moja, Yohana aliishi maisha mepesi kama Munaziri, hata kama hakukuwa anakunywa divai, lakini kizazi hiki kinasema kuwa iko na pepo muchafu. (Hesabu 6:2, 3; Luka 1:15) Kwa upande mwingine, Yesu anaishi kama watu wengine. Anakula na kunywa kwa usawaziko, lakini anashitakiwa kuwa ni mulafi na mwenye anazoea kunywa divai. Inaonekana kuwa haiwezekane kufurahisha watu hao.