Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwbr20 Mwezi wa 11 uku. 1-8
  • Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha
  • Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha—2020
  • Vichwa Vidogo
  • TAREHE 2-8/11
  • TAREHE 9-15/11
  • TAREHE 16-22/11
  • TAREHE 23-29/11
  • TAREHE 30/11–6/12
Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha—2020
mwbr20 Mwezi wa 11 uku. 1-8

Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha

TAREHE 2-8/11

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | KUTOKA 39-40

“Musa Alifuata Maagizo kwa Uangalifu Kabisa”

w11 15/9 uku. 27 fu. 13

Je, Yehova Anakujua?

13 Kwa upande mwingine, Musa alikuwa “mpole zaidi kuliko watu wote waliokuwa juu ya uso wa nchi.” (Hes. 12:3) Alionyesha upole na unyenyekevu wake kwa kuazimia kufuata mwongozo wa Yehova. (Kut. 7:6; 40:16) Hakuna jambo linaloonyesha kwamba Musa alitilia shaka mara nyingi njia ya Yehova ya kufanya mambo au akakasirika kwa sababu ya kulazimika kufuata maagizo ambayo Yehova alitoa. Kwa mfano, Yehova alitoa amri na maagizo madogo-madogo ambayo yangetumiwa kujenga maskani, kama vile rangi ya uzi na hesabu ya vitanzi ambavyo vingetumiwa kutengeneza vitambaa vya mahema. (Kut. 26:1-6) Ikiwa mwanadamu ambaye ni mwangalizi katika tengenezo la Yehova anakupatia maagizo ambayo yanaonekana kuwa na mambo mengi kupita kiasi, huenda nyakati fulani ukavunjika moyo. Hata hivyo, Yehova ni mwangalizi mkamilifu, ambaye anawapa wengine mapendeleo kwa ukarimu na anawaamini watumishi wake. Anapotoa maagizo mengi, anafanya hivyo akiwa na sababu nzuri. Hata hivyo, ona kwamba Musa hakumkasirikia Yehova kwa sababu ya kumpa maagizo mengi, kana kwamba Yehova alimdharau au kumzuia asitumie uwezo wake wa kufikiri au kumnyima uhuru. Badala yake, Musa alihakikisha kwamba wafanyakazi “walifanya vivyo hivyo” katika kufuata miongozo ya Mungu. (Kut. 39:32) Alionyesha unyenyekevu kama nini! Musa alitambua kwamba ilikuwa kazi ya Yehova na kwamba alikuwa tu chombo cha kutumiwa kufanya kazi hiyo.

w05-SW 15/7 uku. 27 fu. 3

Je, Wewe Ni Mwaminifu Katika Mambo Yote?

3 Andiko la Waebrania 3:5 linasema hivi: “Musa akiwa mtumishi alikuwa mwaminifu.” Ni nini kilichomfanya nabii Musa awe mwaminifu? Katika kazi ya kujenga na kusimamisha ile maskani, ‘Musa alifanya kulingana na yote ambayo Yehova alikuwa amemwamuru. Alifanya vivyo hivyo.’ (Kutoka 40:16) Sisi waabudu wa Yehova tunaonyesha uaminifu kwa kumtumikia huku tukiwa watiifu. Bila shaka hilo linamaanisha kuendelea kuwa washikamanifu kwa Yehova tunapokabili majaribu makali. Hata hivyo, uaminifu wetu hauonyeshwi tu tunapokabili majaribu makali. Yesu alisema hivi: “Mtu aliye mwaminifu katika lililo dogo zaidi ni mwaminifu katika lililo kubwa pia, na mtu ambaye si mwaminifu katika lililo dogo zaidi si mwaminifu katika lililo kubwa pia.” (Luka 16:10) Tunapaswa kuwa waaminifu hata katika mambo yanayoonekana kuwa madogo.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

it-2-F 510

Ngozi ya sili

Waisraeli waliipata namna gani. Kama neno la Biblia taʹchash linamaanisha aina fulani ya sili, tunaweza kujiuliza namna gani Waisraeli walipata ngozi za sili. Hata kama inasemekana kama kwa kawaida sili wanapatikana katika maeneo ya Aktiki na Antaktiki, sili fulani wanapenda kuishi fasi kwenye kuwa kivukutu. Leo sili-watawa wangali wanaishi sehemu fulani za Bahari ya Mediterania. Watu wanaendelea kupunguza hesabu za wale wanyama. Inaonekana kama zamani wale wanyama wakuwa wengi mu Bahari ya Mediterania na Bahari Nyekundu. Tena mu 1832, diksionere moja ya Kiingereza Calmet’s Dictionary of the Holy Bible (uku. 139) ilisema hivi: “Wanyama wengi wenye kuitwa sili wanapatikana mu visiwa vidogo mu Bahari nyekundu pembeni ya maeneo yenye kuzungukwa na maji yenye kuitwa péninsule du Sinaï.”​—Ona pia The Tabernacle’s Typical Teaching, by A. J. Pollock, Londres, p. 47.

w15 15/7 uku. 21 fu. 1

Je, Ni Lazima Wengine Watambue Kazi Yako?

Maskani ilipokamilika, wingu “likaanza kufunika hema la mkutano, na utukufu wa Yehova ukaijaza maskani.” (Kut. 40:34) Huo ulikuwa uthibitisho ulio wazi wa kibali cha Yehova! Unafikiri Bezaleli na Oholiabu walihisije wakati huo? Ingawa majina yao hayakuandikwa kwenye vyombo walivyotengeneza, waliridhika sana kwa kujua kwamba Mungu alibariki jitihada zao zote. (Met. 10:22) Katika miaka iliyofuata, walifurahi sana kuona vitu walivyotengeneza vikiendelea kutumiwa katika utumishi wa Yehova. Watakapofufuliwa katika ulimwengu mpya, bila shaka Bezaleli na Oholiabu watafurahi sana kujua kwamba maskani ilitumiwa kwa ajili ya ibada ya kweli kwa miaka 500 hivi!

Hotuba

w16.04 uku. 23-24 fu. 8-10​—Usijiingize Katika Mambo ya Politike ya Ulimwengu huu Wenye Kugawanyika

8 Njia ya pili yenye tunaepuka kujiingiza katika mambo ya politike ya ulimwengu ni kuwa ‘wenye kujihazari [waangalifu] kama nyoka na hata hivyo wasio na hatia [wasio na kosa] kama njiwa.’ (Soma Mathayo 10:16, 17.) Tuko ‘wenye kujihazari’ wakati tunafikiria mbele ya wakati hali zenye hatari. Na tuko “wasio na hatia” wakati hatuache hali hizo zituingize katika mambo ya politike. Tuzungumuzie basi hali fulani zenye hatari na mambo yenye tunaweza kufanya ili tusijiingize kabisa katika mambo ya politike.

9 Mazungumuzo. Tunapaswa kuwa waangalifu sana wakati watu wanaanza kuzungumuzia mambo ya politike. Kwa mufano, wakati tunazungumuza na mutu fulani juu ya Ufalme wa Mungu, tutaepuka kusema kama tunakubaliana ao tunakataa mawazo ya mukubwa fulani wa politike ao ya chama fulani cha politike. Kuliko kuzungumuzia mambo yenye wanadamu wanapenda kufanya ili kumaliza magumu ya wanadamu wenzao, tunatumia Biblia ili kuonyesha mambo yenye Ufalme wa Mungu utafanya ili kumaliza kabisa magumu hayo. Ikiwa watu wanabishana juu ya mambo kama vile, ndoa ya mwanaume na mwanaume ao mwanamuke na mwanamuke, ao kutosha mimba, tunawaambia mambo yenye Neno la Mungu linasema na namna tunajikaza kutumikisha mambo hayo katika maisha yetu. Wakati mutu fulani anasema kama sheria fulani zinapaswa kuondoshwa ao kubadilishwa, hatumuunge mukono, na hatumukaze abadilishe mawazo yake.

10 Vyombo vya kutangaza habari. Wakati fulani, habari inatolewa katika njia yenye kuunga kabisa mukono upande fulani. Jambo hilo linafanyika zaidi sana katika inchi kwenye serikali inaongoza vyombo vya kutangaza habari. Ikiwa shirika fulani ao watangazaji wa habari wanaunga mukono upande fulani, tunapaswa kuwa waangalifu tusianze kufikiri kama wao. Kwa mufano, ujiulize hivi, ‘Ninafurahia kusikiliza mutangazaji wa habari fulani kwa sababu ninakubaliana na mambo yenye anasema juu ya politike?’ Ili kukusaidia usijiingize katika mambo ya politike, epuka kufuata ao kusoma habari zenye kuunga mukono upande fulani katika mambo ya politike. Lakini, ujikaze kutafuta habari zenye haziunge mukono upande fulani. Na sikuzote linganisha mambo yenye unasikia na “maneno yenye afya” yenye kupatikana katika Biblia.​—2 Timotheo 1:13.

TAREHE 9-15/11

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MAMBO YA WALAWI 1-3

“Kusudi ya Matoleo”

it-2-F uku. 847 fu. 1

Matoleo

Matoleo ya kuteketezwa. Matoleo ya kuteketezwa ilitolewa yote ya muzima kwa Mungu; mwenye kutoa hakubakia na sehemu yoyote ya munyama mwenye alitolewa. (Ona Amu 11:30, 31, 39, 40.) Toleo la kuteketezwa ilikuwa ombi kwa Yehova, ya kuonyesha kama alikubali ile zabihu kwa ajili ya zambi yenye ilifanywa. Na njo vile Yesu “toleo la uteketezwa” alifanya, alijitoa wote, kikamili kwa Yehova.

it-2-F uku. 849 fu. 7

Matoleo

Matoleo ya nafaka. Matoleo ya nafaka ilitolewa pamoja na matoleo ya ushirika, matoleo ya kuteketezwa na matoleo kwa ajili ya zambi, lakini kama vile matunda ya kwanza, wakati ingine kila toleo ilitolewa wakati wake. (Kut 29:40-42; Law 23:10-13, 15-18; Hes 15:8, 9, 22-24; 28:9, 10, 20, 26-28; sura 29) Waisraeli walitoa ile matoleo ili kumushukuru Mungu juu ya namna aliwabariki na kuwasaidia wakuwe na maisha ya muzuri. Mara mingi walitoa ile matoleo pamoja na mafuta na ubani. Matoleo ya nafaka ilikuwa ya aina tofauti-tofauti. Ilikuwa ya unga, nafaka yenye kukaangwa, ao keki ya muviringo ao keki yenye kuchomwa, ao yenye kutayarishwa kwenye kikaangio ao katika chungu ya kukaangia. Sehemu fulani ya matoleo ya nafaka ilitiwa ku mazabahu ya toleo la kuteketezwa, makuhani walikula sehemu ingine, na kama ilikuwa matoleo ya ushirika, mutu mwenye alitoa naye pia alishiriki kwa ile matoleo. (Law 6:14-23; 7:11-13; Hes 18:8-11) Matoleo ya nafaka haikupaswa kuwa na chachu ao “asali” (neno lenye kumaanisha pengine maji ya tini ao ya matunda) yenye inaweza kuichachusha.​—Law 2:1-16.

it-2-F 847 fu. 5

Matoleo

Matoleo ya ushirika (ao ya amani). Matoleo ya ushirika yenye Yehova alifurahia ilimaanisha kuwa na amani pamoja na Mungu. Mwabudu na watu wa nyumba yake walipaswa kuwa pale wakati iko inatolewa (kuwa mu kiwanja cha tabenakulo; kulingana na desturi, vibanda vilijengwa pembeni ya pazia yenye ilifunika kile kiwanja; mu hekalu mulikuwa vyumba vya kulia). Kuhani mwenye alisimamia ile kazi, alipata pia sehemu ya ile toleo. Na makuhani wengine wenye walitumika naye walipata sehemu yao. Na mu maana fulani Yehova alifurahia harufu ya moshi ya mafuta ya wanyama wenye walichomwa. Damu, yenye kufananisha uzima, ilitolewa kwa Mungu kuwa yake. Kwa hiyo, ilikuwa sawa vile Yehova, makuhani, na waabudu wake walikuwa wanakula chakula pamoja yenye ilikuwa inamaanisha urafiki wa amani. Kila mutu mwenye angetumia ile chakula wakati wenye alikuwa muchafu (uchafu wowote wenye ulizungumuziwa katika Sheria) ao mwenye angekula nyama kisha wakati wenye ilipaswa kukuliwa (wakati wa kivukutu ilianza kuoza) alipaswa kuondolewa katikati ya watu wake. Mutu wa vile alichafua chakula, pengine sababu alikuwa muchafu ao sababu alikula chakula yenye Mungu aliona kuwa ya kuharibika; ile ilionyesha kama alizarau mambo matakatifu.​—Law 7:16-21; 19:5-8.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

w04-SW 15/5 uku. 22 fu. 1

Mambo Makuu Katika Kitabu cha Mambo ya Walawi

2:13​—Kwa nini chumvi ilipaswa kutolewa “pamoja na kila toleo”? Hiyo haikufanywa ili kuboresha ladha ya dhabihu. Chumvi hutumiwa duniani kama kihifadhi. Yaelekea ilitolewa pamoja na matoleo kwa sababu inawakilisha kutoharibika au kutooza.

it-1-F 1003

Mafuta

Sababu ya kuwa ya ile sheria. Kulingana na agano la Sheria, damu na mafuta vilionekana kuwa vya Yehova tu. Mu damu njo muko uzima, na ni Yehova tu njo anaweza kupatia uzima, kwa hiyo ni yake. (Law 17:11, 14) Mafuta njo ilionekana kuwa sehemu ya muzuri sana ya munyama. Kwa hiyo, mutu mwenye aliitoa, alionyesha kama alijua muzuri kama sehemu za muzuri ni za Yehova, mwenye anatoaka kwa uwingi, na ile ilionyesha kama alikuwa na nia ya kumutolea Mungu kitu ya muzuri sana. Kwa kuwa mafuta ilifananisha toleo ya muzuri sana yenye Waisraeli walimutolea Yehova, ilisemwa kama moshi ya ile mafuta ilikuwa kama “chakula” na ilikuwa na “harufu ya muzuri” kwake. (Law 3:11, 16) Kwa hiyo, mwenye alikula ile sehemu ya mafuta alijichukulia haki ya Yehova na alipaswa kuuawa. Lakini, tofauti na damu, mafuta ingetumiwa mu mambo ingine, kwa mufano kama ilitoka mu munyama mwenye alijikufia ao mwenye aliuawa na munyama mwingine.​—Law 7:23-25.

w04-SW 15/5 uku. 22 fu. 2

Mambo Makuu Katika Kitabu cha Mambo ya Walawi

3:17. Kwa kuwa mafuta yalionwa kuwa sehemu iliyo bora zaidi, yaelekea Waisraeli walikatazwa wasiyale ili wapate kuelewa kwamba sehemu iliyo bora ilikuwa ya Yehova. (Mwanzo 45:18) Hiyo inatukumbusha kwamba ni lazima tumpe Yehova kilicho bora zaidi.​—Mezali 3:9, 10; Wakolosai 3:23, 24.

TAREHE 16-22/11

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MAMBO YA WALAWI 4-5

“Umutolee Yehova Kitu ya Muzuri Zaidi”

it-2-F uku. 848 fu. 12

Matoleo

Matoleo ya hatia. Matoleo ya hatia ilikuwa pia matoleo yenye ilitolewa juu ya zambi fulani, kwa sababu hatia yoyote inaonyesha kama kulikuwa zambi. Ile matoleo iliombwa kuhusiana na zambi fulani za pekee zenye zilifanya mutu akuwe na hatia, na ilikuwa tofauti kidogo na matoleo ingine ya zambi yenye ilikuwa inaomba tu kutengeneza mambo kuhusiana na haki fulani ya mutu yenye ilivunjwa; ikuwe ni haki ya Yehova ao ya taifa lake takatifu. Matoleo ya hatia ilikuwa na kusudi ya kutengeneza mambo kama haki ya Yehova ilivunjwa, ao kusaidia mutenda-zambi mwenye kutubu aepuke matokeo yenye ilitokana na haki fulani za agano na aondolewe nizamu yenye inalingana na zambi yake.​—Ona Isa 53:10.

w09-SW 1/6 uku. 26 fu. 3

Anafikiria Kupungukiwa Kwetu

Kwa kuwa Sheria ilitegemea huruma za Yehova, ilisema hivi: “Ikiwa hana uwezo wa kutoa kondoo, basi atamletea Yehova njiwa-tetere wawili au hua wawili wachanga wawe toleo lake la hatia kwa ajili ya dhambi ambayo ametenda, mmoja kwa ajili ya toleo la dhambi na mmoja kwa ajili ya toleo la kuteketezwa.” (Mstari wa 7) Maneno “ikiwa hana uwezo” yanaweza pia kusemwa “ikiwa mkono wake haungeweza kufikia.” Ikiwa Mwisraeli alikuwa maskini hivi kwamba hangeweza kununua kondoo, basi Mungu alifurahi kupokea kitu ambacho mtoaji angeweza kufikia​—njiwa-tetere wawili au hua wawili.

w09-SW 1/6 uku. 26 fu. 4

Anafikiria Kupungukiwa Kwetu

Lakini namna gani ikiwa mtu huyo hangeweza hata kununua ndege hao wawili? “Basi ataleta sehemu ya kumi ya efa [vikombe nane au tisa] ya unga laini kwa ajili ya toleo la dhambi,” Sheria ilisema. (Mstari wa 11) Kwa ajili ya maskini, Yehova alikubali kwamba toleo la dhambi litolewe bila damu. Katika Israeli, umaskini haukumzuia mtu yeyote asipate baraka ya kupatanishwa au pendeleo la kurudisha amani kati yake na Mungu.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

w16.02 uku. 30 fu. 14

Uige Mufano wa Watumishi Waaminifu wa Yehova

14 Wewe pia unaweza kubakia muaminifu kwa Yehova kwanza, na kwa wengine kwa kuwatendea kwa upole. Kwa mufano, pengine unajua muzuri kwamba ndugu ao dada fulani amefanya zambi nzito. Unaweza kupenda ubakie muaminifu kwake, zaidi sana ikiwa yeye ni rafiki yako wa sana ao mutu wa familia. Lakini, unajua pia kwamba jambo la lazima zaidi ni kubakia muaminifu kwa Yehova. Kwa hiyo, uige mufano wa Nathani kwa kumutii Yehova na kumutendea ndugu ao dada yako kwa upole. Umuambie kama anapaswa kuzungumuza na wazee bila kukawia na kutafuta musaada wao. Ikiwa hafanye hivyo, unapaswa sasa kuwaambia wazee. Ikiwa unafanya hivyo, utaonyesha kwamba uko muaminifu kwa Yehova. Pia, unamutendea ndugu ao dada yako kwa wema kwa sababu wazee wanaweza kumusaidia akuwe tena na urafiki muzuri pamoja na Yehova. Watamushauria kwa wema na upole.​—Soma Mambo ya Walawi 5:1; Wagalatia 6:1.

it-2-F uku. 861 fu. 8

Utakatifu

Wanyama na Mazao. Yehova aliona ngombe-dume, mwana-kondoo dume, na mbuzi dume wenye ni wazaliwa wa kwanza kuwa watakatifu na haikuruhusiwa kuwakomboa. Walipaswa kutolewa kuwa zabihu, na sehemu fulani ilipaswa kupewa makuhani wenye walikuwa watakatifu. (Hes 18:17-19) Matunda ya kwanza na sehemu ya kumi vilikuwa vitakatifu, sawasawa tu na vile zabihu na zawadi zote zilitakaswa kwa ajili ya utumishi katika patakatifu. (Kut 28:38) Vitu vyote vyenye Yehova aliona kuwa vitakatifu, vilipaswa kuonwa kuwa vya maana na havikupaswa kutumiwa mubaya ao kutumiwa mu mambo tu ya kawaida. Mufano wenye unahakikisha ile ni sehemu ya kumi. Kulingana na Sheria, mutu fulani angetia pembeni kitu fulani ili kikuwe sehemu ya kumi, ni kusema, kitu sawa vile sehemu fulani ya mavuno ya ngano, na kisha yeye mwenyewe ao mutu mwingine anabeba ile ngano bila kujua na anaipika, alikuwa na hatia ya kuvunja Sheria ya Mungu kuhusiana na vitu vitakatifu. Kulingana na sheria, alipaswa kuenda mahali patakatifu na kulipa kiasi ileile ya kitu chenye alitumia na kuongeza asilimia 20 ya malipo (20 %), kisha alipaswa kutoa kondoo-dume mwenye hana kasoro wa kundi akuwe zabihu. Njo maana, kila mutu alipaswa kuheshimia sana vitu vitakatifu vyenye vilitolewa kwa Yehova.​—Law 5:14-16.

TAREHE 23-29/11

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MAMBO YA WALAWI 6-7

“Tuonyeshe Shukrani”

w19.11 uku. 22 fu. 9

Mambo Yenye Kitabu cha Mambo ya Mambo ya Walawi Kinatufundisha

9 Jambo la pili: Tunamutumikia Yehova juu tuko wenye shukrani kwake. Ili kukazia jambo hilo, tuzungumuzie matoleo ya ushirika, sehemu ingine ya maana ya ibada ya kweli katika Israeli ya zamani. Katika kitabu cha Mambo ya Mambo ya Walawi, tunajifunza kama Mwisraeli angetoa zabihu ya ushirika ili “kuonyesha shukrani.” (Law. 7:11-13, 16-18) Hakukuwa anatoa toleo hilo juu alilazimishwa kufanya vile, lakini juu alipenda kufanya vile. Kwa hiyo, toleo hilo lilikuwa la kujipendea lenye mutu alikuwa anatoa kwa sababu alimupenda Yehova, Mungu wake. Mutu mwenye alitoa toleo hilo, familia yake, na makuhani walikuwa wanakula nyama ya munyama mwenye alitolewa kuwa zabihu. Lakini sehemu fulani za munyama wa zabihu zilikuwa zinatolewa tu kwa Yehova. Ni sehemu gani?

w00-SW 15/8 uku. 15 fu. 15

Dhabihu Zilizompendeza Mungu

15 Toleo jingine la hiari lilikuwa dhabihu ya ushirika, ambayo yafafanuliwa katika kitabu cha Mambo ya Mambo ya Walawi sura ya 3. Dhabihu ya ushirika yaweza pia kutafsiriwa kuwa “dhabihu ya matoleo ya amani.” Katika Kiebrania, neno “amani” lamaanisha mengi zaidi ya kutokuwa na vita au machafuko. “Katika Biblia, lamaanisha hivyo, na pia lamaanisha hali au uhusiano wenye amani pamoja na Mungu, ufanisi, shangwe, na furaha,” chasema kitabu Studies in the Mosaic Institutions. Hivyo, dhabihu za ushirika zilitolewa si kwa ajili ya kupata amani pamoja na Mungu, kana kwamba kumtuliza, bali ili kushukuru au kusherehekea kwa sababu ya hali nzuri ya amani pamoja na Mungu ambayo hufurahiwa na wale wanaokubaliwa naye. Makuhani na mtoaji walikula dhabihu baada ya kumtolea Yehova damu na mafuta. (Mambo ya Mambo ya Walawi 3:17; 7:16-21; 19:5-8) Katika njia ya mfano na yenye kupendeza, mtoaji, makuhani, na Yehova Mungu walikuwa kana kwamba wanakula pamoja, hilo likionyesha uhusiano wenye amani uliokuwepo miongoni mwao.

w00-SW 15/8 uku. 19 fu. 8

Dhabihu Zilizompendeza Mungu

8 Namna gani mtu aliyetoa toleo? Sheria ilisema kwamba yeyote aliyekuja mbele za Yehova alipaswa kuwa safi, asiye na unajisi. Ilimbidi mtu aliyekuwa najisi kwa sababu yoyote ile atoe kwanza toleo la dhambi au la hatia kusudi arudishe msimamo safi mbele za Yehova ili toleo lake la kuchomwa au dhabihu ya ushirika iweze kukubaliwa Naye. (Mambo ya Mambo ya Walawi 5:1-6, 15, 17) Kwa hiyo, je, sisi huthamini umuhimu wa kudumisha msimamo safi mbele za Yehova siku zote? Tukitaka ibada yetu ikubaliwe na Mungu, yatupasa kuchukua hatua upesi kurekebisha ukiukaji wowote wa sheria za Mungu. Yatupasa kuwa wepesi wa kujinufaisha na njia ya kutoa msaada ambayo Mungu ameandaa​—“wanaume wazee wa kutaniko” na “dhabihu yenye kufunika kwa ajili ya dhambi zetu,” Yesu Kristo.​—Yakobo 5:14; 1 Yohana 2:1, 2.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

it-1-F uku. 889 fu. 2

Moto

Ku tabenakulo na ku hekalu. Moto ulitumiwa katika ibada yenye ilifanywa ku tabenakulo, na kisha ku hekalu. Kila asubui na katikati ya mangaribi mbili, kuhani mukubwa alipaswa kuchoma uvumba juu ya mazabahu ya uvumba. (Kut 30:7, 8) Kulingana na Sheria ya Mungu, ule moto wenye ulikuwa juu ya mazabahu ulipaswa kuendelea kuwaka. (Law 6:12, 13) Wazo lenye kutokana na desturi ya Wayahudi, la kusema kama ule moto wenye uliwaka kwenye mazabahu uliwashwa kwa njia ya muujiza na Mungu, halikubaliwe na Maandiko. Kulingana na maagizo ya kwanza-kwanza yenye Yehova alimupatiaka Musa, watoto wa Haruni walipaswa “kuweka moto kwenye mazabahu na kupanga kuni kwenye moto huo” mbele ya kuweka matoleo kwenye mazabahu. (Law 1:7, 8) Ni kisha kuweka ukuhani wa Haruni, na kisha kutia matoleo kwenye mazabahu, njo moto kutoka kwa Yehova, pengine kutoka katika wingu juu ya tabenakulo, uliteketeza matoleo yenye ilikuwa ku mazabahu. Ule moto wenye uliwaka kwa njia ya muujiza haukuteketeza miti yenye ilikuwa kwenye mazabahu lakini ‘uliteketeza lile toleo la kuteketezwa na vile vipande vya mafuta vyenye vilikuwa juu ya mazabahu.’ Bila shaka, moto wenye uliendelea kuwaka kwenye mazabahu kisha pale, ulitokana pengine na ule wenye ulitoka kwa Mungu na ule wenye waliwakishaka mbele. (Law 8:14–9:24) Vilevile, kisha Sulemani kutoa sala wakati wa kumutolea Yehova hekalu, Yehova alituma moto wenye uliteketeza palepale matoleo yao.​—2Ny 7:1; ona pia Amu 6:21; 1Fa 18:21-39; 1Ny 21:26 ili upate mifano ingine kuhusu namna Yehova alitokezaka moto kwa njia ya muujiza wakati alikubali matoleo ya watumishi wake.

si-SW uku. 27 fu. 15

Kitabu Cha Biblia Namba 3​—Mambo Ya Mambo ya Walawi

15 (3) Matoleo ya dhambi yatakwa kwa dhambi zisizo za kukusudia, au dhambi zilizofanywa kwa kukosea. Aina ya mnyama atolewaye yategemea ni dhambi ya nani iliyokuwa ikipatanishwa​—ile ya kuhani, watu kwa ujumla, jumbe, au mtu wa kawaida. Tofauti na matoleo ya kuteketezwa ya hiari na ya ushirika kwa ajili ya watu mmoja mmoja, matoleo ya dhambi ni ya lazima.​—4:1-35; 6:24-30.

TAREHE 30/11–6/12

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MAMBO YA WALAWI 8-9

“Mambo Yenye Kuonyesha Kama Yehova Iko Anabariki Watu Wake”

it-1-F uku. 1189 fu. 2

Kuwekwa Katika Kazi ya Ukuhani

Musa alinawisha Haruni na watoto wake Nadabu, Abihu, Eleazari, na Itamari (ao aliwaamuru wajinawishe) kwenye beseni ya shaba katika kiwanja na akamuvalisha Haruni nguo zenye utukufu za kuhani mukubwa. (Hes 3:2, 3) Haruni alipambwa vitu vingine vya kuonyesha sifa na madaraka yake. Kisha, Musa akajipakaa tabenakulo mafuta, vyombo vyote, na mazabahu, beseni na vyombo vya kutumikisha, vikakuwa vitakatifu, ao vikawekwa pembeni, ili vitumie tu mu kazi ya Mungu. Ku mwisho Musa akamwanga mafuta juu ya kichwa Haruni.​—Law 8:6-12; Kut 30:22-33; Zb 133:2.

it-1-F uku. 1190 fu. 3

Kuwekwa Katika Kazi ya Ukuhani

Siku ya munane kisha kuwekwa kwao, makuhani, wakiwa na vifaa vyote, wanatumikia kwa mara ya kwanza kwenye mazabahu (bila musaada wa Musa), wanafanya utumishi wa upatanisho kwa ajili ya taifa la Israeli. Waisraeli walikuwa na lazima ya kutakaswa, haiko tu juu walikuwa watenda-zambi, lakini ni juu walikuwa wanatoka tu kufanya mambo ya mubaya, kuabudu kitoto-dume cha zahabu cha ngombe, jambo lenye lilifanya Yehova awakasirikie. (Law 9:1-7; Kut 32:1-10) Mwisho wa ule utumishi wa kwanza wa wale makuhani wenye waliwekwa, Yehova alikubali kazi yenye walifanya, na alionyesha vile kwa kutuma moto kwa njia ya muujiza, wenye ulitoka bila shaka katika nguzo ya wingu juu ya tabenakulo, ule moto ukateketeza matoleo yenye ilikuwa inabakia ku mazabahu.​—Law 9:23, 24.

w19.11 uku. 23 fu. 13

Mambo Yenye Kitabu cha Mambo ya Mambo ya Walawi Kinatufundisha

13 Jambo la ine: Yehova iko anabariki sehemu ya ku dunia ya tengenezo lake. Fikiria jambo lenye lilitokea mu mwaka wa 1512 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, wakati tabenakulo ilisimamishwa kwenye sehemu ya chini ya Mulima Sinai. (Kut 40:17) Musa aliongoza sherehe ya kumuweka Haruni na wana wake ili wakuwe makuhani. Taifa la Israeli lilikusanyika ili kuona namna makuhani watatoa zabihu zao za kwanza za wanyama. (Law. 9:1-5) Yehova alifanya nini ili kuonyesha kama alikubali makuhani wapya wenye waliwekwa? Wakati Musa na Haruni walikuwa wanabariki watu, Yehova alishusha moto kutoka mbinguni na ukateketeza sehemu ya zabihu yenye ilibakia ku mazabahu.​—Soma Mambo ya Walawi 9:23, 24.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

w14 15/11 uku. 9 fu. 6

Sababu Gani unapaswa Kuwa Watakatifu

6 Yehova aliwaomba makuhani Waisraeli wakuwe safi kimwili. Amri hiyo inahusu pia watumishi wa Yehova leo. Wale wenye tunajifunza nao Biblia wanaona kila mara usafi wa mahali petu pa kufanyia ibada; wanaona pia kwamba tuko safi na tunavaa vizuri. Lakini, usafi wa makuhani unatusaidia tutambue kwamba kila mutu ambaye anapanda kwenye mulima ulio juu wa ibada ya Yehova anapaswa kuwa “safi moyoni.” (Soma Zaburi 24:3, 4; Isa. 2:2, 3.) Kwa hiyo, wakati tunamuabudu Mungu, tunapaswa kuwa na akili safi, moyo safi, na mwili safi. Ndio maana tunapaswa kuendelea kujichunguza; kisha kujichunguza, inawezekana wengi kati yetu watakuwa na lazima ya kufanya mabadiliko makubwa ili wakuwe watakatifu. (2 Kor. 13:5) Kwa mufano, muhubiri aliyebatizwa ambaye anatazama kimakusudi pornografia anapaswa kujiuliza hivi: ‘Niko kabisa mutakatifu?’ Kisha, anapaswa kutafuta musaada ili aache tabia hiyo mubaya.​—Yak. 5:14.

it-2-F uku. 310 fu. 5

Musa

Mungu alimufanya Musa akuwe mupatanishi wa agano la Sheria pamoja na Israeli. Ile ilikuwa cheo yenye ilionyesha kama alikuwa rafiki ya Mungu, na hakuna mutu mwingine mwenye alipataka pendeleo ya vile, isipokuwa tu Yesu Kristo, Mupatanishi wa agano jipya. Kupitia damu ya wanyama, Musa alinyunyiza damu ku kitabu cha agano chenye kilikuwa kinamuwakilisha Yehova, “mwenye alikuwa mu ile agano,” na akainyunyiza juu ya watu (bila shaka wazee wenye walimuwakilisha), “wenye pia walifanyiza sehemu ingine ya ile agano.” Kisha akasomea watu kitabu cha agano. Watu wakajibu hivi: “Mambo yote yenye Yehova amesema, tuko tayari kuyafanya.” (Kut 24:3-8; Ebr 9:19) Akiwa mupatanishi, Musa alilkuwa na pendeleo la kuongoza ujenzi wa tabenakulo na kutengenezesha vyombo vya kutumiwa mu tabenakulo, kulingana na vile Mungu alimuonyesha, kisha akaweka ukuhani kwa kutia mafuta tabenakulo na Haruni kuhani mukubwa, kwa kutumia mafuta ya pekee. Kisha akaongoza utumishi wa kwanza-kwanza wa makuhani wenye walikuwa wapya.​—Kut sura 25-29; Law sura 8, 9.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine