Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha
TAREHE 7-13/3
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 1 SAMWELI 12-13
“Kimbelembele Kinapatishaka Mutu Haya”
w00-SW 1/8 uku. 13 fu. 17
Kimbelembele Hutokeza Aibu
17 Ukitazama kijuujuu tu, huenda matendo ya Sauli yakaonekana kuwa yalifaa. Kwani, watu wa Mungu walikuwa “katika dhiki,” na ‘kufadhaishwa,’ wakitetemeka kwa sababu ya hali mbaya waliyokabili. (1 Samweli 13:6, 7) Si vibaya kuchukua hatua ikihitajika. Lakini, kumbuka kwamba Yehova anaweza kusoma mioyo na kutambua nia zetu za ndani kabisa. (1 Samweli 16:7) Kwa hiyo, huenda aliona mambo fulani kuhusu Sauli ambayo hayatajwi moja kwa moja katika masimulizi hayo ya Biblia. Kwa mfano, huenda Yehova aliona kwamba Sauli alikosa subira kwa sababu ya kiburi. Labda Sauli alikasirika sana kwamba yeye—mfalme wa Israeli yote—ati amngoje mtu ambaye alimwona kuwa nabii aliyezeeka, mwenye kuchelewa-chelewa! Kwa vyovyote vile, Sauli alihisi kwamba kuchelewa kwa Samweli kulimpa haki ya kujifanyia mambo mwenyewe na kupuuza maagizo ya wazi ambayo alikuwa amepewa. Matokeo yakawaje? Samweli hakumsifu Sauli kwa hatua aliyochukua. Badala yake, alimkemea akisema: “Ufalme wako hautadumu . . . kwa sababu wewe hukulishika neno lile BWANA alilokuamuru.” (1 Samweli 13:13, 14) Kwa mara nyingine tena, kimbelembele kilitokeza aibu.
w07-SW 15/6 uku. 27 fu. 8
Yehova Anathamini Utii Wako
8 Maelezo ya Biblia kuhusu Mfalme Sauli yanakazia umuhimu wa utii. Sauli alikuwa mtawala mnyenyekevu na mwenye kiasi alipoanza, alikuwa ‘mdogo machoni pake mwenyewe.’ Hata hivyo, baada ya muda, alianza kufanya maamuzi kwa kiburi na kwa kutegemea mawazo yasiyofaa. (1 Samweli 10:21, 22; 15:17) Wakati mmoja, Sauli alipaswa kupigana na Wafilisti. Samweli alimwambia mfalme Sauli amngoje ili aje kumtolea Yehova dhabihu kisha ampe mwongozo zaidi. Hata hivyo, Samweli hakuja haraka kama ilivyotazamiwa, nao watu wakaanza kutawanyika. Sauli alipoona hivyo, “akaitoa dhabihu ya kuteketezwa.” Jambo hilo halikumpendeza Yehova. Mwishowe Samweli alipofika, mfalme alitoa kisingizio cha kutotii kwake. Alisema kwamba kwa sababu Samweli alichelewa, ‘alijilazimisha’ kutoa dhabihu ya kuteketezwa ili kuutuliza uso wa Yehova. Mfalme Sauli aliona kwamba kutoa dhabihu hiyo ni jambo la maana sana kuliko kutii maagizo aliyopewa ya kumngojea Samweli ili atoe dhabihu hiyo. Samweli alimwambia hivi: “Umetenda kipumbavu. Hukuishika amri ya Yehova Mungu wako ambayo alikuamuru.” Sauli alipoteza cheo chake cha kuwa mfalme kwa sababu hakumtii Yehova.—1 Samweli 10:8; 13:5-13.
Mali ya Kiroho
w11-SW 15/7 uku. 13 fu. 15
Je, Utafuata Mwongozo wa Yehova Wenye Upendo?
15 Je, watu hao walifikiria kwamba kwa njia fulani mfalme wa kibinadamu angekuwa halisi zaidi, mwenye kutegemeka zaidi, kuliko Yehova? Ikiwa ndivyo, kwa kweli walikuwa wakifuatia vitu visivyo vya kweli! Na walikuwa katika hatari ya kufuatia vitu vingine vingi vya kishetani visivyo vya kweli. Wafalme wa kibinadamu wangewaongoza kwa urahisi kuabudu sanamu. Watu wanaoabudu sanamu wanakosea kwa kufikiria kwamba vitu vinavyoonekana, yaani, miungu iliyotengenezwa kwa mbao au mawe, kwa njia fulani ni halisi zaidi, ni yenye kutegemeka zaidi kuliko Yehova, Mungu asiyeonekana ambaye aliumba vitu vyote. Lakini kama mtume Paulo alivyosema, sanamu “si kitu.” (1 Kor. 8:4) Haziwezi kuona, kusikia, kuzungumza, au kutenda. Unaweza kuziona na kuzigusa, lakini ikiwa ungeabudu sanamu, kwa kweli ungekuwa ukifuatia kitu kisicho cha kweli, jambo lisilo halisi ambalo lingeleta msiba tu.—Zab. 115:4-8.
TAREHE 14-20/3
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 1 SAMWELI 14-15
“Kutii Ni Muzuri Kuliko Zabihu”
w07-SW 15/6 uku. 26 fu. 4
Yehova Anathamini Utii Wako
4 Akiwa Muumba, tayari Yehova anamiliki vitu vyote vya kimwili tulivyo navyo. Kwa kuwa ndivyo ilivyo, je, kuna kitu chochote ambacho tunaweza kumpa? Ndiyo, tunaweza kumpa kitu fulani chenye thamani sana. Ni kitu gani hicho? Tunaweza kupata jibu katika himizo lifuatalo: “Uwe na hekima, mwanangu, na kuufanya moyo wangu ushangilie, ili nipate kumjibu anayenidhihaki.” (Methali 27:11) Tunaweza kumpa Mungu utii wetu. Hata ingawa tuna hali na malezi tofauti, kila mmoja wetu anapotii anaweza kujibu shtaka lenye uovu la Shetani Ibilisi anayedai kwamba wanadamu hawawezi kuendelea kuwa washikamanifu kwa Mungu wakijaribiwa. Hilo ni pendeleo kubwa kama nini!
it-2-F uku. 429 fu. 1
Kutii
Hakuna jambo yoyote yenye inaweza kukamata nafasi ya kutii. Mungu hawezi kukubali mutu mwenye anakatala kutii. Samweli alimuambia Mufalme Sauli hivi: “Je, Yehova anapendezwa na matoleo ya kuteketezwa na zabihu sawasawa na kutii [sha·maʽʹ] sauti ya Yehova? Angalia! Kutii [neno kwa neno, kusikia] ni muzuri kuliko zabihu, na kusikiliza kwa uangalifu kuliko mafuta ya kondoo-dume.” (1Sa 15:22) Kushindwa kutii ni kukatala neno ya Yehova. Ile inaonyesha kama mutu haamini, na hatumainie kabisa ile neno na Mwenye aliitoa. Kwa hiyo, mutu mwenye anashindwa kutii iko sawa na ule mwenye anafanya uaguzi ao mwenye anafanya ibada ya sanamu. (1Sa 15:23; linganisha na Ro 6:16.) Kusema tu kama tutafanya kitu fulani, lakini hatukifanye, haina maana; kukatala kufanya kitu yenye tuliombwa kufanya ni kukosa kuamini na kuheshimia mutu mwenye alituomba kufanya vile. (Mt 21:28-32) Wale wenye wanasikiliza tu kweli ya Mungu na kuikubali mu akili, lakini hawatende kulingana na yenye walisikia, wanajidanganya wenyewe kwa mawazo ya uongo na hawawezi kubarikiwa. (Yak 1:22-25) Mwana wa Mungu alionyesha kama hata wale wenye wanafanya mambo yenye inafanana na ile yenye tunaombwa kufanya, lakini wanaifanya mu njia ya mubaya na nia ya mubaya hawataingia mu Ufalme na watatupwa mbali kabisa.—Mt 7:15-23.
Mali ya Kiroho
it-2-F uku. 598 fu. 7
Huruma
Kukubali mutu atuchochee kuonyesha huruma yenye haipatane na mapenzi ya Mungu inaweza kuwa na matokeo ya mubaya sana. Mambo yenye ilimupata Mufalme Sauli inaonyesha ile. Waamaleki njo walikuwa watu wa kwanza wenye walipinga Waisraeli wakati walitoka Misri. Wakati ilifika ya kuwahukumu kulingana na vile Mungu alisema. Sauli alikuwa ashaamuriwa kama hapaswe kuwasikilia huruma. Lakini alichochewa na watu wake, na ile ilifanya asitii kabisa amri yenye Yehova alimupatia. Kwa hiyo, Yehova hakumukubali tena kuwa mufalme. (1Sa 15:2-24) Juu tusikataliwe na Yehova sawa vile Sauli, tunapaswa kuendelea kupenda njia zake za haki na zaidi sana kubakia washikamanifu kwake.
TAREHE 21-27/3
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 1 SAMWELI 16-17
“Vita Ni ya Yehova”
“Vita Ni vya Yehova”
Daudi alimuhakikishia Sauli kwa kumuelezea mambo yenye alifanya wakati simba na dubu walishambulia kondoo. Alikuwa anajisifu? Hapana. Daudi alijua namna gani aliweza kupata ushindi. Alisema hivi: ‘Yehova, aliyenikomboa kutoka katika makucha ya simba na kutoka katika makucha ya dubu, yeye ndiye atakayenikomboa kutoka mukononi mwa huyu Mufilisti.’ Sauli alifikia kukubali. Kwa hiyo alimuambia hivi: ‘Enda, na Yehova akuwe pamoja nawe.’—1 Samweli 17:37.
Unapenda kuwa na imani kama Daudi? Kama jibu ni ndiyo, jua kwamba imani ya Daudi haikuwa ndoto ao jambo fulani lenye haliwezi kufanyika. Alikuwa na imani katika Mungu wake kwa sababu ya mambo yenye alijua na mambo yenye alikutana nayo. Alijua kwamba Yehova ni Mulinzi mwenye upendo na Mutimizaji wa ahadi zake. Kama tunapenda kuwa na imani kama hiyo, tunapaswa kujifunza juu ya Mungu wa kweli mwenye kuzungumuziwa katika Biblia. Wakati tunaishi kulingana na mambo yenye tunajifunza, sisi pia tutaona kwamba matokeo mazuri yenye tutapata yatatia nguvu imani yetu.—Waebrania 11:1.
“Vita Ni vya Yehova”
Siku hiyo, jibu la Daudi lilionyesha kwamba alikuwa kabisa na imani kubwa. Wazia tu namna kijana mudogo anamulalamikia Goliathi: ‘Unakuja kwangu ukiwa na upanga na mukuki na fumo, lakini mimi ninakuja kwako nikiwa na jina la Yehova wa majeshi, Mungu wa vikosi vya Israeli, ambaye umemutukana.’ Daudi alijua kwamba silaha na nguvu za mwanadamu haviko vya maana sana. Goliathi alimuzarau Yehova Mungu, na Yehova alipaswa kufanya jambo fulani. Daudi alionyesha kwamba “vita ni vya Yehova.”—1 Samweli 17:45-47.
Daudi aliona unene wa Goliathi na silaha zake. Lakini Daudi hakuacha mambo hayo yamuogopeshe. Hakufanya makosa yenye Sauli na watu wa jeshi lake walifanya. Daudi hakujilinganisha na Goliathi. Lakini, aliona namna Goliathi alionekana wakati alilinganishwa na Yehova. Kwa sababu alikuwa na urefu wa metre 2,9 hivi, Goliathi alikuwa murefu kupita wanaume wengine wote. Lakini Goliathi hakuwa kitu kwa kumulinganisha na Mutawala Mukubwa wa ulimwengu wote. Kwa kweli, kama mwanadamu mwengine yeyote, Goliathi alikuwa kama kidudu tu, na kwa hiyo ilikuwa mwepesi sana kwa Yehova kumuharibu!
“Vita Ni vya Yehova”
Leo, watumishi wa Mungu hawafanye vita ya kimwili. Wakati wa kufanya hivyo umekwisha kupita. (Mathayo 26:52) Lakini, tunapaswa kabisa kuiga imani ya Daudi. Kama yeye, tunapaswa kumuona Yehova kuwa mutu wa kweli, Mungu mwenye tunapaswa tu kutumikia na kuogopa. Wakati fulani, tunaweza kujiona kuwa hatuna uwezo mbele ya magumu yetu, lakini magumu yetu ni bure mbele ya nguvu ya Yehova yenye haina mwisho. Kama tunamuchagua Yehova kuwa Mungu wetu na kutia imani yetu ndani yake kama Daudi, hakuna magumu ao matatizo yenye yanapaswa kutuogopesha. Hakuna jambo lenye Yehova anaweza kushindwa kumaliza!
Mali ya Kiroho
it-2-F uku. 905-906
Sauli
Ni kisha ile na kisha Daudi kutiwa mafuta juu ya kuwa mufalme wa Israeli wa wakati wenye kuya, njo roho ya Yehova ilimuacha Sauli. Kuanzia pale, “roho ya mubaya kutoka kwa Yehova akamutia woga.” Juu Sauli hakukuwa tena na roho ya Yehova, Yehova alifanya iwezekana roho ya mubaya ivuruge sana amani ya akili ya Sauli, hisia, na mawazo yake. Juu Sauli alishindwa kumutii Yehova, ile ilionyesha muelekeo mubaya wa akili na moyo; na njo maana roho ya Mungu haikumulinda ao kumupatia nguvu. Lakini, juu ni Yehova njo aliruhusu “roho ya mubaya” ikamate nafasi ya roho yake na imuvuruge Sauli, watu wangeweza tu kusema kama ni “roho ya mubaya kutoka kwa Yehova.” Njo maana watumishi wa Sauli waliiita “roho ya mubaya kutoka kwa Mungu.” Ili kufuata pendekezo ya mumoja wa watumishi wake, Sauli alimuomba Daudi akuwe anamupigia muziki ili kumutuliza wakati ile “roho ya mubaya” inamusumbua.—1Sa 16:14-23; 17:15.
TAREHE 28/3–TAREHE 3/4
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 1 SAMWELI 18-19
“Tuendelee Kubakia Wanyenyekevu Wakati Tunapata Matokeo ya Muzuri”
w04-SW 1/4 uku. 15 fu. 4
Tegemea Roho ya Mungu Unaposhughulika na Mabadiliko ya Maisha
4 Muda si muda, mvulana huyo aliyekuwa mchungaji angekuwa mashuhuri katika nchi yake. Alialikwa kumhudumia mfalme na kumchezea muziki. Alimuua shujaa wa vita Goliathi, jitu ambalo hata askari wenye uzoefu wa Israeli waliogopa kulikabili. Baada ya kuwekwa kuwa kiongozi wa wanaume wa vita, Daudi alipigana na Wafilisti na kuwashinda. Watu walimpenda na kutunga nyimbo za kumsifu. Awali, mshauri mmoja wa Mfalme Sauli alisema kwamba Daudi mchanga alikuwa “mwenye ustadi wa kukipiga” kinubi na pia “shujaa, mwanamume mwenye nguvu, na mwanamume wa vita na msemaji mwenye akili na mwanamume mwenye umbo zuri.”—1 Samweli 16:18; 17:23, 24, 45-51; 18:5-7.
Unaona Tofauti Yenye Kuwa Kati ya Watu?
6 Watu fulani wanakuwa na majivuno kwa sababu wako na sura ya muzuri, wanajulikana, wako na uwezo fulani katika mambo ya muziki, wako na uwezo fulani wa kimwili, ao cheo cha juu. Daudi alikuwa na mambo hayo yote, lakini aliendelea kuwa munyenyekevu katika maisha yake yote. Kisha kumuua Goliathi na kupewa mutoto wa Mufalme Sauli akuwe bibi yake, Daudi alisema hivi: ‘Mimi ni nani na watu wa ukoo wangu ni nani, familia ya baba yangu, katika Israeli, hata nikuwe mwana-mukwe wa mufalme?’ (1 Sam. 18:18) Ni nini ilimusaidia Daudi aendelee kuwa munyenyekevu? Daudi alikuwa na sifa, uwezo, na mapendeleo mbalimbali kwa sababu Mungu ‘alijishusha,’ ao kujinyenyekeza ili kumufikiria sana. (Zab. 113:5-8) Daudi alijua kama mambo yote ya muzuri yenye alikuwa nayo yalitoka kwa Yehova.—Linganisha na 1 Wakorintho 4:7.
7 Kama Daudi, watu wa Yehova leo wanajikaza kuonyesha unyenyekevu. Tunashangaa kujua kama Yehova, Mutu mukubwa zaidi katika ulimwengu, anaonyesha sifa yenye kupendeza ya unyenyekevu. (Zab. 18:35) Tunatii shauri hili lenye liliongozwa na roho yake: ‘Mujivike [muvae] upendo mwororo wenye huruma, fazili, unyenyekevu wa akili, upole, na ustahimilivu [uvumilivu].’ (Kol. 3:12) Tunajua pia kama upendo ‘haujigambe, haujivune.’ (1 Kor. 13:4) Wakati tunaonyesha unyenyekevu, tunaweza kusaidia watu wamukaribie Yehova. Kama vile bwana wanaweza kuvutwa na mwenendo wa bibi zao bila maneno, wengine wanaweza kumukaribia Mungu wakati wanaona namna watu wake wanaonyesha unyenyekevu.—1 Pet. 3:1.
Mali ya Kiroho
it-2-F uku. 671 fu. 5
Nabii
Hata kama roho ya Yehova njo ilikuwa nachagua manabii, ile haimaanishe kama kila wakati walikuwa naongozwa nayo. Lakini, roho ya Mungu ilikuwa nakuya juu yao wakati fulani, ili kuwafunulia ujumbe wa kutoa. (Eze 11:4, 5; Mik 3:8) Ile ilifanya wakuwe watu tofauti na iliwachochea kusema. (1Sa 10:10; Yer 20:9; Amo 3:8) Hawakufanya tu mambo yenye haikukuwa ya kawaida, lakini pia maneno na namna yao ya kuwa haikuwa ya kawaida kabisa. Kwa sehemu fulani, hii inatusaidia kuelewa maana ya watu wenye ‘walitenda kama manabii.’ (1Sa 10:6-11; 19:20-24; Yer 29:24-32; linganisha na Mdo 2:4, 12-17; 6:15; 7:55.) Namna walijitoa kabisa na bidii yenye walikuwa nayo mu mugawo wao, ilifanya watu wawaone kuwa watu tofauti sana na hata kuwaona sawa vile wenda-wazimu. Na kuko mufano ya mwanaume moya mwenye alionekana vile mbele ya wakubwa wa jeshi, wakati Yehu alitiwa mafuta. Lakini, wakati wale wakubwa walitambua kama ule mwanaume alikuwa nabii, walichukua ujumbe wake kwa uzito sana. (2Fa 9:1-13; linganisha na Mdo 26:24, 25.) Wakati Sauli alikuwa namufuata Daudi, Sauli ‘alitenda kama vile nabii.’ Na ile wakati, alitosha manguo yake, na “akalala muchana wote na usiku huo wote akiwa uchi,” na ni mu ile wakati njo Daudi alifikia kuponyoka. (1Sa 19:18–20:1) Lakini ile haimaanishe kama kila mara manabii walikuwa natembea uchi, juu habari yenye kuwa mu Biblia haionyeshe vile. Mu habari zingine mbili zenye kuwa mu Biblia, manabii walitembea uchi kwa kusudi fulani. Kusudi ilikuwa kuonyesha sehemu fulani ya unabii wao. (Isa 20:2-4; Mik 1:8-11) Kusudi yenye ilifanya Sauli atembee uchi haionyeshwe. Pengine sababu ilikuwa ni juu aonekana kuwa mwanaume bure, ao pengine juu alitoshwa nguo zake za kifalme, ao pengine juu ya kuonyesha kama hana uwezo juu ya mamlaka na nguvu za kifalme za Yehova, ao juu ya sababu ingine.
TAREHE 4-10/4
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 1 SAMWELI 20-22
“Namna ya Kuwa Rafiki Muzuri”
Fanya Urafiki Wenye Nguvu Pamoja na Wengine Mbele Mwisho Ufike
18 Leo, ndugu na dada zetu wako na magumu mbalimbali. Kwa mufano, wengi wanateseka juu ya misiba ya asili ao misiba yenye kuletwa na mwanadamu. Wakati ile misiba inatokea, wamoja kati yetu wanaweza kuwa na uwezo wa kukaribisha marafiki hao katika nyumba zao. Wengine wanaweza kuwa na uwezo wa kutoa feza ili kuwasaidia. Lakini sisi wote tunaweza kumuomba Yehova asaidie ndugu na dada zetu. Wakati tunapata habari kama ndugu ao dada yetu amevunjika moyo, tunaweza kukosa jambo la kusema ao namna ya kutenda. Lakini sisi wote tunaweza kusaidia. Kwa mufano, tunaweza kupitisha wakati fulani pamoja na rafiki yetu. Tunaweza kumusikiliza kwa huruma wakati iko anazungumuza. Na tunaweza kuzungumuzia pamoja naye andiko fulani lenye tunapendaka sana. (Isa. 50:4) Jambo la maana zaidi ni kuwa pamoja na marafiki wako wakati wako na lazima yako.—Soma Mezali 17:17.
w08-SW 15/2 uku. 8 fu. 7
Tembea Katika Njia za Yehova
7 Mungu anataka tuwe marafiki wenye kutegemeka. (Met. 17:17) Yonathani, mwana wa Mfalme Sauli, alikuwa rafiki ya Daudi. Yonathani aliposikia kwamba Daudi alikuwa amemuua Goliathi, “nafsi ya Yonathani ikashikamana na nafsi ya Daudi, na Yonathani akaanza kumpenda kama nafsi yake mwenyewe.” (1 Sam. 18:1, 3) Yonathani hata alimwonya Daudi Sauli alipotaka kumuua. Daudi alipokimbia, Yonathani alikutana naye na kufanya agano pamoja naye. Karibu Sauli amuue Yonathani alipomwambia kumhusu Daudi, lakini marafiki hao wawili walikutana na kuanzisha tena urafiki wao. (1 Sam. 20:24-41) Walipokutana mara ya mwisho, Yonathani aliutia nguvu mkono wa Daudi “kuhusiana na Mungu.”—1 Sam. 23:16-18.
w09-SW 15/10 uku. 19 fu. 11
Kudumisha Urafiki Katika Ulimwengu Usio na Upendo
11 Uwe mshikamanifu. Sulemani aliandika hivi: “Rafiki wa kweli anapenda nyakati zote, naye ni ndugu aliyezaliwa kwa ajili ya wakati wa taabu.” (Met. 17:17) Alipokuwa akiandika maneno hayo, huenda Sulemani alikuwa akifikiria urafiki ambao baba yake, Daudi, alikuwa nao pamoja na Yonathani. (1 Sam. 18:1) Mfalme Sauli alitaka mwana wake Yonathani awe mrithi wa kiti cha ufalme wa Israeli. Lakini Yonathani alikubali uhakika wa kwamba Yehova alimchagua Daudi kwa ajili ya pendeleo hilo. Tofauti na Sauli, Yonathani hakumwonea wivu Daudi. Hakuchukizwa na pongezi ambazo Daudi alipewa, wala hakuamini uchongezi ambao Sauli alieneza kumhusu Daudi. (1 Sam. 20:24-34) Je, sisi ni kama Yonathani? Marafiki wetu wanapopata mapendeleo, je, tunafurahi pamoja nao? Wanapopatwa na matatizo, je, tunawafariji na kuwategemeza? Tukisikia porojo zenye kuumiza zikienezwa kumhusu rafiki yetu, je, tunafanya haraka kuziamini? Au, kama Yonathani, tunamtetea rafiki yetu kwa ushikamanifu?
Mali ya Kiroho
w05-SW 15/3 uku. 24 fu. 4
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Samweli wa Kwanza
21:12, 13. Yehova anatarajia tutumie uwezo wetu wa kufikiri na stadi zetu ili kushughulikia hali ngumu maishani. Ametupatia Neno lake lililoongozwa na roho, ambalo hutupa busara, ujuzi, na uwezo wa kufikiri. (Methali 1:4) Pia tuna msaada wa wazee Wakristo waliowekwa rasmi.
TAREHE 18-24/4
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 1 SAMWELI 23-24
“Umungojee Yehova kwa Uvumilivu”
w04-SW 1/4 uku. 16 fu. 8
Tegemea Roho ya Mungu Unaposhughulika na Mabadiliko ya Maisha
8 Daudi alikataa kumdhuru Sauli. Kwa kuwa alikuwa na imani na subira, aliridhika kuacha mambo mikononi mwa Yehova. Baada ya mfalme huyo kuondoka pangoni, Daudi alimwita kwa sauti na kumwambia: “Yehova na ahukumu kati yangu na wewe; na Yehova anilipizie kisasi kutoka kwako, lakini mkono wangu mwenyewe hautakuja juu yako.” (1 Samweli 24:12) Ingawa alijua kwamba Sauli alikuwa amefanya kosa, Daudi hakulipiza kisasi, wala hakumtukana Sauli. Katika pindi nyingine kadhaa, Daudi alijizuia asilipize kisasi. Badala yake, alimtegemea Yehova arekebishe mambo.—1 Samweli 25:32-34; 26:10, 11.
w04-SW 1/6 uku. 22-23
Je, Hali Zako Hutawala Maisha Yako?
Jambo la tatu la kujifunza ni kwamba badala ya kutumia njia zisizo za kimaandiko ili kurekebisha hali zetu, tunapaswa kumngojea Yehova. Mwanafunzi Yakobo aliandika: “Acheni uvumilivu ukamilishe kazi yake, ili muwe kamili na timamu katika mambo yote, bila kukosa kitu chochote.” (Yakobo 1:4) Tunapaswa kuacha uvumilivu “ukamilishe kazi yake” kwa kuvumilia majaribu hadi mwisho bila kutumia njia zisizo za kimaandiko ili kuyakomesha upesi. Hivyo, imani yetu itajaribiwa na kusafishwa, na itafunuliwa kama imani yetu ina nguvu ya kututegemeza. Yosefu na Daudi walikuwa na uvumilivu wa aina hiyo. Hawakujaribu kutafuta suluhisho ambalo lingeweza kumkasirisha Yehova. Badala yake, walijitahidi kadiri walivyoweza kulingana na hali zao. Waliendelea kumngojea Yehova, nao wakapokea baraka nyingi sana kwa kufanya hivyo. Wote wawili walitumiwa na Yehova kuokoa na kuongoza watu wake.—Mwanzo 41:39-41; 45:5; 2 Samweli 5:4, 5.
Sisi pia tunaweza kukabili hali ambazo zitatushawishi kutumia njia zisizo za kimaandiko. Kwa mfano, je, unavunjika moyo kwa sababu hujapata mwenzi wa ndoa anayefaa? Ikiwa ndivyo, epuka kishawishi chochote cha kutotii amri ya Yehova ya kuoa “katika Bwana tu.” (1 Wakorintho 7:39) Je, una matatizo katika ndoa yako? Badala ya kuathiriwa na roho ya ulimwengu inayochochea mtengano na talaka, jitahidi kushirikiana na mwenzi wako kusuluhisha matatizo. (Malaki 2:16; Waefeso 5:21-33) Je, una magumu ya kutunza familia yako kwa sababu ya hali za kiuchumi? Kumngojea Yehova hutia ndani kuepuka kufanya mambo yanayotiliwa shaka au yasiyo halali ili kujaribu kupata pesa. (Zaburi 37:25; Waebrania 13:18) Kwa kweli, sote tunapaswa kujitahidi kadiri tuwezavyo kulingana na hali zetu na kuacha Yehova atuthawabishe. Tunapofanya hivyo, na tuazimie kumngojea Yehova ili atoe suluhisho lifaalo.—Mika 7:7.
Mali ya Kiroho
Usiache Jambo Lolote Likuzuie Kupata Zawadi
11 Ikiwa tunakomalisha upendo na wema katika moyo wetu, hatutakuwa wepesi kuonea wengine wivu. Neno la Mungu linasema hivi: ‘Upendo ni wenye ustahimilivu na wenye fazili. Upendo hauna wivu.’ (1 Kor. 13:4) Ili kuepuka wivu kukomaa katika moyo wetu, tunapaswa kujikaza kuona mambo namna Mungu anayaona, ni kusema, kuona ndugu na dada zetu kuwa washiriki wa mwili uleule wa Kristo. Hilo litatusaidia kujitia pa nafasi ya wengine kwa kufuata shauri hili lenye liliongozwa na roho ya Mungu: “Kiungo kimoja kikitukuzwa, vile viungo vingine vyote vinashangilia pamoja nacho.” (1 Kor. 12:16-18, 26) . Fikiria mufano wa Yonathani, mutoto wa Mufalme Sauli. Hakumuonea Daudi wivu wakati alichaguliwa kuwa mufalme kuliko yeye. Lakini, alimutia Daudi moyo. (1 Sam. 23:16-18) Sisi pia tunaweza kuiga wema na upendo wa Yonathani.
TAREHE 25/4–TAREHE 1/5
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 1 SAMWELI 25-26
“Unatendaka Palepale Bila Kufikiri?”
Alitenda kwa Busara
10 Askari hao wenye bidii wa Daudi wanawatendea wachungaji hao wa Nabali namna gani? Ingekuwa rahisi kwao kunyanganya kondoo mara kwa mara, lakini hawafanye hivyo. Kuliko kufanya hivyo, wanalinda wanyama wa Nabali na watumishi wake. (Soma 1 Samweli 25:15, 16.) Siku hizo, kondoo na wachungaji walikuwa wanapambana na hatari nyingi. Wanyama hatari wa porini walikuwa wengi, na mupaka wa kusini wa Israeli ulikuwa karibu sana, kwa hiyo, vikundi vya wanyanganyi na wezi kutoka upande huo vilishambulia watu mara kwa mara.
11 Bila shaka, ilikuwa vigumu kuendelea kuwalisha wanaume hao wote jangwani. Kwa hiyo, siku moja Daudi anamutumia Nabali wajumbe kumi ili kuomba musaada. Daudi anachagua kwa hekima wakati wa kufanya hivyo. Ni wakati wa sikukuu ya kukata kondoo manyoya, wakati huo kwa kawaida watu wanafanya karamu na kutendeana kwa ukarimu. Tena Daudi anachagua kwa uangalifu maneno ya adabu watakayomuambia Nabali. Hata anajitambulisha kwa Nabali kwa kutumia maneno “Daudi mwana wako,” labda anatambua kwa adabu kama Nabali anamushinda miaka. Nabali anafanya nini?—1 Sam. 25:5-8.
12 Anakasirika sana! Yule kijana aliyetajwa mwanzoni anamuelezea Abigaili jinsi Nabali ‘aliwakemea kwa sauti kali,’ watumishi wa Daudi. Kwa sababu ya uchoyo, Nabali anafoka vikali kwa kuwa wanamuomba maji, nyama, na mukate wake wenye bei sana. Anamuchekelea Daudi, anamuona kuwa mutu wa bure na hata anamulinganisha na mutumishi anayetoroka bwana wake. Inawezekana Nabali ana mawazo kama ya Sauli, ambaye anamuchukia Daudi. Nabali na Sauli hawaone mambo kama Yehova. Mungu anamupenda Daudi na hamuone kuwa mutumwa muasi, lakini anamuona kuwa mufalme wa Israeli wa wakati ujao.—1 Sam. 25:10, 11, 14.
Alitenda kwa Busara
18 Anabeba kosa la bwana yake na anamuomba Daudi amusamehe yeye. Anakubali kama bwana yake ni mutu asiyefaa kitu kama jina lake linavyoonyesha, labda ili kumusaidia Daudi atambue kwamba kumuazibu mutu kama huyo ni kujishushia heshima. Anaonyesha kwamba anaamini Daudi ni mutumishi wa Yehova, na anatambua kama vita ambayo Daudi anapigana ni ‘vita ya Yehova.’ Pia, Abigaili anaonyesha kama anajua ahadi ya Yehova kumuhusu Daudi na ufalme, kwa sababu anasema hivi: “Yehova . . . hakika atakuweka kuwa kiongozi juu ya Israeli.” Zaidi ya hayo, anamushauri Daudi asifanye jambo lolote ambalo linaweza kumufanya awe na deni la damu ao asifanye jambo lolote ambalo baadaye litakuwa ‘sababu ya kufazaika,’ ni kusema, litasumbua zamiri yake. (Soma 1 Samweli 25:24-31.) Hayo ni maneno mema na yenye kugusa moyo kabisa!
Mali ya Kiroho
Alitenda kwa Busara
16 Je, hilo linamaanisha kama Abigaili ni mwenye kuasi ukichwa wa bwana yake? Hapana; kumbuka kwamba Nabali alimutukana vibaya mutumishi mutiwa-mafuta wa Yehova, tendo ambalo linaweza kufanya watu wengi wasio na kosa katika nyumba ya Nabali wauawe. Ikiwa Abigaili hafanye jambo lolote, kosa la bwana yake linaweza pia kuwa juu yake. Kwa hiyo, anapaswa kwanza kumutii Mungu kuliko kumutii bwana yake.