Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • bt sura 26 uku. 203-210
  • “Hakuna Hata Mumoja Wenu Mwenye Atapotea”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Hakuna Hata Mumoja Wenu Mwenye Atapotea”
  • “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ‘Upepo Ulikuwa Unatoka Upande wa Mbele’ (Mdo. 27:1-7a)
  • “Tulikuwa Tunarushwa-rushwa kwa Nguvu na Zoruba” (Mdo. 27:7b-26)
  • “Wote Wakafika Salama Kwenye Inchi Kavu” (Mdo. 27:27-44)
  • “Fazili Nyingi Sana” (Mdo. 28:1-10)
  • Paulo Anapelekwa Roma
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Ukuwe Hodari​—Yehova Ni Musaidizi Wako
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • “Kutoa Ushahidi Kamili”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
“Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
bt sura 26 uku. 203-210

SURA YA 26

“Hakuna Hata Mumoja Wenu Mwenye Atapotea”

Wakati Paulo anavunjikiwa na mashua, anaonyesha imani kubwa na upendo mukubwa

Inategemea Matendo 27:1–28:10

1, 2. Paulo atafanya safari ya namna gani, na pengine iko na mahangaiko gani?

FESTO alimuambia Paulo hivi: “Utaenda kwa Kaisari.” Kisha kusikia ile maneno, inawezekana Paulo aliwaza sana juu ya mambo yenye ingemufikia wakati angeenda kwa Kaisari. Paulo amefanya miaka mbili mu gereza, kwa hiyo mu safari ya murefu ya kuenda Roma, atafurahia kuona mambo ingine. (Mdo. 25:12) Lakini Paulo amesafiri mara mingi mu bahari, na wakati fulani safari haikupita muzuri. Kwa hiyo, iko na wasiwasi juu ya ile safari. Na tena, kujua kama ataonana na Kaisari pengine kunafanya ajiulize maulizo mingi.

2 Paulo amekuwa “katika hatari za bahari,” mara mingi. Alivunjikiwa na mashua mara tatu, na hata alipitisha usiku mumoja na muchana mumoja katika bahari kubwa. (2 Ko. 11:25, 26) Zaidi ya ile, hii safari iko tofauti na safari zake zingine za umisionere zenye alifanya na iko huru. Paulo atafanya safari ya murefu sana akiwa mufungwa​—atafanya safari ya umbali wa kilometre 3000 hivi kutoka Kaisaria kuenda Roma. Atafika na iko muzima? Na hata kama anafika na iko muzima, atahukumiwa kifo wakati atafika? Kumbuka kama atasambishwa na mutawala mwenye mamlaka zaidi mu ulimwengu wa Shetani mu ile wakati.

3. Paulo aliazimia kufanya nini, na tutazungumuzia nini mu hii sura?

3 Kisha mambo yote yenye umesoma kuhusu Paulo, unawaza kabisa kama alikosa tumaini wakati alifikiria mambo yenye ingeweza kumufikia? Hapana! Alijua kama atapata magumu, lakini hakujua ni magumu ya aina gani. Paulo aliona kama haina maana kupoteza furaha yake ya kazi ya kuhubiri kwa kuhangaikia mambo yenye hana uwezo wa kubadilisha. (Mt. 6:27, 34) Alijua kama Yehova alipenda atumie kila nafasi ili kuhubiri habari njema ya Ufalme, na hata kuhubiria watu wenye mamlaka. (Mdo. 9:15) Paulo aliazimia kutimiza ile kazi, hata apate magumu ya namna gani. Bila shaka, na siye tunapenda kufanya vile. Tuchunguze basi ile safari yenye Paulo alifanya na tuone mambo yenye mufano wake unatufundisha.

‘Upepo Ulikuwa Unatoka Upande wa Mbele’ (Mdo. 27:1-7a)

4. Paulo alianza safari yake mu mashua ya namna gani, na ni nani njo walimusindikiza?

4 Ofisa Muroma mwenye kuitwa Yulio aliombwa apeleke Paulo na wafungwa wengine fulani Roma. Walikamata mashua yenye ilikuwa tu imefika Kaisaria. Ile mashua ilikuwa imetoka Adramitiamu, bandari (port) yenye kuwa upande wa mangaribi wa Asia Ndogo, ngambo ingine ya muji wa Mitilene katika kisiwa ya Lesbo. Ile mashua ingepita upande wa kaskazini na kisha kuelekea upande wa mangaribi, na ingekuwa nasimama ili kushusha na kukamata mizigo. Mashua za vile hazikukuwa muzuri kwa watu kusafiri ndani, zaidi sana wafungwa. (Ona kisanduku “Kusafiri mu Mashua za Biashara.”) Jambo ya kufurahisha ni kama, mu ile mashua yenye ilikuwa na kikundi ya wafungwa, haiko Paulo tu njo alikuwa Mukristo. Kulikuwa Wakristo wengine wawili hivi wenye walimusindikiza, ni kusema, Aristarko na Luka. Na bila shaka, Luka njo aliandika hii habari. Hatujue ikiwa wale wanaume wawili waaminifu walijilipia ile safari ao waliruhusiwa kusafiri bure juu walionwa kuwa watumishi wa Paulo.​—Mdo. 27:1, 2.

KUSAFIRI MU MASHUA ZA BIASHARA

Zamani mashua zilikuwa natumiwa zaidi sana ili kusafirisha mizigo, haiko ili kusafirisha watu. Watu wenye walipenda kusafiri walipaswa kutafuta mashua ya biashara yenye ilikuwa naenda fasi kwenye walipenda kuenda. Walipaswa kusikilizana bei na wenye mashua na kisha kungoya mupaka wakati mashua itaondoka.

Maelfu ya mashua ilikuwa naenda na kurudia mu Bahari ya Mediterania. Ilikuwa nasafirisha chakula na vitu vingine. Watu wengi wenye walisafiri mu zile mashua walikuwa nalala tu inje kwenye mashua, pengine mu hema yenye walikuwa wanajijengea usiku na kubomoa kila asubui. Walikuwa nabeba kila kitu yenye walikuwa nayo lazima juu ya safari, kutia ndani chakula na vitu vya kulalia ao kujifunika.

Muda wa safari ulitegemea upepo. Kwa sababu ya hali ya hewa ya mubaya ya mu kipindi ya baridi, mara mingi mashua za mingi za biashara hazikukuwa nasafiri mu ile kipindi. Ni kusema kuanzia katikati ya Mwezi wa 11 mupaka katikati ya Mwezi wa 3.

Mashua ya zamani na sehemu zake kubwa ine, kutoka sehemu ya nyuma mupaka ya mbele. 1. Makasia. 2. Tanga kuu. 3. Nanga. 4. Tanga la mbele.

5. Paulo alionana na nani Sidoni, na ile inaweza kutufundisha nini?

5 Kisha kusafiri siku moya mu bahari, ni kusema kilometre 110 hivi upande wa kaskazini, mashua ilisimama Sidoni, eneo ya pembeni ya bahari katika Siria. Inaonekana kama Yulio hakumutendea Paulo sawa wafungwa wengine. Inawezekana ni juu Paulo alikuwa raia wa Roma na alikuwa hayahukumiwa. (Mdo. 22:27, 28; 26:31, 32) Yulio alimuacha Paulo atoke ndani ya mashua ili aonane na Wakristo wenzake. Bila shaka ndugu na dada walifurahi kumuhangaikia Paulo, mwenye alikuwa amefanya muda murefu mu gereza! Na weye unaweza kutafuta nafasi za kuonyesha wengine ukaribishaji wageni ili na weye utiwe moyo?​—Mdo. 27:3.

6-8. Kisha kutoka Sidoni, mashua ilisimama wapi na Paulo alipata nafasi gani za kuhubiri?

6 Mashua ikatoka Sidoni na ikaendelea kusafiri pembeni-pembeni ya inchi kavu na kupita Kilikia, karibu na Tarso kwenye Paulo alikomalia. Luka hazungumuzie fasi zingine kwenye walisimama, lakini alionyesha kama walikuwa mu hatari wakati alisema ‘upepo ulikuwa unatokea upande wa mbele.’ (Mdo. 27:4, 5) Hata vile, tunaweza kuwa hakika kama mutume Paulo alitumia kila nafasi yenye alipata ili kutangazia wengine habari njema. Bila shaka alihubiria wafungwa wenzake na watu wengine wenye walikuwa mu mashua, sawa vile watu wenye walitumika mu mashua, maaskari, na pia watu wenye alikutana nao ku bandari mbalimbali kwenye mashua ilikuwa inasimama. Kama Paulo, leo siye pia tunatumia nafasi zenye tunapata ili kuhubiria wengine.

7 Kisha wakati fulani mashua ilifika Mira, bandari yenye kuwa kusini mwa Asia Ndogo. Kule Paulo na wengine walikamata mashua ingine yenye ingewafikisha Roma kwenye walikuwa naenda. (Mdo. 27:6) Ile wakati, mbegu zenye zilikuwa natoka Misri njo zilikuwa naenda Roma, na zilikuwa naingia mu mashua ku bandari ya Mira. Yulio alipata mashua ya vile na kisha akaambia maaskari wake na wafungwa waingie ndani. Inawezekana ile mashua ilikuwa kubwa zaidi kupita ile ya kwanza. Ilikuwa na mizigo ya mingi ya mbegu na mulikuwa watu 276, ni kusema watu wenye kutumika mu mashua, maaskari, wafungwa, na pengine watu wengine wenye walikuwa naenda Roma. Bila shaka, mu ile mashua ya mupya mulikuwa watu wengi zaidi wenye Paulo angehubiria, na tunaweza kuwa hakika kama alifanya vile.

8 Kisha pale Wangesimama mu eneo ya Kinido, kusini-mangaribi mwa Asia Ndogo. Kama hali ya hewa iko muzuri, mashua ingeweza kufika pale kisha siku moja hivi. Lakini Luka anasema kama “kisha kusafiri polepole kwa siku nyingi, tukafika kwa shida kule Kinido.” (Mdo. 27:7a) Safari haikukuwa mwepesi juu hali ya hewa haikukuwa muzuri. (Ona kisanduku “Upepo wa Mediterania Wenye Kupiga Kutokea Mbele.”) Fikiria hali ya watu wenye kuwa mu mashua wakati mashua iko napita mu upepo mukali na mawimbi ya maji.

UPEPO WA MEDITERANIA WENYE KUPIGA KUTOKEA MBELE

Upepo na vipindi vya mwaka njo vilikuwa nasaidia wenye kuendesha mashua za biashara wajue ni wakati gani watasafiri na ni wapi watapita mu Mediterania ao mu Bahari Kubwa. Katika upande wa mashariki wa ile bahari, kwa ukawaida upepo ulikuwa unatoka mangaribi kuenda mashariki kuanzia Mwezi wa 6 mupaka wa 9. Ile ilifanya ikuwe mwepesi kusafiri kuelekea upande wa mashariki. Ni vile Paulo alisafiri wakati alikuwa anarudia mu safari yake ya tatu ya umisionere. Yeye na wenzake walikuwa mu mashua yenye ilitoka Mileto, ikapita Rode, na kisha ikasimama Patara. Ilikuwa safari ya moja kwa moja mupaka Tiro, ku sehemu ya pembeni ya bahari mu eneo ya Foinike. Luka anasema kama walipita kisiwa ya Kipro yenye ilikuwa upande wao wa kushoto. Ni kusema, walikuwa nasafiri kuelekea upande wa kusini wa Kipro.​—Mdo. 21:1-3.

Sasa, iliwezekana kusafiri na upepo uko napiga sehemu ya mbele ya mashua, ni kusema, kuelekea upande wa mangaribi? Kama upepo uliruhusu, mashua zingeweza kusafiri kuelekea mangaribi. Lakini wakati fulani, ile haikuwezekana kabisa. Kitabu fulani inasema kama “mu kipindi ya baridi, hali ya hewa inazoea kubadilika na zoruba zenye nguvu zinatokaka upande wa mashariki wa Mediterania na kuleta upepo mukali. Wakati fulani ule upepo unakuwaka mukali sana, sana kabisa. Na mara mingi unakuwaka na mvua kubwa sana na hata teluji.” Ilikuwa hatari sana kusafiri mu hali ya hewa ya vile. (The International Standard Bible Encyclopedia)

Mu kipindi yoyote ya mwaka, mashua zingeenda kuelekea kaskazini mupaka sehemu ya pembeni-pembeni ya Palestina na kuendelea upande wa mangaribi kupitia Pamfilia. Mu ile njia, upepo wenye kutoka ku inchi kavu na maji yenye kushuka kuelekea mangaribi, ilifanya ikuwe mwepesi kwa mashua kusafiri. Njo kwenye mashua ya kwanza ya mu safari ya Paulo ya kuenda Roma akiwa mufungwa ilipitia. Lakini upepo ungebadilika na kuwa hatari haraka sana. (Mdo. 27:4) Inawezekana mashua ya kusafirisha mbegu yenye Luka anazungumuzia sana mu habari yake ilisafiri kuelekea kaskazini kutoka Misri, na kisha ikazunguka na kuingia mu sehemu ya bahari yenye kutulia yenye ilikuwa kati ya Kipro na Asia Ndogo. Kutoka Mira, kapitene alipenda kuendelea kuelekea upande wa mangaribi, azunguke chini ya Ugiriki, kisha apande kuelekea upande wa mangaribi wa Italia. (Mdo. 27:5, 6) Lakini, upepo na kipindi ya mwaka ilifanya mambo isikuwe vile walitazamia!

“Tulikuwa Tunarushwa-rushwa kwa Nguvu na Zoruba” (Mdo. 27:7b-26)

9, 10. Kulitokea magumu gani wakati mashua ilikuwa mu maeneo ya karibu na Krete?

9 Kapitene wa mashua alipenda waendelee sehemu ya mangaribi kutoka Kinido, lakini Luka mwenye alikuwa pale anasema kama ‘upepo uliwazuia kusonga mbele.’ (Mdo. 27:7b) Wakati mashua ilianza kuenda mbali na inchi kavu, ilipoteza njia na upepo mukubwa kutoka kaskazini-mangaribi ukaisukuma kusini, pengine kwa mwendo wa mbio sana. Sawa tu vile kisiwa ya Kipro ilikuwa imelinda mashua wakati wa upepo mukali, mara hii ni kisiwa ya Krete njo ilifanya vile. Wakati mashua ilipita Salmone, ku sehemu ya mwisho ya mashariki ya Krete, hali ilikuwa muzuri kidogo. Juu ya nini? Juu mashua ilikuwa ku sehemu ya kusini ya kisiwa, kwenye upepo haukukuwa nguvu sana. Wazia namna wale wenye walikuwa mu mashua walitulia! Lakini watu wenye kutumika mu mashua walijua kama kipindi ya baridi ilikuwa inakaribia, na mu ile kipindi ilikuwa hatari kusafiri mu bahari. Walikuwa na sababu za kuwa na wasiwasi.

10 Luka anasema hivi: “Tukasafiri kwa shida karibu-karibu na inchi kavu [ya Krete], tukafika mahali kwenye kunaitwa Bandari ya Muzuri, karibu na muji wa Lasea.” Kwa sababu walikuwa karibu na inchi kavu walilindwa ili wasipigwe na upepo, hata vile ilikuwa nguvu kuongoza mashua. Lakini ku mwisho walipata fasi ya muzuri kwenye wangeweza kushusha nanga, mu sehemu ya bahari yenye kuingia kwenye inchi kavu, yenye inasemekana kama ilikuwa mu ile eneo, mbele tu ya kuelekea kaskazini. Walibakia pale kwa muda gani? Luka anasema kama walibakia pale kwa “wakati mwingi,” lakini ilikuwa hatari kuendelea kubakia pale. Mu Mwezi wa 9 na wa 10, ilikuwa hatari sana kusafiri mu bahari.​—Mdo. 27:8, 9.

11. Paulo alipatia wale wenye walikuwa mu mashua shauri gani, lakini walikamata uamuzi gani?

11 Pengine watu fulani wenye walikuwa mu ile mashua waliomba Paulo mashauri juu alizoea kusafiri mu Bahari ya Mediterania. Aliwaambia mashua isiendelee na safari. Kama ingeendelea kungekuwa “uharibifu na upotevu mukubwa,” pengine hata watu wangekufa. Lakini muendesha-mashua na mwenye ile mashua walipenda kuendelea na safari, pengine juu waliona kama walipaswa kabisa kupata fasi yenye ilikuwa salama zaidi. Walisadikisha Yulio na watu wengine wengi kama wanapaswa kujaribu kufika Feniki, bandari yenye ilikuwa mbali kidogo na kwenye walikuwa, pengine ilikuwa bandari kubwa zaidi na ilikuwa na fasi kubwa zaidi ya kuwekea mashua, na wangeweza kubakia pale mupaka mwisho wa kipindi ya baridi. Kwa hiyo, wakati upepo wenye ulionekana kuwa muzuri ulipiga kutoka kusini, mashua iliondoka.​—Mdo. 27:10-13.

12. Kisha mashua kutoka Krete, ilipambana na magumu gani, na wale wenye kutumika mu mashua walifanya nini ili kujaribu kuepuka musiba?

12 Kisha kukakuwa “upepo mukali” kutoka kaskazini-mashariki. Kwa wakati fulani walipata ulinzi nyuma ya “kisiwa kidogo chenye kuitwa Kauda,” ku kilometre 65 hivi kutoka ile fasi yenye kuitwa Bandari ya Muzuri. Lakini mashua ilikuwa ingali mu hatari ya kusukumwa kusini na kukwama mu muchanga pembeni ya bahari, mu eneo ya Afrika. Juu ya kuepuka ile hatari, watu wenye kutumika mu mashua walikamata mashua ya kidogo yenye ilikuwa nakokotwa na mashua yao na waliingiza mu ile mashua kubwa. Haikukuwa mwepesi kufanya vile juu inawezekana ile mashua ya kidogo ilikuwa imeyala maji. Kisha wakazungusha makamba ao minyororo ku ile mashua kubwa na kuikaza juu isivunjike. Na kisha wakafungua kamba zenye kufunga tanga na wakapiganisha ili kuelekeza mashua katika ule upepo mupaka zoruba ipite. Wazia namna ile hali ingeogopesha kabisa. Hata kisha kufanya ile mambo yote, mashua iliendelea ‘kurushwa-rushwa kwa nguvu na zoruba.’ Siku ya tatu wakatupa kamba za mashua ndani ya maji, pengine juu mashua iendelee kubakia juu ya maji.​—Mdo. 27:14-19.

13. Pengine hali ilikuwa namna gani mu mashua wakati wa zoruba?

13 Bila shaka wenye walikuwa mu ile mashua waliogopa sana. Lakini Paulo na wenzake walikuwa hakika kama hawatakufa. Mbele ya pale, Yesu alikuwa amehakikishia Paulo kama atatoa ushahidi katika Roma, na kisha pale malaika alimuhakikishia tena ile jambo. (Mdo. 19:21; 23:11) Lakini, kwa majuma mbili, usiku na muchana, zoruba kubwa sana iliendelea kupiga. Kwa sababu ya mvua yenye iliendelea kunyesha na mawingu ya mweusi yenye ilifanya mwangaza wa jua na wa nyota usionekane, mwenye kuendesha mashua hakujua ni wapi mashua ilikuwa ao ni wapi mashua ilikuwa inaenda. Haikuwezekana hata kula chakula kwa sababu ya baridi, mvua, kuchoka bahari, na woga. Nani njo angekumbuka chakula!

14, 15. (a) Wakati Paulo alizungumuza na watu wenye walikuwa mu mashua, juu ya nini aliwakumbusha onyo yenye aliwapatiaka? (b) Ujumbe wenye tumaini wenye Paulo alitolea watu unaweza kutufundisha nini?

14 Paulo anasimama na kuwakumbusha angalisho yenye aliwapatia. Lakini hafanye vile juu ya kuwahukumu kwa kusema, ‘si niliwaambia!’ Hali ya mubaya yenye walikuwa ndani ilionyesha tu kama shauri ya Paulo ilikuwaka ya hekima. Kisha akawaambia hivi: “Sasa ninawatia moyo musiogope, kwa maana hakuna hata mumoja wenu mwenye atapotea, mashua tu ndiyo itapotea.” (Mdo. 27:21, 22) Bila shaka ile maneno iligusa moyo wa wale wenye walikuwa wanamusikiliza! Bila shaka Paulo naye alifurahi sana juu Yehova alikuwa amemupatia ujumbe wenye tumaini wa kuambia wengine. Ni jambo ya maana tukumbuke kama Yehova anaona uzima wa kila mwanadamu kuwa wa maana. Kila mutu iko na samani kwake. Mutume Petro aliandika hivi: “Yehova . . . hataki mutu yeyote aharibiwe lakini anataka wote wafikie kutubu.” (2 Pe. 3:9) Kwa hiyo ni jambo ya haraka sana tujikaze kuambia watu wengi zaidi kadiri inawezekana ujumbe wenye tumaini wenye Yehova anatupatia! Maisha ya watu, yenye Yehova anaona kuwa ya maana, iko mu hatari.

15 Inawezekana Paulo alikuwa nahubiria watu wengi wenye walikuwa mu mashua kuhusu ‘tumaini la ahadi yenye Mungu alitoa.’ (Mdo. 26:6; Kol. 1:5) Sasa, wakati watu wote walikuwa wanawaza kama mashua itavunjika, Paulo aliwatolea sababu ya kuwa na tumaini kama wataokoka. Aliwaambia hivi: “Usiku huu malaika wa Mungu mwenye mimi ni mali yake . . . alisimama karibu yangu na akasema: ‘Usiogope, Paulo. Unapaswa kusimama mbele ya Kaisari, na angalia! Mungu amekupatia wale wote wenye wanasafiri pamoja na wewe.’” Kisha Paulo akawaambia: “Kwa hiyo, wanaume, Musiogope, kwa maana ninamuamini Mungu kwamba itakuwa kabisa kama vile niliambiwa.”​—Mdo. 27:23-26.

“Wote Wakafika Salama Kwenye Inchi Kavu” (Mdo. 27:27-44)

Paulo nasali mu mashua yenye kuyala watu. Watu fulani wenye kuchoka wanainamisha vichwa na wengine wako naangalia. Mikate iko ku vitu fulani vya mbao.

“Akatoa shukrani kwa Mungu mbele yao wote.”​—Matendo 27:35

16, 17. (a) Paulo alitumia nafasi gani ili kusali, na matokeo ilikuwa nini? (b) Namna gani maneno ya Paulo ilitimia?

16 Kisha majuma mbili yenye mashua ilisukumwa na upepo ku kilometre 870 hivi, wenye kutumika mu mashua walitambua kama inawezekana wanakaribia inchi kavu, pengine juu walisikia mawimbi iko napiga ku inchi kavu yenye ilikuwa karibu. Waliachilia nanga ku sehemu ya nyuma ya mashua ili wasikokotwe na mawimbi na kuongoza sehemu ya mbele ya mashua kuelekea inchi kavu. Walikuwa najaribu kuongoza mashua ku inchi kavu. Ile wakati walijaribu kutoka mu mashua lakini maaskari waliwazuia. Paulo akaambia ofisa wa jeshi na maaskari wake hivi: “Kama watu hawa hawabakie katika mashua, hamuwezi kuokoka.” Sasa mashua ilikuwa natulia kidogo, kwa hiyo Paulo akawaambia watu wakule chakula na akawahakikishia tena kama hawatakufa. Kisha Paulo “akatoa shukrani kwa Mungu mbele yao wote.” (Mdo. 27:31, 35) Kwa kutoa ile sala ya shukrani, aliwekea Luka, Aristarko, na Wakristo wengine leo mufano muzuri. Je, sala zenye unatoa mbele ya watu wengi, zinatia wengine moyo na kuwafariji?

17 Kisha sala ya Paulo, “wakajipa moyo na wakaanza kula.” (Mdo. 27:36) Kisha wakapunguza uzito wa mashua kwa kutupa mizigo fulani ya ngano mu maji na ile ilifanya mashua ipande zaidi juu ya maji kwa sababu ilikuwa nakaribia inchi kavu. Wakati asubui ilifika, wenye kutumika mu mashua walikata nanga, wakafungua kamba za makasia na wakapandisha tanga ili waweze kuelekeza mashua mupaka ku inchi kavu. Kisha, sehemu ya mbele ya mashua ikakwama, pengine kwa sababu ya muchanga ao matope, na kisha omo, ni kusema sehemu ya mbele ya mashua, ikaanza kuvunjika kwa sababu ya mawimbi yenye nguvu yenye ilikuwa naipiga. Maaskari fulani walitaka kuua wafungwa ili hata mumoja wao asikimbie, lakini Yulio aliwazuia kufanya vile. Aliambia watu wote waogelee ao wabane ku kitu fulani yenye itawasaidia kufika ku inchi kavu. Mambo yenye Paulo alitabiri ilitimia, watu wote 276 waliokoka. Kwa kweli, “wote wakafika salama kwenye inchi kavu.” Lakini walijikuta sasa wapi?​—Mdo. 27:44.

“Fazili Nyingi Sana” (Mdo. 28:1-10)

18-20. Namna gani watu wa Malta walionyesha “fazili nyingi sana,” na Mungu alifanya muujiza gani kupitia Paulo?

18 Wale watu wenye waliokoka walikuwa ku kisiwa ya Malta kusini mwa Sisili. (Ona kisanduku “Malta Ilikuwa Wapi?”) Watu wa mu ile kisiwa wenye walikuwa nasema luga ya kigeni waliwaonyesha “fazili nyingi sana.” (Mdo. 28:2) Waliwasha moto kwa ajili ya wale watu wenye walikuwa wamelowana na wenye walikuwa natetemeka kwa sababu ya baridi. Ile moto iliwasaidia kupata kifukutu hata kama kulikuwa baridi na mvua. Kisha, kukatokea muujiza fulani.

19 Paulo alipenda kusaidia. Kwa hiyo, alianza kukusanya kuni na kuziweka kwenye moto. Wakati alikuwa nafanya vile, nyoka-kipiri mwenye sumu akatoka ndani ya kuni, akamuuma, na kumubana kwenye mukono. Watu wa Malta waliwaza kama ile ilikuwa alama ya malipizi kutoka kwa Mungu.a

20 Watu wa mu ile kisiwa wenye waliona namna Paulo aliumwa na nyoka waliwaza kama “atavimba.” Kitabu kimoja kinasema kama mu luga ya kwanza-kwanza neno yenye ilitumiwa hapa ilikuwa “neno ya kinganga.” Haishangaze kuona kama Luka, mwenye alikuwa munganga alitumia ile neno ya kinganga. (Mdo. 28:6; Kol. 4:14) Lakini, Paulo akakunguta mukono wake na ule nyoka akatoka na hakuumia hata kidogo.

21. (a) Ni mifano gani yenye kuwa mu habari yenye Luka aliandika yenye inaonyesha kama alizungumuzia mambo bila makosa na waziwazi? (b) Paulo alifanya muujiza gani na ile ilifanya watu wa Malta watende namna gani?

21 Mukubwa fulani mwenye kuitwa Publio, mwenye alikuwa na mashamba, alikuwa naishi mu ile eneo. Pengine yeye njo alikuwa ofisa Muroma mwenye mamlaka zaidi katika Malta. Luka anamuita “mukubwa wa kisiwa hicho.” Ile jina ya cheo imepatikana ku maandishi mbili ya Wamalta. Alionyesha ukaribishaji-wageni kwa kupatia Paulo na wenzake fasi ya kubakia kwa siku tatu. Lakini, baba ya Publio alikuwa mugonjwa. Hapa tena Luka anafasiria ugonjwa wake kwa kutumia maneno yenye kuwa wazi kabisa. Aliandika kama ule mwanaume “alikuwa amelala katika kitanda akiwa na ugonjwa wa homa na wa kuhara damu.” Alitumia maneno ya kinganga wakati alizungumuzia ugonjwa wa ule mwanaume. Paulo alisali, akaweka mikono yake juu ya ule mwanaume, kisha ule mwanaume akapona. Kwa sababu watu wa Malta walishangazwa sana na ule muujiza, walileta watu wengine ili waponyeshwe, na walileta pia zawadi ili kutimiza mahitaji ya Paulo na ya wenzake.​—Mdo. 28:7-10.

22. (a) Namna gani mutu fulani mwenye elimu amesifu mambo yenye Luka aliandika kuhusu safari ya kuenda Roma? (b) Tutazungumuzia nini mu sura yenye kufuata?

22 Kufikia hapa, mambo yenye tumezungumuzia kuhusu safari ya Paulo imeelezwa muzuri bila makosa. Mutu fulani mwenye elimu alisema hivi: “Habari yenye Luka aliandika . . . ni moja kati ya habari zenye kuelezwa waziwazi mu Biblia yote. Namna aliandika habari zenye kuhusu kusafiri mu bahari mu karne ya kwanza na namna alifasiria hali za mu Mediterania ya mashariki ni yenye kuwa wazi kabisa na yenye haina makosa.” Inawezekana Luka alikuwa naandika matukio ya kila siku mu buku fulani wakati alikuwa nasafiri na Paulo. Na inawezekana habari yake ilitegemea ile mambo yenye alikuwa anaandika. Kama ni vile, alikuwa na mambo mingi ya kuandika mu sehemu yenye ilifuata ya safari. Ni nini yenye ingemufikia Paulo wakati mwishowe angefika Roma? Tutazungumuzia ile mu sura yenye kufuata.

MALTA ILIKUWA WAPI?

Kuko visiwa mingi tofauti-tofauti vyenye watu wenye elimu wanawazia kama njo kisiwa ya “Malta,” kwenye mashua ilivunjikiaka Paulo. Wamoja wanawaza kama ni kisiwa yenye kuwa karibu na kisiwa ya Korfu, mangaribi mwa sehemu ya Ugiriki yenye kuwa pembeni ya bahari. Pendekezo ingine inategemea neno “Malta” yenye inatumiwa mu kitabu ya Matendo. Neno yake ya Kigiriki ni Me·liʹte. Kwa hiyo, wengine wanawaza kama ilikuwa kisiwa Melite Illyrica, yenye inaitwa leo Mljet, yenye haiko mbali na inchi kavu mu inchi ya Kroatia, mu Bahari ya Adriatiki.

Ni kweli kwamba Matendo 27:27 inataya “Bahari ya Adria,” lakini mu siku za Paulo, “Adria” ilikuwa sehemu kubwa sana kuliko Bahari ya Adriatiki ya leo. Ilitia ndani Bahari ya Ionia na bahari zenye kuwa upande wa mashariki wa Sisili na wa mangaribi wa Krete. Kwa hiyo ilitia ndani bahari yenye kuwa karibu na Malta ya leo.

Mashua yenye Paulo alikuwa ndani ilisukumwa kusini kutoka Kinido kuelekea kusini mwa Krete. Kwa sababu ya upepo mukali wenye ulikuwa mu ile zoruba, ingekuwa nguvu sana mashua igeuke na kuelekea sehemu za kaskazini sawa vile Mljet ao kisiwa yenye kuwa karibu na Korfu. Kwa hiyo, uwezekano mukubwa ni kwamba Malta ilikuwa upande wa mangaribi. Inawezekana ni mu kisiwa ya Malta yenye kuwa kusini mwa Sisili njo kwenye mashua yenye Paulo alikuwaka ndani ilivunjikiaka.

a Kwa sababu watu walijua ule nyoka, ile inaonyesha kama ile wakati nyoka-vipiri walikuwa mu ile kisiwa. Leo, mu eneo ya Malta hamuna nyoka-vipiri. Pengine ni juu tangu ule wakati wenye Paulo alikuwa Malta, kwa miaka mingi hali ya mazingira imebadilika sana. Ao juu watu wameongezeka sana mu ile kisiwa, pengine nyoka-vipiri wote waliuawa.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine