Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwbr21 Mwezi wa 9 uku. 1-10
  • Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha (9/2021)

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha (9/2021)
  • Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku la Mukutano Utumishi na Maisha—2021
  • Vichwa Vidogo
  • TAREHE 6-12/09
Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku la Mukutano Utumishi na Maisha—2021
mwbr21 Mwezi wa 9 uku. 1-10

Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha

TAREHE 6-12/09

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | KUMBUKUMBU LA TORATI 33-34

“Tafuta Kimbilio mu ‘Mikono ya Milele’ ya Yehova”

it-2-F uku. 1200

Yeshuruni

Jina ya cheo yenye Waisraeli walipewa. Mu Septante ya Kigiriki “Yeshuruni” ni neno yenye inatumiwa ili kumaanisha upendo, juu inatafsiriwa “mupendwa.” Jina “Yeshuruni” ilipaswa kukumbusha Waisraeli kama ni watu wenye Yehova alifanya nao agano na kama walipaswa kuendelea kuwa waaminifu kwake. (Kum 33:5, 26; Isa 44:2) Lakini mu Kumbukumbu la Torati 32:15, jina Yeshuruni inatumiwa mu maana tofauti. Israeli hakuishi kulingana na jina yake Yeshuruni, juu alifikia kuwa na kiburi, kuacha mwenye alimufanya, na kuzarau Mwokozi wake.

rr uku. 120, kisanduku

Jambo la Kutusaidia Tusimame Tena kwa Miguu Yetu

Kumbuka kwamba miaka mingi mbele ya siku za Ezekieli, nabii Musa alisema kwamba Yehova iko na nguvu lakini pia iko na nia ya kutumia ile nguvu ili kusaidia watu wake. Musa aliandika hivi: “Mungu ni kimbilio tangu nyakati za zamani, mikono yake ya milele iko chini yako.” (Kum. 33:27) Tunaweza kuwa hakika kwamba, kama tunamulilia Yehova Mungu wetu wakati wa magumu, atatia mikono yake yenye upendo chini yetu, atatuinua kwa upole, na atatusaidia tusimame tena kwa miguu yetu.​​—Eze. 37:10.

w11-SW 15/9 uku. 19 fu. 16

Kimbia Shindano la Mbio kwa Uvumilivu

16 Sawa na Abrahamu, Musa hakuona utimizo wa ahadi ya Mungu katika maisha yake. Kabla tu ya Waisraeli kuingia katika Nchi ya Ahadi, Mungu alimwambia Musa hivi: “Kutoka mbali utaiona nchi, lakini hutaingia katika nchi ninayowapa wana wa Israeli.” Ilikuwa hivyo kwa sababu mapema yeye na Haruni, ‘walitenda isivyofaa kumwelekea Mungu katikati ya wana wa Israeli kwenye maji ya Meriba,’ walipokasirishwa na uasi wa watu. (Kum. 32:51, 52) Je, Musa alivunjika moyo au kuwa na kinyongo? Hapana. Alitangaza baraka juu ya Waisraeli na akamalizia kwa maneno haya: “Una furaha, Ee Israeli! Ni nani aliye kama wewe, kikundi cha watu kinachofurahia wokovu wa Yehova, aliye ngao ya msaada wako, na Yule aliye upanga wako wa adhama?”​—Kum. 33:29.

Mali ya Kiroho

it-2-F uku. 312 fu. 4

Musa

Wakati Musa alikufa, alikuwa na miaka 120. Biblia inasema hivi juu ya nguvu yake ya kimwili: “Macho yake hayakukuwa yamefifia, na nguvu zake hazikukuwa zimeisha.” Yehova alimuzikaka fasi yenye mupaka leo, hakuna mutu mwenye anajua. (Kum. 34:5-7) Pengine, Yehova alifanyaka vile juu ya kuzuia Waisraeli wasiangukie mu mutego ya ibada ya uwongo ya kufanya kaburi ya musa kuwa fasi takatifu ya kuabudia. Maneno yenye Yuda, mwanafunzi Mukristo na ndugu ya Yesu Kristo alisema, inaonyesha kama inawezekana Ibilisi alipenda kutumia mwili ya musa kwa ajili ya ile kusudi. Alisema hivi: “Wakati Mikaeli, ule malaika mukubwa alishindana na Ibilisi na kubishana naye juu ya mwili wa Musa, hakupima hata kidogo kumuhukumu kwa matukano, lakini alimwambia: ‘Yehova akukemee.’” (Yuda 9) Mbele waingie mu Kanaani, chini ya uongozi wa Yoshua, Waisraeli walifanya siku 30 na wako wanamulia Musa.​—Kum 34:8.

TAREHE 13-19/09

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | YOSHUA 1-2

“Namna ya Kufanya Njia Yako Ikuwe na Matokeo ya Muzuri”

w13 15/1 uku. 8 fu. 7

Uwe Hodari Yehova Yupo Pamoja Nawe!

7 Tunapaswa kujifunza na kutumikisha mambo tunayojifunza katika Neno la Mungu ili tuwe na uhodari unaohitajiwa ili kufanya mapenzi ya Mungu. Yoshua alipokamata nafasi ya Musa, Yehova alimuambia hivi: ‘Uwe hodari na mwenye nguvu sana ili uangalie kufanya kulingana na sheria yote ambayo Musa mutumishi wangu alikuamuru. . . . Kitabu hiki cha sheria kisiondoke katika kinywa chako, nawe ukisome kwa sauti ya chini muchana na usiku, upate kuangalia kufanya kulingana na yote ambayo yameandikwa ndani yake; kwa maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha utatenda kwa hekima.’ (Yos. 1:7, 8) Yoshua alifuata shauri hilo, na ‘alifanikisha njia yake.’ Ikiwa tunamuiga, tutakuwa na uhodari mwingi zaidi na tutafanikiwa katika kazi ya Mungu.

w13 15/1 uku. 11 fu. 20

Uwe Hodari Yehova Yupo Pamoja Nawe!

20 Si rahisi kushikamana na ibada ya kweli katika ulimwengu huu muovu na wenye majaribu mengi. Hata hivyo, hatuko pekee yetu. Mungu yupo pamoja nasi. Mwana wake, ambaye ni Kichwa cha kutaniko yupo pia pamoja nasi. Tuko pia na Mashahidi wenzetu zaidi ya 7 000 duniani pote. Basi, acheni sisi wote pamoja tuendelee kuwa na imani na kutangaza habari njema na kuchunga katika akili yetu andiko letu la mwaka wa 2013: “Uwe hodari na mwenye nguvu. . . . Yehova Mungu wako yupo pamoja nawe.”​—Yos. 1:9.

Mali ya Kiroho

w04-SW 12/1 9 fu. 1

Mambo Makuu Katika Kitabu cha Yoshua

2:4, 5​—Kwa nini Rahabu anawaelekeza vibaya wanaume wa mfalme ambao wanawatafuta wapelelezi? Rahabu anahatarisha uhai wake kwa kuwaficha wapelelezi hao kwa sababu amesitawisha imani katika Yehova. Kwa hiyo, hayuko chini ya wajibu wowote kuwaeleza wanaume wanaokusudia kuwadhuru watu wa Mungu mahali walipo wapelelezi. (Mathayo 7:6; 21:23-27; Yohana 7:3-10) Kwa kweli, Rahabu ‘alitangazwa kuwa mwadilifu kwa matendo,’ kutia ndani tendo la kuwaelekeza vibaya wajumbe wa mfalme.​—Yakobo 2:24-26.

TAREHE 20-26/09

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | YOSHUA 3-5

“Yehova Anabariki Wenye Wanatenda kwa Imani”

it-2-F uku. 63

Yordani

Mara mingi, fasi kwenye bahari ya Galilaya inaingia sana, urefu kuenda ndani wa Yordani unakuwaka kati ya metre 1 na 3, na upana kati ya metre 27 na 30. Lakini mu Mwezi ya 4, Yordani inayalaka sana na kuvuka mipaka yake. Na ile inafanyaka upana na urefu wake kuenda ndani, ukuwe mukubwa sana. (Yos 3:15) Mu ile kipindi ingekuwa nguvu kwa taifa ya Israeli, yenye ilitia ndani wanaume, wanamuke na watoto kuvuka Yordani, zaidi sana karibu na Yeriko. Pale, maji inapitaka mbio sana hivi kwamba hivi karibuni, ilifikia kubeba watu fulani wenye kuogelea. Lakini kuhusu Waisraeli, Yehova alifanyaka muujiza ya kusimamisha maji ya Yordani, na ile ilifanyaka wavuke ku udongo yenye kukauka. (Yos 3:14-17) Miaka fulani kisha, muujiza ya vile ilifanyika mara moja wakati Eliya alikuwa na Elisha, na mara ingine wakati Elisha alikuwa yeye peke.​—2Fa 2:7, 8, 13, 14.

w13 15/9 uku. 16 fu. 17

Furahia Vikumbusho vya Yehova

17 Namna gani matendo ya imani yanatusaidia tumutegemee Yehova? Fikiria simulizi la Biblia kuhusu namna Waisraeli walivyoingia katika Inchi ya Ahadi. Yehova alikuwa amewaagiza makuhani wachukue sanduku la agano na kuingia katika Muto Yordani. Lakini, Waisraeli wengine walipokuwa wakikaribia muto huo, waliona kwamba mvua ya majira ya kuchipua ilikuwa imeufanya muto ujae sana. Waisraeli wangefanya nini? Je, wangebaki pembeni ya muto na kungojea majuma fulani ao muda murefu zaidi mupaka wakati maji yangepunguka? Sivyo, walimutegemea kabisa Yehova na kufuata muongozo wake. Matokeo yalikuwa nini? Biblia inasema: ‘Mara tu miguu ya makuhani waliolichukua Sanduku ilipotumbukizwa katika maji ya ukingoni, ndipo maji yanayoshuka kutoka juu yakaanza kusimama, . . . wakati huohuo wale makuhani wakaendelea kusimama bila kusonga kwenye inchi kavu na watu wakavuka mbele ya Yeriko.’ (Yos. 3:12-17) Wazia namna gani walitiwa moyo walipoona maji hayo mengi yakisimama! Bila shaka, imani ya Waisraeli katika Yehova ilitiwa nguvu kwa sababu walitegemea uongozi wake.

w13 15/9 uku. 16 fu. 18

Furahia Vikumbusho vya Yehova

18 Ni kweli kwamba leo Yehova hafanye miujiza kama hiyo kwa ajili ya watu wake, lakini anabariki matendo yao ya imani. Roho yake inawapa nguvu ya kutimiza kazi aliyowatolea ya kuhubiri ujumbe wa Ufalme ulimwenguni pote. Tena, kisha ufufuo wake, Shahidi wa kwanza wa Yehova, ambaye ni Kristo Yesu, aliwahakikishia wanafunzi wake kwamba atawategemeza katika kazi hiyo ya maana sana alipowaambia hivi: ‘Kwa hiyo nendeni mukafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote . . . mimi nipo pamoja nanyi siku zote mupaka umalizio wa mufumo wa mambo.’ (Mt. 28:19, 20) Mashahidi wengi ambao hapo zamani walikuwa wenye kusikia haya ao kuwaogopa watu wamejionea namna roho takatifu imewatolea ujasiri wa kuzungumuza na watu wasiowajua katika mahubiri.​—Soma Zaburi 119:46; 2 Wakorintho 4:7.

Mali ya Kiroho

w04-SW 1/12 uku. 9 fu. 2

Mambo Makuu Katika Kitabu cha Yoshua

5:14, 15​—“Mkuu wa jeshi la Yehova” ni nani? Yaelekea mkuu anayekuja kumwimarisha Yoshua wakati Nchi ya Ahadi inapoanza kutwaliwa, ni “Neno,” yaani, Yesu Kristo kabla hajawa mwanadamu. (Yohana 1:1; Danieli 10:13) Ni jambo lenye kuimarisha kama nini kuwa na uhakika kwamba Yesu Kristo aliyetukuzwa yuko pamoja na watu wa Mungu leo wanapoendelea na vita vya kiroho!

TAREHE 27/09–TAREHE 3/10

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | YOSHUA 6-7

“Epuka Mambo Yenye Haina Mafaa”

w10-SW 15/4 uku. 20 fu. 5

Usiruhusu Macho Yako Yaone Mambo Yasiyofaa!

5 Karne nyingi baadaye, macho ya Mwisraeli anayeitwa Akani yalimshawishi kuiba vitu fulani kutoka katika jiji lililotekwa la Yeriko. Mungu alikuwa ameamuru vitu vyote vya jiji hilo viharibiwe isipokuwa vitu fulani ambavyo vingewekwa katika hazina ya Yehova. Waisraeli walionywa hivi: “Mjiepushe tu na kitu kilichotengwa kwa ajili ya kuharibiwa, msije mkawa na tamaa” na kuchukua vitu kutoka katika jiji hilo. Akani alipokosa kutii, Waisraeli walishindwa vitani katika jiji la Ai, na wachache wakauawa. Akani hakukubali kwamba aliiba mpaka alipofunuliwa. Akani alisema: “Nilipoona” vitu hivyo, ‘ndipo nikavitamani, halafu nikavichukua.’ Tamaa yake ya macho ilifanya aangamizwe pamoja na “kila kitu kilichokuwa chake.” (Yos. 6:18, 19; 7:1-26) Akani alitamani moyoni vitu ambavyo hakupaswa kuchukua.

w97-SW 15/8 uku. 28 fu. 2

Kwa Nini Lililo Baya Liripotiwe?

Sababu moja ya kuripoti kosa ni kwamba jambo hilo huhifadhi usafi wa kutaniko. Yehova ni Mungu safi, Mungu mtakatifu. Yeye hutaka wale wote ambao humwabudu wawe safi kiroho na kiadili. Neno lake lililopuliziwa laonya kwa upole hivi: “Kama watoto watiifu, komeni kuwa mkifanyizwa kulingana na mtindo wa tamaa zenu mlizokuwa nazo hapo zamani katika kutokuwa kwenu na ujuzi, bali, kwa kupatana na Mtakatifu aliyewaita, nyinyi wenyewe pia iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote, kwa sababu imeandikwa: ‘Lazima mwe watakatifu, kwa sababu mimi ni mtakatifu.’” (1 Petro 1:14-16) Watu mmoja-mmoja wazoeao ukosefu wa usafi au utendaji makosa wanaweza kuliletea kutaniko zima unajisi na hali ya kutopendelewa na Yehova ikiwa hatua ya kuwasahihisha au kuwaondoa watu haitachukuliwa.​—Linganisha Yoshua, sura ya 7.

w10-SW 15/4 uku. 21 fu. 8

Usiruhusu Macho Yako Yaone Mambo Yasiyofaa!

8 Tamaa ya macho na ya mwili inaweza pia kuwa na uvutano mbaya juu ya Wakristo wa kweli. Kwa hiyo, Neno la Mungu linatutia moyo tujitie nidhamu kuhusu mambo tunayoona na kutamani. (1 Kor. 9:25, 27; soma 1 Yohana 2:15-17.) Mwanamume mwadilifu Ayubu alitambua kwamba kuna uhusiano wenye nguvu kati ya kuona na kutamani. Alisema hivi: “Nimefanya agano pamoja na macho yangu. Basi nawezaje kukaza fikira kwa bikira?” (Ayu. 31:1) Ayubu hakukataa tu kumgusa mwanamke kwa njia potovu lakini hangeruhusu hata akili yake ifikirie jambo kama hilo. Yesu alikazia kwamba ni lazima tulinde akili zetu kutokana na mawazo mapotovu aliposema hivi: “Kila mtu ambaye anaendelea kumtazama mwanamke na kumtamani tayari amefanya uzinzi pamoja naye moyoni mwake.”​—Mt. 5:28.

Mali ya Kiroho

w15 15/11 uku. 15 fu. 2-3

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Wakati wa zamani, muji ulikamatwa wakati maaskari waliuzunguka na kuwa tayari kuushambulia. Ikiwa maaskari walizunguka muji kwa muda murefu, watu wa muji huo walipaswa kula sehemu kubwa zaidi ya chakula chenye walikuwa wameweka. Kisha, wakati maaskari walikamata muji, walichukua kila kitu chenye walipenda, na pia chakula chenye watu waliacha. Ndiyo sababu watu wenye kuchimba vitu vya zamani walipata chakula kidogo sana ao hawakupata chakula chochote nafasi penye palikuwa miji ya zamani katika Palestina yenye maaskari walizunguka kwa muda murefu mbele waikamate. Lakini, mambo ilikuwa tofauti juu ya muji wa Yeriko. Kitabu Biblical Archaeology Review kinasema hivi: “Kati ya vitu vyenye vilivumbuliwa, kulikuwa vyombo vya udongo, lakini nafaka (mbegu) ndiyo ilikuwa nyingi sana.” Kitabu hicho kinaongeza hivi: “Ilikuwa jambo la pekee sana kupata kiasi kikubwa sana cha mbegu.”

Biblia inasema kwamba Waisraeli hawakuchukua chakula chenye kilikuwa katika muji wa Yeriko kwa sababu Yehova alikuwa amewakataza kufanya hivyo. (Yoshua 6:17, 18) Biblia inasema tena kwamba Waisraeli walikamata muji wa Yeriko katika majira ya kuchipua, kisha tu wakati wa mavuno, wakati watu wa Yeriko walikuwa wameweka mbegu nyingi sana. (Yoshua 3:15-17; 5:10) Kwa hiyo, kwa sababu kulikuwa mbegu nyingi sana wakati muji wa Yeriko ulikamatwa, hilo linahakikisha kwamba ulikamatwa kisha kuzungukwa kwa muda mufupi, kama vile tu Biblia inasema.

TAREHE 4-10/10

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | YOSHUA 8-9

“Habari ya Wagibeoni Inaweza Kutufundisha Nini?”

it-1-F uku. 1046

Gibeoni

Gibeoni na Yoshua. Mu siku za Yoshua, Wahivi, wenye walikuwa kati ya mataifa saba ya Wakanaani yenye ilipaswa kuharibiwa, njo walikuwa naishi Gibeoni. (Kum 7:1, 2; Yos 9:3-7) Wagibeoni waliitwa pia Waamori, juu inaonekana kama jina Waamori, ilikuwa inatumiwa wakati fulani kwa Wakanaani wote. (2Sa 21:2; linganisha na Mwa 10:15-18; 15:16.) Tofauti na Wakanaani wengine, Wagibeoni walielewa kama hata kama walikuwa na majeshi yenye nguvu na hata kama muji yao ilikuwa mukubwa, kushindana na Waisraeli ingekuwa kupoteza wakati bure juu ni Yehova njo alikuwa nawapigania. Lakini, kisha Yeriko na Ai kuharibiwa, Wanaume wa Gibeoni, wenye pengine waliwakilisha pia miji tatu ya Wahivi, ni kusema Kefira, Beeroti, na Kiriat-yearimu (Yos 9:17), walituma watu waende Gilgali, ili wamuone Yoshua na kumuomba afanye amani pamoja nao. Wale Wagibeoni, walienda na wanavala viato na nguo zenye kuzeeka, walikuwa na chupa za ngozi za kuwekea divai zenye kuzeeka, magunia yenye kuzeeka, na mikate ya kukauka na kuvunjika-vunjika. Walisema kama wanatoka mu inchi ya mbali, yenye haikukuwa kati ya mataifa yenye Waisraeli walipaswa kupigana nayo. Mambo yenye ilifikia Wamisri, na wafalme wa Amori, ni kusema Sihoni na Ogu, ilifanya waamini kama ni Yehova njo alipigania Waisraeli. Vile walisema kama wanatoka mu “inchi ya mbali sana,” walitumia hekima kwa kuepuka kusema mambo yenye ilipitika Yeriko na Ai, juu haingewezekana wapate ile habari mbele waanze ile yenye waliita safari ya murefu. Wanaume wenye waliwakilisha Waisraeli walichunguza na kukubali ile habari na wakafanya agano pamoja nao ili kuwaacha waishi.​—Yos 9:3-15.

w11 15/11 uku. 8 fu. 14

“Usitegemee Uelewaji Wako Mwenyewe”

14 Kwa kuwa hatukamilike, hata wazee wenye uzoefu, tusikose kumuomba Yehova uongozi tunapochukua maamuzi. Fikiria jinsi Yoshua aliyechukua nafasi ya Musa na wanaume wazee Waisraeli walikosa kumuomba Yehova uongozi wakati Wagibeoni wenye busara walidanganya kwa kujifanya kama watu waliotoka mbali. Bila kumuuliza Yehova, Yoshua na wengine walikubali kufanya amani na Wagibeoni hao, na wakafanya agano pamoja nao. Hata ikiwa Yehova mwishowe alikubali mapatano hayo, yeye aliandikisha habari hiyo katika Biblia ili tujue kwamba Yoshua na wazee wa Israeli walikosa kufuata uongozi wake.​—Yos. 9:3-6, 14, 15.

w04-SW 15/10 uku. 18 fu. 14

“Ondoka, Zunguka Katika Nchi”

14 Wawakilishi hao walisema: “Watumishi wako wametoka nchi ya mbali sana kwa sababu ya jina la Yehova Mungu wako.” (Yoshua 9:3-9) Mavazi na vyakula vyao vilifanya ionekane kama walikuwa wametoka mbali, lakini kwa kweli Gibeoni lilikuwa kilometa 30 hivi kutoka Gilgali. [19] Kwa kusadiki hilo, Yoshua na wakuu walifanya mkataba wa amani pamoja na Wagibeoni na majiji ya karibu yaliyokuwa na uhusiano na Gibeoni. Je, ujanja wa Wagibeoni ulikuwa tu njia ya kujiepusha na kifo? Hapana, ujanja huo ulionyesha tamaa yao ya kupata kibali cha Mungu wa Israeli. Yehova aliwakubali Wagibeoni, nao wakawa “wakusanyaji wa kuni na watekaji wa maji kwa ajili ya kusanyiko na kwa ajili ya madhabahu ya Yehova,” wakileta kuni kwa ajili ya madhabahu ya dhabihu. (Yoshua 9:11-27) Wagibeoni waliendelea kuonyesha utayari wao wa kufanya kazi za hali ya chini katika utumishi wa Yehova. Yaelekea baadhi yao walikuwa kati ya Wanethini waliorudi kutoka Babiloni na kutumika kwenye hekalu lililojengwa upya. (Ezra 2:1, 2, 43-54; 8:20) Tunaweza kuiga mtazamo wao kwa kujitahidi kudumisha amani pamoja na Mungu, na kuwa tayari kufanya hata kazi za hali ya chini katika utumishi wake.

Mali ya Kiroho

it-2-F uku. 523

Kutundika

Mu sheria yenye Yehova alipatia Waisraeli, watenda zambi fulani walikuwa natundikwa ku muti kisha kuuawa. Walionwa kuwa wenye “kulaaniwa na Mungu,” na walitiwa fasi kwenye kila mutu angeweza kuwaona juu ikuwe mufano ya kuonya. Maiti ilipaswa kutoshwa ku muti na kuzikwa mbele ikuwe usiku, juu kuiacha ku muti usiku yote ingekuwa kuchafua inchi yenye Yehova alipatia Waisraeli. (Kum 21:22, 23) Waisraeli walifuata ile sheria hata kama mutu mwenye aliuawa hakukuwa Mwisraeli.​—Yos 8:29; 10:26, 27.

Hotuba

nwt uku. 1948

Agano. Mapatano mazito, ao makubaliano, kati ya Mungu na wanadamu ao kati ya wanadamu wawili ili kufanya ao kutokufanya jambo fulani. Nyakati fulani ni upande mumoja tu ndio ulikuwa na daraka la kutimiza masharti ya agano hilo (agano la upande mumoja, lenye kwa kawaida lilikuwa ahadi). Nyakati zingine pande zote mbili zilipaswa kutimiza masharti ya agano hilo (agano la pande mbili). Zaidi ya maagano yenye Mungu alifanya pamoja na wanadamu, Biblia inataja pia maagano kati ya wanadamu, makabila, mataifa, ao vikundi vya watu. Kati ya maagano yenye yamekuwa na matokeo makubwa sana kuko agano lenye Mungu alifanya pamoja na Abrahamu, Daudi, taifa la Israeli (agano la Sheria), na Israeli wa Mungu (agano jipya).​—Mwa 9:11; 15:18; 21:27; Kut 24:7; 2Ny 21:7.

it-1-F uku. 81 fu. 2

Maagano Ingine. (a) Yoshua na wakubwa wa Waisraeli walifanya agano pamoja na wakaaji wa muji ya Gibeoni ili kuwaacha waishi. Ni kweli, Wakanaani walikuwa wenye kulaaniwa, na Waisraeli walipaswa kuwaangamiza. Lakini agano ilionwa kuwa kifungo ya nguvu sana. Njo maana Waisraeli walipaswa kuacha Wagibeoni waendelee kuishi. Hata vile, hawakuponyoka laana, walifanywa kuwa watumwa wa kukusanya kuni na wa kushota maji kwa ajili ya mukusanyiko wa Israeli. (Yos 9:15, 16, 23-27) (b) Yoshua pamoja na Waisraeli wengine walifanya agano ya kumutumikia Yehova. (Yos 24:25, 26) (c) Wakati walikuwa Mispa, wazee wa Gileadi walifanya agano pamoja na Yifta ya kumufanya kuwa kiongozi wa wakaaji wa Gileadi kama Yehova anamupatia ushindi juu ya Waamoni. (Amu 11:8-11) (d) Agano kati ya Yonatani na Daudi. (1Sa 18:3; 23:18) (e) Agano kati ya kuhani Yehoyada na wakubwa wa walinzi wa Kare na wa walinzi wa nyumba za mufalme . (2Fa 11:4; 2Ny 23:1-3) (f) Agano ya Waisraeli pamoja na Yehova ya kufukuza wanamuke wageni. (Ezr 10:3) (g) Agano ya Yehova ya kutoa mutumishi wake ili akuwe agano ya watu. (Isa 42:6; 49:8) (h) Agano kati ya Daudi na wanaume wa Israeli, yenye walifanyia Hebroni. (1Ny 11:3) (i) Agano yenye watu walifanya, wakati Asa alikuwa mufalme, ya kumutafuta Yehova kwa moyo na kwa nafsi yao yote. (2Ny 15:12) (j) Yosia alifanya agano pamoja na Yehova wakati alisema kama atatii amri zake kulingana na mambo yenye iliandikwa mu sheria. (2Ny 34:31) (k) Watawala wa Yerusalemu walijindanganya kwa kujisifu kama walifanya “agano pamoja na kifo.”​—Isa 28:14, 15, 18.

TAREHE 11-17/10

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | YOSHUA 10-11

“Yehova Anapigania Israeli”

it-1-F uku. 48

Adoni-sedeki

Alikuwa mufalme wa Yerusalemu wakati Waisraeli waliingia mu Inchi ya Ahadi. Adoni-sedeki alijiunga na wafalme wengine wenye walikuwa ku upande wa mangaribi wa Yordani na wakafanya mapatano ili kupigana na majeshi yenye Yoshua alikuwa anaongoza. (Yos 9:1-3) Lakini, Wahivi wakaaji wa Gibeoni, walifanya amani pamoja na Yoshua. Juu ya kufanya kusikuwe tena mutu mwenye atajiunga na adui, Adoni-sedeki alijiunga na wafalme wengine ine wa Waamori, na kupiga kambi ili kupigana na Gibeoni. Yoshua alisaidia kabisa Wagibeoni na kupiga bila huruma ile majeshi yote yenye iliungana. Ile ilifanya wale wafalme tano wakimbilie Makeda, kwenye walinaswa ndani ya pango. Yoshua yeye peke njo aliua Adoni-sedeki na wale wafalme wengine ine mbele ya majeshi yake, na akawatundika ku miti. Kisha pale, maiti yao ilirudishwa mu pango, na ni ile njo ilifikia kuwa kaburi yao.​—Yos 10:1-27.

it-1-F uku. 1028

Mvua ya Majiwe

Yehova Aliitumia. Mvua ya majiwe ni moja kati ya njia zenye Yehova alitumia wakati fulani ili kutimiza maneno yake, na ili kuonyesha nguvu yake kubwa. (Zb 148:1, 8; Isa 30:30) Yehova alitumia kwa mara ya kwanza mvua ya majiwe wakati alileta pigo ya saba mu Misri. Ile mvua iliharibisha mimea, miti, na kuua watu na Wanyama wote wenye walikuwa mu mashamba. Lakini, haikuua Waisraeli wenye walikuwa Gosheni. (Kut 9:18-26; Zb 78:47, 48; 105:32, 33) Wakati Waisraeli walikuwa mu Inchi ya Ahadi, chini ya uongozi wa Yoshua, walisaidia Wagibeoni wenye waliogopeshwa na wafalme tano wa Waamori wenye waliungana. Ni mu ile wakati njo Yehova alitumia tena mvua ya majiwe ili kupiga Waamori. Watu wenye mvua ya majiwe iliua ile siku, walikuwa wengi kupita wenye Waisraeli waliua.​—Yos 10:3-7, 11.

w04-SW 1/12 uku. 11 fu. 1

Mambo Makuu Katika Kitabu cha Yoshua

10:13​—Jambo hilo lisilo la kawaida linawezekanaje? “Je, jambo lolote ni kubwa mno isivyo kawaida kwa Yehova,” Muumba wa mbingu na dunia? (Mwanzo 18:14) Yehova akitaka anaweza kufanya dunia isizunguke hivi kwamba mtu akiwa duniani ataona ni kana kwamba jua na mwezi zimesimama. Au anaweza kuacha dunia na mwezi ziendelee kuzunguka lakini apinde miali ya jua na mwezi ili nuru kutoka kwa mianga hiyo iendelee kuangaza. Vyovyote iwavyo, “hakuna siku ambayo imepata kuwa kama hiyo” katika historia ya wanadamu.​—Yoshua 10:14.

Mali ya Kiroho

w09-SW 15/3 uku. 32 fu. 5

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Uhakika wa kwamba vitabu fulani vinatajwa katika Biblia na vilitumiwa kama vyanzo vya habari haupaswi kutufanya tukate kauli kwamba viliandikwa kwa mwongozo wa roho ya Mungu. Hata hivyo, Yehova Mungu amehifadhi maandishi yote yenye “neno la Mungu wetu,” na neno hilo “litadumu mpaka wakati usio na kipimo.” (Isa. 40:8) Ndiyo, habari ambazo Yehova aliamua ziandikwe katika vile vitabu 66 vya Biblia ndizo tunazohitaji tu ili ‘tuwe na uwezo kamili, na vifaa kamili kwa ajili ya kila kazi njema.’​—2 Tim. 3:16, 17.

TAREHE 18-24/10

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | YOSHUA 12-14

“Umufuate Yehova kwa Moyo Wako Wote”

w04-SW 1/12 uku. 12 fu. 2

Mambo Makuu Katika Kitabu cha Yoshua

14:10-13. Ingawa ana umri wa miaka 85, Kalebu anaomba kazi ngumu ya kuwafukuza watu katika eneo la Hebroni. Eneo hilo linakaliwa na Waanakimu​—watu wakubwa isivyo kawaida. Kwa msaada wa Yehova, shujaa huyo wa vita mwenye uzoefu anafanikiwa, na Hebroni lawa jiji la makimbilio. (Yoshua 15:13-19; 21:11-13) Kielelezo cha Kalebu kinatutia moyo tusiogope migawo migumu ya kiroho.

w06-SW 1/10 uku. 18 fu. 11

Kuwa Hodari Kupitia Imani na Kumwogopa Mungu

11 Imani hiyo hukua. Inakua tunapoishi kulingana na kweli, ‘tunapoonja’ faida zake, ‘tunapoona’ sala zetu zikijibiwa, na kutambua mwongozo wa Yehova maishani mwetu kwa njia nyingine. (Zaburi 34:8; 1 Yohana 5:14, 15) Tunaweza kuwa na hakika kwamba imani ya Yoshua na Kalebu iliimarishwa walipoonja wema wa Mungu. (Yoshua 23:14) Fikiria mambo haya: Waliokoka safari ya miaka 40 nyikani kama Mungu alivyoahidi. (Hesabu 14:27-30; 32:11, 12) Walipewa kazi ya pekee wakati wa ile miaka sita ya kuteka Kanaani. Hatimaye, walifurahia maisha marefu na afya nzuri na hata wakapewa urithi wao. Yehova huwapa thawabu wale walio waaminifu na wanaomtumikia kwa uhodari!​—Yoshua 14:6, 9-14; 19:49, 50; 24:29.

Mali ya Kiroho

it-1-F uku. 1032

Gebali

Yehova alitia inchi ya Wagebali kati ya maeneo yenye Waisraeli wangekamata mu siku za Yoshua. (Yos 13:1-5) Wachunguzi wanasema kama ile haipatane na akili juu Gebali ilikuwa mbali ku upande wa kaskazini wa Israeli (karibu kilometre 100 kutoka Dani, upande wa kaskazini), na wanasema kama inawezekana haikufikia kuwa mu mikono ya Waisraeli. Wasomi fulani wanasema kama inawezekana maneno ya Kiebrania ya hii andiko ilibadilishwa na kama zamani ilikuwa inasomwa hivi: “inchi yenye kuwa karibu na Lebanoni,” ao ‘mupaka ku mupaka wa Wagebali.’ Lakini, inaomba kujua kama juu Yehova atimize ahadi zenye kuwa mu Yoshua 13:2-7, Waisraeli walipaswa kufuata mambo yenye aliwaambia. Kwa hiyo, inawezekana Waisraeli hawakupata inchi ya Gebali juu ya kukosa kutii.​—Linganisha na Yos 23:12, 13.

TAREHE 25-31/10

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | YOSHUA 15-17

“Linda Uriti Yako ya Maana Sana”

it-1-F uku. 1101 fu. 2

Hebroni

Wakati Waisraeli walikuwa mu eneo ya kusini ya Kanaani, walipiga wakaaji wa Hebroni, na mufalme wao (inawezekana mwenye alianza kutawala kisha Hohamu). (Jos 10:36, 37) Lakini, hata kama Waisraeli wenye walikuwa chini ya uongozi wa Yoshua walipiga Wakanaani, inaonekana kama hawakuweka mara moja kambi za kijeshi ili kulinda maeneo yenye walishinda. Kwa hiyo, Waanaki walianza kuishi tena mu Hebroni, inawezekana wakati Waisraeli walikuwa napigana fasi ingine. Njo maana, kisha wakati fulani, Kalebu (ao watoto wa Yuda wenye walikuwa chini ya uongozi wa Kalebu) walifikia kuwanyanganya ile muji. (Yos 11:21-23; 14:12-15; 15:13, 14; Amu 1:10) Ku mwanzo, Hebroni ilipewa Kalebu wa kabila ya Yuda. Lakini, kisha wakati fulani, ilifikia kuwa muji takatifu ya makimbilio na pia muji ya kikuhani. Lakini, “eneo la mashamba la [Hebroni]” na makao yake, vilikuwa uriti wa Kalebu.​—Yos 14:13, 14; 20:7; 21:9-13.

it-2-F uku. 1097

Kazi ya Kulazimishwa

Zamani, maneno “kazi ya kulazimshwa” (Kiebrania, mas) ilikuwa natumiwa sana, juu mara mingi watu wenye walikuwa nakamatwa wakati ya vita, walikuwa nafanywa kuwa watumwa. (Kum 20:11; Yos 16:10; 17:13; Est 10:1; Isa 31:8; Omb 1:1) Wakati Waisraeli walikuwa mu utumwa Misri, wakubwa wa kazi ya kulazimishwa waliwapatia kazi ya kulazimishwa yenye ilitia ndani kujenga miji ya kuwekea vitu, ni kusema Pitomu na Raamsesi. (Kut 1:11-14) Kisha tu Israeli kuingia mu Inchi ya Ahadi, kuliko kufuata maagizo ya Yehova ya kufukuza Wakanaani wote mu inchi na kuwaangamiza, waliwapatia kazi ya nguvu, ni kusema kazi ya kulazimishwa. Na ile ilikuwa na matokeo ya mubaya sana juu ilifanya Waisraeli waanze kuabudu miungu ya uwongo. (Yos 16:10; Amu 1:28; 2:3, 11, 12) Mufalme Sulemani aliendelea kuandikisha kwa ajili ya kazi ya kulazimishwa wazao wa Wakanaani, ni kusema, Waamori, Wahiti, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi.​—1Fa 9:20, 21.

it-1-F uku. 390 fu. 4

Kanaani

Hata kama Wakanaani wengi waliokoka, ile haimaanishe kama Yehova hakutimiza ahadi yake. Tunaweza tu kusema kama “Yehova alipatia Israeli inchi yote yenye aliapia mababu zao,” aliwapatia “pumuziko pande zote,” na kama “hakuna ahadi hata moja yenye haikutimia kati ya ahadi zote za muzuri zenye Yehova aliahidi nyumba ya Israeli; zote zilitimia.” (Yos 21:43-45) Maadui wote wenye walizunguka Waisraeli waliwaogopa sana; na hakuna jambo yenye walifanya juu ya kuvuruga usalama wao. Mungu alikuwaka alishasema kama atafukuza Wakanaani “hatua kwa hatua.” Aliamua kufanya vile, juu wanyama wasiongezeke mu inchi yenye imekuwa ukiwa. (Kut 23:29, 30; Kum 7:22) Wakanaani, walikuwa na vyombo vya hali ya juu vya vita, kutia ndani magari ya vita yenye miundu ya chuma. Ile ingefanya Waisraeli washindwe kukamata maeneo fulani ya Wakanaani. Lakini, ile haimaanishe kama Yehova alishindwa kutimiza ahadi yake. (Yos 17:16-18; Amu 4:13) Habari yenye kuwa mu Biblia inaonyesha kama, sababu yenye ilifanya Waisraeli washindwe kukamata maeneo fulani, ni kukosa kuwa waaminifu.​—Hes 14:44, 45; Yos 7:1-12.

Mali ya Kiroho

w15-SW 15/7 uku. 32

JE, WAJUA?

Je, zamani nchi ya Israeli ilikuwa na misitu kama Biblia inavyosema?

BIBLIA inasema kwamba maeneo fulani ya Nchi ya Ahadi yalikuwa na misitu na miti mingi. (1 Fal. 10:27; Yos. 17:15, 18) Hata hivyo, wanapoona eneo kubwa lisilo na misitu katika Israeli ya leo, wengine wanatilia shaka ukweli wa jambo hilo.

Kitabu kimoja (Life in Biblical Israel) kinaeleza kwamba “zamani kulikuwa na misitu mingi katika nchi ya Israeli kuliko ilivyo leo.” Eneo la nyanda za juu lilikuwa na misonobari (Pinus halepensis), mialoni (Quercus calliprinos), na miti ya terebinthi (Pistacia palaestina). Huko Shefela, eneo lenye milima linaloanzia kwenye safu za milima ya kati hadi Pwani ya Mediterania, kulikuwa na miti mingi ya tini za mikuyu (Ficus sycomorus).

Kitabu kingine (Plants of the Bible) kinasema kwamba maeneo fulani ya nchi ya Israeli leo hayana miti kabisa. Ni nini kimechangia jambo hilo? Kitabu hicho kinaeleza hivi kuhusu jinsi jambo hilo lilivyotokea hatua kwa hatua: “Mwanadamu ameharibu sana uoto wa asili, hasa ili kupanua mashamba na maeneo ya malisho, na vilevile kupata vifaa vya kujengea na nishati.”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine