Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha
TAREHE 3-9/12
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATENDO 9-11
Kutaniko “Likaingia Katika Kipindi cha Amani”
WATU wenye kusafiri wanakaribia Damasko, kwenye wanapanga kutimiza mawazo yao ya mubaya. Ni wenye kukasirika sana. Wanachukia wanafunzi wa Yesu. Watawatosha kwa nguvu mu nyumba zao, watawafunga, watawapatisha haya, na kuwapeleka Yerusalemu mbele ya Sanhedrini.
2 Tayari kiongozi wa kile kikundi, Sauli, iko na hatia ya damu ya mumoja wa wale wanafunzi. Siku fulani tu zenye zimepita, wakati wenzake walikuwa wanapiga Stefano majiwe, mwanafunzi wa Yesu mwenye bidii, juu wamuue, Sauli alikuwa anaangalia na kukubaliana nao. (Mdo. 7:57–8:1) Sauli hajatosheka kutesa wafuasi wa Yesu wenye wanaishi Yerusalemu, na anaendelea kuchochea mateso. Anataka kumaliza kabisa ile zehebu yenye kuitwa “Ile Njia.”—Mdo. 9:1, 2; ona sanduku yenye kichwa “Mamlaka ya Sauli Jijini Damasko,” kwenye ukurasa wa 61.
Tupendezwe na Yehova Mufinyanzi Wetu
4 Yehova haone watu namna tunawaona. Lakini, anachunguza moyo na anaona kabisa kila mumoja wetu vile iko ndani. (Soma 1 Samweli 16:7b.) Yehova alionyesha ile jambo wakati alianzisha kutaniko la Kikristo. Alivuta kwake na kwa Mwana wake watu mingi wenye watu fulani wangeweza kuona kuwa hawako wa maana. (Yoh. 6:44) Kwa mufano, mutu mumoja kati ya wale watu alikuwa Mufarisayo mwenye kuitwa Sauli, “mutu mwenye kumutukana Mungu na mutesaji na mutu mwenye zarau.” (1 Ti. 1:13) Lakini Yehova alichunguza moyo wake na hakumuona kuwa udongo wenye hauna maana. (Mez. 17:3) Aliona kama Sauli angeweza kufinyangwa na kuwa ‘chombo chenye alichagua’; angeweza kuhubiri “kwa mataifa na vilevile kwa wafalme na kwa wana wa Israeli.” (Mdo. 9:15) Pia, Yehova alichagua kufinyanga wengine “kwa matumizi yenye kuheshimika.” Kati yao kulikuwa watu wenye zamani walikuwa walevi, waasherati, na watu wenye walikuwa wanaiba. (Ro. 9:21; 1 Ko. 6:9-11) Kujifunza maandiko kuliwasaidia wafanye imani yao kwa Yehova ikuwe nguvu na waliacha Yehova awafinyange.
Kutaniko “Likaingia Katika Kipindi cha Amani”
15 Wazia namna watu walishangaa, wengine waliumia mu moyo na kukasirika wakati Sauli alianza kuhubiri Yesu mu masinagogi! Waliuliza: “Je, huyu haiko ule mutu mwenye alishambulia wale wenye wanaitia jina hilo kule Yerusalemu?” (Mdo. 9:21) Wakati alikuwa anaeleza sababu yenye ilifanya abadilike, Sauli “alihakikisha kupatana na akili kwamba huyu ndiye Kristo.” (Mdo. 9:22) Lakini, haiko watu wote njo wanaweza kusadikishwa vile. Kwa mufano, kila mutu mwenye anashikilia mapokeo ao mwenye kiburi hawezi kusadikishwa kupatana na akili. Lakini Sauli hakuacha.
bt uku 60-61 fu. 5-6
Kutaniko “Likaingia Katika Kipindi cha Amani”
5 Wakati Yesu alimusimamisha Sauli mu njia ya kuendea Damasko, hakumuuliza: “Sababu gani unatesa wanafunzi wangu?” Lakini, alimuuliza: “Sababu gani unanitesa?” (Mdo. 9:4) Ni kusema, Yehova anaona kama majaribu yenye inapata wafuasi wake, ni kama vile inamupata yeye mwenyewe.—Mt. 25:34-40, 45.
6 Kama wanakutesa kwa sababu ya kumuamini Kristo, ujue kama Yehova na Yesu wanaelewa hali yako. (Mt. 10:22, 28-31) Pengine ile jaribu haitaondolewa sasa. Kumbuka, wakati walikuwa wanaua Stefano, na tena wakati walikuwa wanatosha wanafunzi waaminifu kwa nguvu mu nyumba zao kule Yerusalemu, Yesu alikuwa anatazama Sauli na kuona yote yenye alikuwa anafanya. (Mdo. 8:3) Lakini, Yesu hakumaliza ile jaribu. Lakini, Yehova, kupitia Kristo, alipatia Stefano na wanafunzi wengine nguvu yenye walikuwa nayo lazima ili wabakie waaminifu.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mdo 10:6
Simoni, mutengenezaji wa ngozi: Mutengenezaji wa ngozi alitumika na ngozi za wanyama. Alitumia maji ya chokaa juu atoshe manyoya yote ao nyama yoyote na mafuta kwenye ngozi. Kisha alitengeneza ile ngozi ya nyama na maji-maji fulani ya kuregeza ngozi ili kutengeneza vitu vya ngozi. Ile kazi ilikuwa inatoa harufu ya mubaya na iliomba kutumia maji mingi, ni ile ilifanya Simoni aishi karibu na bahari, pengine pembeni ya Yopa. Kulingana na Sheria ya Musa, mutu mwenye alitumika na wanyama wenye kufa alionekana kuwa asiye safi. (Law 5:2; 11:39) Kwa hiyo, Wayahudi mingi walizarau watengenezaji wa ngozi na walisita kukaa nao mu nyumba moja. Tena, Talmudi ilifikia kusema kama kazi ya mutu mwenye kutengeneza ngozi ni ya hali ya chini sana kuliko hata kazi ya mutu mwenye kulokota mavi. Lakini, Petro hakuacha ubaguzi imufanye akatae kuishi mu nyumba moja na Simoni. Pengine hii namna ya kuona mambo ya Petro ilimutayarisha kwa ajili ya mugawo wenye angepata, mugawo wa kutembelea mutu mwenye hakukuwa Muyahudi. Watu fulani wenye elimu ya Biblia wanasema kama neno ya Kigiriki byr·seusʹ yenye kutafsiriwa “mutengenezaji wa ngozi” ilikuwa jina yenye walimupanga Simoni.
TAREHE 10-16/12
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATENDO 12-14
“Kujaa na Furaha na Roho Takatifu”
4 Lakini, sababu gani roho takatifu ilisema waweke pembeni Barnaba na Sauli ‘kwa ajili ya kazi’? (Mdo. 13:2) Biblia haiseme. Lakini, tunajua kama roho takatifu iliongoza mambo ili wale wanaume wachaguliwe. Hakuna kwenye tunasoma kama manabii na walimu kule Antiokia walipinga ile uamuzi. Lakini, waliunga mukono kabisa ile uamuzi. Wazia vile Barnaba na Sauli walijisikia wakati, bila wivu yoyote, ndugu zao wa kiroho ‘walifunga na kusali na kuweka mikono yao juu yao, na kuwaacha waende zao.’ (Mdo. 13:3) Na sisi, tunapaswa kuunga mukono wale wenye wanapata mapendeleo ya kiteokrasi, kutia ndani wanaume wenye wanawekwa kuwa waangalizi mu kutaniko. Kuliko kuwasikilia wivu, tunapaswa ‘kuwafikiria sana katika upendo kwa sababu ya kazi yao.’—1 Te. 5:13.
‘Walisema bila woga kwa mamlaka ya Yehova’
5 Ku mwanzo, Paulo na Barnaba walisimama Ikoniamu, muji wenye kujaa desturi za Kigiriki, moja kati ya miji ya Galatia, katika Roma. Ile muji ilikuwa na Wayahudi wenye kujulikana sana na wageuzwa-imani mingi wenye hawakukuwa Wayahudi. Kulingana na desturi yao, Paulo na Barnaba waliingia ndani ya sinagogi na kuanza kuhubiri. (Mdo. 13:5, 14) Walisema “muzuri sana mupaka watu wengi, Wayahudi na pia Wagiriki wakakuwa waamini.”—Mdo. 14:1.
Tumutumikie Mungu kwa Uaminifu Hata Kama Kuko “Taabu Nyingi”
4 Kisha kutembelea muji wa Derbe, Paulo na Barnaba “wakarudia Listra, Ikoniamu, na Antiokia. Kule wakatia wanafunzi nguvu, kwa kuwatia moyo wabakie katika imani na kusema: ‘Lazima tuingie katika Ufalme wa Mungu kupitia taabu nyingi.’” (Mdo. 14:21, 22) Ile maneno inaweza kushangaza sana. Kwa kweli, wakati Paulo alisema kama watu watapata “taabu nyingi,” ile ingeweza kuogopesha watu kuliko kuwatia moyo. Namna gani basi Paulo na Barnaba ‘waliwatia moyo’ wanafunzi kupitia ile ujumbe yenye ilionyesha kama wangepata mateso mingi?
5 Tunaweza kupata jibu kwa kuchunguza maneno ya Paulo kwa uangalifu. Hakusema tu: ‘Lazima tuvumilie taabu nyingi.’ Lakini alisema: “Lazima tuingie katika Ufalme wa Mungu kupitia taabu nyingi.” Kwa hiyo, Paulo alitia wanafunzi moyo kwa kukazia faida ya kubakia waaminifu. Zawadi yenye wangepata haikukuwa tu ndoto. Lakini, Yesu alisema kama ‘ule atavumilia mupaka mwisho ataokolewa.’—Mt. 10:22.
w08 15/5 uku. 32 fu. 7
Mambo Makubwa ya Kitabu cha Matendo
12:21-23; 14:14-18. Herode aliitika utukufu wenye Mungu tu njo alistahili. Alikuwa tofauti kabisa na Paulo na Barnaba wenye bila kukawia walikatala sifa ao heshima yenye hawakustahili! Hatupaswe kutamani kupata utukufu kwa sababu ya mambo yenye tunatimiza mu utumishi wa Yehova.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mdo 13:9
Sauli, mwenye kuitwa pia Paulo: Kuanzia ku hii andiko, Sauli anaitwa Paulo. Paulo alizaliwa Mwebrania, mwanainchi wa Roma. (Mdo 22:27, 28; Flp 3:5) Kwa hiyo, pengine kuanzia utoto alikuwa na jina ya Kiebrania Sauli na jina ya Kiroma Paulo. Haikukuwa jambo ya kushangaza kuona Wayahudi wa ile wakati wenye waliishi inje ya Israeli, kukuwa na majina mbili. (Mdo 12:12; 13:1) Watu fulani wa jamaa ya Paulo walikuwa pia na majina ya Kiroma ao ya Kigiriki zaidi ya majina yao ya Kiebrania. (Ro 16:7, 21) Kwa sababu Paulo alikuwa “mutume kwa mataifa,” alipewa kazi ya kutangazia wenye hawakukuwa Wayahudi habari njema. (Ro 11:13) Inaonekana aliamua kutumia jina yake ya Kiroma; pengine aliona kama kufanya vile ingesaidia wamukubali zaidi. (Mdo 9:15; Ga 2:7, 8) Watu fulani wanasema kama alikamata jina ya Kiroma kwa heshima ya Sergio Paulo. Lakini inaonekana kama haiko vile, kwa sababu Paulo aliendelea kuwa na ile jina hata kisha kutoka Kipro. Wengine wanasema kama Paulo hakupenda kutumia jina yake ya Kiebrania kwa sababu namna wanaitamka mu Kigiriki inafanana sana na neno ingine ya Kigiriki yenye kuwa na maana ya mutu (ao munyama) mwenye anatembea kwa majivuno.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mdo 7:58
Sauli: Maana yake “Iliombwa [kwa Mungu]; Kuulizwa [Mungu].” Sauli, mwenye alijulikana pia kwa jina yake ya Kiroma Paulo, alikuwa, “wa kabila la Benyamini, Mwebrania mwenye alizaliwa na Waebrania.” (Flp 3:5) Kwa kuwa Sauli alizaliwa mwanainchi wa Roma (Mdo 22:28), inapatana na akili kusema kama wazazi wake Wayahudi pengine walimupatia jina ya Kiroma Paulus, ao Paulo, jina yenye kumaanisha “Kidogo; Mudogo.” Tangu utoto, pengine alikuwa na ile majina yote. Pengine wazazi wake walimupatia jina ya Sauli kwa sababu mbalimbali. Sauli ilikuwa jina ya maana sana kwa watu wa kabila la Benyamini kwa sababu mufalme wa kwanza mwenye alitawala Israeli alikuwa Mubenyamini na jina yake ilikuwa Sauli. (1Sa 9:2; 10:1; Mdo 13:21) Ao pengine wazazi wake walimupatia ile jina kwa sababu ya jambo yenye ilimaanisha. Tena pengine walimupatia ile jina kwa sababu jina ya baba yake ilikuwa pia Sauli, na kulingana na desturi yao, mutoto alibeba jina ya baba yake. (Linganisha na Lu 1:59.) Hata sababu ikuwe nini, wakati alipatikana na Wayahudi wenzake alipaswa kutumia jina yake ya Kiebrania, ni kusema, Sauli; zaidi sana kwa sababu alikuwa anasoma ili akuwe Mufarisayo na kuishi kama Mufarisayo. (Mdo 22:3) Na miaka mingi kisha kuwa Mukristo, inaonekana kama watu walimujua sana mu jina yake ya Kiebrania.—Mdo 11:25, 30; 12:25; 13:1, 2, 9.
Paulo: Mu Tafsiri ya Swahili-Congo ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, jina Pauʹlos, yenye inatoka mu Kilatini Paulus, yenye kumaanisha “Kidogo; Mudogo” inatumiwa mara 158 ili kuzungumuzia mutume Paulo na mara moja ili kuzungumuzia Sergio Paulo, gavana wa Kipro.—Mdo 13:7.
TAREHE 17-23/12
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATENDO 15-16
“Kukosa Kupatana”
8 Luka anaendelea: “Lakini kisha Paulo na Barnaba kukosa kupatana na kubishana sana na watu hao, ikapangwa [na wazee] kuwa Paulo, Barnaba, na wamoja kati ya wale wengine wapande kuenda kwa mitume na wazee kule Yerusalemu juu ya jambo hilo.” (Mdo. 15:2) Maneno ‘kukosa kupatana na kubishana’ inaonyesha kama kila upande ulishikilia sana maoni yake, na kutaniko ya Antiokia haingeweza kumaliza ile mambo. Juu kuendelee kuwa amani na umoja, kutaniko ilitenda kwa hekima wakati iliamua kufikisha ile mambo mbele ya “mitume na wazee kule Yerusalemu,” wenye walikuwa baraza lenye kuongoza. Ile mufano ya wazee wa Antiokia inaweza kutufundisha nini?
Wakristo wa Kweli Wanaheshimia Neno la Mungu
6 Andiko yenye ilisaidia kumaliza ile tatizo ni Amosi 9:11, 12. Andiko ya Matendo 15:16, 17 inarudilia ile andiko ya Amosi na inasema hivi: “Nitarudia na kusimamisha tena hema ya Daudi yenye imeanguka; na nitajenga upya mabomoko yake na kulirudisha tena, ili watu wenye wanabakia wamutafute Yehova kwa bidii, pamoja na watu wa mataifa yote, watu wenye wanaitwa kwa jina langu, ni vile Yehova anasema.”
7 Lakini mutu anaweza kusema, ‘ile andiko haiseme kama haikukuwa jambo ya lazima Watu wa Mataifa wenye waliamini kutahiriwa.’ Ni kweli, lakini ni vile Wayahudi wenye waligeuka kuwa Wakristo wangeelewa mambo. Sababu gani? Kwa sababu Wayahudi waliona ‘watu wa mataifa’ wenye walitahiriwa kuwa ndugu zao. (Kut. 12:48, 49) Kwa mufano, kulingana na tafsiri ya Giguet ya Septante, Esta 8:17 inasema hivi: ‘Watu wengi wa Mataifa walitahiriwa, na wakakuwa Wayahudi.’ Kwa hiyo, wakati Maandiko ilitabiri kama mabaki ya nyumba ya Israeli (Wayahudi na wageuzwa-imani wenye walitahiriwa) pamoja na “watu wa mataifa yote” (Watu wa Mataifa wenye hawatahiriwe) wangekuwa taifa moja yenye kuitwa kwa jina ya Mungu, mambo ilikuwa sasa wazi. Watu wa Mataifa wenye walipenda kuwa Wakristo haikukuwa lazima watahiriwe.
‘Kutia Nguvu Makutaniko’
18 Paulo na Timoteo walifanya kazi pamoja miaka mingi. Walikuwa wahubiri wenye kusafiri, walifanya kazi mbalimbali kwa jina ya baraza lenye kuongoza. Biblia inasema: “Wakati walikuwa wanapita katika miji, walikuwa wanawapatia maagizo yenye yalikuwa yameamuliwa na mitume na wazee wenye walikuwa Yerusalemu ili wayashike.” (Mdo. 16:4) Bila shaka makutaniko ilifuata mwongozo wa mitume na wazee wenye walikuwa Yerusalemu. Kwa sababu ya kutii “makutaniko yakaendelea kuwa nguvu katika imani na hesabu ya waamini iliendelea kuongezeka siku kwa siku.”—Mdo. 16:5.
Mufano ya Mitume wa Yesu ya Kuendelea Kukesha Inatufundisha Nini?
8 Ile habari inaweza kutufundisha nini? Roho ya Mungu ilimuonyesha Paulo fasi ya kuhubiri kisha tu Paulo kuanza safari ya kuenda Asia. Kisha tu Paulo kukaribia Bitinia Yesu alimutolea maagizo. Na mwishowe, kisha tu Paulo kufika Troa Yesu alimuongoza Makedonia. Kwa sababu Yesu njo Kichwa cha kutaniko, leo anaweza kutuongoza kwa namna ile ile. (Kol. 1:18) Kwa mufano, pengine umekwisha kufikiria kufanya kazi ya upainia ao kuhamia mu eneo yenye kuwa na lazima ya wahubiri. Lakini inawezekana Yesu alikuongoza kupitia roho ya Mungu kisha tu wewe kukamata hatua fulani ili kufikia ile muradi. Fikiria hii mufano: Shofere anaweza kuongoza motokari yake kushoto ao kuume kama tu ile motokari ni yenye kutembea. Vile vile, Yesu anaweza kutuongoza ili tupanue utumishi wetu kama tu tunakamata hatua na kujikaza kufikia muradi yetu.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mdo 16:37
sisi ni Waroma: Ni kusema, Wanainchi wa Roma. Paulo na pengine Sila pia walikuwa wanainchi wa Roma. Kulingana na sheria ya Roma, mwanainchi Muroma alikuwa na haki ya kusikilizwa mbele ya kuhukumiwa na hakupaswa hata kidogo kupewa malipizi mbele ya watu kama tribinali haijaonyesha kama iko na hatia. Mwanainchi yeyote wa Roma alikuwa na haki na mapendeleo fulani kote kwenye alikuwa katika Utawala wa Roma. Alipaswa kutii sheria ya Roma, hapana sheria za miji ya majimbo. Wakati alishitakiwa, angeitika kusamba kulingana na sheria za eneo yenye alipatikana ndani, lakini alikuwa pia na haki ya kusikiwa kwenye tribinali ya Roma. Kama anahukumiwa kifo, alikuwa na haki ya kusamba mbele ya mutawala wa Roma. Mutume Paulo alihubiri sana katika Utawala wote wa Roma. Maandiko inaonyesha kuwa alitumia haki zake za kuwa mwanainchi wa Roma mara tatu. Ya kwanza ni hii, wakati aliwaambia waamuzi Wafilipi kuwa wamevunja haki zake kwa kumupiga.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mdo 22:25
muroma: Ni kusema, mwanainchi wa Roma. Paulo alitumia haki yake ya kuwa mwanainchi wa Roma mara tatu. Hapa ni mara ya pili anaitumia. Kwa kawaida, wakubwa wa Roma hawakujiingiza sana mu mambo ya Wayahudi. Lakini, kama Waroma walijiingiza mu mambo ya kusamba ya Paulo haiko tu kwa sababu kulitokea fujo wakati alitembelea ku hekalu lakini pia ni kwa sababu alikuwa mwanainchi wa Roma. Kuwa mwanainchi wa Roma kulipatia mutu haki na mapendeleo fulani yenye watu wote walijua na kuheshimia mu ile utawala. Kwa mufano, sheria ilikataza kufunga ao kupiga Muroma mwenye alikuwa hayahukumiwa, kwa sababu ni watumwa tu njo walitendewa vile.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mdo 25:11
Ninapeleka kesi yangu ya hukumu kwa Kaisari!: Mu Biblia, Paulo anatumia haki yake ya kuwa mwanainchi wa Roma mara tatu. Hapa ni mara ya pili anaitumia. (Kama unapenda kujua fasi ingine mbili kwenye aliitumia, ona nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mdo 16:37; 22:25.) Mutu alikuwa na ruhusa ya kuomba wamupeleke asambe kwa Kaisari mbele ya kutangaza hukumu, kisha kutangaza hukumu, ao wakati wowote wa kusamba. Ilionekana kama Festo hakupenda kuhukumu yeye peke, na ilionekana kama hakukukuwa tumaini yoyote ya kutendewa kwa haki kule Yerusalemu. Kwa hiyo Paulo aliomba asambe mbele ya tribinali kubwa sana ya Roma. Inaonekana kama makosa ingine, kwa mufano kama wanakuta mutu iko naiba, iko nanyanganya, ao iko naleta muvurugo, ule mutu alipaswa kusamba kwanza, lakini hakukuwa na haki ya kuomba tena wamusikilize. Pengine njo sababu, mbele ya kuitika ombi ya Paulo, Festo alizungumuza kwanza na “mukusanyiko wa washauri.” (Mdo 25:12) Kisha, Festo alimupeleka Paulo mbele ya Herode Agripa wa Pili, mwenye alikuja kumutembelea, ili apate habari fulani zenye kuwa wazi za kutumia “Augusto”, ni kusema, Nero, wakati watamutolea mambo ya Paulo. (Mdo 25:12-27; 26:32; 28:19) Lakini ombi ya Paulo ilikuwa na kusudi ingine, alipenda afike Roma. (Mdo 19:21) Ahadi ya Yesu ya unabii na ujumbe wa malaika wenye Paulo alipata kisha, ilionyesha kama Mungu njo alikuwa anaongoza mambo.—Mdo 23:11; 27:23, 24.
TAREHE 24-30/12
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATENDO 17-18
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mdo 17:2, 3
akafikiri: Paulo hakuwaambia tu habari njema. Aliifasiria na kufikiri nao kupitia Maandiko, ni kusema, Maandiko ya Kiebrania yenye iliongozwa na roho ya Mungu. Hakusoma tu Maandiko, lakini alifikiri kupitia Maandiko, na alipatanisha namna yake ya kufikiri na wasikilizaji wake. Tendo ya Kigiriki di·a·leʹgo·mai imetafsiriwa kuwa “kubadilishana mawazo; kuzungumuza; kusimulia.” Inaleta wazo ya kuzungumuza na watu. Ile neno ya Kigiriki inatumiwa pia mu Mdo 17:17; 18:4, 19; 19:8, 9; 20:7, 9.
kuhakikisha kwa kutumia mambo yenye kuandikwa: Neno ya Kigiriki yenye ilitumiwa hapa, inatafsiriwa neno kwa neno “kuweka pembeni (kutia pembeni).” Ile inaweza kuonyesha kama Paulo alilinganisha kwa uangalifu unabii mbalimbali kuhusu Masiya wenye kupatikana mu Maandiko ya Kiebrania na mambo yenye ilitokea mu maisha ya Yesu, ili kuonyesha namna Yesu alitimiza ile unabii mbalimbali.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mdo 17:17
soko: Ile soko (Kigiriki, a·go·raʹ) yenye ilikuwa kaskazini-mangaribi ya Atene, ilikuwa na ukubwa wa hektare 5). Ile soko haikukuwa tu fasi ya kuuza na kuuzisha. Ilikuwa fasi ya biashara, fasi ya kuzungumuzia mambo ya politike na mambo ingine ya maisha.” Watu wa Atene walipenda kukusanyika pale na watu wenye akili walipenda kukutana pale ili kuzungumuza.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mdo 17:22, 23
Kwa Mungu Mwenye Hajulikane: Neno ya Kigiriki A·gnoʹstoi the·oiʹ ilikuwa inaandikwa ku mazabahu fulani ya Atene. Watu wa Atene walijenga hekalu na mazabahu mingi kwa sababu waliogopa miungu. Walijenga hata mazabahu kwa miungu ya kuwazia-wazia tu, kama vile mungu-Kujulikana sana, mungu-Kiasi, mungu-Nguvu, mungu-Kusadikisha, na mungu-Huruma. Pengine kwa sababu waliogopa kama wanaweza kusahau mungu fulani, walijenga mazabahu “Kwa Mungu Mwenye Hajulikane,” ili ule mungu asiwakasirikie. Kupitia ile mazabahu, watu walionyesha kama kuko Mungu mwenye hawaelewe muzuri. Kwa ufundi, Paulo alitumia ile mazabahu ili aanzishe mazungumuzo na wale watu wa Atene juu ya Mungu, Mungu wa Kweli, mwenye mupaka pale walikuwa hawajue.
w08 15/5 uku. 32 fu. 5
Mambo Makubwa Katika Kitabu cha Matendo
18:18—Ni naziri gani yenye Paulo alifanya? Watu fulani wenye elimu ya Biblia wanasema kama Paulo alifanya naziri ya Wanaziri. (Hes. 6:1-21) Lakini Biblia haiseme kama Paulo alifanya naziri gani. Tena, Maandiko haiseme kama Paulo alifanya ile naziri mbele ao kisha kuwa Mukristo ao kama alikuwa ameanza ao kumaliza ile naziri. Ikuwe vile ao hapana, haikukuwa zambi kufanya naziri ya vile.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mdo 18:21
kama Yehova anapenda: Ni maneno yenye kuonyesha kama mutu anapaswa kutia mapenzi ya Mungu mbele wakati anafanya ao anapanga kufanya mambo fulani. Mutume Paulo hakusahau hii kanuni. (1Ko 4:19; 16:7; Ebr 6:3) Na mwanafunzi Yakobo alitia moyo wasomaji wake waseme: “Kama Yehova anapenda, tutaishi na kufanya hiki ao kile.” (Yak 4:15) Ile maneno haipaswe kuwa tu ya kurudilia-rudilia bila kujua maana yake; mutu mwenye anasema “kama Yehova anapenda” anapaswa kujikaza kutenda kulingana na mapenzi ya Yehova. Haiko maneno ya kusema tu kwa sauti lakini mara nyingi inapaswa kuwa kwanza mu moyo.—Ona kwa ajili ya funzo kuhusu Mdo 21:14; 1Ko 4:19; Yak 4:15 na Nyongeza A5.
TAREHE 31/12–6/1
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATENDO 19-20
“Muchunge Kundi ya Mungu Yenye Kuwa Chini ya Uangalizi Wenu”
5 Ule mutume aliandika kama wanaume wazee walipaswa ‘kuchunga kundi ya Mungu yenye ilikuwa chini ya uangalizi wao.’ Ilikuwa jambo ya maana sana kwao kujua kama kundi ni ya Yehova na Yesu Kristo. Wazee walipaswa kutoa hesabu kuhusu namna walichunga kondoo wa Mungu. Tuseme kama rafiki yako wa sana anakuomba umuchungie watoto wakati haiko. Hautawachunga muzuri na kuwapatia chakula? Kama mutoto moja anagonjwa, hautafanya yako yote ili apate musaada wa matunzo yenye iko nayo lazima? Vile vile, wazee mu kutaniko ‘wanachunga kutaniko ya Mungu, yenye alinunua kwa damu ya Mwana wake mwenyewe.’ (Mdo. 20:28) Wanajua kama kila kondoo alinunuliwa kwa damu ya bei sana ya Kristo Yesu. Kwa kuwa watatoa hesabu, wazee wanakulisha, wanalinda, na kuhangaikia kundi.
Wazee Wakristo Ni “Wafanyakazi Wenzenu kwa Ajili ya Furaha Yenu”
15 Kukuwa muchungaji ni kazi ya nguvu. Kuko wakati wazee wanakosa usingizi ili kusali kwa ajili ya kutaniko ao ili kuwasaidia waamini wenzao kiroho. (2 Ko. 11:27, 28) Lakini, sawa mutume Paulo, wazee wanatimiza muzuri kabisa daraka yao namna inafaa na kwa furaha. Mutume Paulo aliandikia Wakorinto hivi: “Kwa furaha nyingi sana nitajitoa na tena nitatolewa kwa ajili ya [nafsi] zenu.” (2 Ko. 12:15, La Sainte Bible en Swahili de la R.D. Congo) Bila shaka, kwa sababu alipenda ndugu zake, Paulo alijitoa kabisa ili kuwatia nguvu. (Soma 2 Wakorinto 2:4; Flp. 2:17; 1 Te. 2:8) Kwa hiyo, haishangaze kuona namna ndugu na dada walimupenda sana mutume Paulo!—Mdo. 20:31-38.
“Niko Safi Kutokana na Damu ya Watu Wote”
20 Maisha ya Paulo ilikuwa tofauti kabisa na ile ya watu wenye walifikia kutumia kundi mubaya. Alifanya kazi ya kimwili na kujitegemeza ili asikuwe muzigo kwa kutaniko. Hakujikaza kusaidia waamini wenzake juu apate faida fulani. Paulo alitia moyo wazee wa Efeso waonyeshe roho ya kujitolea. Aliwaambia: “Munapaswa kusaidia wale wenye kuwa wazaifu, na munapaswa kuweka katika akili maneno ya Bwana Yesu, wakati yeye mwenyewe alisema, ‘Kuko furaha zaidi katika kutoa kuliko katika kupokea.’”—Mdo. 20:35.
‘Kuongezeka na Kuwa Nguvu Zaidi’ Hata Kama Kulikuwa Upinzani
11 Inawezekana Paulo alikuwa anazungumuza kila siku mu ile jumba ya masomo kuanzia saa tano (11H00) mupaka saa kumi (16H00). (Mdo. 19:9) Kwa kuwa zile saa zilikuwa za kifukutu sana, pengine watu mingi walikuwa wameacha kazi zao ili wakule na kupumuzika. Kama Paulo alifanya vile mu miaka mbili, ni kusema, alitumia zaidi ya saa 3000 mu kufundisha. Basi, hii ni sababu ingine yenye ilifanya neno ya Yehova iendelee kuongezeka na kuwa nguvu zaidi. Paulo alikuwa na bidii na alibadilika kulingana na hali. Alibadilisha programu yake ili ahubiri kulingana na mahitaji ya watu wa ile eneo. Alipata matokeo gani? “wote wenye walikuwa wanaishi katika jimbo la Asia wakasikia neno la Bwana, Wayahudi na Wagiriki pia.” (Mdo. 19:10) Ni kweli kwamba alitoa ushahidi kwa ukamili.
‘Kuongezeka na Kuwa Nguvu Zaidi’ Hata Kama Kulikuwa Upinzani
15 Jambo yenye ilipata watoto wa Skewa iliacha watu wamuogope Mungu. Ile woga ilisukuma watu mingi wakuwe waamini na waache tabia za kupashana habari na mashetani. Mambo ya uchawi ilikuwa na sehemu kubwa mu maisha ya Waefeso. Hirizi, uchawi, na nyimbo za uchawi ilikuwa mambo ya kawaida na kulikuwa vitabu mingi ya ile mambo. Kwa hiyo, Waefeso mingi walichochewa kutoa vitabu vyao vya uchawi na kuvichoma mbele ya watu. Kulingana na feza za leo, vile vitabu vilikuwa na bei ya makumi ya maelfu ya dolare. Luka anasema: “Kwa njia yenye nguvu, neno la Yehova likaendelea kuongezeka na kuwa lenye nguvu zaidi.” (Mdo. 19:17-20) Ni ushindi kabisa ya ile kweli juu ya uongo na roho waovu! Wale watu waaminifu walituachia mufano muzuri yenye tunaweza kufuata leo. Na sisi tunaishi mu ulimwengu mwenye watu mingi wako na tabia za kupashana habari na mashetani. Tukivumbula kama tuko na kitu fulani chenye kupatana na zile tabia, tunapaswa kufanya namna Waefeso walifanya, ni kusema, kukiharibisha kabisa! Na tuepuke kabisa zile tabia zenye kuchukiza, hata kama tutapoteza mambo mingi.