Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwbr21 Mwezi wa 11 uku. 1-11
  • Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha (11/2021)

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha (11/2021)
  • Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku la Mukutano Utumishi na Maisha—2021
  • Vichwa Vidogo
  • TAREHE 1-7/11
Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku la Mukutano Utumishi na Maisha—2021
mwbr21 Mwezi wa 11 uku. 1-11

Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha

TAREHE 1-7/11

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | YOSHUA 18-19

“Namna Inchi Iligawanywa Ilionyesha Hekima ya Yehova”

it-1-F uku. 933 fu. 5

Mupaka

Kwa hiyo inaonekana kama namna inchi iligawanywa kati ya makabila, ilitegemea mambo mbili: kupiga kura na ukubwa wa kabila. Pengine kura ilikuwa inaonyesha tu fasi yenye ilikuwa karibu na eneo yenye kila kabila ingepata, kwa kuonyesha ni wapi uriti wa kila kabila ungekuwa. Kwa mufano, upande wa kaskazini ao kusini, mashariki ao mangaribi, mu eneo tambarare la pembeni ya bahari ao mu eneo lenye milima. Yehova njo alifanya kukuwe mupango wa kupiga kura, na ile njo ingefanya kusikuwe wivu ao ugomvi kati ya makabila. (Mez 16:33) Kupitia ile mupango, Yehova angeweza pia kuongoza mambo mu njia ya kwamba hali ya kila kabila ipatane na unabii wenye kuwa mu Mwanzo 49:1-33, wenye muzee wa ukoo Yakobo alitoa na iko ku kitanda mbele akufe.

it-1-F uku. 1107 fu. 6

Uriti

Maeneo ya Uriti. Yehova njo alipatia watoto Waisraeli uriti, na ni yeye njo alionyesha Musa mipaka ya ile inchi. (Hes 34:1-12; Yos 1:4) Musa njo alipatia eneo watoto wa Gadi, watoto wa Rubeni, na nusu ya kabila ya Manase. (Hes 32:33; Yos 14:3) Makabila ingine ilipata uriti kwa kura chini ya uongozi wa Yoshua na Eleazari. (Yos 14:1, 2) Ili kutimiza unabii wa Yakobo wenye kuwa mu Mwanzo 49:5, 7, Simeoni na Lawi, hawakupewa sehemu fulani ya pekee ili ikuwe uriti wao. Eneo ya Simeoni ilikuwa ndani ya eneo ya Yuda (na ilitia ndani miji yenye kuzungukwa) (Yos 19:1-9), lakini Lawi alipewa miji 48 mu eneo yote ya Israeli. Juu Walawi walipewa kazi ya pekee ya kufanya mahali patakatifu, Yehova alisema kama atakuwa uriti wao. Walikuwa napewa kila sehemu moja ya kumi kuwa uriti wao kwa sababu ya utumishi wenye walikuwa wanatimiza. (Hes 18:20, 21; 35:6, 7) Kila familia ilikuwa napata mugawo mu eneo ya kabila yake. Vile familia zilikua naongezeka, iliomba pia watoto wapate uriti, ile ilifanya inchi ikuwe nagawanywa mu sehemu kidogo-kidogo.

it-1-F uku. 933 fu. 6

Mupaka

Kisha kura kuonyesha fasi yenye kabila fulani itariti, iliomba sasa kufikiria ukubwa wa kabila ili kujua ukubwa wa eneo yenye ile kabila ilipaswa kupewa. “Munapaswa kugawanya inchi hiyo kwa kura ili kuwa uriti kati ya familia zenu. Kwa kikundi kikubwa mutaongeza uriti wake, na kwa kikundi kidogo mutapunguza uriti wake. Uriti wa kila mutu utakuwa mahali kwenye kura yake itaangukia.” (Hes 33:54) Uamuzi wa kupiga kura ili kuonyesha fasi yenye kabila fulani ilipaswa kuriti haukuwa unabadilika, lakini kulikuwa kunafanywa mabadiliko fulani kuhusu ukubwa wa uriti. Kwa mufano, wakati ilionekana kama eneo ya Yuda ilikuwa kubwa sana, sehemu fulani za ile eneo zilipunguzwa na zikapewa kabila la Simeoni.​—Yos 19:9.

Mali ya Kiroho

it-1-F uku. 934 fu. 1

Mupaka

Habari kuhusu kugawanywa kwa eneo yenye ilikuwa upande wa mangaribi wa Yordani, inaonyesha kama kura za kwanza kupigwa, ni kura ya Yuda (Yos 15:1-63), ya Yosefu (Efraimu) (Yos 16:1-10), na ya nusu ya kabila ya Manase yenye ilikuwa upande wa mangaribi wa Yordani, (Yos 17:1-13) juu mipaka ya miji yao inatajwa. Kisha pale, kazi ya kugawanya inchi ilisimama, juu kambi ya Israeli ilihama kutoka Gilgali kuenda Shilo. (Yos 14:6; 18:1) Biblia haiseme kama ile kazi ilisimama masiku ngapi, lakini Yoshua alifikia kufokea makabila saba yenye ilibakia, juu ilichelewa kukamata sehemu ya inchi yenye ilikuwa ilishabakia. (Yos 18:2, 3) Kuko mafasirio mbalimbali yenye inatolewa ili kuonyesha sababu zenye zilifanya ile makabila saba ichelewe kufanya vile. Kulingana na maelezo ya watu fulani, waliona kama haiko lazima wafanye haraka ili kukamata sehemu yenye ilibakia ya inchi, juu walikuwa walishabeba vitu mingi wakati wa vita na juu waliwaza kama inawezekana Wakanaani hawangewashambulia palepale. Zaidi ya ile, kusitasita kukamata maeneo ya musingi yenye maadui wao walitegemea, inaweza kuwa sababu ingine yenye ilifanya wachelewe. (Yos 13:1-7) Tena, tofauti na maeneo ingine yenye ilikuwa ilishagawanywa, inawezekana ile makabila haikujua muzuri ile sehemu ya inchi ya ahadi yenye ilikuwa ilishabakia.

TAREHE 8-14/11

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | YOSHUA 20-22

“Hawakuelewa Muzuri​—Ile Inatufundisha Nini?”

w06-SW 15/4 uku. 5 fu. 3

Mambo Yanayoweza Kukusaidia Kuwasiliana na Mwenzi Wako

Kuzungumza mambo waziwazi kunaweza kuzuia kutoelewana. Mapema katika historia ya Waisraeli, makabila ya Rubeni, Gadi, na nusu ya kabila la Manase ambayo yaliishi mashariki mwa Mto Yordani, yalijenga “madhabahu kubwa yenye kuonekana wazi” kando ya Yordani. Makabila mengine hayakuelewa ni kwa nini walifanya hivyo. Makabila yaliyokuwa magharibi yalijitayarisha kwa ajili ya vita yakifikiri kwamba ndugu zao waliokuwa ng’ambo ya Yordani walikuwa waasi. Hata hivyo, kabla ya kuanza vita, makabila hayo yalituma wajumbe ili kuzungumza na makabila ya mashariki. Walitenda kwa hekima! Walipata kujua kwamba madhabahu hiyo haikuwa kwa ajili ya matoleo ya kuteketezwa wala dhabihu zisizo halali. Badala yake, yale makabila ya mashariki yaliogopa kwamba huenda baadaye yale makabila mengine yangewaambia: “Hamna fungu lolote katika Yehova.” Madhabahu hiyo ingekuwa ushahidi wa kwamba makabila hayo ya mashariki pia yalimwabudu Yehova. (Yoshua 22:10-29) Waliita madhabahu hiyo Ushahidi, labda kwa sababu ilithibitisha kwamba walimkubali Yehova kuwa Mungu wa kweli.​—Yoshua 22:34.

w08-SW 15/11 uku. 18 fu. 5

“Tufuatilie Mambo Yanayofanya Kuwe na Amani”

Huenda Waisraeli fulani walifikiri kwamba tayari kulikuwa na uthibitisho wa kutosha wa kosa na kwamba kuwashambulia kwa ghafula kungezuia watu wengi wasife. Hata hivyo, badala ya kutenda kwa haraka, makabila yaliyokuwa magharibi mwa Yordani yalituma wajumbe ili kuzungumzia tatizo hilo na ndugu zao. Yaliuliza hivi: “Mmefanya tendo gani hili la kukosa uaminifu juu ya Mungu wa Israeli kwa kugeuka nyuma msimfuate Yehova leo?” Kwa kweli, makabila ambayo yalijenga madhabahu hayo hayakutenda hivyo kwa sababu ya kukosa uaminifu. Lakini makabila hayo yangeshughulikia shtaka hilo jinsi gani? Je, yangewashambulia washtaki wao kwa maneno makali au kukataa kuzungumza nao? Makabila yaliyoshtakiwa yalijibu kwa upole, na yakaeleza waziwazi kwamba matendo yao yalichochewa na tamaa yao ya kumtumikia Yehova. Jibu lao la upole lilidumisha uhusiano wao mzuri pamoja na Mungu na liliokoa uhai. Kuzungumza kwa utulivu kulitatua tatizo hilo na kurudisha amani.​—Yos. 22:13-34.

Mali ya Kiroho

it-1-F uku. 390 fu. 4

Kanaani

Hata kama Wakanaani wengi waliokoka, ile haimaanishe kama Yehova hakutimiza ahadi yake. Tunaweza tu kusema kama “Yehova alipatia Israeli inchi yote yenye aliapia mababu zao,” aliwapatia “pumuziko pande zote,” na kama “hakuna ahadi hata moja yenye haikutimia kati ya ahadi zote za muzuri zenye Yehova aliahidi nyumba ya Israeli; zote zilitimia.” (Yos 21:43-45) Maadui wote wenye walizunguka Waisraeli waliwaogopa sana; na hakuna jambo yenye walifanya juu ya kuvuruga usalama wao. Mungu alikuwaka alishasema kama atafukuza Wakanaani “hatua kwa hatua.” Aliamua kufanya vile, juu wanyama wasiongezeke mu inchi yenye imekuwa ukiwa. (Kut 23:29, 30; Kum 7:22) Wakanaani, walikuwa na vyombo vya hali ya juu vya vita, kutia ndani magari ya vita yenye miundu ya chuma. Ile ingefanya Waisraeli washindwe kukamata maeneo fulani ya Wakanaani. Lakini, ile haimaanishe kama Yehova alishindwa kutimiza ahadi yake. (Yos 17:16-18; Amu 4:13) Habari yenye kuwa mu Biblia inaonyesha kama, sababu yenye ilifanya Waisraeli washindwe kukamata maeneo fulani, ni kukosa kuwa waaminifu.​—Hes 14:44, 45; Yos 7:1-12.

TAREHE 15-21/11

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | YOSHUA 23-24

“Yoshua Anatolea Taifa Angalisho ya Mwisho”

it-1-F uku. 82 fu. 2

Agano

Hali ilikuwa tofauti wakati Waisraeli walifika Kanaani, mu inchi ya ahadi. Juu ya kutimiza ahadi yenye alipatia mababu zao, Mungu Mwenye Mamlaka Makubwa, alipatia Israeli inchi yote juu wairiti. Hawakuingia mule sawa vile wakaaji wageni; tena Yehova aliwakataza kufanya maagano pamoja na mataifa ya kipagani ya mu ile inchi. (Kut 23:31-33; 34:11-16) Walipaswa kufuata tu sheria za Mungu, hapana za ile mataifa yenye ilipaswa kufukuzwa. (Law 18:3, 4; 20:22-24) Waliambiwa wasifanye maagano yoyote ya ndoa pamoja na ile mataifa. Ile maagano, haingefanya tu waoe wanamuke wapagani, lakini pia ingefanya wakuwe na uhusiano na familia zao za kipagani na wajiingize mu desturi na mazoea yao ya dini ya uongo, na ile ingefanya wakuwe waasi-imani na waangukie mu mutego.​—Kum 7:2-4; Kut 34:16; Jos 23:12, 13.

w07-SW 1/11 uku. 26 fu. 19-20

Neno la Yehova Halikosi Kamwe Kutimia

19 Bila shaka, kutokana na yale ambayo tumejionea wenyewe, tunaweza kusema hivi: “Halikukosa kutimia hata neno moja kati ya maneno yote mema ambayo Yehova Mungu wenu amewaambia ninyi. Yote yametimia kwenu. Halikukosa kutimia hata neno moja kati ya hayo.” (Yoshua 23:14) Yehova anawakomboa, anawalinda, na kuwatunza watumishi wake. Je, unaweza kutaja ahadi yake yoyote ambayo imekosa kutimia kwa wakati alioweka? Haiwezekani. Kwa hekima, tunaliamini Neno la Mungu lenye kutegemeka.

20 Namna gani wakati ujao? Yehova ametuambia kwamba wengi wetu tunaweza kuwa na tumaini la kuishi katika dunia iliyogeuzwa kuwa paradiso yenye kupendeza. Wachache kati yetu wana tumaini la kutawala pamoja na Kristo mbinguni. Hata tuwe na tumaini gani, tuna sababu nzuri za kuendelea kuwa waaminifu kama Yoshua. Siku moja tumaini letu litatimia. Kisha tutafikiria ahadi zote ambazo Yehova alitoa, na sisi pia tutasema: ‘Zote zimetimia.’

Mali ya Kiroho

w04-SW 1/12 uku. 12 fu. 1

Mambo Makuu Katika Kitabu cha Yoshua

24:2​—Je, Tera, baba ya Abrahamu alikuwa mwabudu-sanamu? Hapo mwanzo, Tera hakuwa mwabudu wa Yehova Mungu. Yaelekea aliabudu mungu-mwezi aliyeitwa Sin​—mungu aliyekuwa maarufu huko Uru. Kulingana na mapokeo ya Kiyahudi, huenda hata Tera alitengeneza sanamu. Hata hivyo, Abrahamu anapotii amri ya Mungu na kuondoka Uru, Tera anaambatana naye hadi Harani.​—Mwanzo 11:31.

TAREHE 22-28/11

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | WAAMUZI 1-3

“Hadisi ya Uhodari na Werevu”

w04-SW 15/3 uku. 31 fu. 3

Ehudi Avunja Nira ya Mkandamizaji

Mbinu za Ehudi hazikufaulu kwa sababu ya werevu wake au kwa sababu maadui hawakuwa na uwezo. Kutimizwa kwa makusudi ya Mungu hakutegemei uwezo wa kibinadamu. Ehudi alifaulu hasa kwa sababu Mungu alimuunga mkono kwa kuwa alitenda kulingana na mapenzi Yake yasiyoshindwa ili kuwaokoa watu Wake. Mungu alimsimamisha Ehudi, ‘na wakati Yehova alipowasimamishia watu wake waamuzi, Yehova alikuwa pamoja na mwamuzi huyo.’​—Waamuzi 2:18; 3:15.

w04-SW 15/3 uku. 30 fu. 1-3

Ehudi Avunja Nira ya Mkandamizaji

Hatua ya kwanza ambayo Ehudi alichukua ni ‘kujifanyia upanga’ wenye makali kuwili ambao ulikuwa mfupi kuweza kufichwa chini ya mavazi yake. Huenda alitarajia kupekuliwa. Kwa kawaida panga ziliwekwa upande wa kushoto wa mwili, ambapo watu waliotumia mkono wa kuume wangeweza kuzichomoa upesi. Kwa kuwa alitumia mkono wa kushoto, Ehudi alificha silaha yake “chini ya vazi lake kwenye paja lake la kuume,” upande ambao yaelekea walinzi wa mfalme hawangepekua. Kwa hiyo, Ehudi ‘akampa Egloni mfalme wa Moabu ushuru huo’ bila kuzuiwa.​—Waamuzi 3:16, 17.

Habari kuhusu matukio ya mwanzo-mwanzo katika ua wa Egloni hazijatajwa. Biblia inasema tu hivi: “Ikawa kwamba [Ehudi] alipokuwa amemaliza kutoa ule ushuru, mara moja akawaambia watu waende zao, wale waliobeba ule ushuru.” (Waamuzi 3:18) Baada ya kupeleka ushuru huo, Ehudi aliwasindikiza wale walioubeba hadi mahali salama mbali na makao ya Egloni, kisha akawaaga na kurudi. Kwa nini? Je, alikuwa ameingia kwa mfalme pamoja na wanaume hao kwa sababu ya ulinzi, kufuata utaratibu, au labda walikuwa tu wabebaji wa ushuru? Na je, alitaka waondoke kwa sababu ya usalama wake kabla ya kutekeleza mbinu yake? Hata sababu iwe nini, Ehudi alirudi kwa ujasiri katika jumba la mfalme akiwa peke yake.

“[Ehudi] akageuka na kurudi alipofika mahali penye machimbo yaliyokuwa katika Gilgali, akasema: ‘Nina neno la siri kwako, Ee mfalme.’” Biblia haielezi jinsi alivyofaulu kuingia tena mbele za Egloni. Je, walinzi hawakushuku chochote? Je, walifikiri kwamba Mwisraeli mmoja hangeweza kuhatarisha uhai wa bwana wao? Kwa kurudi peke yake, je, Ehudi alionyesha kwamba alikuwa akiwasaliti Waisraeli wenzake? Vyovyote vile, Ehudi alitafuta nafasi ya kuzungumza faraghani pamoja na mfalme, naye akaipata.​—Waamuzi 3:19.

Mali ya Kiroho

w05-SW 15/1 uku. 24 fu. 7

Mambo Makuu Katika Kitabu cha Waamuzi

2:10-12. Tunapaswa kuwa na programu ya kawaida ya funzo la Biblia ili ‘tusisahau matendo ya Yehova.’ (Zaburi 103:2) Wazazi wanahitaji kukazia kweli ya Neno la Mungu katika mioyo ya watoto wao.​—Kumbukumbu la Torati 6:6-9.

TAREHE 29/11–5/12

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | WAAMUZI 4-5

“Yehova Anatumia Wanamuke Wawili ili Kuokoa Watu Wake”

w15 1/8 uku. 12 fu. 6

‘Nilisimama Kama Mama Katika Israeli’

Jina Sisera liliwaogopesha na kuwatetemesha sana Waisraeli. Dini ya Wakanaani na desturi yao havikukuwa na huruma, vilikuwa na mambo kama vile ukahaba kwenye hekalu na kuunguza watoto ili kuwatoa kwa miungu yao. Hali ilikuwa namna gani kwa sababu ya kutawaliwa na jenerali Mukanaani na jeshi lake? Wimbo wa Debora unaonyesha kama ilikuwa vigumu kusafiri katika inchi na hakuna mutu aliishi tena katika vijiji. (Waamuzi 5:6, 7) Wazia namna watu walikuwa wanatetemeka katika mapori na vilima, waliogopa kulima ao kuishi katika vijiji vyenye havina ukuta, na kusafiri katika barabara ili wasishambuliwe, watoto wao wasikamatwe, na bibi zao wasilalwe kinguvu.

w15 1/8 uku. 13 fu. 1

‘Nilisimama Kama Mama Katika Israeli’

Watu waliishi katika woga kwa miaka 20, mupaka wakati Yehova aliona kuwa watu wake wenye vichwa vigumu walikuwa tayari kubadilika. Ao kama vile maneno yaliyoongozwa na roho ya Mungu katika wimbo wa Debora na Baraka yanasema, ‘Mupaka mimi, Debora, niliposimama, mupaka niliposimama kama mama katika Israeli.’ Hatujue ikiwa Debora, bibi ya mwanaume mwenye kuitwa Lapidothi, alikuwa na watoto, lakini neno mama lilitumiwa kwa njia ya mufano. Kwa kweli, Yehova alimupatia Debora kazi ya kulinda watu wake kama mama. Yehova alimuambia Debora aite muamuzi Baraka, mwanaume mwenye nguvu na mwenye imani, ili apigane vita na Sisera.​—Waamuzi 4:3, 6, 7; 5:7.

w15 1/8 uku. 15 fu. 2

‘Nilisimama Kama Mama Katika Israeli’

Yaeli alipaswa kufikiri haraka. Alimupatia Sisera nafasi ya kupumzikia. Sisera alimuambia Yaeli asiambie mutu yeyote mwenye anakuja kumutafuta kama alikuwa pale. Wakati Sisera alilala, Yaeli alimufunika, na wakati alimuomba maji, alimupatia maziwa mazito. Mara moja, Sisera akalala usingizi muzito. Kisha Yaeli akakamata vyombo viwili vya nyumbani vyenye wanawake wenye kukaa katika mahema walikuwa wanatumia mara nyingi na kwa ufundi. Alitumia nyundo (marteau) na chombo fulani chenye kuwa kama musumari. Yaeli aliinama karibu na kichwa cha Sisera, sasa alikuwa mbele ya jambo ngumu zaidi lenye alipaswa kufanya ili kutimiza hukumu ya Mungu. Kuwa na mashaka ao kusita kidogo kungemuletea hatari. Yaeli aliwaza juu ya watu wa Mungu na namna mutu huyo alikuwa amewatesa kwa miaka mingi? Ao alifikiria pendeleo la kujiunga upande wa Yehova? Habari hiyo haiseme kitu juu ya mambo hayo. Tunajua tu kama alitenda bila kukawia. Aliua Sisera!​—Waamuzi 4:18-21; 5:24-27.

Mali ya Kiroho

w05-SW 15/1 uku. 25 fu. 5

Mambo Makuu Katika Kitabu cha Waamuzi

5:20​—Nyota zilipiganaje zikiwa mbinguni kwa niaba ya Baraka? Biblia haisemi kama jambo hilo lilihusisha msaada wa malaika, vipande vingi vya mawe kutoka kwenye nyota ambavyo vilionwa kuwa ishara mbaya na wanaume wenye hekima wa Sisera, au labda ubashiri wa Sisera ambao haukutimia. Lakini bila shaka Mungu aliingilia kati kwa njia fulani.

Hotuba

w06-SW 1/3 uku. 28-29

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Paulo aliwaandikia Wakristo wa kutaniko la Korintho hivi: “Kama ilivyo katika makutaniko yote ya watakatifu, wanawake na wakae kimya katika makutaniko, kwa maana hairuhusiwi kwao kusema.” (1 Wakorintho 14:33, 34) Ili tuelewe vizuri maneno hayo, ni muhimu tuchunguze muktadha wa shauri hilo la Paulo.

Kwenye 1 Wakorintho sura ya 14, Paulo alizungumzia mambo yanayohusiana na mikutano ya kutaniko la Kikristo. Alieleza kuhusu mambo yaliyopaswa kuzungumziwa kwenye mikutano hiyo na akapendekeza jinsi ilivyopaswa kuendeshwa. (1 Wakorintho 14:1-6, 26-34) Zaidi ya hayo, alikazia kusudi la mikutano ya Kikristo, yaani, “ili kutaniko lijengwe.”​—1 Wakorintho 14:4, 5, 12, 26.

Agizo la Paulo kuhusu “kukaa kimya” linarudiwa mara tatu kwenye 1 Wakorintho sura ya 14. Kila mara, linatolewa kwa kikundi tofauti kutanikoni, lakini katika pindi zote hizo, linatolewa kwa sababu ileile, yaani, ili ‘mambo yote yatendeke kwa adabu na kwa mpango.’​—1 Wakorintho 14:40.

Kwanza, Paulo alisema: “Mtu akisema kwa lugha, na wawe wawili au, ikiwa ni zaidi, watatu, wasipite hapo, na kwa zamu; na mtu fulani atafsiri. Lakini ikiwa hakuna mtafsiri, na akae kimya katika kutaniko na aseme moyoni mwake mwenyewe na kwa Mungu.” (1 Wakorintho 14:27, 28) Hilo halikumaanisha kwamba mtu huyo hakupaswa kamwe kusema kwenye mikutano, lakini lilimaanisha kwamba kulikuwa na nyakati ambapo alipaswa kukaa kimya. Ni wazi kwamba kusudi la mikutano, ambalo ni kujengana, lisingetimizwa ikiwa mtu huyo angezungumza katika lugha isiyoeleweka.

Pili, Paulo alisema: “Manabii wawili au watatu na waseme, na wale wengine waitambue maana. Lakini ikiwa kuna ufunuo kwa mwingine wakati ameketi hapo, yule wa kwanza na akae kimya.” Hilo halikumaanisha kwamba yule nabii wa kwanza hakupaswa kusema kwenye mikutano, lakini linamaanisha tu kwamba nyakati nyingine alihitaji kukaa kimya. Kisha, yule aliyepata ufunuo kwa njia ya kimuujiza angehutubia kutaniko, na kusudi la mkutano lingetimizwa, yaani, “wote watiwe moyo.”​—1 Wakorintho 14:26, 29-31.

Tatu, Paulo alisema hivi kuhusu wanawake Wakristo peke yao: “Wanawake na wakae kimya katika makutaniko, kwa maana hairuhusiwi kwao kusema, bali na wajitiishe.” (1 Wakorintho 14:34) Kwa nini Paulo alitoa amri hiyo kwa akina dada? Aliitoa ili kuwe na utaratibu kutanikoni. Alisema hivi: “Basi, ikiwa wanataka kujifunza jambo fulani, acheni wawaulize waume zao wenyewe nyumbani, kwa maana inafedhehesha kwa mwanamke kusema katika kutaniko.”​—1 Wakorintho 14:35.

Labda dada wengine walikuwa wakipinga yale yaliyosemwa kutanikoni. Shauri la Paulo liliwasaidia akina dada kuepuka roho hiyo inayosababisha mvurugo na kukubali kwa unyenyekevu mahali pao katika mpango wa Yehova wa ukichwa, hasa kuhusiana na waume zao. (1 Wakorintho 11:3) Isitoshe, kwa kukaa kimya, akina dada wangeonyesha kwamba hawakutamani daraka la kuwa walimu kutanikoni. Alipomwandikia Timotheo, Paulo alionyesha kwamba haingefaa kwa mwanamke kuwa mwalimu kutanikoni: “Simruhusu mwanamke kufundisha, wala kuwa na mamlaka juu ya mwanamume, bali kuwa kimya.”​—1 Timotheo 2:12.

Je, hilo linamaanisha kwamba mwanamke Mkristo hapaswi kamwe kusema wakati wa mkutano wa kutaniko? Hapana. Wakati wa Paulo kulikuwa na pindi ambazo wanawake Wakristo, labda wakiwa wamechochewa na roho takatifu, walisali au walitoa unabii kutanikoni. Katika pindi kama hizo, walitambua mahali pao kwa kufunika vichwa vyao. (1 Wakorintho 11:5) Isitoshe, wakati wa Paulo na pia leo, akina dada na ndugu wanahimizwa kutoa tangazo la hadharani la tumaini lao. (Waebrania 10:23-25) Zaidi ya kufanya hivyo katika mahubiri, akina dada hutangaza tumaini lao na kuwatia wengine moyo wakati wa mikutano ya kutaniko wanapoombwa kutoa maelezo yaliyotayarishwa vizuri na pia kwa kukubali migawo ya kufanya maonyesho au kutoa hotuba za wanafunzi.

Hivyo, wanawake Wakristo ‘hukaa kimya’ kwa kutojaribu kuchukua daraka la mwanamume na kufundisha kutaniko. Hawatokezi maswali yanayosababisha ubishi ambayo yanaweza kupinga mamlaka ya wale wanaofundisha kutanikoni. Kwa kutimiza daraka lao kutanikoni, dada Wakristo husaidia sana kutokeza hali ya amani ambayo hufanya “mambo yote [kwenye mikutano ya kutaniko] yatendeke kwa ajili ya kujengana.”​—1 Wakorintho 14:26, 33.

TAREHE 6-12/12

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | WAAMUZI 6-7

“Uende na Nguvu Zenye Uko Nazo”

w02-SW 15/2 uku. 6-7

Kanuni za Kimungu Zaweza Kukufaidi

Gideoni, mmoja wa waamuzi wa Waebrania wa kale, hakujitukuza bali alijieleza kwa njia ya unyofu. Hakujipendekeza kuongoza Waisraeli. Hata hivyo, Gideoni alipochaguliwa kuwa kiongozi, yeye alikumbuka alikuwa duni tu. Gideoni alisema: “Tazama jamaa zangu ndio walio maskini sana katika Manase, na mimi ndimi niliye mdogo katika nyumba ya baba yangu.”​—Waamuzi 6:12-16.

w05-SW 15/7 uku. 16 fu. 3

“Upanga wa Yehova na wa Gideoni!”

Wazia hofu inayowakumba Wamidiani! Kwa ghafula, kimya cha usiku kinakatizwa na kishindo cha kuvunjwa kwa ile mitungi 300, kupigwa kwa zile baragumu 300, na makelele ya wale watu 300. Wamidiani wanashtuliwa hasa wanaposikia maneno haya, “Upanga wa Mungu na wa Gideoni!,” nao wanapaaza kilio. Katika hali hiyo, hawawezi kuwatambua maadui wao. Wale watu 300 wanaendelea kusimama mahali pao Yehova anapowafanya maadui wao wauane. Wamidiani wanashindwa kabisa, hawawezi kutoroka, nao maadui waliosalia wanafuatiliwa na kuuawa. Hivyo, Wamidiani hawawezi kamwe kuwakandamiza Waisraeli tena. Hatimaye, uvamizi wa muda mrefu wa Wamidiani waliomiliki nchi ya Waisraeli unakomeshwa.​—Waamuzi 7:19-25; 8:10-12, 28.

Mali ya Kiroho

w05-SW 15/1 uku. 26 fu. 6

Mambo Makuu Katika Kitabu cha Waamuzi

6:25-27. Gideoni alitumia busara ili kutowakasirisha wapinzani wake bila sababu. Tunapohubiri habari njema, tunapaswa kuwa waangalifu tusiwakasirishe wengine bila sababu kwa namna tunavyozungumza.

TAREHE 13-19/12

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | WAAMUZI 8-9

“Ni Muzuri Zaidi Kuwa na Unyenyekevu Kuliko Kiburi”

w00-SW 15/8 uku. 25 fu. 4

Unafanyaje Kunapotokea Kutoelewana?

Gideoni, aliyekuwa akipigana vikali na Wamidiani, aliwaita Waefraimu wamsaidie. Hata hivyo, baada ya vita, Waefraimu walimgeuka Gideoni na kulalamika kwamba hakuwaita mwanzoni mwa vita. Masimulizi yasema kwamba ‘waliteta naye sana.’ Gideoni akawajibu hivi: “Je! mimi nimefanya nini sasa kama mlivyofanya ninyi? Hayo masazo ya zabibu za Efraimu si mema kuliko mavuno ya Abiezeri? Mungu amewatia hao wakuu wa Midiani, Orebu na Zeebu, mikononi mwenu; na mimi nilipata kufanya nini kama mlivyofanya ninyi?” (Waamuzi 8:1-3) Kwa maneno yake yaliyoteuliwa vizuri na yenye kutuliza, Gideoni aliepuka jambo ambalo lingekuwa vita vikali kati ya makabila. Huenda watu wa kabila la Efraimu walikuwa wenye majivuno na kiburi. Hata hivyo, hilo halikumzuia Gideoni asijitahidi kupata suluhisho la amani. Je, nasi twaweza kufanya hivyo?

w17.01 uku. 20 fu. 15

Sababu Gani Sifa ya Kiasi Ingali ya Maana?

15 Gideoni ni mufano wa muzuri zaidi wa mutu mwenye alionyesha sifa ya kiasi. Wakati Yehova alimupatia mugawo wa kukomboa Waisraeli kutoka kwa Wamidiani, Gideoni alisema hivi: ‘Elfu yangu ndiyo ndogo zaidi katika Manase, na mimi ndiye mudogo zaidi katika nyumba ya baba yangu.’ (Waamuzi 6:15) Lakini, Gideoni alimutegemea Yehova na alikubali mugawo huo. Kisha Gideoni alihakikisha kama alielewa kabisa mambo yenye Yehova alimuomba afanye na alimuomba muongozo wake katika sala. (Waamuzi 6:36-40) Gideoni alikuwa mwanaume mwenye nguvu na ujasiri, lakini pia alikuwa na hekima na muangalifu. (Waamuzi 6:11, 27) Tena, wakati watu walipenda kumufanya akuwe kiongozi juu yao, alikataa. Kisha kufanya mambo yenye Yehova alimuomba afanye, alirudia nyumbani kwake.​—Waamuzi 8:22, 23, 29.

w08-SW 15/2 uku. 9 fu. 9

Tembea Katika Njia za Yehova

9 Ili tuwe marafiki wa Mungu, ni lazima tuwe “wanyenyekevu katika akili.” (1 Pet. 3:8; Zab. 138:6) Umuhimu wa unyenyekevu unaonyeshwa katika Waamuzi sura ya 9. Yothamu, mwana wa Gideoni alisema hivi: “Hapo zamani za kale, miti ilienda kumtia mafuta mfalme juu yao.” Mzeituni, mtini, na mzabibu ulitajwa. Miti hiyo iliwakilisha watu waliostahili lakini ambao hawakutafuta kuwatawala Waisraeli wenzao. Lakini mkwamba, ambao haufai kwa kazi yoyote ile ila kwa kuni, uliwakilisha utawala wa Abimeleki mwenye kiburi, muuaji aliyetamani kuwatawala wenzake. Ingawa ‘alijitwalia ukuu juu ya Israeli kwa miaka mitatu,’ alikufa kifo cha mapema. (Amu. 9:8-15, 22, 50-54) Ni vizuri kama nini kuwa “wanyenyekevu katika akili”!

Mali ya Kiroho

it-1-F uku. 784 fu. 5

Efodi, 1

Gideoni alipenda kumuletea Yehova sifa na kukumbuka ushindi wenye alikuwa amepatia Israeli. Lakini efodi ‘ilikuwa mutego kwa Gideoni na kwa nyumba yake’ juu Waisraeli walifanya uasherati wa kiroho pamoja nayo kwa kuiabudu. (Amu 8:27) Lakini, Biblia haiseme kama Gideoni naye aliiabudu; tunasema vile, juu mutume Paulo anamutaya kati ya “wingu kubwa” ya mashahidi wa Yehova waaminifu wenye waliishi mbele ya Kristo.​—Ebr 11:32; 12:1.

TAREHE 20-26/12

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | WAAMUZI 10-12

“Yefta Alikuwa Mutu wa Kiroho”

w16.04 uku. 5 fu. 9

Tunakubaliwa na Mungu Ikiwa Tunabakia Waaminifu Kwake

9 Inawezekana mufano wa Yosefu ulimusaidia Yeftha. Pengine alijifunza namna Yosefu alisamehe ndugu zake hata kama walimuchukia. (Mwanzo 37:4; 45:4, 5) Pengine kufikiria sana mufano huo kulimusaidia Yeftha atende katika njia yenye kumupendeza Yehova. Yeftha aliumia kabisa kwa sababu ya jambo lenye ndugu zake walimutendea. Lakini kupigana kwa ajili ya jina la Yehova na watu wake ndilo lilikuwa jambo la maana zaidi kuliko namna Yeftha mwenyewe alikuwa anajisikia. (Waamuzi 11:9) Aliazimia kuendelea kuwa muaminifu kwa Yehova. Hilo lilifanya yeye na Waisraeli wengine wabarikiwe na Yehova.​—Waebrania 11:32, 33.

it-2-F uku. 1202 fu. 6

Yefta

Yefta, mwanaume mwenye bidii, alitenda bila kukawia. Alitumia mufalme wa Waamoni ujumbe kwa kusema kama Waamoni walishambulia inchi ya Waisraeli. Mufalme alijibia kama inchi yenye Waisraeli walikamata ilikuwa ya Waamoni. (Amu 11:12, 13) Ile haikuonyesha kama Yefta ni mupiganaji vita mwenye hana huruma ao mupiganaji vita mwenye hajue kitu, lakini ilionyesha kama ni mutu mwenye alijifunza historia, zaidi sana historia kuhusu namna Mungu alishugulika na watu wake. Alipinga maneno ya mufalme wa Waamoni kwa kusema kama (1) Israeli haikusumbua Waamoni, Wamoabu, na Waedomu (Amu 11:14-18; Kum 2:9, 19, 37; 2Ny 20:10, 11); (2) Wakati Waisraeli walikuwa wanapigana, ile inchi haikukuwa ya Waamoni, lakini ilikuwa mu mikono ya Waamori Wakanaani, na Mungu alikuwa alishatia Sihoni mufalme wao na inchi yake mu mikono ya Waisraeli; (3) Mu miaka 300 yenye Waisraeli walikuwa wamefanya mule, Waamoni hawakuwasumbua. Sasa, nini njo ingefanya waseme kama ile inchi ni yao?​—Amu 11:19-27.

it-2-F uku. 1202 fu. 7

Yefta

Yefta aligusia kishina kabisa ya mambo, wakati alisema kama ile tatizo ilihusu ibada. Alisema kama Yehova Mungu alikuwa alishaka patia Israeli ile inchi, njo maana hawangeweza kukata hata sehemu kidogo ya ile inchi na kuipatia waabudu wa Mungu wa uwongo. Alisema kama Kemoshi njo mungu wa Waamoni. Watu fulani walisema kama alikosea. Lakini, hata kama Milkomu njo alikuwa mungu wa Waamoni, ka Kemoshi, mungu wa Wamoabu, ile mataifa yote ilikuwa naabudu miungu mingi. Wanamuke wa kigeni, walifanya hata Sulemani afanye kosa ya kuingiza ibada ya Kemoshi mu Israeli. (Amu 11:24; 1Fa 11:1, 7, 8, 33; 2Fa 23:13) Zaidi ya ile, kulingana na wasomi fulani, “Kemoshi” inaweza kumaanisha “Mushindi, Mwenye kushindana”. (ona Gesenius’s Hebrew and Chaldee Lexicon, yenye ilitafsiriwa na S. Tregelles mu 1901, uku. 401.) Inawezekana Yefta alizungumuzia ule mungu juu Waamoni walikuwa nasema kama ni ule mungu njo iko na uwezo wa ‘kushinda’ ao ‘wakushindana’ na wengine na kuwapatia inchi.

Mali ya Kiroho

it-2-F uku. 1201

Yefta

Yefta, Mutoto Mwenye Kujulikana Kisheria. Mama yake na Yefta, alikuwaka “kahaba;” lakini, ile haimaanishe kama Yefta alizaliwaka mu ukahaba ao kama alikuwa mutoto mwenye hajulikane kisheria. Mama yake alikuwaka njo kahaba mbele akuwe bibi wa pili wa Gileadi, alifanya tu sawa Rahabu, mwenye naye alikuwaka kahaba lakini kisha, akaolewa na Salmoni. (Amu 11:1; Yos 2:1; Mt 1:5) Jambo yenye inaonyesha kama Yefta alijulikana kisheria, ni kwamba ndugu zake wenye Gileadi alizalaka na bibi yake wa kwanza, walimufukuzaka juu asikuwe muriti pamoja nao. (Amu 11:2) Zaidi ya ile, Yefta alifikia kukubaliwa kuwa kiongozi wa wanaume wa Gileadi (wenye kati yao, ndugu za Yefta walionekana sawa vile watu wa maana zaidi). (Amu 11:11) Tena, Yefta alimutolea Mungu zabihu ku tabenakulo. (Amu 11:30, 31) Mutoto mwenye hakujulikana kisheria, hangefanya ile mambo yote, juu sheria ilisema hivi waziwazi: “Mwana-haramu yeyote hapaswe kuingia katika kutaniko la Yehova. Hata kufikia kizazi cha kumi (10), muzao wake yeyote hapaswe kuingia katika kutaniko la Yehova.”​—Kum 23:2.

TAREHE 27/12–2/01

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | WAAMUZI 13-14

“Habari ya Manoa na Bibi Yake Inaweza Kufundisha Nini Wazazi?”

w13 15/8 uku. 16 fu. 1

Wazazi​—Muwazoeze Watoto Wenu Tangu Utoto Muchanga

Fikiria Manoa aliyekuwa wa kabila la Dani, na aliyeishi katika muji wa Sora katika Israeli. Malaika wa Yehova alimuelezea bibi ya Manoa, aliyekuwa tasa, kwamba angezaa mwana. (Amu. 13:2, 3) Mwanaume huyo mwaminifu na bibi yake walitazamia kwa furaha sana kupata mutoto. Hata hivyo, kuna mambo ambayo yaliwahangaisha. Kwa hiyo Manoa alisali hivi: ‘Nakuomba razi, Yehova. Tafazali, yule mutu wa Mungu wa kweli ambaye ulimutuma na arudi kwetu tena, atufundishe yale tunayopaswa kumutendea huyo mutoto atakayezaliwa.’ (Amu. 13:8) Manoa na bibi yake walitafuta kujua namna gani wangemulea mutoto wao. Bila shaka, walimufundisha mwana wao Samsoni, sheria ya Mungu, na walipata matokeo mazuri. Biblia inasema hivi: ‘Baada ya muda roho ya Yehova ikaanza kumuchochea [Samsoni].’ Matokeo yalikuwa mazuri kwa sababu mwamuzi Samsoni alifanya mambo mengi ya ajabu.​—Amu. 13:25; 14:5, 6; 15:14, 15.

w05-SW 15/3 uku. 25-26

Samsoni Ashinda kwa Nguvu za Yehova!

Samsoni alipoendelea kukua, ‘Yehova aliendelea kumbariki.’ (Waamuzi 13:24) Siku moja, Samsoni aliwaendea baba na mama yake na kuwaambia: “Nimemwona mwanamke mmoja huko Timna kati ya binti za Wafilisti, basi sasa mniletee mwanamke huyo awe mke wangu.” (Waamuzi 14:2) Hebu wazia jinsi walivyoshangaa. Badala ya kuwakomboa Waisraeli kutoka mikononi mwa wakandamizaji wao, mwana wao alitaka kufanya mapatano ya ndoa pamoja nao. Kumwoa mwanamke ambaye alikuwa mwabudu wa miungu ya kipagani kulikuwa kinyume cha Sheria ya Mungu. (Kutoka 34:11-16) Hivyo, wazazi wake walikataa na kumwambia: “Je, hakuna mwanamke yeyote kati ya binti za ndugu zako na kati ya watu wangu wote, hivi kwamba uende kumchukua mwanamke kutoka kwa Wafilisti wasiotahiriwa?” Lakini bado Samsoni alisisitiza hivi: “Nileteeni huyo, kwa maana ndiye anayestahili kabisa machoni pangu.”​—Waamuzi 14:3.

Mali ya Kiroho

w05-SW 15/3 uku. 26 fu. 1

Samsoni Ashinda kwa Nguvu za Yehova!

Mwanamke huyo Mfilisti alikuwaje mwenye ‘kustahili kabisa’ machoni pa Samsoni? Si katika maana ya kwamba alikuwa “mrembo na mwenye kuvutia,” chasema kichapo Cyclopedia cha McClintock na Strong, “bali alistahili katika maana ya kwamba angeweza kumsaidia kutimiza lengo lake.” Kutimiza lengo gani? Andiko la Waamuzi 14:4 linaeleza kwamba Samsoni “alikuwa akitafuta nafasi ya kuwapiga Wafilisti.” Samsoni alipendezwa na mwanamke huyo kwa lengo hilo. Samsoni alipokuwa mtu mzima, ‘roho ya Yehova ilianza kumchochea,’ au ilimsukuma kutenda. (Waamuzi 13:25) Kwa hiyo, roho ya Yehova ndiyo iliyomchochea Samsoni kufanya ombi lisilo la kawaida la kupewa mke na pia ndiyo iliyomchochea muda wote aliotumika akiwa mwamuzi juu ya Israeli. Je, Samsoni alipata nafasi aliyokuwa akitafuta? Kwanza, acheni tuone jinsi Yehova alivyomhakikishia kwamba angemtegemeza.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine