Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwbr20 Mwezi wa 1 uku. 1-7
  • Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha
  • Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha—2020
  • Vichwa Vidogo
  • TAREHE 6-12/1
  • TAREHE 13-19/1
  • TAREHE 20-26/1
  • TAREHE 27/1–2/2
Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha—2020
mwbr20 Mwezi wa 1 uku. 1-7

Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha

TAREHE 6-12/1

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MWANZO 1-2

“Yehova Anaumba Uzima Katika Dunia”

it-1-F uku. 563 fu. 2-4

Uumbaji

Siku ya Kwanza, wakati Mungu alisema “Kukuwe mwangaza,” kwa kweli mwangaza wenye kutawanyika ulipita ndani ya mawingu, hata kama vitu vyenye kutoa ule mwangaza vilikuwa bado havijaonekana kutoka kwenye uso wa dunia. Inaonekana kama ile ilifanyika hatua kwa hatua, sawa vile mutafsiri, J. W. Watts anaonyesha: “Na hatua kwa hatua kukakuwa mwangaza.” (Mwa 1:3, A Distinctive Translation of Genesis) Mungu alitenganisha mwangaza na giza, akaita mwangaza Muchana na giza Usiku. Ile inaonyesha kama dunia ilikuwa inazunguka kwenye muhimili wake na wakati uleule ilikuwa inazunguka jua, ili pande zake, ni kusema upande wa mashariki na wa mangaribi, zikuwe na vipindi vya mwangaza na giza.​—Mwa 1:3, 4.

Siku ya Pili, Mungu alifanya anga kwa kufanya kukuwe mugawanyiko “kati ya maji na maji.” Maji fulani ilibakia ku dunia, lakini kiasi kikubwa cha maji kilipandishwa juu kabisa ya uso wa dunia, na katikati ya ile maji yenye ilipandishwa na yenye ilibakia kukakuwa anga. Mungu akaita anga Mbingu; lakini ile ilihusiana na dunia, kwa sababu Biblia haiseme kama maji yenye ilipandishwa juu ya anga ilifunika nyota ao vitu vingine vyenye kuwa mbinguni.​—Mwa 1:6-8; ona ANGA.

Siku ya Tatu, kupitia uwezo wa Mungu wenye ulikuwa unafanya miujiza, maji ilikusanywa pamoja, na inchi kavu ikatokea, na Mungu akaita ile inchi kavu Dunia. Pia, ni katika ile siku njo Mungu aliwekea atomu za vitu mbalimbali kanuni za uzima; ile ilifanya majani, mimea, na miti ya matunda vifikie kuwa; vile vitu havikutokea kwa bahati ao kupitia mageuzi. Kila kimoja kati ya vile vitu tatu kilikuwa na uwezo wa kuzaana kulingana na “aina” yake.​—Mwa 1:9-13.

it-1-F uku. 563 fu. 7-10

Uumbaji

Inapendeza pia kujua kama, tendo la Kiebrania ba·raʼʹ, lenye linamaanisha “kuumba,” halitumiwe katika Mwanzo 1:16. Pa nafasi yake, tendo la Kiebrania ʽa·sahʹ, lenye linamaanisha “kufanya,” njo linatumiwa. Kwa kuwa jua, mwezi, na nyota viko katika “mbingu” zenye zinatajwa mu Mwanzo 1:1, ni kusema viliumbwa zamani mbele ya Siku ya Ine. Siku ya Ine, Mungu akaanza “kufanya” vile vitu vikuwe na uhusiano wa mupya kuelekea uso wa dunia na anga lenye kuwa juu yake. Kusema kama, “Mungu akaviweka katika anga la mbingu ili viangazie dunia,” kungeweza kumaanisha kama sasa vilifikia kuonekana kutoka kwenye uso wa dunia, sawa vile vilikuwa katika anga. Tena, vitu vya kutoa mwangaza vilipaswa kutumika kama “alama ya vipindi na siku na miaka,” kisha vingefikia kumuongoza mutu mu njia mbalimbali.​—Mwa 1:14.

Siku ya Tano Mungu aliumba nafsi za kwanza zenye haziko za kibinadamu ku dunia. Mungu hakuumba tu kiumbe kimoja na kupanga kijigeuze na kutokeza aina zingine, lakini kwa nguvu yake aliumba viumbe mingi vyenye uzima. Biblia inasema: “Mungu akaumba viumbe vikubwa vya bahari na viumbe vyote vyenye uzima vyenye kutembea na kujaa katika maji kulingana na aina yavyo na kila kiumbe chenye kuruka na chenye mabawa kulingana na aina yacho.” Kisha Mungu akaona kama vitu vyenye alifanya vilikuwa vya muzuri, kwa hiyo akavibariki na kuviambia “mukuwe wengi,” ile ingewezekana sababu Mungu alipatia vile viumbe vya aina mbalimbali uwezo wa kuzaana “kulingana na aina yao.”​—Mwa 1:20-23.

Siku ya Sita “Mungu akafanya wanyama wa pori kulingana na aina yao na wanyama wa kufugwa kulingana na aina yao na wanyama wote wenye kutambaa kulingana na aina yao.” Ule uumbaji pia ulikuwa wa muzuri, sawasawa na vitu vingine vyote vyenye Mungu alikuwa ameumba.​—Mwa 1:24, 25.

Kuelekea mwisho wa Siku ya Sita ya kazi yake ya uumbaji, Mungu aliumba kiumbe cha aina ya mupya kabisa, cha hali ya juu kupita wanyama hata kama kilikuwa cha hali ya chini kwa kulinganisha na malaika. Kile kiumbe kilikuwa mutu, mwenye aliumbwa kwa mufano wa Mungu na kwa sura yake. Wakati Mwanzo 1:27 inasema hivi kwa kifupi kuhusu mwanadamu: “Mwanaume na mwanamuke [Mungu] aliwaumba,” habari ingine yenye kufanana na ile yenye kuwa mu Mwanzo 2:7-9 inaonyesha kama Yehova Mungu alifanya mwanaume kutoka katika mavumbi ya udongo, akapulizia katika matundu ya pua yake pumuzi ya uzima, na kisha mutu akakuwa nafsi yenye uzima, na Mungu akamupatia chakula na makao yenye kuwa paradiso. Mu hii hali Yehova alitumia vitu vyenye kuwa ku dunia ili kufanya mwanaume, na kisha kumuumba, akafanya mwanamuke kwa kutumia ubavu mumoja wa ule mwanaume, ni kusema, Adamu. (Mwa 2:18-25) Kisha mwanamuke kuumbwa, mutu akakuwa “aina” kamili.​—Mwa 5:1, 2.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

w15 1/6 uku. 5

Sayansi na Maisha Yako

Wakati dunia na ulimwengu vilianza

Wanasayansi wanawaza kama kumepita miaka miliare 4 hivi tangu dunia ilianza, na miaka miliare 13 ao 14 hivi tangu ulimwengu ulianza. Biblia haionyeshe ni wakati gani ulimwengu uliumbwa. Hakuna nafasi inasema kama dunia iko na maelfu fulani tu ya miaka. Andiko la kwanza katika Biblia linasema hivi: “Hapo mwanzo Mungu aliumba mbingu na dunia.” (Mwanzo 1:1) Maneno hayo yanasaidia wanasayansi wakati wanatumia kanuni za sayansi ili kujua ulimwengu ulianza wakati gani.

it-2-F uku. 16-17

Yesu Kristo

Haiko Muumbaji Kama Mungu. Hata kama Mwana alishiriki katika kazi ya uumbaji, ile haikumufanya akuwe Muumbaji kama Baba yake. Uwezo wa kuumba ulitoka kwa Mungu kupitia roho yake takatifu, ao nguvu yake ya utendaji. (Mwa 1:2; Zb 33:6) Na juu Yehova njo Chanzo cha uzima, yeye njo aliumba vitu vyote vyenye uzima, vyenye kuonekana na vyenye havionekane. (Zb 36:9) Kwa hiyo, Mwana hakukuwa Muumbaji kama Mungu lakini alikuwa fundi ao chombo chenye Yehova, Muumbaji, alitumia ili kuumba. Maandiko yote inasema kama Mungu njo Muumbaji, Yesu naye alisema vile.​—Mt 19:4-6; ona UUMBAJI.

Hotuba

w08 1/2 uku. 5

Jinsi Jibu la Biblia Linavyoleta Amani ya Kweli ya Akili

Kujua kwamba “kila familia . . . duniani hupata jina kutokana” na Mungu kunabadili maoni yetu kuhusu watu wengine. (Waefeso 3:15) Kuwa na ujuzi huo pia kunaongoza jinsi tunavyojiona na kuona matatizo yetu. Fikira zetu zitabadilika katika njia zifuatazo.

Tunapokabili maamuzi mazito, hatutahangaishwa kupita kiasi na maoni ya watu yenye kupingana. Badala yake, tutategemea kabisa mashauri ya Biblia. Kwa nini? Kwa sababu “Andiko lote limeongozwa na roho ya Mungu nalo ni lenye faida kwa kufundisha, kwa kukaripia, kwa kunyoosha mambo, kwa kutia nidhamu katika uadilifu, ili mtu wa Mungu awe na uwezo kamili, akiwa na vifaa kamili kwa ajili ya kila kazi njema.”​—2 Timotheo 3:16, 17.

Ni kweli kwamba ili kufuata mashauri ya Biblia tunapaswa kujitahidi na kujitia nidhamu. Nyakati nyingine huenda mwongozo wake ukatulazimu kutenda kwa njia ambazo zinaonekana hazipatani na mwelekeo wetu. (Mwanzo 8:21) Hata hivyo, tukikubali kwamba tuliumbwa na Baba wa mbinguni mwenye upendo, ni jambo linalopatana na akili kukata kauli kwamba anajua njia bora zaidi ambayo tunapaswa kufuata. (Isaya 55:9) Neno lake linatuhakikishia hivi: “Mtegemee Yehova kwa moyo wako wote wala usitegemee uelewaji wako mwenyewe. Mtambue yeye katika njia zako zote, naye atanyoosha mapito yako.” (Methali 3:5, 6) Tukitumia shauri hilo, mahangaiko mengi tunayopata tunapokabili matatizo na maamuzi yatakwisha.

Tunapobaguliwa, hatutalemewa na hisia za kujiona hatufai, na kufikiri kwamba kwa njia fulani hatuna thamani kama watu wa rangi au jamii nyingine. Badala yake, tutajiheshimu kwa usawaziko. Kwa nini? Kwa sababu Baba yetu, Yehova Mungu, “hana ubaguzi, bali katika kila taifa mtu ambaye anamwogopa na kutenda uadilifu anakubalika kwake.”​—Matendo 10:34, 35.

Tukijua hivyo, hatutaruhusu ubaguzi utufanye tuwe na mtazamo mbaya kuelekea watu wengine. Tutaelewa kwamba hatuna sababu yoyote halali ya kujiona kuwa bora kuliko watu wa jamii nyingine, kwa kuwa Mungu “alifanya kutoka kwa mtu mmoja kila taifa la watu, ili wakae juu ya uso wa dunia nzima.”​—Matendo 17:26.

Bila shaka, kujua kwamba tuliumbwa na kwamba Muumba wetu anatujali ni msingi wa kupata amani ya kweli ya akili. Lakini tunahitaji kufanya mengi zaidi ili tudumishe amani ya ndani.

TAREHE 13-19/1

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MWANZO 3-5

“Matokeo ya Mubaya Sana ya Uongo wa Kwanza”

w17.02 uku. 5 fu. 9

Kusudi la Yehova Litatimia!

9 Shetani Ibilisi alitumia nyoka ili kudanganya Eva akose kumutii Baba yake, Yehova. (Soma Mwanzo 3:1-5; Ufunuo 12:9) Kwa sababu watoto wa Mungu wanadamu hawakuruhusiwa kula matunda ya “kila muti wa bustani,” Shetani alifanya jambo hilo lionekane kuwa tatizo. Ni kama vile alikuwa anasema hivi: ‘Ni kusema hamuwezi kufanya mambo yenye munapenda?’ Kisha akamuambia hivi: ‘Hakika hamutakufa.’ Huo ulikuwa uongo. Kisha akajaribu kumusadikisha Eva kama hakukuwa na lazima ya kusikiliza Mungu. Shetani alisema hivi: ‘Kwa maana Mungu anajua kwamba siku ileile mutakapokula matunda yake macho yenu yatafunguliwa.’ Shetani alikuwa anasema kama Yehova hakupenda wakule matunda ya muti huo kwa sababu hilo lingewapatia ujuzi fulani wa pekee. Mwishowe, alitoa ahadi hii ya uongo: ‘Mutakuwa kama Mungu, mukijua mema na mabaya.’

w00 15/11 uku. 25-26

Twaweza Kujifunza Kutokana na Wenzi Wawili wa Kwanza wa Kibinadamu

Je, dhambi ya Hawa haingeweza kuepukika? La hasha! Ebu jiweke katika hali yake. Dai la nyoka lilipotosha kabisa yale ambayo Mungu na Adamu walikuwa wamesema. Ungeonaje ikiwa mtu usiyemjua angedai kwamba mpendwa ambaye unamwamini ni mdanganyifu? Hawa alipaswa kutenda tofauti, alipaswa kuchukizwa na kughadhabishwa, hata kukataa kusikiliza. Kwani, nyoka alikuwa na haki gani kutilia shaka uadilifu wa Mungu na maneno ya mume wake? Kwa kuheshimu kanuni ya ukichwa, Hawa alipaswa kutafuta ushauri kabla ya kufanya uamuzi wowote. Twapaswa kutafuta ushauri vilevile iwapo tunaarifiwa kinyume cha maagizo ya Mungu. Lakini, Hawa aliamini maneno ya yule Mshawishi na kutaka kujiamulia mema na mabaya. Kadiri alivyozidi kutafakari jambo hilo, ndivyo alivyozidi kupendezwa nalo. Jinsi alivyokosea kwa kudumisha akilini tamaa mbaya badala ya kuiondoa ama kuzungumza mambo hayo pamoja na kichwa chake cha jamaa!​—1 Wakorintho 11:3; Yakobo 1:14, 15.

Adamu Amsikiliza Mkewe

Punde si punde Hawa alimshawishi Adamu kujiunga naye katika dhambi. Kwa nini Adamu alikubali kwa urahisi hivyo? (Mwanzo 3:6, 17) Adamu alikabili uchaguzi uliohusisha uaminifu. Je, angemtii Muumba wake, aliyempatia vyote alivyokuwa navyo, kutia ndani Hawa, mwenzi wake mpendwa? Je, Adamu angetafuta mwelekezo wa Mungu kuhusu jambo ambalo angefanya sasa? Au, mwanamume huyo angemwunga mkono mke wake? Bila shaka Adamu alijua kwamba Hawa hangepata kamwe kile alichotarajia kupata kwa kula tunda lililokatazwa. Mtume Paulo alipuliziwa na Mungu kuandika hivi: “Adamu hakudanganywa, bali mwanamke alidanganywa kabisa akaja kuwa katika ukiukaji-sheria.” (1 Timotheo 2:14) Kwa hiyo, Adamu alikataa kimakusudi kumtii Yehova. Hofu ya kutenganishwa na mke wake ilikuwa kubwa kuliko imani yake katika uwezo wa Mungu wa kurekebisha hali hiyo.

w12 1/9 uku. 4 fu. 2

Je, Kweli Mungu Anawahangaikia Wanawake?

Je, wanawake walilaaniwa na Mungu?

Jibu ni hapana. Ni “yule nyoka wa zamani, anayeitwa Ibilisi,” ndiye “amelaaniwa” na Mungu. (Ufunuo 12:9; Mwanzo 3:14) Mungu aliposema kama Adamu ‘atamutawala’ bibi yake, hakumaanisha kama sasa wanaume wanapaswa kuanza kuwaonea wanawake. (Mwanzo 3:16) Mungu alikuwa tu ameona mbele ya wakati matokeo mabaya ambayo zambi itawaletea bibi na bwana wa kwanza.

w04 1/1 uku. 29 fu. 2

Mambo Makuu Kutoka Katika Kitabu cha Mwanzo​—I

3:17​—Udongo ulilaaniwa katika njia gani, na kwa muda gani? Laana iliyotamkwa juu ya udongo ilimaanisha kwamba ingekuwa vigumu sana kuulima. Wazao wa Adamu waliathiriwa sana na matokeo ya kulaaniwa kwa udongo ambao ulitokeza mibaruti kiasi kwamba Lameki, baba ya Noa, alitaja “maumivu ya mikono yetu yanayoletwa na udongo ambao Yehova amelaani.” (Mwanzo 5: 29) Baada ya Gharika, Yehova alimbariki Noa na wanawe na kuwaeleza kusudi Lake kwamba waijaze dunia. (Mwanzo 9:1) Yaonekana laana ya Mungu juu ya udongo iliondolewa.​—Mwanzo 13:10.

it-1-F uku. 672

Maumivu ya Kuzaa

Ni taabu ao mateso ya kuzaa. Kisha Eva, mwanamuke wa kwanza, kufanya zambi, Mungu alimuambia ile ingekuwa na matokeo gani kuhusu kuzaa. Kama angebakia mutiifu, Mungu angeendelea kumubariki na kuzaa kungeleta furaha ya kweli, kwa sababu, “baraka ya Yehova ndiyo inamufanya mutu kuwa tajiri, naye haongeze maumivu yoyote pamoja nayo.” (Mez 10:22) Lakini sasa, kwa sababu ya namna mwili wenye haukamilike unafanya kazi, kwa kawaida kuzaa kungeleta maumivu. Njo maana, Mungu alisema hivi (kama vile mara mingi mambo yenye anaruhusu inaonyeshwa kuwa ni yeye anaifanya): “Nitaongeza sana maumivu ya mimba yako; utazaa watoto kwa maumivu.”​—Mwa 3:16.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

it-2-F uku. 105

Lameki

Maneno yenye Lameki alitunga kwa ajili ya bibi zake (Mwa 4:23, 24) inaonyesha roho ya jeuri yenye ilienea wakati huo. Lameki alisema hivi: “Musikie sauti yangu, ninyi bibi za Lameki; musikilize maneno yangu: Nimemuua mutu mumoja kwa sababu aliniumiza, ndiyo, kijana mwanaume kwa sababu alinipiga. Kama Kaini atalipizwa kisasi mara saba (7), basi Lameki ni mara makumi saba na saba (77).” Kwa kweli Lameki alikuwa anaonyesha kama tendo lake lilikuwa la kujilinda, alionyesha kama hakuua kwa makusudi sawa vile Kaini alifanyaka. Lameki alisema kama, ili kutafuta kujilinda, aliua mutu mwenye alimupiga na kumuumiza. Kwa hiyo, kupitia maneno yake, alikuwa anaomba alindwe ili mutu yeyote asimulipize kisasi kwa sababu alikuwa ameua mutu mwenye alimushambulia.

it-1-F 352

Kutukana Mungu

Kwa kweli, “kuitia jina la Yehova” kwenye kulianza wakati wa Enoko mbele ya Garika, hakukuwa kwa njia yenye kuwa sawa ao yenye kufaa, kwa sababu bila shaka, muda murefu mbele ya pale, Abeli alikuwa anazungumuza na Mungu kwa kutumia jina la Mungu. (Mwa 4:26; Ebr 11:4) Kama vile watu fulani wenye elimu wanaonyesha, ikiwa ile namna ya kuitia jina la Mungu ilikuwa mu maana ya mubaya na ikiwa walitumia jina la Yehova mu njia yenye haifae ili kuzungumuzia wanadamu ao sanamu, basi ile ingekuwa tendo la kumutukana Mungu.​—Ona ENOKO.

TAREHE 20-26/1

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MWANZO 6-8

“Ni Vile Alifanya Kabisa”

w18.02 uku. 4 fu. 4

Uige Imani na Utii wa Noa, Danieli, na Ayubu

4 Magumu yenye Noa alipambana nayo. Kufikia wakati wa Enoko, baba ya tate (nkambo) ya Noa, watu walikuwa wamekuwa wabaya sana. Walikuwa hata wanasema “mambo yote ya kushtua” juu ya Yehova. (Yuda 14, 15) Jeuri iliendelea kuongezeka. Kwa kweli, katika siku za Noa, ‘dunia [ilikuwa] imejaa jeuri.’ Malaika wabaya walivaa miili ya wanadamu, wakachukua wanawake, na kuzaa watoto wenye jeuri wenye hawakukuwa wa kawaida. (Mwa. 6:2-4, 11, 12) Lakini, Noa alikuwa tofauti kabisa. ‘Noa alipata kibali machoni pa Yehova. . . . Alionekana kuwa mutu asiye na kosa kati ya watu wa siku zake. Noa alitembea pamoja na Mungu wa kweli.’​—Mwa. 6:8, 9.

w13 1/4 uku. 14 fu. 1

Noa “Alitembea Pamoja na Mungu wa Kweli”

Kazi ilichukua makumi ya miaka, labda miaka 40 mupaka 50. Kulikuwa miti ya kuangusha, vipande vya miti vya kukokota, kuvikatakata na kuvichonga na hata kuviunganisha pamoja. Safina ilipaswa kuwa na gorofa tatu, vyumba mbalimbali, na mulango kwenye upande wake mumoja. Ni wazi kwamba kulikuwa madirisha kwenye sehemu ya juu, pande zote, na paa ambayo labda ilikuwa yenye kuinuka kidogo katikati na yenye kupakwa lami ndogo ili maji yaweze kuteremuka.​—Mwanzo 6:14-16.

w11 15/9 uku. 18 fu. 13

Kimbia Shindano la Mbio kwa Uvumilivu

13 Ni nini kilichowasaidia watumishi hao wa Yehova kuvumilia na kufanikiwa katika shindano la mbio? Ona yale ambayo Paulo aliandika kumhusu Noa. (Soma Waebrania 11:7.) Kuja kwa “gharika ya maji duniani [ambayo ingeharibu] wote wenye mwili” lilikuwa jambo ambalo Noa ‘alikuwa bado hajaona.’ (Mwa. 6:17) Ni jambo ambalo halikuwa limewahi kutukia kabla ya hapo, jambo la ajabu kabisa. Hata hivyo, Noa hakuwa na shaka au hata kufikiri kwamba gharika haingeweza kuja kamwe. Kwa nini? Kwa sababu alikuwa na imani kwamba jambo lolote ambalo Yehova alisema, angetimiza. Noa hakufikiri kwamba jambo ambalo aliombwa afanye lilikuwa gumu sana. Badala yake, “alifanya vivyo hivyo.” (Mwa. 6:22) Tukifikiria mambo yote ambayo Noa alipaswa kufanya, yaani, kujenga safina, kukusanya wanyama, kujaza chakula ndani ya safina kwa ajili ya wanadamu na wanyama, kuhubiri ujumbe wa kuonya, na kujenga hali ya kiroho ya familia yake, haikuwa rahisi kwake kufanya “vivyo hivyo.” Hata hivyo, imani ya Noa na uvumilivu wake uliokoa uhai na kumletea yeye na familia yake baraka nyingi.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

w04 1/1 uku. 29 fu. 7

Mambo Makuu Kutoka Katika Kitabu cha Mwanzo​—I

7:2​—Ni nini kilichotumiwa kutofautisha wanyama safi na wasio safi? Yaonekana njia ya kutofautisha wanyama safi na wasio safi ilitegemea dhabihu zilizotolewa katika ibada, bali si kama mnyama huyo alifaa kuliwa au la. Mwanadamu hakuwa akila nyama kabla ya Gharika. Maneno “safi” na “-sio safi” yalianza kutumiwa kuhusu chakula katika Sheria ya Musa tu, nayo yaliacha kutumiwa sheria hiyo ilipokoma. (Matendo 10:9-16; Waefeso 2:15) Yaonekana, Noa alijua ni mnyama yupi aliyefaa kutolewa dhabihu katika ibada ya Yehova. Mara tu alipotoka katika safina, Noa ‘alimjengea Yehova madhabahu na kuchukua baadhi ya wanyama wote walio safi na baadhi ya viumbe wote wanaoruka ambao ni safi, akatoa matoleo ya kuteketezwa juu ya ile madhabahu.’​—Mwanzo 8:20.

w04 1/1 uku. 30 fu. 1

Mambo Makuu Kutoka Katika Kitabu cha Mwanzo​—I

7:11​—Maji yaliyosababisha Gharika duniani pote yalitoka wapi? Katika kipindi cha pili, au “siku” ya pili ya uumbaji, wakati “anga” la dunia lilipofanywa, kulikuwa maji “yaliyo chini ya anga” na maji “yaliyo juu ya anga.” (Mwanzo 1:6, 7) Maji yaliyokuwa “chini” ni yale ambayo tayari yalikuwa duniani. Maji yaliyokuwa “juu” ni unyevunyevu mwingi uliokuwa angani juu ya dunia, ambao ulifanyiza “kilindi kikubwa cha maji.” Maji hayo yote yalimwagika juu ya dunia katika siku za Noa.

TAREHE 27/1–2/2

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MWANZO 9-11

“Dunia Yote Iliendelea Kuwa na Luga Moja”

it-1-F uku. 255

Babiloni Mukubwa

Namna Bibiloni ya Zamani Ilikuwa. Muji wa Babiloni ulianzishwa katika Bonde la Shinari wakati wenye watu walijaribu kujenga Munara wa Babeli. (Mwa 11:2-9) Sababu ya kujenga ule Munara na ule muji haikukuwa kutukuza jina la Mungu, lakini wajenzi walikuwa na kusudi la ‘kujifanyia jina kubwa.’ Minara ya ziggourat yenye imevumbuliwa mu mabomoko ya Babiloni ya zamani na pia mu maeneo ingine ya Mesopotamia inaweza kuhakikisha kama ule munara wa Babeli ulikuwa wa kidini, hata kama ulikuwa na umbo gani ao ulijengwa namna gani. Tendo la Yehova la kusimamisha kazi ya kujenga hekalu linaonyesha wazi kama ile kazi ilichochewa na dini ya uongo. Hata kama jina la Kiebrania la muji huo, ni kusema Babeli, linamaanisha “Muvurugo,” jina la Kisumeri la muji huo (Ka-dingir-ra) na jina lake la Kiakadi (Bab-ilu), yote mbili inamaanisha “Mulango Mukubwa wa Mungu.” Kwa hiyo, wakaaji wenye walibakia katika muji walibadilisha muundo wa jina la muji huo ili kuepuka maana ya kwanza yenye kulaumika, lakini muundo mupya wa jina hilo uliendelea kuhusianisha muji huo na dini.

it-2-F uku. 111 fu. 6

Luga

Habari yenye kuwa katika Mwanzo inaonyesha kama watu fulani wenye waliishi kisha Garika walijiunga pamoja ili kufanya kazi yenye ilipingana na mapenzi ya Mungu, kama vile alikuwa ameambia Noa na watoto wake wanaume. (Mwa 9:1) Kuliko kusambaa na ‘kujaza dunia,’ waliazimia kufanya wanadamu wote waishi fasi moja, fasi yenye ilifikia kuitwa Bonde la Shinari katika Mesopotamia. Kwa kweli, ile ingefikia kuwa pia mahali pakubwa pa ibada, kwenye kungekuwa munara wa kidini.​—Mwa 11:2-4.

it-2-F uku. 111 fu. 7

Luga

Mungu Mweza-Yote, alisimamisha ule mupango wenye kuchochewa na kiburi kwa kuvunja umoja wao katika namna ya kufanya kazi; alifanya vile kwa kuvuruga luga yenye watu wote walikuwa wanazungumuza. Ile ilifanya wasiweze kuongoza kazi yoyote ili kutimiza mupango wao na ilifanya wasambae mu maeneo yote ya dunia. Muvurugo wa luga zao ungezuia pia maendeleo ya wakati wenye kuja ya kufuata njia ya mubaya ya kumupinga Mungu, ao ungefanya ile maendeleo ikuwe polepole, kwa sababu ingekuwa nguvu kwa wanadamu kuunganisha uwezo wao wa kiakili na wa kimwili ili kutimiza mipango ya kujitafutia makubwa. Tena, ule muvurugo ungefanya ikuwe nguvu kutumia ujuzi wenye vikundi mbalimbali vya luga vyenye viliundwa vilikuwa vimepata​—haiko ujuzi wenye kutoka kwa Mungu, lakini wenye walikuwa wamepata kupitia utafiti mbalimbali wa wanadamu. (Linganisha na Muh 7:29; Kum 32:5.) Kwa hiyo, hata kama muvurugo wa luga ulikuwa jambo kubwa lenye lilileta mugawanyiko kati ya wanadamu, uliletea wanadamu faida juu ulifanya mipango ya mubaya na yenye kuwa hatari isitimie. (Mwa 11:5-9; linganisha na Isa 8:9, 10.) Kufikiria ao kuona tu maendeleo fulani mu siku zetu yenye kutokana na ujuzi wa ulimwengu wenye watu wamepata na namna wanautumia mubaya, kunatusaidia kuelewa mambo yenye Mungu aliona mbele ya wakati kuwa ingetokea ikiwa angeruhusu kazi ya kujenga Babeli iendelee.

it-2-F uku. 375

Mataifa

Watu walikuwa wametenganishwa kwa sababu hawangeweza tena kuzungumuza luga moja. Kwa hiyo, kila kikundi cha luga kilifikia kuwa na desturi yake, ufundi wake, tabia yake, na dini yake​—kila kikundi kilifikia kuwa na namna yake ya kufanya mambo. (Law 18:3) Kwa sababu watu wa vikundi mbalimbali walikuwa wametanganishwa na Mungu, walitengeneza sanamu mingi za miungu yao ya uongo.​—Kum 12:30; 2Fal 17:29, 33.

it-1-F uku. 421 fu. 4

Hamu

Inawezekana kama Kanaani alihusika moja kwa moja katika jambo hilo na kama Hamu, baba yake, hakumurekebisha. Ao Noa, kwa kuongozwa na roho ya Mungu ili kusema kwa njia ya unabii, aliona mbele ya wakati kama wazao wa Kanaani wangeriti mwelekeo mubaya wa Hamu wenye pengine ulikuwa tayari umeonekana kwa mutoto wake Kanaani. Ile laana ilitimia kwa sehemu fulani wakati Waisraeli wenye walikuwa wazao wa Shemu walipata ushindi juu ya Wakanaani. Wakanaani wenye hawakuharibiwa (kama vile Wagibeoni [Yos 9]) walifanywa kuwa watumwa wa Israeli. Kisha mamia ya miaka, ile laana ilitimizwa zaidi wakati wazao wa Kanaani, mutoto wa Hamu, walianza kutawaliwa na Mamlaka makubwa ya wazao wa Yafeti, ni kusema, Umedi na Uajemi, Ugiriki, na Roma.

it-2-F uku. 403

Nimrodi

Ku mwanzo wa ufalme wake, Nimrodi alitawala miji ya Babeli, Ereki, Akadi, na Kalne, ile miji yote ilikuwa mu inchi ya Shinari. (Mwa 10:10) Kwa hiyo, inawezekana ni chini ya uongozi wake njo kazi ya kujenga Babeli na munara wa Babeli ilianza. Ile maelezo inapatana na mawazo ya zamani ya Wayahudi. Yosefo aliandika hivi: “Pole kwa pole [Nimrodi] aligeuza namna mambo ilikuwa na kuanzisha utawala wa kinguvu, alionyesha kama njia moja tu ya kufanya watu waache kumuogopa Mungu ni kuwafanya waendelee kutegemea nguvu yake yeye. Alisema kama atalipiza Mungu kisasi kama anaharibu tena dunia kwa maji; kwa sababu angejenga munara murefu sana wenye maji haingeweza kufikia na kama angelipiza kisasi kwa ajili ya kuharibiwa kwa mababu zao. Watu walikuwa tayari kufuata mashauri ya [Nimrodi], kwa kuwaza kama kumutii Mungu ni utumwa; kwa hiyo walianza kujenga munara . . . na ulipanda haraka sana mu njia yenye haikuwaziwa.”​—Antiquités judaïques, I, 114, 115 (IV, 2, 3).

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine