Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha
TAREHE 2-8/09
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | WAEBRANIA 7-8
“Kuhani Milele kwa Mufano wa Melkisedeki”
it-2-F uku. 249
Melkisedeki
Mufalme wa Salemu ya zamani na “kuhani wa Mungu Mwenye Kuwa Juu Zaidi,” Yehova. (Mwa 14:18, 22) Ni yeye njo kuhani wa kwanza mwenye Maandiko inazungumuzia; ukuhani wake ulianza wakati fulani mbele ya mwaka wa 1933 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu. Kwa sababu Melkisedeki alikuwa mufalme wa Salemu, jina lenye linamaanisha “Amani,” mutume Paulo anamuzungumuzia kuwa “Mufalme wa Amani” na, kulingana na jina lake, anamuita kuwa “Mufalme wa Haki.” (Ebr 7:1, 2) Inawezekana Salemu ya zamani njo ilikuwa eneo la kwanza-kwanza la muji wa Yerusalemu, na jina “Salemu” lilifikia kuwa sehemu ya jina Yerusalemu, na ile inafanya wakati fulani Yerusalemu iitwe “Salemu.”—Zb 76:2.
Kisha Abramu (Abrahamu) kupata ushindi juu ya Kedorlaoma na wafalme wenye walikuwa pamoja naye, alikuja kwenye Bonde la Shave ao “Bonde la mufalme.” Kule, Melkisedeki alimuletea Abrahamu “mukate na divai” na akamubariki, kwa kusema hivi: “Abramu abarikiwe na Mungu Mwenye Kuwa Juu Zaidi, Mutengenezaji wa mbingu na dunia; na atukuzwe Mungu Mwenye Kuwa Juu Zaidi, mwenye ametia wakandamizaji wako katika mikono yako!” Kwa hiyo, Abrahamu akamupatia Melkisedeki, kuhani-mufalme, “sehemu moja ya kumi ya kila kitu,” ni kusema ya “vitu vya maana” vyenye alikuwa amepata kisha kupata ushindi mu vita yenye alipigana na wafalme wenye walikuwa wameungana.—Mwa 14:17-20; Ebr 7:4.
it-2-F uku. 250 fu. 3
Melkisedeki
Ni mu maana gani Melkisedeki hakukuwa na “mwanzo wa siku wala mwisho wa uzima”?
Paulo alizungumuzia jambo fulani la pekee kuhusu Melkisedeki. Alisema hivi juu yake: “Kwa kuwa hana baba, hana mama, hana ukoo, na hana mwanzo wa siku wala mwisho wa uzima, lakini akiwa amefanywa kama Mwana wa Mungu, anaendelea kuwa kuhani kwa wakati wote.” (Ebr 7:3) Sawa vile watu wengine, Melkisedeki alizaliwa na alikufa. Lakini, Biblia haitaje majina ya baba na mama yake, haizungumuzie kizazi chake na watoto wake, na haina habari yoyote juu ya mwanzo ao mwisho wa maisha yake. Kwa hiyo, Melkisedeki njo alistahili kabisa kumufananisha Yesu Kristo, mwenye ukuhani wake hauna mwisho. Sawa vile Melkisedeki hakukuwa na kuhani mwenye alimutangulia ao mwenye alikamata nafasi yake kisha, vilevile Kristo hakukuwa na kuhani mukubwa mwenye alimutangulia mwenye alikuwa sawa yeye, na Biblia inaonyesha kama hakuna mwenye atakamataka nafasi yake. Tena, hata kama Yesu alizaliwa mu kabila la Yuda na mu kizazi cha Mufalme Daudi, kizazi chake cha hapa ku dunia hakikukuwa na uhusiano wowote na ukuhani wake, ao haiko kupitia kile kizazi njo alifikia kuwa kuhani na mufalme. Ile mambo yote ilitokana na kiapo chenye Yehova alimufanyia.
it-2-F uku. 249
Melkisedeki
Kufananishwa kwa Ukuhani wa Kristo. Mu unabii moja wenye unahusu Masiya, Yehova alimuapia hivi “Bwana” wa Daudi: “Wewe ni kuhani milele kwa mufano wa Melkisedeki!” (Zb 110:1, 4) Ile maneno yenye kuongozwa na roho ya Mungu ilipatia Waisraeli sababu ya kuona kama ni Masiya mwenye aliahidiwa njo angekuwa kuhani na mufalme. Mu barua yenye mutume Paulo aliandikia Waebrania, alifanya wasikuwe na mashaka yoyote juu ya ule mwenye alitaribiriwa, wakati alizungumuzia “Yesu, mwenye amekuwa kuhani mukubwa milele kwa mufano wa Melkisedeki.”—Ebr 6:20; 5:10; ona AGANO.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
w00 15/8 uku. 14 fu. 11
Zabihu Zenye Zilimupendeza Mungu
11 Mutume Paulo anasema kama “kila kuhani mukubwa anawekwa ili kutoa zawadi na pia zabihu.” (Waebrania 8:3) Ona kwamba, Paulo anatenganisha matoleo ya kuhani mukubwa wa Israeli ya zamani mu sehemu mbili, ni kusema, “zawadi” na “zabihu,” ao “zabihu kwa ajili ya zambi.” (Waebrania 5:1) Kwa kawaida, watu wanatoa zawadi ili kuonyesha upendo na shukrani, na pia ili kukomalisha urafiki, au kutafuta kukubaliwa. (Mwanzo 32:20; Mezali 18:16) Vilevile, matoleo mingi yenye Sheria iliomba kutoa inaweza kuonwa kuwa “zawadi” zenye zilitolewa kwa Mungu juu ya kutafuta kukubaliwa naye. Kama mutu alikosa kutii Sheria alipaswa kutoa malipo, na juu ya kutoa ile malipo, iliomba kutoa “zabihu kwa ajili ya zambi.” Mu vitabu tano vya kwanza vya Biblia, zaidi sana mu Kutoka, Mambo ya Walawi, na Hesabu, muko habari mingi sana kuhusu aina mbalimbali za zabihu na matoleo. Hata kama inaweza kuwa nguvu sana kwetu kujua na kukumbuka zile habari zote, ni jambo la lazima tuchunguze mambo fulani ya maana kuhusu aina mbalimbali za zabihu.
it-1-F uku. 79 fu. 7
Agano
Namna gani agano la Sheria lilifikia kuwa “lenye halifae tena”?
Lakini, agano la Sheria lilifikia kuwa “lenye halifae tena” wakati Mungu alisema kupitia nabii Yeremia kama kungekuwa agano jipya. (Yer 31:31-34; Ebr 8:13) Agano la Sheria lilifikia mwisho wake mu mwaka wa 33 wakati Kristo alikufa kwenye muti wa mateso (Kol 2:14), na kwa hiyo agano jipya likakamata nafasi ya agano la Sheria.—Ebr 7:12; 9:15; Mdo 2:1-4.
Hotuba
it-1-F uku. 80 fu. 5-7
Agano jipya. Yehova alitabiri agano jipya kupitia nabii Yeremia kati ya mwaka wa 601 na 700 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu. Na alisema kama halitakuwa sawa agano la Sheria lenye Waisraeli walivunja. (Yer 31:31-34) Mbele ya kifo chake, katika usiku wa tarehe 14 mwezi wa Nisani mwaka wa 33, wakati alianzisha Chakula cha Mangaribi cha Bwana, Yesu Kristo alisema kama agano jipya litakubaliwa kisheria kupitia zabihu yake. (Lu 22:20) Siku 50 kisha Yesu kufufuliwa na siku 10 kisha yeye kufika kwa Baba yake, alipatia roho takatifu wanafunzi wake wenye walikuwa wamekusanyika mu chumba kimoja cha juu mu Yerusalemu, roho yenye Yehova alimupatia.—Mdo 2:1-4, 17, 33; 2Ko 3:6, 8, 9; Ebr 2:3, 4.
Watu wenye kufanyiza agano jipya ni Yehova, kwenye upande mumoja, na kwenye upande mwingine ni “Israeli wa Mungu,” ni kusema, wana wa Mungu wenye walizaliwa kwa roho katika uhusiano na Kristo, wenye wanafanyiza kutaniko lake ao mwili wake. (Ebr 8:10; 12:22-24; Ga 6:15, 16; 3:26-28; Ro 2:28, 29) Agano jipya linakubaliwa kisheria kupitia damu yenye ilimwangwa ya Yesu Kristo (zabihu ya uzima wake wa kibinadamu), yenye samani yake ilitolewa kwa Yehova kisha Yesu kufika mbinguni. (Mt 26:28) Wakati mutu anachaguliwa na Mungu ili kuishi mbinguni (Ebr 3:1), Mungu anafanya ule mutu aingie mu agano lake kupitia zabihu ya Kristo. (Zb 50:5; Ebr 9:14, 15, 26) Yesu Kristo njo mupatanishi wa agano jipya (Ebr 8:6; 9:15) na yeye njo Uzao wa kwanza-kwanza wa Abrahamu. (Ga 3:16) Kwa sababu Yesu ni mupatanishi wa agano jipya, anasaidia wale wenye kuwa mu agano hilo kuwa sehemu ya uzao wa kweli wa Abrahamu (Ebr 2:16; Ga 3:29), na ile inawezekana kupitia musamaha wa zambi zao. Yehova anawatangaza kuwa wenye haki.—Ro 5:1, 2; 8:33; Ebr 10:16, 17.
Wana hao wa Mungu wenye walizaliwa kwa roho, ni kusema, ndugu za Kristo watiwa-mafuta wa wanafikia kuwa makuhani wa cheo cha chini wa Kuhani Mukubwa, katika “ukuhani wa kifalme.” (1Pe 2:9; Ufu 5:9, 10; 20:6) Wakristo hao wanafanya kazi ya ukuhani, “utumishi mutakatifu” (Flp 2:17), na wanaitwa “watumishi wa agano jipya.” (2Ko 3:6) Wakristo hao watiwa-mafuta wanapaswa kufuata hatua za Kristo kwa ukaribu sana, na kwa uaminifu mupaka kifo; kisha Yehova atawafanya kuwa wafalme na makuhani, na kuwafanya wakuwe washiriki katika makao ya kiroho, na atawapatia zawadi ya kutokufa na kutokuharibika wakati watakuwa wariti pamoja na Kristo mbinguni. (1Pe 2:21; Ro 6:3, 4; 1Ko 15:53; 1Pe 1:4; 2Pe 1:4) Kusudi la agano jipya ni kuchukua kati ya watu, watu fulani kwa ajili ya jina la Yehova ili wakuwe sehemu ya “uzao” wa Abrahamu. (Mdo 15:14) Wanakuwa “bibi-arusi” wa Kristo, wenye Kristo anaingiza mu agano kwa ajili ya Ufalme, ili watawale pamoja naye. (Yoh 3:29; 2Ko 11:2; Ufu 21:9; Lu 22:29; Ufu 1:4-6; 5:9, 10; 20:6) Kusudi la agano jipya linaendelea mupaka wale wote wenye kufanyiza “Israeli wa Mungu” wakuwe wamefufuliwa na kupata kutokufa mbinguni.
TAREHE 9-15/09
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | WAEBRANIA 9-10
“Kivuli cha Mambo ya Muzuri Yenye Yatakuja”
it-2-F uku. 490
Musamaha
Mu sheria yenye Mungu alipatia taifa la Israeli, alionyesha kama ili mutu mwenye alimutendea Mungu zambi ao mwanadamu mwenzake asamehewe, alipaswa kwanza kutubu zambi yake kulingana na namna Sheria ilionyesha, na mara mingi, kutoa zabihu ya damu kwa Yehova. (Law 5:5–6:7) Ile ilionyesha uhakika wa hii maneno ya Paulo: “Ndiyo, kulingana na Sheria karibu vitu vyote vinatakaswa kupitia damu, na kama damu haimwangwe hakuna musamaha wenye unatokea.” (Ebr 9:22) Lakini, damu ya zabihu za wanyama haingeweza kabisa kumaliza zambi na kufanya watu wakuwe na zamiri yenye kuwa safi kabisa. (Ebr 10:1-4; 9:9, 13, 14) Tofauti na ile, agano jipya lenye lilitabiriwa lilifanya iwezekane watu kupata musamaha wa kweli, wenye unategemea zabihu ya bei ya ukombozi ya Yesu Kristo. (Yer 31:33, 34; Mt 26:28; 1Ko 11:25; Efe 1:7) Hata wakati Yesu alikuwa ku dunia, alionyesha kama alikuwa na mamlaka ya kusamehe zambi wakati aliponyesha mutu mwenye kupooza.—Mt 9:2-7.
cf uku. 183 fu. 4
“Endelea Kunifuata”
4 Maandiko haiseme kitu kuhusu namna Yesu alifika mbinguni, namna walimupokea, na furaha yenye alikuwa nayo wakati alikutana tena na Baba yake. Lakini, Biblia ilionyesha mbele ya wakati mambo yenye ingetendeka mbinguni kisha tu Yesu kurudia kule. Wayahudi walizoea kufanya sherehe fulani takatifu kwa zaidi ya miaka 1500. Siku moja kila mwaka, kuhani mukubwa alikuwa anaingia Patakatifu Zaidi mu hekalu juu ya kunyunyiza mbele ya sanduku la agano damu ya zabihu zenye zilitolewa Siku ya Upatanisho. Ile siku, kuhani mukubwa alifananisha Masiya. Kisha Yesu kurudia mbinguni, alitimiza mara moja kwa wakati wote maana ya unabii wenye ulihusu ile sherehe. Aliingia mbinguni mbele ya utukufu wa Yehova, patakatifu zaidi katika ulimwengu wote, na kumupatia Baba yake samani ya zabihu yake ya bei ya ukombozi. (Waebrania 9:11, 12, 24) Je, Yehova aliikubali?
it-2-F uku. 548 fu. 6
Ukamilifu
Kukamilika kwa Sheria ya Musa. Kati ya mambo mbalimbali yenye ilikuwa mu Sheria yenye Mungu alipatia Waisraeli kupitia Musa, kulikuwa pia mupango wa kuweka makuhani na wa kutoa zabihu mbalimbali za wanyama. Hata kama ile mipango yote ilitoka kwa Mungu na ilikuwa kamilifu, Sheria, ukuhani wake, na zabihu havikuleta ukamilifu kwa watu wenye walikuwa chini ya Sheria, kama vile mutume Paulo mwenye aliongozwa na roho anaonyesha. (Ebr 7:11, 19; 10:1) Lakini kuliko kuwafanya wakuwe huru kutoka katika zambi na kifo, Sheria ilifanya zambi ikuwe wazi zaidi. (Ro 3:20; 7:7-13) Lakini ile mambo yote yenye Mungu aliwapatia, ilitimiza kusudi lenye Mungu alikuwa nalo; Sheria ilitumika kama “mulinzi” mwenye aliongoza watu kwa Kristo, na ilikuwa “kivuli [kamili] cha mambo ya muzuri yenye yatakuja.” (Ga 3:19-25; Ebr 10:1) Kwa hiyo, wakati Paulo anazungumuza juu ya “kile chenye Sheria ilishindwa kufanya kwa sababu ilikuwa zaifu kupitia mwili” (Ro 8:3), iko anazungumuzia kuhani mukubwa muyahudi mwenye hakukuwa na uwezo (mwenye aliwekwa na Sheria ili kusimamia zabihu zenye watu walikuwa wanatoa na mwenye alikuwa anaingia na zabihu ya damu mahali Patakatifu Zaidi Siku ya Kufunika Zambi) wa “kuokoa kwa ukamili” wale wenye alitumikia, sawa vile Waebrainia 7:11, 18-28 inafasiria. Hata kama kutoa zabihu kupitia ukuhani wa Haruni kulifanya watu waendelee kukubaliwa na Mungu, ile haikuwafanya wasahau kama walikuwa watenda-zambi. Ni ile njo mutume Paulo anazungumuzia wakati anasema kama zabihu za kufunika zambi hazingeweza “kufanya wale wenye wanakaribia wakuwe wakamilifu,” ni kusema, kuhusiana na zamiri yao. (Ebr 10:1-4; linganisha na Ebr 9:9.) Kuhani mukubwa hakukuwa na uwezo wa kutoa bei ya ukombozi yenye iliombwa ili watu wakombolewe kabisa kutoka katika zambi. Ile inawezekana tu kupitia kazi ya ukuhani wa milele wa Yesu na zabihu yake yenye kufaa.—Ebr 9:14; 10:12-22.
w92 1/3 uku. 31 fu. 4-6
Maulizo ya Wasomaji Wetu
Paulo alisema kama kifo kilikuwa cha lazima juu ya kufanya maagano kati ya Mungu na wanadamu ikubaliwe kisheria. Mufano moja ni wa agano la Sheria. Musa njo alikuwa mupatanishi wa agano hilo, ni kusema mwenye aliongoza mapatano kati ya Waisraeli wa kimwili na Mungu. Kwa hiyo, Musa alikuwa na daraka la maana na ni yeye njo mwanadamu mwenye alikuwa anashugulika na Waisraeli wakati walikuwa wanaingia mu agano hilo. Kwa hiyo, Musa angeonekana kuwa yeye njo mwanadamu mwenye alifanya agano la Sheria lenye lilianzishwa na Yehova. Lakini je, iliomba Musa amwange damu yake juu agano la Sheria lianze kufanya kazi? Hapana. Kuliko kufanya vile, damu ya wanyama wenye walitolewa njo ilikamata nafasi ya damu ya Musa.—Waebrania 9:18-22.
Tuseme nini juu ya agano jipya kati ya Yehova na taifa la Israeli ya kiroho? Yesu Kristo alikuwa na daraka la utukufu la kuwa, Mupatanishi kati ya Yehova na Israeli ya kiroho. Hata kama Yehova njo mwenye alianzisha agano hilo, agano lenyewe lilimutegemea Yesu Kristo. Zaidi ya kuwa Mupatanishi wa agano hilo, Yesu alishugulika moja kwa moja katika mwili na wale wenye wangekuwa wa kwanza kuingizwa mu agano hilo. (Luka 22:20, 28, 29) Tena, alistahili kutoa zabihu yenye ilihitajiwa juu agano hilo likubaliwe kisheria. Ile zabihu haikukuwa ya wanyama lakini ya uzima mukamilifu wa mwanadamu. Kwa hiyo, Paulo angeweza kuzungumuzia Yesu kuwa mwanadamu mwenye alifanya agano jipya. Kisha ‘Kristo . . . kuingia mbinguni kwenyewe, ili sasa aonekane mbele ya Mungu kwa ajili yetu,’ agano jipya lilikubaliwa kisheria.—Waebrania 9:12-14, 24.
Wakati Paulo alizungumuzia Musa na Yesu kuwa wanadamu wenye walifanya maagano, hakumaanisha kama wao njo walianzisha ile maagano, maagano yenye kwa kweli ilikuwa imefanywa na Mungu. Lakini, wanadamu hao wawili walikuwa wapatanishi, walishiriki kwa ukaribu sana ili kufanyiza ile maagano. Na mu kila hali, kifo kilihitajiwa; kifo cha wanyama chenye kilikamata nafasi ya Musa, na kifo cha Yesu mwenye alitoa damu yake mwenyewe kwa ajili ya wale wenye wako mu agano jipya.
it-1-F uku. 263-264
Ubatizo
Luka anasema kama Yesu alikuwa anasali wakati alikuwa anabatizwa. (Lu 3:21) Tena, mu barua yake kwa Waebrania Paulo anasema kama wakati Yesu Kristo alikuja “katika ulimwengu” (ni kusema, hapana wakati alizaliwa juu hangeweza kusoma na kusema hii maneno, lakini wakati alitoa maisha yake kwa kubatizwa na kuanza kazi yake ya kuhubiri) alikuwa anasema hivi, kulingana na Zaburi 40:6-8 (LXX): “Haukutamani zabihu na toleo, lakini ulitayarisha mwili kwa ajili yangu. . . . Angalia! Nimekuja (katika kitabu cha kukunjwa imeandikwa juu yangu) Ee Mungu, kufanya mapenzi yako.” (Ebr 10:5-9) Yesu alizaliwa katika taifa la Wayahudi, kwa hiyo alikuwa mwanainchi wa taifa hilo lenye lilikuwa katika agano pamoja na Mungu, ni kusema, agano la Sheria. (Kut 19:5-8; Ga 4:4) Ile inaonyesha kama wakati Yesu aliomba Yohana amubatize, alikuwa tayari katika uhusiano wa agano pamoja na Yehova Mungu. Na ile wakati, alifanya zaidi ya mambo yenye Sheria ilimuomba afanye. Alikuwa anajitoa yeye mwenyewe kwa baba yake, Yehova, ili kufanya “mapenzi” yake: alitoa mwili wake wenye “ulitayarishwa” na kufanya zabihu za wanyama zenye zilikuwa zinatolewa kulingana na Sheria zifikie mwisho. Mutume Paulo anasema hivi: “Kwa ‘mapenzi’ hayo sisi tumetakaswa kupitia toleo la mwili wa Yesu Kristo mara moja kwa wakati wote.” (Ebr 10:10) Kuhusu Yesu, mapenzi ya Baba ilitia ndani pia kazi yenye kuhusu Ufalme, na Yesu alijitoa pia kwa ajili ya ile kazi. (Lu 4:43; 17:20, 21) Yehova alionyesha kama alikubali kujitoa kwa Mwana wake, wakati alimutia mafuta kwa roho takatifu na kusema: “Wewe ni Mwana wangu, mupendwa; nimekukubali.”—Mk 1:9-11; Lu 3:21-23; Mt 3:13-17.
TAREHE 16-22/09
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | WAEBRANIA 11
“Faida ya Kuwa na Imani”
Onyesha Imani Yako Katika Ahadi za Yehova
6 Katika andiko la Waebrania 11:1, Biblia inafasiria maana ya imani. (Soma.) (1) Imani “ni tarajio lililohakikishwa la mambo yanayotumainiwa.” Kati ya mambo yenye ‘tunatumainia’ kuko pia ahadi za Mungu juu ya wakati unaokuja. Kwa mufano, tuko hakika kama mambo ya mubaya yataisha na kama kutakuwa dunia mupya. (2) Imani ni ‘usibitisho ulio wazi,’ ao uhakikisho wenye kusadikisha wa, ‘mambo halisi ingawa hayaonekane.’ Hata kama hatuwezi kuona na macho yetu, tunajua kama Yehova Mungu, Yesu Kristo, na malaika wako kabisa, na pia Ufalme wa mbinguni uko. (Waebrania 11:3) Namna gani tunaweza kuonyesha kama tuko kabisa na imani katika ahadi za Mungu na katika mambo yenye hatuwezi kuona? Tunafanya hivyo kupitia namna tunatumia maisha yetu na kupitia maneno na matendo yetu.
‘Musawabishaji wa Wale Wanaomutafuta kwa Bidii’
Tunaweza kufanya nini ili tumupendeze Yehova? Paulo anaandika hivi: ‘Bila imani haiwezekani kamwe kumupendeza Mungu vema.’ Ona kwamba Paulo haseme kuwa ni vigumu kumupendeza Mungu bila imani. Lakini, mutume Paulo anasema kwamba haiwezekani kumupendeza Mungu bila imani. Kwa maneno mengine, imani ni sifa ya maana sana ili kumupendeza Mungu.
Ni imani ya namna gani ambayo inamupendeza Yehova? Kumuamini Mungu kunapaswa kutia ndani mambo mawili. Jambo la kwanza, ni ‘lazima tuamini kwamba yeye yuko.’ Tafsiri zingine za Biblia zinasema “uamini kwamba yeye ni mutu kwelikweli” na “uamini kwamba yeye yuko.” Namna gani tunaweza kumupendeza Mungu ikiwa tuna mashaka kwamba yeye yuko? Hata hivyo, imani ya kweli inahusisha mambo mengi, kwa sababu hata mashetani wanaamini kwamba Yehova yuko. (Yakobo 2:19) Kuamini kwamba Mungu ni mutu kwelikweli kunapaswa kutuchochea kutenda, ni kusema, kuonyesha imani yetu kwa kuishi maisha ambayo yanamupendeza.—Yakobo 2:20, 26.
Jambo la pili, ni ‘lazima tuamini kwamba’ Mungu ni ‘musawabishaji.’ Mutu ambaye ana imani ya kweli ana uhakika kabisa kwamba bidii yake ya kuishi maisha ambayo yanamupendeza Mungu si ya bure. (1 Wakorintho 15:58) Hatuwezi kumupendeza Yehova ikiwa tuna mashaka juu ya uwezo wake ao nia yake ya kutupatia zawadi. (Yakobo 1:17; 1 Petro 5:7) Mutu ambaye anasema kwamba Mungu hawahangaikie watu, hapendezwe na watu, na kwamba si mukarimu, mutu huyo hamujue Mungu ambaye anazungumuziwa katika Biblia.
Ni nani ambao Yehova anapatia zawadi? Paulo anasema kwamba ni ‘wale wanaomutafuta kwa bidii.’ Kitabu kimoja cha watafsiri wa Biblia kinasema kwamba neno la Kigiriki ambalo linatafsiriwa ‘wanaomutafuta kwa bidii,’ halimaanishe “kuenda kutafuta inje” lakini, linamaanisha kufanya bidii ya kumukaribia Mungu ili “kumuabudu.” Kitabu kingine kinaeleza kwamba neno hilo la Kigiriki linaonyesha nguvu na kufanya bidii nyingi. Ndiyo, Yehova anawapatia zawadi wale ambao imani yao inawachochea kumuabudu kwa moyo wenye kujaa upendo na bidii.—Mathayo 22:37.
Tia Nguvu Imani Yako Katika Mambo Yenye Unatumainia
10 Katika Waebrania sura ya 11, mutume Paulo anasema hivi: “Wanawake waliwapokea wafu wao kwa ufufuo; lakini watu wengine waliteswa kwa sababu hawakukubali kuachiliwa huru kupitia fidia [zabihu ya ukombozi] fulani, ili waupate ufufuo ulio bora.” (Waebrania 11:35) Wengi walivumilia majaribu na waliendelea kuwa washikamanifu kwa Mungu kwa sababu walikuwa na imani yenye nguvu katika tumaini la ufufuo lenye Mungu alikuwa ameahidi. Walijua kama wakati unaokuja, Yehova angewafufua na wangeishi tena milele hapa duniani. Fikiria mufano wa Nabothi na Zekaria. Walipigwa majiwe mupaka kufa kwa sababu walimutii Mungu. (1 Wafalme 21:3, 15; 2 Mambo ya Nyakati 24:20, 21) Danieli alitupwa katika shimo la simba wenye njaa, na marafiki wake walitupwa katika moto wenye kuwaka sana. Walikuwa tayari kufa kuliko kukosa ushikamanifu kwa Yehova. Wanaume hao walikuwa na imani yenye nguvu kuwa Yehova angewapatia roho yake takatifu na kuwasaidia waendelee kuvumilia mateso hayo.—Danieli 3:16-18, 20, 28; 6:13, 16, 21-23; Waebrania 11:33, 34.
11 Manabii wengi, kama vile Mikaya na Yeremia, walizarauliwa na kufungwa katika gereza. Wengine, kama vile Eliya, “walitembea huku na huku katika majangwa na milima na mapango na mashimo ya dunia.” Watu wote hao walivumilia majaribu na waliendelea kuwa washikamanifu kwa Mungu kwa sababu walikuwa na “tarajio lililohakikishwa la mambo yanayotumainiwa.”—Waebrania 11:1, 36-38; 1 Wafalme 18:13; 22:24-27; Yeremia 20:1, 2; 28:10, 11; 32:2.
it-1-F uku. 907-908
Imani
Mifano ya Zamani ya Imani. Kila mutu mwenye Paulo anataja mu ‘wingu kubwa la mashahidi’ (Ebr 12:1) alikuwa na musingi wenye kufaa wa imani. Kwa mufano, Abeli alijua kabisa ahadi ya Mungu kuhusu “uzao” wenye ungeponda kichwa cha “nyoka.” Na alijionea utimizo wa hukumu yenye Yehova alipatia wazazi wake katika Edeni. Inje ya Edeni, Adamu na familia yake walipata chakula kwa jasho kwa sababu Yehova alikuwa amelaani udongo, na laana hiyo ilifanya udongo uzae miiba na michongoma. Inawezekana Abeli aliona namna Eva alitamani sana bwana yake na namna Adamu alimutawala bibi yake. Na bila shaka alikuwa anasikia mama yake iko anazungumuzia maumivu ya mimba. Tena, njia ya kuingia mu shamba la Edeni ilikuwa inachungwa na makerubi na upanga wenye kuwaka. (Mwa 3:14-19, 24) Ile yote ilifanyiza “uhakikisho wenye uko wazi,” wenye ulifanya Abeli aamini kama ni kupitia ‘ahadi ya uzao’ njo watu wangekombolewa. Kwa hiyo, imani ilimusukuma Abeli ‘amutolee Mungu zabihu,’ zabihu yenye ilionekana kuwa ya maana sana kuliko ya Kaini.—Ebr 11:1, 4.
‘Alimupendeza Mungu Vema’
Kwa hiyo, ni katika maana gani Enoko “alihamishwa ili asione kifo”? Inaonekana kwamba, kwa upendo, Yehova alihamisha uzima wa Enoko katika kifo ili maadui wake wasimuue bila huruma. Lakini kwanza Enoko alitolewa ‘ushahidi kwamba alimupendeza Mungu vema.’ Namna gani? Mbele tu ya kifo chake, pengine Enoko alipewa maono kutoka kwa Mungu, yenye yalionyesha dunia yenye kuwa paradiso. Kupitia alama hiyo yenye kuonyesha kwamba Yehova anamukubali, Enoko akalala usingizi katika kifo. Kuhusu Enoko na wanaume na wanawake wengine waaminifu, mutume Paulo aliandika hivi: “Katika imani hawa wote walikufa.” (Waebrania 11:13) Inawezekana kisha hapo maadui wake walitafuta mwili wake, lakini ‘haukupatikana popote,’ pengine Yehova alifanya upotee ili wasiutendee mubaya ao kuutumia katika ibada ya uongo.
TAREHE 23-29/09
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | WAEBRANIA 12-13
“Nizamu—Inaonyesha upendo wa Yehova”
Usitazame “Mambo Yaliyo Nyuma”
18 Shauri nzito. Tuseme nini ikiwa tumechunga kinyongo kwa sababu ya mashauri fulani tuliyopewa zamani? Hilo linaweza kutuumiza na kusumbua akili yetu, na hivyo kutufanya tuvunjike moyo. (Ebr. 12:5) Iwe ‘tunapuuza’ shauri kwa kuwa hatulikubali ao ‘tunazimia’ ao kuregea kwa sababu tunalikubali, na hivyo kulitumia, matokeo ni yaleyale—hatufaidike kabisa na haturekebishwe nalo. Ni vizuri kabisa kufuata maneno ya Sulemani: ‘Shika nizamu; usiiache. Ilinde, kwa maana hiyo ndiyo uzima wako.’ (Met. 4:13) Kama shofere anayetii ishara za barabarani, wewe pia kubali mashauri, tumia mashauri unayopewa, na usonge mbele.—Met. 4:26, 27; Soma Waebrania 12:12, 13.
‘Wakati Wowote Munaposali, Semeni, Baba’
Baba mwenye upendo anawarekebisha watoto wake, kwa sababu anataka wawe watu wazuri. (Waefeso 6:4) Baba huyo habadilike-badilike anapowarekebisha watoto wake, lakini hafanye hivyo kwa ukali. Vilevile, wakati fulani Baba yetu wa mbinguni anaweza kuona kuwa ni jambo la lazima kuturekebisha. Lakini kila mara Mungu anapoturekebisha, anafanya hivyo kwa upendo na upole. Yesu alimuiga Baba yake, kwa sababu hakuwa mukali alipowarekebisha wafuasi wake hata ikiwa wakati fulani hawakutenda kwa haraka waliporekebishwa.—Mathayo 20:20-28; Luka 22:24-30.
Sikiliza Nizamu ili Ukuwe na Hekima
18 Hata kama nizamu inaweza kuleta maumivu, kuko jambo lingine lenye kuleta maumivu hata zaidi, ni kusema, matokeo ya mubaya sana yenye tunaweza kupata kwa sababu ya kukataa nizamu. (Ebr. 12:11) Fikiria mifano mbili, mufano wa Kaini na wa Mufalme Zedekia. Wakati Kaini alichukia sana ndugu yake Abeli na kutaka kumuua, Mungu alimuonya hivi: ‘Kwa nini umewaka hasira na kwa nini uso wako umekunjamana? Ukigeuka utende mema, je, hautainuliwa? Lakini usipogeuka utende mema, kuna zambi inayovizia katika mwingilio, nayo inakutamani wewe. Je, wewe utaishinda?’ (Mwa. 4:6, 7) Kaini hakusikiliza. Kisha akaua ndugu yake. Kwa kweli, Kaini alijiletea yeye mwenyewe maumivu na mateso! (Mwa. 4:11, 12) Ikiwa angesikiliza onyo la Yehova, hangepatwa na mateso hayo yote.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
Kimbia Shindano la Mbio kwa Uvumilivu
11 ‘Wingu kubwa la mashahidi’ halikukuwa tu watu wenye kuangalia, wenye walikaa tu ili kuangalia shindano la mbio, ao ili kuona namna mukimbiaji ao kikundi chenye walipenda sana kinapata ushindi. Lakini, wao pia walikuwa wanakimbia sawa vile wakimbiaji mu shindano la mbio. Na walikimbia mupaka wakapata ushindi. Hata kama wamekufa, wanaweza kuonekana kuwa wakimbiaji wenye uhodari wenye wanaweza kutia moyo wakimbiaji wapya katika shindano hilo la mbio. Wazia namna mukimbiaji angejisikia ikiwa angejua kwamba wakimbiaji wenye uwezo wanamuzunguka, ao wanamuangalia wakati iko anakimbia. Je, hangejikaza kabisa au hata kufanya yote yenye anaweza mu ile shindano? Mashahidi hao wa zamani wangeweza kushuhudia kwamba inawezekana mutu kupata ushindi mu ile shindano ya mufano hata kama iko nguvu namna gani. Kwa hiyo, kuendelea kufikiria mufano wa ‘wingu hilo la mashahidi,’ kungefanya Wakristo Waebrania wa wakati wa mitume wakuwe na uhodari na ‘wakimbie kwa uvumilivu shindano la mbio,’ na sisi pia tunaweza kufanya vile leo.
w89 15/12 uku. 22 fu. 10
Kutoa Zabihu Zenye Zinamupendeza Yehova
10 Kwa hiyo, Waebrania walipaswa kuepuka ‘kupotoshwa na mafundisho mbalimbali na yenye kuwa mageni’ ya wafuasi wa dini ya Kiyahudi. (Wagalatia 5:1-6) ‘Moyo unatiwa nguvu kupitia fazili zenye hazistahiliwe za Mungu’ ili ubakie imara katika kweli, haiko kupitia ile mafundisho. Inawezekana ni kwa sababu watu walibishana juu ya chakula na zabihu, njo maana Paulo alisema kama moyo hautiwe nguvu kupitia “vyakula, vyenye haviletee faida wale wenye wanajishugulisha navyo.” Mutu anapata baraka za kiroho kwa kujitoa kwa Mungu na kukubali bei ya ukombozi, haiko kwa kuhangaikia chakula fulani mu njia yenye haifae ao kushika siku fulani. (Waroma 14:5-9) Tena, zabihu ya Kristo ilifanya zabihu za Walawi zikuwe bila faida yoyote.—Waebrania 9:9-14; 10:5-10.
TAREHE 30/09–6/10
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | YAKOBO 1-2
“Njia Yenye Inaongoza Kwenye Zambi na Kifo”
Jaribu
Mutu anajaribiwa wakati anavutiwa na jambo fulani—zaidi sana jambo la mubaya. Tukamate mufano. Wazia kwamba wakati uko unauza vitu, unaona kitu fulani kizuri. Mara moja wazo la kuiba bila kukamatwa linakuja katika akili yako. Lakini zamiri yako inakukataza! Kwa hiyo, unatosha wazo hilo katika akili na kuondoka. Wakati huo jaribu linapitilia mbali, umelishinda.
MAMBO BIBLIA INASEMA
Kujaribiwa hakufanye ukuwe mutu mubaya. Biblia inasema kwamba sisi wote tunapatwa na majaribu. (1 Wakorintho 10:13) Jambo la maana kabisa ni namna tunatenda wakati tunajaribiwa. Watu fulani wanaendelea kukaza akili yao juu ya tamaa mbaya na siku fulani wanaangukia katika tamaa hiyo. Wengine wanaondoa haraka tamaa hiyo kama kitu kibaya.
‘Kila mutu hujaribiwa kwa kuvutwa na kushawishiwa na tamaa yake mwenyewe.’—Yakobo 1:14.
Jaribu
Biblia inaonyesha hatua zenye zinaongoza kwenye matendo mabaya. Yakobo 1:15 inasema hivi: ‘Tamaa [mbaya] wakati imetunga mimba, huzaa zambi.’ Kwa kifupi, wakati tunaendelea kukaza akili juu ya tamaa mbaya, tunafikia hatua yenye hatuwezi tena kuepuka kutenda kulingana na tamaa hiyo kama vile mwanamuke mwenye mimba anapaswa tu kuzaa. Lakini, tunaweza kuepuka kuwa watumwa wa tamaa mbaya. Tunaweza kuzuia tamaa hizo.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
it-2-F uku. 168 fu. 3
Mwangaza
Yehova ni “Baba wa miangaza ya mbinguni.” (Yak 1:17) Yeye njo “anatoa jua kwa ajili ya mwangaza muchana, sheria za mwezi na nyota kwa ajili ya mwangaza usiku” (Yer 31:35) na tena yeye njo anatoa mwangaza wote wa kiroho. (2Ko 4:6) Sheria yake, maamuzi yake ya hukumu, na neno lake ni mwangaza kwa wale wenye wanakubali viwaongoze. (Zb 43:3; 119:105; Mez 6:23; Isa 51:4) Muandikaji mumoja wa Zaburi alisema hivi: “Kupitia mwangaza wako tunaweza kuona mwangaza.” (Zb 36:9; linganisha na Zb 27:1; 43:3.) Sawa tu vile mwangaza wa jua unaendelea kuongezeka mupaka “muchana kamili,” ni vile pia njia ya wenye haki, yenye inaangaziwa na hekima ya Mungu, inakuwa na mwangaza zaidi na zaidi. (Mez 4:18) Tunatembea katika mwangaza wa Yehova wakati tunafuata njia zake. (Isa 2:3-5) Kwa upande mwingine, wakati mutu anaangalia mambo mu njia yenye haifae au yenye haiko safi, anakuwa mu giza kubwa la kiroho. Njo maana Yesu alisema: “Kama jicho lako ni lenye wivu, mwili wako wote utakuwa wenye giza. Kama mwangaza wenye kuwa ndani yako kwa kweli ni giza, basi giza hilo ni kubwa sana!”—Mt 6:23; linganisha na Kum 15:9; 28:54-57; Mez 28:22; 2Pe 2:14.
it-2-F uku. 162 fu. 7
Sheria
“Sheria ya Kifalme.” Inaitwa “sheria ya kifalme” kwa sababu sawa vile tu mufalme iko mukubwa na ni wa maana sana kuliko watu wenye anaongoza, ni vile pia sheria ya kupenda jirani yako iko kubwa na ni ya maana sana kuliko sheria zingine zote zenye zinahusu uhusiano na watu wengine. (Yak 2:8) Upendo njo ulikuwa musingi wa Agano la Sheria; na “unapaswa kumupenda jirani yako kama wewe mwenyewe” (sheria ya kifalme) ilikuwa ya pili kati ya amri zenye Sheria yote na Manabii vilitegemea. (Mt 22:37-40) Hata kama Wakristo hawako chini ya agano la Sheria, wanaongozwa na sheria ya Mufalme Yehova na Mwana wake, Mufalme Yesu Kristo, kuhusiana na agano jipya.