Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwbr22 Mwezi wa 11 uku. 1-11
  • Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha
  • Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha (2022)
  • Vichwa Vidogo
  • TAREHE 7-13/11
  • TAREHE 14-20/11
  • TAREHE 21-27/11
  • TAREHE 28/11–4/12
  • TAREHE 5-11/12
  • TAREHE 12-18/12
  • TAREHE 19-25/12
  • TAREHE 26/12–1/1
Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha (2022)
mwbr22 Mwezi wa 11 uku. 1-11

Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha

TAREHE 7-13/11

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 2 WAFALME 5-6

“Wale Wenye Kuwa Pamoja na Sisi Ni Wengi Kuliko Wale Wenye Kuwa Pamoja Nao”

it-1-F uku. 728 fu. 5

Elisha

Waisraeli Wanakombolewa ili Wasishambuliwe na Wasiria. Wakati wa utawala wa Mufalme Yehoramu wa Israeli, Wasiria wanafanya mupango ya kushambulia Waisraeli kwa kushitukia. Zaidi ya mara moya, Elisha anajulisha Mufalme Yehoramu mambo yenye Wasiria wako natayarisha. Na ile inafanya mipango ya Ben-hadadi wa Pili ishindwe. Kwanza Ben-hadadi anawaza kama kuko musaliti kati ya watu wake. Lakini wakati anafikia kujua kwenye ile tatizo inatokea, anatuma maaskari wake Dotani, wanazunguka ile muji na farasi na magari ya vita juu ya kumukamata Elisha. (PICHA, Buk. 1, uku. 950) Mutumishi wa Elisha anaogopa sana, lakini Elisha anasali kwa Mungu afungue macho ya ule mutumishi, “na angalia! eneo lenye milima lilikuwa limejaa farasi na magari ya vita ya moto kumuzunguka Elisha pande zote.” Sasa, wakati Wasiria wanakaribia sana, Elisha anaomba muujiza tofauti, anaomba hivi: “Tafazali, piga taifa hili kwa upofu.” Elisha anaambia Wasiria, “munifuate,” lakini hawakamate ku mukono ili kuwaongoza, ile inaonyesha kama walipigwa na upofu wa kiakili, hapana upofu wa kimwili. Hawamutambue Elisha, mwenye walikuya kukamata, na hata hawajue kwenye iko anawapeleka.​—2Fa 6:8-19.

w13 15/8 uku. 30 fu. 2

Elisha Aliona Magari ya Vita Yenye Moto​—Je, Wewe Pia Unayaona?

Ijapokuwa alizungukwa na maadui huko Dothani, Elisha alibaki mutulivu. Sababu gani? Sababu alikuwa amesitawisha imani yenye nguvu kumuelekea Yehova. Sisi pia tunahitaji imani kama hiyo. Kwa hiyo, tunapaswa kumuomba Mungu roho yake takatifu ili tuwe na imani na sifa zingine za tunda la roho ya Mungu.​—Lu. 11:13; Gal. 5:22, 23.

it-1-F uku. 409 fu. 4

Upofu

Upofu wenye Elisha aliomba Yehova apige jeshi ya Wasiria, haiko upofu wa kimwili, lakini ni upofu wa kiakili. Kama maaskari wote walipigwa na upofu wa kimwili, ingeomba wawakamate ku mukono ili kuwaongoza. Lakini habari inaonyesha tu kama Elisha aliwaambia: “Njia haiko hii, na ule muji haiko huu. Munifuate.” Kuhusu ile jambo William James anasema hivi mu kitabu yake Principles of Psychology: (1981, Buk. 1, uku. 59) “Jambo fulani ya pekee kuhusu matatizo fulani ya ubongo (désordres corticaux) ni upofu wa kiakili. Ile haimaanishe kama mutu hawezi kuona. Lakini, hawezi kuelewa mambo yenye anaona. Kulingana na saikolojia tunaweza kusema hivi: Ni kupoteza uhusiano kati ya uwezo wa kuona na kuelewa maana ya vitu vyenye mutu iko naona; na jambo yoyote yenye inaweza kufanya kusikuwe njia kati ya uwezo wa kuona na mawazo inaweza kuleta ile tatizo.” Inaonekana ule njo upofu yenye Yehova aliondoa kwa maaskari Wasiria wakati walifika Samaria. (2Fa 6:18-20) Na inawezekana ule njo upofu wenye wanaume wa Sodoma walipigwa, juu Biblia inasema kama kuliko kuhangaika kuhusu kupoteza uwezo wao wa kuona, waliendelea kutafuta mulango wa nyumba ya Loti.​—Mwa 19:11.

Mali ya Kiroho

w05-SW 1/8 uku. 9 fu. 2

Mambo Makuu Katika Kitabu cha Pili cha Wafalme

5:15, 16​—Kwa nini Elisha hakukubali zawadi ya Naamani? Elisha alikataa zawadi hiyo kwa sababu alitambua kwamba muujiza wa kumponya Naamani ulifanywa kwa nguvu za Yehova, bali si kwa nguvu zake. Hangefikiria kamwe kupata faida kutokana na kazi aliyopewa na Mungu. Leo, waabudu wa kweli hawataki kujifaidi kupitia utumishi wao kwa Yehova. Wao hutii shauri hili la Yesu: “Mlipokea bure, toeni bure.”​—Mathayo 10:8.

TAREHE 14-20/11

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 2 WAFALME 7-8

“Yehova Alifanya Jambo Yenye Haikutazamiwa”

it-1-F uku. 729 fu. 1

Elisha

Lakini, kisha pale, Mufalme Ben-hadadi wa Pili, anakuya tena kupiganisha Israeli, hapana kwa kushambulia kwa kushitukia, lakini kwa nguvu na maaskari wake wanazunguka Samaria kwa ajili ya vita. Juu waliizunguka kwa muda murefu, hali ikakuwa mubaya sana mupaka mufalme akajulishwa kama mwanamuke moya alikula mutoto wake. Muzao wa Ahabu, “mwana wa muuaji,” Mufalme Yehoramu anaapa kama atamuua Elisha. Lakini hatimize ile kiapo yenye alifanya haraka-haraka. Wakati Yehoramu anafika kwa Elisha pamoya na kamanda wake musaidizi, anasema kama hana tena tumaini kuwa Yehova atawasaidia. Elisha anamuhakikishia mufalme kama kutakuwa chakula mingi siku yenye kufuata. Kamanda musaidizi wa mufalme anachekelea ile maneno ya Elisha, na ile inafanya Elisha amuambie hivi: “Utaona jambo hilo kwa macho yako mwenyewe, lakini hautakula vyakula hivyo.” Yehova anafanya maaskari Wasiria wasikie makelele ya mingi sana mu kambi yao, na ile inafanya wawaze kama mataifa mingi sana imejiunga na inakuya na maaskari wengi sana ili kuwapiganisha. Kwa hiyo wanakimbia, wanaacha kambi yao na chakula yote yenye ilikuwa ndani. Wakati mufalme anapata habari kama Wasiria wamekimbia, anaweka kamanda wake musaidizi ili alinde mulango mukubwa wa Samaria. Wakati Waisraeli wenye njaa wanakimbilia mu kambi ya Wasiria ili kukamata chakula, wanamukanyanga-kanyanga ule kamanda wa mufalme mupaka anakufa. Aliona chakula lakini hakuikula.​—2Fa 6:24–7:20.

Mali ya Kiroho

it-2-F uku. 108 fu. 6

Taa

Wafalme wa Uzao wa Daudi. Yehova Mungu alimuweka Daudi akuwe mufalme wa Israeli, na kwa muongozo wa Yehova, Daudi aliongoza taifa kwa hekima. Kwa hiyo, Daudi aliitwa “taa ya Israeli.” (2Sa 21:17) Mu agano ya ufalme yenye Yehova alifanya pamoya na Daudi, alimuahidi hivi: “Kiti chako cha ufalme kitafanywa kuwa imara kabisa milele.” (2Sa 7:11-16) Kwa hiyo, wafalme wa uzao wa Daudi kupitia mwana wake Sulemani, walikuwa kama “taa” kwa Israel.​—1Fa 11:36; 15:4; 2Fa 8:19; 2Ny 21:7.

TAREHE 21-27/11

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 2 WAFALME 9-10

“Alitenda kwa Uhodari, Bila Kusita, na kwa Bidii”

w11 15/11 uku. 3 fu. 2

Yehu Aliitegemeza Ibada Safi Kwa Bidii

Yehu alipewa mugawo fulani wakati taifa la Israeli lilikuwa katika hali mbaya. Inchi ilikuwa katika uvutano mwovu wa Yezebeli. Mume wa Yezebeli Ahabu, alikuwa tayari amekufa, kwa hiyo alikuwa mujane na pia mama wa mufalme Yehoramu aliyekuwa akitawala. Yezebeli aliwatia watu moyo wamwabudu Baali kuliko kumwabudu Yehova; aliwauwa manabii wa Mungu, na kupotosha watu kupitia “uasherati” na “ulozi” wake. (2 Fa. 9:22; 1 Fa. 18:4, 13) Yehova aliamuru nyumba yote ya Ahabu iharibiwe, kutia ndani mufalme Yehoramu na Yezebeli. Ni Yehu aliyepewa mugawo huo.

w11 15/11 uku. 4 fu. 2-3

Yehu Aliitegemeza Ibada Safi Kwa Bidii

Yehu alikataa kuwaambia lolote wale wajumbe wawili waliotumwa kukutana naye. Kisha alikutana na Mufalme Yehoramu na rafiki yake Ahazia, mufalme wa Yuda, kila mumoja akiwa katika gari lake la vita. Yehoramu akamuuliza, “Je, kuna amani, Yehu?” Yehu akamujibu kwa hasira eti: “Kunaweza kuwa na amani gani wakati kungali na uasherati wa Yezebeli mama yako na ulozi wake mwingi?” Yehoramu aliogopeshwa na jibu lake, akageuka ili kukimbia. Lakini Yehu alikuwa mwenye kutembeza mbio kuliko yeye, akachukua mushale, akamupiga Yehoramu, mushale huo ukapita katika moyo wa mufalme Yehoramu, naye akaanguka katika gari lake na akafa. Ijapokuwa Ahazia alikimbia, baadaye, Yehu alimupata na akamuua.​—2 Fa. 9:22-24, 27.

Mutu mwingine wa nyumba ya Ahabu aliyeuawa ni Malkia Yezebeli. Yehu alimwita Yezebeli kuwa “mutu aliyelaaniwa.” Yehu alipofika Yezreeli, alimwona Yezebeli akitazama chini kupitia dirisha la jumba la kifalme. Akaamuru waziwazi wakuu wa makao ya mufalme wamutupe Yezebeli chini kupitia dirisha. Kisha akaamuru punda zake zimukanyage-kanyage mwanamuke huyo aliyepotosha Israeli. Baadaye, Yehu aliwauwa watu wengine wengi wa nyumba ya Ahabu.​—2 Fa. 9:30-34; 10:1-14.

w11 15/11 uku. 5 fu. 3-4

Yehu Aliitegemeza Ibada Safi Kwa Bidii

Ni kweli kwamba Yehu alimwanga damu nyingi. Lakini, Maandiko yanamutaja kuwa mwanaume mwenye ujasiri ambaye alikomboa Israeli na utawala wenye kukandamiza wa Yezebeli na familia yake. Mufalme yeyote wa Israeli ambaye angependa kupata matokeo hayo, angepaswa kuwa mwanaume mwenye ujasiri, mwenye kuazimia, na mwenye bidii. Kamusi moja ya Biblia ilieleza: “Ilikuwa kazi ngumu na ilitimizwa kwa ukamili. Kutenda bila bidii hakungeweza kumaliza ibada ya Baali katika Israeli.”

Bila shaka unatambua kwamba Wakristo leo wanapatikana katika hali zinazoomba kutumia sifa fulani kama za Yehu. Kwa mufano, tunaweza kutenda namna gani tunaposhawishiwa kufanya mambo ambayo Yehova anakataza? Tunapaswa kuwa tayari kutupilia mbali mambo hayo na kufanya hivyo kwa bidii. Wakati uhusiano wetu na Mungu unahusika, hatuwezi kuvumilia ushindani wowote kumuelekea Yehova.

Mali ya Kiroho

w11 15/11 uku. 5 fu. 6-7

Yehu Aliitegemeza Ibada Safi Kwa Bidii

Labda Yehu alifikiri kwamba ili ufalme wa Israeli usitegemee ule wa Yuda iliomba kuwe utengano wa kidini kati ya falme hizo mbili. Kwa hiyo, Yehu alijaribu kufanya kama wafalme wa Israeli waliotangulia, yaani kutenganisha falme hizo mbili kwa kuruhusu ibada ya ndama iendelee. Hivyo, Yehu alikosa imani kwa Yehova ambaye alimufanya kuwa mufalme.

Yehova alimupongeza Yehu kwa kuwa ‘alitenda vema kwa kufanya yaliyo sawa machoni pake.’ Hata hivyo, Yehu “hakuwa mwangalifu ili atembee katika sheria ya Yehova, Mungu wa Israeli, kwa moyo wake wote.” (2 Fa. 10:30, 31) Tunapofikiria mambo ambayo Yehu alifanya hapo mbele, tunaweza kuona jambo hilo kuwa lenye kushangaza na lenye kuhuzunisha. Lakini, tunajifunza somo fulani. Ni lazima tuchukue kwa uzito uhusiano wetu pamoja na Yehova. Kila siku, ni lazima tuonyeshe uaminifu wetu kwa Mungu kwa kujifunza Neno lake, kutafakari juu ya neno hilo, na kusali kutoka moyoni kwa Baba yetu wa mbinguni. Acheni basi, tuwe waangalifu kabisa ili tuendelee kutembea katika sheria ya Yehova kwa moyo wetu wote.​—1 Ko. 10:12.

TAREHE 28/11–4/12

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 2 WAFALME 11-12

“Mwanamuke Mubaya na Mwenye Kimbelembele Anapewa Malipizi”

it-1-F uku. 217

Atalia

Sawa vile mama yake Yezebeli, Atalia alimuchochea bwana yake, Yehoramu, kufanya mambo ya mubaya mbele ya macho ya Yehova mu utawala wake wa miaka munane. (1Fa 21:25; 2Ny 21:4-6) Na kama mama yake, Atalia alimwanga damu ya watu wengi wenye hawakukuwa na kosa. Wakati mutoto wake, mufalme mubaya Ahazia, alikufa kisha kutawala kwa mwaka moya, Atalia aliua watoto wote wa mufalme isipokuwa tu mutoto Yehoashi, mwenye kuhani mukubwa na bibi yake walificha; bibi ya kuhani mukubwa alikuwa shangazi yake na Yehoashi. Mu ile wakati Atalia alijifanya mwenyewe kuwa malkia na alitawala miaka sita, kuanzia mwaka wa 905-899 hivi M.K.Y. (2Ny 22:11, 12) Wana wa Atalia waliiba vitu vitakatifu mu hekalu ya Yehova na wakavitolea Baali.​—2Ny 24:7.

it-1-F uku. 217

Atalia

Wakati Yehoashi alieneza miaka saba, Kuhani Mukubwa Yehoyada mwenye kumuogopa Mungu aliacha kumuficha, na akamuweka kuwa mufalme juu yeye njo alistahili kuwa mufalme. Wakati Atalia alisikia makelele, alienda mbio ku hekalu, na wakati aliona mambo yenye ilikuwa natendeka kule, alisema hivi kwa sauti kubwa: “Ni mupango mubaya! Ni mupango mubaya!” Yehoyada akaamuru wamutoshe inje na wamuue kwenye muingilio wa mulango mukubwa wa nyumba ya mufalme. Pengine yeye njo alikuwa wa mwisho mu uzao wa mufalme mubaya sana Ahabu. (2Fa 11:1-20; 2Ny 22:1–23:21) Hii maneno ilikuwa ya kweli kabisa: “Hakuna neno hata moja la Yehova lenye Yehova amesema juu ya nyumba ya Ahabu lenye litakosa kutimia”!​—2Fa 10:10, 11; 1Fa 21:20-24.

Mali ya Kiroho

it-2-F uku. 1185 fu. 7

Yehoashi

Wakati yote yenye Yehoyada alikuwa muzima, Yehoashi alikuwa mutawala muzuri. Juu Yehoyada alikuwa kama baba na mushauri wake. Kufikia wakati alikuwa na miaka 21, alikuwa alishaoa bibi wawili. Jina ya bibi yake moya ilikuwa Yehoadani. Kwa hiyo, Yehoashi akakuwa na watoto wanaume na watoto wanamuke. Ile ilifanya uzao wa Daudi wenye kupeleka kwa Masiya, wenye kulibakia kidogo upotee, ukuwe nguvu tena.​—2Fa 12:1-3; 2Fa 24:1-3; 25:1.

TAREHE 5-11/12

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 2 WAFALME 13-15

“Kujikaza kwa Moyo Wote Kunaletaka Baraka Mingi”

w10-SW 15/4 uku. 26 fu. 11

Je, Unamfuata Kristo kwa Ukamili?

11 Ili kuonyesha faida ya kumtumikia Mungu kwa bidii, ona jambo lililotukia katika maisha ya Mfalme Yehoashi wa Israeli. Akiwa na wasiwasi kwamba Siria ingeishambulia na kuishinda Israeli, Yehoashi alienda kumwona Elisha huku akilia. Nabii huyo alimwagiza Yehoashi apige mshale nje kupitia dirisha kuelekea Siria, ili kuonyesha jinsi ambavyo Yehova angewasaidia kushinda taifa hilo. Bila shaka, jambo hilo lilipaswa kumtia nguvu mfalme huyo. Kisha, Elisha akamwambia Yehoashi achukue mishale yake na kuipiga chini. Yehoashi alipiga chini mara tatu tu. Hilo lilimkasirisha sana Elisha, kwa kuwa kupiga mishale chini mara tano au sita kungeonyesha kwamba ‘Siria ingepigwa kufikia hatua ya kuimaliza.’ Sasa Yehoashi angeshinda mara tatu tu. Kwa kuwa hakuonyesha bidii, Yehoashi hakufanikiwa sana. (2 Fa. 13:14-19) Tunajifunza somo gani kutokana na simulizi hilo? Yehova atatubariki sana ikiwa tu tutafanya kazi yake kwa moyo wote na kwa bidii.

w13 1/11 uku. 11 fu. 5-6

‘Musawabishaji wa Wale Wanaomutafuta kwa Bidii’

Ni nani ambao Yehova anapatia zawadi? Paulo anasema kwamba ni ‘wale wanaomutafuta kwa bidii.’ Kitabu kimoja cha watafsiri wa Biblia kinasema kwamba neno la Kigiriki ambalo linatafsiriwa ‘wanaomutafuta kwa bidii,’ halimaanishe “kuenda kutafuta inje” lakini, linamaanisha kufanya bidii ya kumukaribia Mungu ili “kumuabudu.” Kitabu kingine kinaeleza kwamba neno hilo la Kigiriki linaonyesha nguvu na kufanya bidii nyingi. Ndiyo, Yehova anawapatia zawadi wale ambao imani yao inawachochea kumuabudu kwa moyo wenye kujaa upendo na bidii.​—Mathayo 22:37.

Namna gani Yehova anawapatia zawadi waabudu wake waaminifu? Amewaahidi kuwapatia zawadi nzuri sana wakati unaokuja, zawadi ambayo inaonyesha ukarimu na upendo wake mukubwa, ni kusema, uzima wa milele katika Paradiso duniani. (Ufunuo 21:3, 4) Hata sasa, wale ambao wanamutafuta Yehova kwa bidii wanapata baraka nyingi sana. Kwa musaada wa roho yake takatifu na hekima iliyo katika Neno lake, wanafurahia kuishi maisha mazuri na yenye kutosheleza.​—Zaburi 144:15; Mathayo 5:3.

Mali ya Kiroho

w05-SW 1/8 uku. 11 fu. 3

Mambo Makuu Katika Kitabu cha Pili cha Wafalme

13:20, 21​—Je, muujiza huu unaunga mkono kuabudu mabaki ya vitu vya kale vya kidini? La. Biblia haionyeshi kwamba mifupa ya Elisha iliabudiwa. Nguvu za Mungu ndizo zilizotokeza muujiza huo, sawa na ilivyokuwa katika miujiza yote ambayo Elisha alifanya alipokuwa hai.

TAREHE 12-18/12

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 2 WAFALME 16-17

“Uvumilivu wa Yehova Uko na Mipaka”

it-2-F uku. 868 fu. 4

Shalmanesa

Utawala wa Israeli. Wakati wa utawala wa Mufalme Hoshea wa Israeli (758-740 hivi M.K.Y.), Shalmanesa wa Tano alikamata Palestina, Hoshea akakuwa mutumishi wake na akamulazimisha kulipa ushuru kila mwaka. (2Fa 17:1-3) Lakini, wakati fulani Mufalme Hoshea hakulipa ushuru na ikaonekana kwamba alikuwa nafanya mupango mubaya na Mufalme So wa Misri. Kwa hiyo, Shalmanesa akamufunga. Na kisha, Shalmanesa na majeshi yake wakazunguka Samaria kwa miaka tatu kwa ajili ya vita. Ku mwisho akakamata ule muji wenye ngome, na akapeleka Waisraeli mu uhamisho.​—2Fa 17:4-6; 18:9-12; linganisha na Ho 7:11; Eze 23:4-10.

it-1-F uku. 402 fu. 7

Utekwa

Sababu yenye ilifanya ufalme wa makabila kumi ya kaskazini ya Israeli na ufalme wa Yuda wa makabila mbili ya kusini iende mu utekwa ni ileile: wote waliacha ibada safi ya Yehova na wakaanza kuabudu miungu ya uongo. (Kum 28:15, 62-68; 2Fa 17:7-18; 21:10-15) Lakini, Yehova, kwa upande wake aliendelea kuwatumia manabii wake ili wawaonye lakini hawakubadilika. (2Fa 17:13) Hakuna hata mufalme moya wa makabila kumi ya Israeli mwenye alimaliza kabisa ibada ya uongo yenye Yeroboamu, mufalme wa kwanza wa Israeli alianzisha. Ufalme wa Yuda, haukusikiliza maonyo ya moja kwa moja ya Yehova, na haukupata somo juu ya namna makabila kumi ya Israeli ilienda mu utekwa. (Yer 3:6-10) Wakaaji wa mataifa yote mbili walifikia kupelekwa mu uhamisho, na kila taifa ilipelekwa zaidi ya mara moya.

Mali ya Kiroho

it-2-F uku. 878 fu. 8

Musamaria

Neno “Wasamaria” inaonekana mara ya kwanza mu Maandiko kisha ufalme wa Samaria wa makabila kumi ya Israeli kukamatwa mu mwaka wa 740 M.K.Y.; ile neno ilitumiwa ili kuzungumuzia wale wenye walikuwa wanaishi mu ufalme wa kaskazini mbele ukamatwe ili kuwatofautisha na wageni wenye waliletwa kutoka mu maeneo ingine ya Utawala wa Waashuru. (2Fa 17:29) Inaonekana kama Waashuru hawakupeleka mu uhamisho wakaaji wote wa Israeli, juu habari yenye kuwa mu 2Mambo ya Nyakati 34:6-9 (linganisha na 2Fa 23:19, 20) inaonyesha kama wakati wa utawala wa Mufalme Yosia kulikuwa kungali Waisraeli mu inchi. Kisha, neno “Wasamaria” ilianza kumaanisha wazao wa wale wenye walibakia Samaria na wale wenye waliletwa na Waashuru. Na inawezekana wengine walikuwa wazao wa ndoa kati ya Waisraeli na wale wageni. Miaka mingi kisha pale, neno “Musamaria” ilikuwa na maana ya kidini, hapana ya kikabila ao ya kipolitike. Neno “Musamaria” ilitumiwa juu ya kumaanisha mutu mwenye alikuwa mu kikundi kidogo ya kidini yenye iliendelea sana karibu na Shekemu na Samaria ya zamani, na mutu mwenye alikuwa na imani tofauti na ya dini ya Wayahudi.​—Yoh 4:9.

TAREHE 19-25/12

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 2 WAFALME 18-19

“Namna Maadui Wetu Wanajaribu Kutufanya Tukuwe Zaifu”

w05-SW 1/8 uku. 11 fu. 5

Mambo Makuu Katika Kitabu cha Pili cha Wafalme

18:19-21, 25​—Je, Hezekia alikuwa amefanya mapatano na Misri? La. Rabshake alitoa shtaka la uwongo, na pia alidanganya alipodai kwamba amekuja kwa “kupewa mamlaka kutoka kwa Yehova.” Mfalme Hezekia mwaminifu alimtegemea Yehova peke yake.

w10-SW 15/7 uku. 13 fu. 3

“Usiogope. Mimi Mwenyewe Nitakusaidia”

Rabshake alitumia mawazo ya hila ili kujaribu kupanda mashaka katika akili za watu. Alisema: “Je, [Yehova] siye ambaye mahali pake pa juu na madhabahu zake Hezekia ameondoa? . . . Yehova mwenyewe aliniambia, ‘Nenda juu ya nchi hii, nawe lazima uiharibu.’ (2Fa. 18:22, 25) Hivyo, Rabshake alidai kwamba Yehova hangewapigania watu Wake kwa sababu hakupendezwa nao. Lakini hiyo haikuwa kweli. Yehova alipendezwa na Hezekia na Wayahudi waliorudi kwenye ibada ya kweli.​—2 Fa. 18:3-7.

w13 15/11 uku. 19 fu. 14

Ni Nani Walio Wachungaji Saba na Watawala Wadogo Wanane Leo?

14 Mufalme wa Ashuru na jeshi lake walipiga kambi huko Lakishi, kusini-mangaribi mwa Yerusalemu. Kutoka huko, mufalme huyo alituma wajumbe watatu ili waambie watu wa Yerusalemu wakubali kushindwa. Musemaji wake, aliyeitwa Rabshake, alitumia njia mbalimbali za ujanja. Akisema katika Kiebrania, aliwaambia watu wasimusikilize mufalme Hezekia na wajitiishe kwa Waashuru. Aliwaahidi kwa uongo kwamba atawapeleka katika inchi ambamo wangefurahia maisha. (Soma 2 Wafalme 18:31, 32.) Kisha Rabshake alionyesha kwamba kama vile miungu ya mataifa ilivyoshindwa kuokoa waabudu wake, Yehova hangeweza kuokoa Wayahudi katika mikono ya Waashuru. Kwa hekima, watu hawakusikiliza maneno yake ya uongo. Leo, watumishi wa Yehova wanafuata mufano wao.​—Soma 2 Wafalme 18:35, 36.

yb74 uku. 177 fu. 1

Sehemu ya 2​—Alemanye

Inashangaza kuona kama maaskari wa SS, wenye mara mingi walitumia ujanja juu ya kufanya watu watie sinyatire ku makaratasi, waliwageuka kisha wao kutia sinyatire na waliwasumbua kuliko zamani. Karl Kirscht anahakikisha ile jambo, anasema hivi: “Kuliko watu wengine wote, Mashahidi wa Yehova walidanganywa sana mu kambi za mateso. Maaskari wa SS waliwaza kama ile njo ilikuwa njia ya kuwasadikisha watie sinyatire kwenye makaratasi. Walituomba tufanye vile tena na tena. Mashahidi fulani walitia sinyatire, lakini mara mingi iliomba kuchunga zaidi ya mwaka ili waachiliwe. Mu ile wakati maaskari wa SS walikuwa wanawatukana mbele ya watu na kuwaita wanafiki na watu wenye woga. Na waliwakaza watembee mbele ya ndugu zao mbele waruhusiwe kutoka mu kambi.”

Mali ya Kiroho

it-1-F uku. 170 fu. 3

Vitu vya Zamani Vyenye Kuvumbuliwa

Kwa mufano, habari yenye kuwa mu Biblia inaonyesha kama Mufalme Senakeribu wa Waashuru aliuawa na wana wake wawili, Adrameleki na Shareza, na Esar-hadoni, mwana wake mwingine akakuwa mufalme pa nafasi yake. (2Fa 19:36, 37) Lakini, maandishi fulani ya Wababiloni inaonyesha kama siku ya 20 ya mwezi wa Tebeti, Senakeribu aliuawa na mwana wake mwenye aliasi. Berossus, kuhani wa Babiloni wa mu karne ya tatu M.K.Y., na Nabonido, mufalme wa Babiloni wa mu karne ya sita M.K.Y., walikubaliana na wazo ya kama Mufalme Senakeribu aliuawa na mwana wake mumoja tu. Mu vipande vya mabamba vyenye vilivumbuliwa hivi karibuni vya Esar-hadoni, mwana mwenye alikuwa mufalme pa nafasi ya Senakeribu, Esar-hadoni anasema waziwazi kama ndugu zake (kwa uwingi) waliasi na kuua baba yao na kisha wakakimbia. Kuhusu ile jambo, Philip Biberfeld, alisema hivi mu kitabu yake Universal Jewish History (1948, Buk. 1, uku. 27): “Maandishi ya Historia ya Babiloni, Nabonido, na Berossus walikosea; habari ya Biblia tu njo inaonekana kuwa ya kweli. Maandishi ya Esar-hadoni ilihakikisha kama hata mambo ya kidogo-kidogo yenye Biblia ilisema kuhusu ile jambo ni ya kweli. Na mambo yenye inazungumuzia kuhusu historia ya Wababiloni na historia ya Waashuru inaonekana kuwa ya bila makosa kuliko hata maandishi ya Wababiloni. Ile jambo inaonyesha kama tunapaswa kuwa waangalifu sana wakati tunachunguza maandishi ingine yenye haipatane na mambo yenye Biblia inasema.”

TAREHE 26/12–1/1

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 2 WAFALME 20-21

“Sala Ilifanya Yehova Atende”

ip-1-SW uku. 394 fu. 23

Mfalme Apata Thawabu kwa Sababu ya Imani Yake

23 Karibu wakati Senakeribu ajapo kwanza dhidi ya Yuda, Hezekia awa mgonjwa mahututi. Isaya amwambia kwamba atakufa. (Isaya 38:1) Mfalme huyo mwenye umri wa miaka 39 avunjika moyo kabisa. Yeye ahangaikia, si hali njema yake pekee, bali pia ya wakati ujao wa watu. Yerusalemu na Yuda zimo katika hatari ya kuvamiwa na Waashuri. Hezekia akifa, ni nani atakayeongoza pigano? Wakati huo, Hezekia hana mwana wa kuchukua utawala. Kupitia sala yenye bidii, Hezekia amwomba Yehova amrehemu.​—Isaya 38:2, 3.

w17.03 uku. 21 fu. 16

Umutumikie Yehova kwa Moyo Mukamilifu!

16 Kisha, Hezekia akakuwa mugonjwa na kukaribia kufa. Wakati huo wa magumu, alimuomba Yehova akumbuke uaminifu wake na amusaidie. (Soma 2 Wafalme 20:1-3.) Yehova alisikia sala ya Hezekia na akamuponyesha. Biblia inatuambia kama, leo hatuwezi kutazamia kuwa Mungu ataponyesha magonjwa yetu kwa muujiza ao kufanya maisha yetu yakuwe ya murefu zaidi. Lakini, kama Hezekia, tunaweza kumutegemea Yehova ili atusaidie. Tunaweza kumuambia hivi: ‘Nakuomba, Ee Yehova, tafazali ukumbuke jinsi nilivyotembea mbele zako kwa ukweli na kwa moyo mukamilifu.’ Unaamini kuwa Yehova atakuhangaikia sikuzote, hata wakati unagonjwa?​—Zaburi 41:3.

g01-SW 22/7 uku. 13 fu. 4

Sala Yaweza Kunisaidiaje?

Katika nyakati za Biblia, wanaume fulani wenye imani walijibiwa sala zao moja kwa moja, au hata kupitia miujiza. Kwa mfano, Mfalme Hezekia alipojua kwamba ana ugonjwa usiotibika, alimwomba Mungu dua ili amwokoe. Mungu alijibu hivi: “Nimeyasikia maombi yako, na kuyaona machozi yako; tazama, nitakuponya.” (2 Wafalme 20:1-6) Wanaume na wanawake wengine wenye kumhofu Mungu waliona Mungu akiwaokoa kimuujiza.​—1 Samweli 1:1-20; Danieli 10:2-12; Matendo 4:24-31; 10:1-7.

Mali ya Kiroho

it-2-F uku. 406 fu. 4

Kifaa cha kusawazisha

Kifaa cha kusawazisha kinaweza kutumiwa juu ya kujenga nyumba muzuri, ao kupima kama ile nyumba iko muzuri juu iendelee kutumikishwa. Yehova aliahidi kama atanyoosha juu ya Yerusalemu ‘kamba ya kupimia yenye ilitumiwa juu ya Samaria na atatumia kifaa cha kusawazisha chenye kilitumiwa juu ya nyumba ya Ahabu.’ Mungu alikuwa amepima watu wa Samaria na watu wa nyumba ya Mufalme Ahabu na kuona kama walikuwa watu wabaya sana, na ile ilifanya waharibiwe. Vilevile, Mungu angehukumu Yerusalemu na watawala wake, angeonyesha wazi makosa yao na kuharibu ule muji. Na ile jambo ilitukia mu 607 Mbele ya kuzaliwa kwa Yesu. (2Fa 21:10-13; 10:11) Kupitia Isaya, watu wengi wenye majivuno na watawala wa Yerusalemu waliambiwa hii maneno ya Yehova kuhusu musiba wenye ungewapata: “Nitafanya haki kuwa kamba ya kupimia na uadilifu kuwa kifaa cha kusawazisha.” Kanuni za haki ya kweli na uadilifu wa kweli vingesaidia kujua ni nani watumishi waaminifu wa Mungu na ni nani hawako watumishi waaminifu wa Mungu. Na ile ingefanya wenye wako waaminifu waokolewe, na wenye hawako waaminifu waharibiwe.​—Isa 28:14-19.

Hotuba: Namna Gani Tunaweza Kusali kwa Ajili ya Wale Wenye Kuteswa?

w20.11 uku. 15 fu. 14

Ukuwe Hodari​—Yehova Ni Musaidizi Wako

Tunaweza kufanya nini? Tunaweza kusali “kwa ajili ya wafalme na wale wote wenye mamlaka” wakati wanapenda kukamata maamuzi yenye inaweza kuwa na matokeo juu ya maisha yetu ya Kikristo na utumishi wetu. (1 Ti. 2:1, 2, maelezo ya chini; Ne. 1:11) Kama vile Wakristo wa karne ya kwanza walifanya, sisi pia tunapaswa kusali sana kwa ajili ya ndugu na dada zetu wenye kuwa mu gereza. (Soma Matendo 12:5; Ebr. 13:3) Zaidi ya ile, tunaweza kusali kwa ajili ya walinzi wa gereza wenye wako wanasimamia ndugu na dada zetu wenye kuwa mu gereza. Tunaweza kumulilia Yehova, awachochee ili watendee wale ndugu na dada zetu kwa “fazili za kibinadamu,” kama vile Yulio alimutendea Paulo.​—Mdo. 27:3, maelezo ya chini.

Hotuba: Iga Bidii ya Yehova na Yesu.

w13 15/5 uku 8-9 fu. 3-6

Je, Una “Bidii kwa Ajili ya Kazi Njema”?

3 Linapozungumuzia mambo ambayo utawala wa Mwana wa Mungu utafanya, andiko la Isaya 9:7 linasema hivi: “Bidii ya Yehova wa majeshi itafanya hayo.” Maneno hayo yanatuhakikishia kama Baba yetu wa mbinguni anapenda kabisa wanadamu waokolewe. Kwa kuwa Yehova ni mwenye bidii, hilo linatuonyesha waziwazi kwamba sisi wahubiri wa Ufalme, tunapaswa kutegemeza kazi ambayo Mungu ametutolea kwa moyo wetu wote, kwa furaha, na kwa bidii. Tamaa yetu kubwa ya kuwasaidia watu wamujue Mungu inaonyesha kwamba tunamuiga Yehova. Kwa hiyo, kwa kuwa tunafanya kazi pamoja na Mungu, je, tumeazimia sisi wenyewe kufanya mengi katika kazi ya kuhubiri kadiri hali zetu zinavyoruhusu?​—1 Ko. 3:9.

4 Tufikirie pia bidii ya Yesu. Alituachia mufano mukamilifu wa kuendelea kuhubiri kwa biii. Ijapokuwa alipambana na upinzani mukali, Yesu aliendelea kuhubiri kwa bidii mupaka kifo chake chenye maumivu mengi. (Yoh. 18:36, 37) Alipokaribia kufa kifo cha kujizabihu, Yesu aliongeza bidii yake ili kuwasaidia wengine wamujue Yehova

5 Kwa mufano, mwishoni mwa mwaka wa 32, Yesu alizungumuzia mufano wa mutu aliyekuwa na muti wa tini katika shamba lake la mizabibu ambao haukuzaa hata tunda moja kwa miaka mitatu. Mutunza​-mizabibu alipoambiwa kwamba akate muti huo, aliomba apewe wakati ili kuutilia mbolea. (Soma Luka 13:6-9.) Wakati Yesu alizungumuzia mufano huo, ni hesabu ndogo tu ya wanafunzi ndio ilikuwa imekubali mahubiri yake. Lakini kama mufano huo wa mutunza-mizabibu ulivyoonyesha, Yesu alitumia wakati mufupi uliobaki, ao miezi sita hivi, ili kuhubiri sana katika Yudea na Perea. Siku chache mbele ya kifo chake, Yesu aliwalilia Wayahudi wenzake ambao ‘walisikia kwa masikio yao bila kuitikia.’​—Mt. 13:15; Lu. 19:41.

6 Kwa kuwa tunakaribia sana mwisho, hauone kwamba ni jambo la maana tuongeze bidii yetu katika kazi ya kuhubiri? (Soma Danieli 2:41-45.) Tuna pendeleo nzuri la kuwa Mashahidi wa Yehova! Ni sisi tu ndio tunaowatolea watu tumaini la kweli kuhusu matatizo yanayowapata wanadamu. Mwandishi wa gazeti moja aliandika karibuni kwamba watu wengi hawana jibu la ulizo hili: “Sababu gani watu wazuri wanapatwa pia na mambo mabaya?” Sisi Wakristo tuna daraka na pendeleo la kuwatolea watu wanaopendezwa jibu la Biblia kwa ulizo hilo na kwa maulizo mengine. Tuna kila sababu ya ‘kuwaka roho’ tunapofanya kazi ambayo Mungu ametutolea. (Ro. 12:11) Kwa baraka ya Mungu, bidii yetu katika kazi ya kuhubiri inaweza kuwasaidia wengine wamujue na kumupenda Yehova.

Hotuba: Kazi Yenye Kuleta Furaha

km 8/03 uku. 1

Kazi Inayoburudisha

1 Ujumbe wa Biblia unaburudisha wote wanaoukubali na kuutumikisha katika maishani yao. (Zab. 19:7, 8) Unawasaidia wajiweke huru kutoka katika mafundisho ya uwongo na mazoea yenye kuumiza na unatoa tumaini la wakati ujao lenye kutegemeka. Hata hivyo, si wale wanaopokea habari njema peke yao ndio wanaofaidika. Wale wanaoshiriki na wengine kweli za Biblia zenye kuburudisha wanaburudishwa wenyewe pia.​—Mez. 11:25.

2 Huduma Inatutia Nguvu: Yesu alisema kwamba wale wanaokubali nira ya kuwa wanafunzi Wakristo, inayotia ndani kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi, ‘watapata burudisho kwa ajili ya nafsi zao.’ (Mt. 11:29) Yeye mwenyewe alitambua kwamba kutolea wengine ushahidi kunatia nguvu. Kulikuwa kama chakula kwake. (Yoh. 4:34) Alipotuma wale wanafunzi 70 waende kuhubiri, hao walishangilia walipoona jinsi Yehova alivyotegemeza jitihada zao.​—Luka 10:17.

3 Vivyo hivyo, Wakristo wengi leo wanatiwa nguvu kwa kushiriki katika kazi ya kuhubiri. Dada mmoja alisema: “Huduma huburudisha kwa kuwa inafanya maisha yangu yawe na kusudi. Ninaposhiriki katika utumishi, sifikirii sana matatizo yangu ya kibinafsi na mikazo ninayopata kila siku.” Mhudumu mwingine mwenye bidii alisema: “Ninaposhiriki huduma, Yehova huwa halisi kwangu kila siku na ninapata kiasi fulani cha amani na furaha ya moyoni isiyoweza kupatikana kwa njia nyingine yoyote.” Ni pendeleo kama nini tulilo nalo kuwa “wafanyakazi wenzi wa Mungu”!​—1 Ko. 3:9.

4 Nira ya Kristo Ni ya Fadhili: Ingawa Wakristo wanahimizwa ‘wajikakamue wenyewe kisulubu,’ Yesu hatuombi zaidi ya yale tunayoweza kutoa. (Luka 13:24) Kwa kweli, anatualika kwa upendo ‘tujitie chini ya nira yake pamoja naye.’ (Mt. 11:29, kielezi-chini) Wale wanaolazimika kupambana na hali ngumu wanaweza kuwa na uhakika kwamba utumishi wao wa nafsi yote, hata ikiwa ni mdogo, unapendeza Mungu.​—Marko 14:6-8; Kol. 3:23.

5 Ni jambo lenye kuburudisha kama nini kutumikia Mungu anayethamini lolote tunalofanya kwa ajili ya jina lake! (Ebr. 6:10) Na tujitahidi sikuzote kumtolea kilicho bora tulicho nacho.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine