Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • jy sura 15 uku. 40-uku. 41 fu. 6
  • Anafanya Muujiza Wake wa Kwanza

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Anafanya Muujiza Wake wa Kwanza
  • Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Muujiza wa Pili Katika Kana
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Miujiza ya Yesu Inaweza Kutufundisha Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
  • Yesu Anaonyesha Bidii kwa Ajili ya Ibada ya Kweli
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
jy sura 15 uku. 40-uku. 41 fu. 6
Kwenye karamu ya ndoa katika Kana, Yesu anaambia wale wenye kufanya kazi wajaze mitungi maji

SURA YA 15

Anafanya Muujiza Wake Wa Kwanza

YOHANA 2:1-12

  • KARAMU YA NDOA KATIKA KANA

  • YESU ANAGEUZA MAJI KUWA DIVAI

Ni siku ya tatu tangu Natanaeli akuwe mumoja kati ya wanafunzi wa kwanza-kwanza wa Yesu. Yesu pamoja na pengine wanafunzi fulani kati ya wanafunzi wake wa kwanza wanaenda kaskazini katika wilaya ya Galilaya, eneo la kwao. Wanaenda Kana, muji kwenye Natanaeli alitoka. Kana inapatikana katika vilima kaskazini mwa Nazareti, nafasi kwenye Yesu alikomalia. Wamealikwa kwenye karamu ya ndoa katika Kana.

Mama ya Yesu amekuja pia kwenye karamu hiyo. Kwa kuwa Maria ni rafiki wa familia ya wale wenye kufunga ndoa, inaonekana iko anasaidia katika kazi ya kuhangaikia wageni wengi. Kwa hiyo, bila kukawia, anatambua kuwa wanakosa kitu fulani, na anamuelezea Yesu jambo hilo: “Hawana divai.”—Yohana 2:3.

Kwa kweli, Maria anaomba Yesu afanye jambo fulani kuhusu ukosefu huo wa divai. Kwa kutumia maneno ya mufano, Yesu anajibu hivi: “Mwanamuke, je, jambo hilo linatuangalia mimi na wewe?” (Yohana 2:4) Kwa kuwa yeye ni Mufalme mwenye amechaguliwa na Mungu, Yesu anapaswa kufanya kazi zake kwa kuongozwa na Baba yake wa mbinguni, hapana na familia ao marafiki. Kwa hekima, Maria anaacha mambo katika mikono ya mutoto wake, kwa kuambia tu wale wenye walikuwa wanafanya kazi: “Mufanye jambo lolote lenye atawaambia.”—Yohana 2:5.

Hapo kunapatikana mitungi sita ya maji yenye kutengenezwa kwa majiwe, na kila mutungi unaweza kuchukua zaidi ya litre 40 ya maji. Yesu anawaambia wale wenye kufanya kazi: “Mujaze mitungi hiyo maji.” Kisha anasema: “Sasa mushote kidogo na mupelekee musimamizi wa karamu.”—Yohana 2:7, 8.

Musimamizi wa karamu ya ndoa anamupongeza bwana-arusi juu ya divai ya muzuri sana

Musimamizi wa karamu anashangaa kuona divai ya muzuri, lakini hajue kama imetengenezwa kwa njia ya muujiza. Kwa hiyo anamuita bwana-arusi na kumuambia hivi: “Watu wengine wanatoa divai ya muzuri kwanza, kisha wanatoa divai yenye haina nguvu wakati watu wamelewa. Wewe umeweka divai ya muzuri mupaka sasa.”—Yohana 2:10.

Huu ndio muujiza wa kwanza wenye Yesu anafanya. Wakati wanafunzi wake wa kwanza wanaona muujiza huo, imani yao katika Yesu inatiwa nguvu. Kisha hapo, Yesu, mama yake, na ndugu-nusu zake wanasafiri kuenda muji wa Kapernaumu upande wa kaskazini-mangaribi pembeni ya Bahari ya Galilaya.

  • Karamu ya ndoa katika Kana ilifanyika wakati gani katika utumishi wa Yesu?

  • Namna gani Yesu anamujibu mama yake wakati anamuambia kama hakuna divai?

  • Yesu anafanya muujiza gani, na hilo linakuwa na matokeo gani juu ya wengine?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine