Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha
TAREHE 3-9/7
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | EZRA 4-6
“Musijiingize Katika Kazi Hiyo”
Unaona Mambo Yenye Zekaria Aliona?
13 Kazi ya kujenga upya hekalu ilikatazwa. Lakini Kuhani Mukubwa Yeshua (Yoshua) na Gavana Zerubabeli, wanaume wenye walichaguliwa ili kuongoza watu, “wakaanza kujenga upya nyumba ya Mungu.” (Ezr. 5:1, 2) Pengine Wayahudi fulani waliwaza kama ile ilikuwa uamuzi wa mubaya. Wayahudi hawangeweza kuficha kama walikuwa wanajenga hekalu na walijua kama maadui wao wangefanya yote yenye wangeweza ili kusimamisha kazi. Yoshua na Zerubabeli, wenye waliongoza kazi, walikuwa na lazima ya uhakikisho wenye kuonyesha kama Yehova alikuwa anawaunga mukono. Na waliupata. Namna gani?
w86 1/2 uku. 29, kisanduku fu. 2-3
Yehova “Alikuwa Analinda Wazee”
Kisha Wayahudi kutoka mu uhamisho mu Babiloni, walifanya miaka 16 bila kutenda. Nabii Hagai na Zekaria waliwachochea ili watoke mu ile hali, na wakarudilia kazi ya kujenga tena hekalu. Lakini, kisha wakati kidogo wakubwa wa Waajemi walijaribu kuzuia kazi isiendelee. Wale wapinzani waliuliza hivi: “Ni nani mwenye aliwapatia amri ya kujenga nyumba hii?”—Ezr. 5:1-3.
Jibu ya ile ulizo haikukuwa mwepesi. Wazee wangeacha wale watu wawaogopeshe, kazi ya kujenga hekalu ingesimama palepale. Na kama wazee wangekasirisha wale wakubwa, palepale kazi ya kujenga hekalu ingekatazwa kabisa. Kwa hiyo, wale wazee (wenye bila shaka, waliongozwa na Gavana Zerubabeli na Kuhani Mukubwa Yoshua) walijibu kwa busara lakini mu njia yenye kufaa. Walikumbusha wale wakubwa amri yenye Koreshi alitoaka, yenye ilipatia Wayahudi ruhusa ya kuendelea na ile kazi. Wale wakubwa walijua kama kulingana na sheria ya Waajemi, amri yenye kutolewa na mufalme haiwezi kubadilishwa. Kwa hiyo, waliepuka kupinga amri ya mufalme. Basi, kazi iliendelea mupaka wakati Mufalme Dario alitoa pia amri ya kuendeleza kazi.—Ezr. 5:11-17; 6:6-12.
Unaona Mambo Yenye Zekaria Aliona?
7 Badiliko fulani yenye ilitokea ilitia moyo kwa kiasi fulani wale wenye walikuwa wanajenga hekalu. Ni badiliko gani? Mu 520 M.K.Y., mufalme mupya, Dario wa kwanza alikuwa anatawala Uajemi. Mu mwaka wa pili wa utawala wake, alivumbula kama kazi ya kujenga hekalu ilikatazwa na ile haikupatana na sheria. Kisha Dario alitoa amri ili waendelee na kazi. (Ezr. 6:1-3) Ile tangazo ya mufalme ilishangaza kila mutu, lakini alifanya zaidi ya ile. Mufalme aliamuru watu wenye kuwazunguka waache kupinga Wayahudi na wawapatie makuta na kila kitu yenye walikuwa nayo lazima juu wamalize kazi ya kujenga upya hekalu! (Ezr. 6:7-12) Matokeo ilikuwa kwamba, Wayahudi walimaliza kazi ya kujenga hekalu kisha miaka ine hivi, mu 515 M.K.Y.—Ezr. 6:15.
Unaona Mambo Yenye Zekaria Aliona?
16 Njia ingine yenye Yehova anatumia ili kututolea muongozo ni “mutumwa muaminifu na mwenye busara.” (Mt. 24:45) Wakati fulani, mutumwa muaminifu anaweza kututolea muongozo wenye hatuelewe kabisa. Kwa mufano, tunaweza kupewa maagizo fulani kuhusu namna ya kujitayarisha juu tuweze kupambana na musiba wa asili wenye pengine tunaweza kuwaza kama hautatokea mu eneo yetu. Ao pengine tunaweza kuwaza kama mutumwa muaminifu anapitisha mipaka wakati anatutolea maagizo fulani juu ya ugonjwa fulani wenye kuambukiza. Tunapaswa kufanya nini ikiwa tunawaza kama maagizo yenye walitutolea haiko ya hekima? Tunaweza kupata faida kwa kufikiria namna Waisraeli walipata faida kwa kutenda kupatana na shauri yenye Yoshua na Zerubabeli waliwatolea. Tunaweza pia kufikiri juu ya habari za Biblia zenye tulishasoma. Wakati fulani, watu wa Mungu walitolewa muongozo wenye ulionekana sawa vile hauko wa muzuri ku macho ya wanadamu, lakini wenye ulifikia kuokoa uzima wao.—Amu. 7:7; 8:10.
Mali ya Kiroho
w93-SW 15/6 uku. 32 fu. 3-5
Je! Waweza Kuitumaini Biblia?
Sarafu hii ilifanyizwa katika Tarso, jiji moja katika sehemu ya kusini-mashariki mwa nchi ambayo sasa ni Uturuki. Sarafu hiyo ilitokezwa wakati wa utawala wa gavana Mwajemi Mazaeus katika karne ya nne K.W.K. Inamtambulisha kuwa gavana wa mkoa wa “Ng’ambo ya Mto,” yaani, Mto Frati.
Lakini kwa nini fungu hilo la maneno ni lenye kupendeza? Kwa sababu utaona kichwa icho hicho cha cheo katika Biblia yako. Ezra 5:6–6:13 laonyesha barua kati ya Mfalme Mwajemi Dario na gavana aitwaye Tatenai. Suala lilikuwa juu ya kujenga upya kwa Wayahudi hekalu lao katika Yerusalemu. Ezra alikuwa mnakiliji stadi wa Sheria ya Mungu, na ungemtazamia kuwa dhahiri, sahihi katika yale aliyoandika. Utaona kwenye Ezra 5:6 and 6:13 kwamba alimwita Tatenai “liwali [gavana, NW] wa ng’ambo wa Mto.”
Ezra aliyaandika maneno hayo karibu 460 K.W.K., yapata miaka 100 kabla ya sarafu hii kuundwa. Ah, kuna watu wengine ambao huenda wakahisi kwamba kichwa cha cheo cha ofisa wa kale ni jambo dogo lisilo na maana. Lakini ikiwa unaweza kuwategemea waandishi wa Biblia katika hata mambo hayo madogo-madogo, je, hilo lisiongeze uhakika wako katika mambo yale mengine waliyoandika?
TAREHE 10-16/7
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | EZRA 7-8
“Matendo ya Ezra Ilimutukuza Yehova”
w00-SW 1/10 uku. 14 fu. 8
Funzo—Lenye Kuthawabisha na Lenye Kufurahisha
8 Naam, kupenda Neno la Yehova kwapaswa kutoka kwenye moyo, ambao ni msukumo wa hisia-moyo. Twapaswa kupendezwa kurudiarudia mafungu kadhaa ambayo tumetoka tu kusoma. Lazima tutafakari juu ya mambo ya kiroho yenye kina na kuyazingatia. Hilo hutaka kutafakari kwa ukimya pamoja na sala. Kama vile Ezra, twahitaji kutayarisha mioyo yetu kwa ajili ya kusoma na kujifunza Neno la Mungu. Imeandikwa hivi kumhusu: “Huyo Ezra alikuwa ameuelekeza moyo wake kuitafuta sheria ya BWANA, na kuitenda, na kufundisha maagizo na hukumu katika Israeli.” (Ezra 7:10) Ona kwamba Ezra alikusudia kufanya mambo matatu alipokuwa akitayarisha moyo wake: kujifunza, kutumia kibinafsi mambo aliyojifunza, na kufundisha. Twapaswa kufuata kielelezo chake.
si-SW uku. 75 fu. 5
Kitabu Cha Biblia Namba 13—Mambo ya Nyakati wa Kwanza
5 Hakuna aliyestahili zaidi ya Ezra kukusanya historia hiyo yenye uasilia na iliyo sahihi. “Kwa maana huyo Ezra alikuwa ameuelekeza moyo wake kuitafuta sheria ya BWANA [Yehova, NW], na kuitenda, na kufundisha maagizo na hukumu katika Israeli.” (Ezra 7:10) Yehova alimsaidia kupitia roho takatifu. Mtawala wa ulimwengu Mwajemi alitambua hekima ya Mungu katika Ezra na akampa mamlaka nyingi juu ya raia katika wilaya ya utawala ya Yuda. (7:12-26) Hivyo akiwa na mamlaka ya kimungu na ya kifalme, Ezra angeweza kukusanya simulizi lake kutokana na hati bora zaidi zilizokuwapo.
it-1-F uku. 1155-1156 fu. 9
Unyenyekevu
Unatoa Mwongozo Wenye Kufaa. Mutu mwenye anajinyenyekeza mbele ya Mungu anaweza kutazamia kama Mungu atamuongoza. Ezra alikuwa na daraka kubwa ya kuongoza Wayahudi kutoka Babiloni ili kurudia Yerusalemu. Alipaswa kuongoza wanaume 1500; zaidi ya wale wanaume kulikuwa makuhani, Wanetini, wanamuke na watoto. Tena, walikuwa wanabeba kiasi kubwa ya zahabu na feza vyenye wangetumia ili kufanya hekalu ipendeze. Walikuwa na lazima ya ulinzi mu safari. Lakini, Ezra hakupenda kuomba mufalme wa Waajemi awapatie maaskari ili wawasindikize. Juu ile ingeonyesha kama wanategemea nguvu ya wanadamu. Na tena mbele ya pale alikuwa amemuambia hivi mufalme: “Mukono mwema wa Mungu wetu uko juu ya wale wote wenye kumutafuta.” Kwa hiyo, aliambia watu wafunge ili wajinyenyekeze mbele ya Yehova. Waliomba Mungu na Mungu akawasikiliza na kuwalinda mu njia ili maadui wasiwashambulie; na walimaliza ile safari yenye kuwa hatari kwa usalama. (Ezr 8:1-14, 21-32) Juu nabii Danieli, mwenye alikuwa mu uhamisho Babiloni alijinyenyekeza mbele ya Mungu kwa kutafuta muongozo na uelewaji, Yehova alionyesha kabisa kama alimukubali kwa kumutumia malaika katika maono.—Da 10:12.
Mali ya Kiroho
w06-SW 15/1 uku. 19 fu. 10
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Ezra
7:28–8:20—Kwa nini Wayahudi wengi huko Babiloni hawakutaka kwenda Yerusalemu pamoja na Ezra? Hata ingawa zaidi ya miaka 60 ilikuwa imepita tangu kikundi cha kwanza cha Wayahudi kirudi katika nchi yao, Yerusalemu lilikuwa na watu wachache sana. Kurudi Yerusalemu kungemaanisha kuanza maisha mapya katika hali ngumu na zenye hatari. Hali ya Yerusalemu wakati huo haingewawezesha Wayahudi waliokuwa na ufanisi huko Babiloni kufanikiwa kimwili. Pia, safari ya kurudi ilikuwa hatari. Wale waliorudi walihitaji kuwa na imani yenye nguvu katika Yehova, bidii kwa ajili ya ibada ya kweli, na ujasiri ili wahamie Yerusalemu. Hata Ezra alijiimarisha kulingana na mkono wa Yehova uliokuwa juu yake. Baada ya kutiwa moyo na Ezra, familia 1,500 ambazo huenda zilikuwa na watu 6,000 zilikubali kurudi. Baada ya Ezra kuchukua hatua za ziada, Walawi 38 na Wanethini 220 walikubali kurudi.
TAREHE 17-23/7
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | EZRA 9-10
“Kukosa Kutii Kunaletaka Matokeo ya Kuumiza Sana”
w06-SW 15/1 uku. 20 fu. 1
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Ezra
9:1, 2—Ni kwa njia gani kufunga ndoa pamoja na watu wa nchi kulikuwa hatari? Taifa lililorudishwa lilipaswa kulinda ibada ya Yehova hadi Masihi aje. Kufunga ndoa pamoja na wakaaji wengine wa nchi kulihatarisha ibada ya kweli. Kwa kuwa watu fulani walikuwa wamefanya mapatano ya ndoa pamoja na watu walioabudu sanamu, huenda hatimaye taifa lote lingemezwa na mataifa ya kipagani. Ibada safi ingetoweka duniani. Basi, Masihi angekuja kwa nani? Haishangazi kwamba Ezra alishtuka alipoona mambo yaliyotendeka!
w09-SW 1/10 uku. 10 fu. 6
Yehova Anataka Nini Kutoka Kwetu?
Kutii kwa hiari kutatuletea baraka. Musa aliandika hivi: “Kuzishika amri . . . ninazokuamuru wewe leo, [ni] kwa faida yako.” (Mstari wa 13) Naam, kila amri ya Yehova, kila kitu anachotaka tufanye, ni kwa faida yetu. Mbona isiwe hivyo? “Mungu ni upendo,” inasema Biblia. (1 Yohana 4:8) Kwa hiyo, ametupa amri ambazo zitatuletea faida za kudumu. (Isaya 48:17) Kufanya yale ambayo Yehova anataka kutoka kwetu kutatuzuia tusikatishwe tamaa sasa na kutatuletea baraka za milele chini ya Ufalme wake.
Mali ya Kiroho
w06-SW 15/1 uku. 20 fu. 2
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Ezra
10:3, 44—Kwa nini watoto walifukuzwa pamoja na wake? Ikiwa watoto wangebaki, huenda wake waliofukuzwa wangerudi kwa ajili yao. Isitoshe, kwa kawaida watoto wadogo huhitaji kutunzwa na mama zao.
TAREHE 24-30/7
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | NEHEMIA 1-2
“Mara Moja Nikasali”
w08-SW 15/2 uku. 3 fu. 5
Endelea Kumweka Yehova Mbele Yako Daima
5 Nyakati nyingine, huenda tukahitaji kuomba msaada wa Mungu haraka. Pindi moja, Mfalme Artashasta wa Uajemi alitambua kwamba Nehemia, mnyweshaji wake alikuwa na huzuni. “Ni jambo gani hili unalotaka?” akauliza mfalme. “Mara moja [Nehemia] akasali kwa Mungu wa mbinguni.” Nehemia alitoa sala fupi ambayo inaelekea ilikuwa ya kimyakimya. Lakini, Mungu alimjibu, kwa sababu mfalme alimpa Nehemia msaada wa kujenga upya kuta za Yerusalemu. (Soma Nehemia 2:1-8.) Ndiyo, hata sala fupi ya kimyakimya inaweza kuwa na matokeo mazuri.
be-SW uku. 177 fu. 4
Kutoa Hotuba Bila Kutazama Sana Maandishi
Unapoitwa kwa ghafula ueleze juu ya imani yako, ni nini kinachoweza kukusaidia kufaulu? Mwige Nehemia, ambaye alisali kwa ukimya kabla ya kujibu swali la Mfalme Artashasta. (Neh. 2:4) Kisha, tayarisha haraka akilini jambo utakalosema. Tunaweza kuorodhesha hivi hatua hizo kuu: (1) Chagua jambo moja au mambo mawili ambayo unapaswa kutia ndani ya jibu lako (unaweza kuchagua jibu katika kitabu Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko). (2) Amua maandiko ambayo utatumia kuunga mkono mambo hayo. (3) Fikiria jinsi utakavyoanzisha mazungumzo kwa busara ili mwenye kuuliza swali aweze kusikiliza. Kisha anza kuzungumza.
Mali ya Kiroho
w86 15/2 uku. 25
Ibada ya Kweli Inapata Ushindi
Hapana. Kwa wakati fulani Nehemia alikuwa anasali “muchana na usiku” juu ya hali ya mubaya ya Yerusalemu (1:4, 6) Wakati alipata nafasi ya kuambia Mufalme Artashasta kuhusu tamaa yake ya kujenga tena kuta za Yerusalemu, Nehemia alisali tena. Kwa hiyo, alifanya jambo yenye alikuwa alishafanya tena na tena. Yehova alijibia sala yake na alipewa kazi ya kujenga tena kuta za muji.
Jambo Yenye Tunajifunza: Nehemia alitafuta mwongozo wa Yehova. Mbele ya kukamata uamuzi mukubwa siye pia tunapaswa ‘kudumu katika sala’ na kutenda kulingana na muongozo wenye Yehova ametupatia.—Waroma 12:12.
TAREHE 31/7–6/8
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | NEHEMIA 3-4
“Unaona Kazi ya Mikono Kuwa ya Hali ya Chini?”
w06-SW 1/2 uku. 10 fu. 1
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Nehemia
3:5, 27. Hatupaswi kuona kazi ya mkono inayofanywa kwa kusudi la kuendeleza ibada ya kweli kuwa yenye kutushushia heshima, kama walivyofanya “watu wa [Watekoa] walio mashuhuri.” Badala yake, tunaweza kuwaiga Watekoa wa kawaida waliojitolea kwa hiari.
Yehova Atakutumia Namna Gani?
11 Miaka mingi kisha pale, watoto wanamuke wa Shalumu walikuwa kati ya watu wenye Yehova alitumia ili kutengeneza kuta za Yerusalemu. (Ne. 2:20; 3:12) Hata kama baba yao alikuwa mukubwa wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, watoto wanamuke wa Shalumu walikuwa tayari kufanya kazi ya nguvu na ya hatari. (Ne. 4:15-18) Walikuwa tofauti kabisa na wanaume wa maana kati ya Watekoa, wenye “hawakutaka kujishusha ili kushiriki” katika kazi hiyo! (Ne. 3:5) Wazia furaha yenye watoto wanamuke wa Shalumu walisikia wakati kazi ilimalizika kisha siku 52 tu! (Ne. 6:15) Leo, dada wenye roho ya kujitoa wanafurahi sana kusaidia katika aina hii ya pekee ya utumishi mutakatifu: kujenga na kutunza majengo yenye tunatumia juu ya ibada ya Yehova. Tuko na lazima ya dada hao wenye uwezo, wenye bidii, na washikamanifu ili kutimiza kazi hiyo.
w04-SW 1/8 uku. 18 fu. 16
Kusitawisha Maoni ya Kristo Kuhusu Umashuhuri
16 Wakristo wote, vijana kwa wazee, wanapaswa kujitahidi kusitawisha maoni ya Kristo kuhusu umashuhuri. Katika kutaniko kuna kazi mbalimbali zinazopaswa kufanywa. Usikasirike kamwe unapoombwa ufanye kazi ambazo huenda zikaonekana kuwa za hali ya chini. (1 Samweli 25:41; 2 Wafalme 3:11) Wazazi, je, mnawatia moyo watoto na matineja wenu wafanye kwa furaha kazi yoyote wanayopewa, iwe ni kwenye Jumba la Ufalme, kusanyikoni, au mahali pa kusanyiko? Je, wao huona mkifanya kazi za hali ya chini? Ndugu mmoja, ambaye sasa anatumika katika makao makuu ya ulimwengu ya Mashahidi wa Yehova, anakumbuka waziwazi kielelezo cha wazazi wake. Alisema: “Namna walivyofanya kazi ya kusafisha Jumba la Ufalme au mahali pa kusanyiko ilinionyesha kwamba waliona kazi hiyo kuwa muhimu. Mara nyingi walifanya kazi za kunufaisha kutaniko au akina ndugu, hata iwe kazi hizo zilionekana kuwa za hali ya chini kadiri gani. Mtazamo huo umenisaidia kukubali kwa furaha kazi yoyote hapa Betheli.”
Mali ya Kiroho
w06-SW 1/2 uku. 9 fu. 1
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Nehemia
4:17, 18—Mtu angeweza kufanyaje kazi ya kujenga upya kwa mkono mmoja tu? Kwa wale waliochukua mizigo, hilo halingekuwa tatizo. Mizigo ilipowekelewa kichwani au begani mwao, waliisawazisha kwa mkono mmoja, huku “mkono wa pili ukiwa umeshika silaha.” Wajenzi waliohitaji kutumia mikono yao miwili kufanya kazi ‘walijifunga, kila mmoja upanga wake kiunoni mwake, wakijenga.’ Walikuwa tayari kutenda iwapo wangeshambuliwa na adui.
Hotuba: Endelea Kuwa na Mawazo ya Muzuri Hata Kama Watu Hawapendezwe
Ona Mema kwa Sababu ya Kazi Yako Ngumu
1 Mungu alipomuumba mwanadamu, alikusudia mwanadamu ‘aone mema kwa sababu ya kazi yake ngumu.’ (Mhu. 2:24) Lakini, ikiwa hatupate matokeo mazuri katika mahubiri, tunaweza kuvunjika moyo na hivyo kupoteza furaha yetu na kupunguza bidii yetu. Ni nini kinachoweza kutusaidia tuendelee kuwa na maoni yanayofaa juu ya kazi yetu ya kuhubiri?
2 Usifikiri Kama Watu Wote Watakubali: Kumbuka kwamba hata kama ni watu wachache tu ndio waliokubali mafundisho ya Yesu, bila shaka mahubiri yake yalikuwa na matokeo mazuri. (Yoh. 17:4) Katika mufano wake wa mupandaji, Yesu alitabiri kwamba mwishowe mioyo ya watu wengi zaidi haingekubali ujumbe wa ufalme unaofananishwa na mbegu. (Mt. 13:3-8, 18-22) Hata hivyo, kwa kuwa tunajikaza sana, tunatimiza kazi kubwa.
3 Namna ya Kuzaa Matunda Mengi: Kulingana na mufano wa Yesu, wale wanaokubali ujumbe ‘wanazaa matunda.’ (Mt. 13:23) Kisha ngano kuota na kukomaa, haizae muti mudogo wa ngano lakini inazaa mbegu mupya. Kwa hiyo, matunda ambayo Mukristo anazaa hayafananishe tu wanafunzi wapya, lakini yanafananisha kupanda mbegu nyingi za ufalme, ni kusema, kuhubiri kuhusu Ufalme. Kwa kufanya hivyo tunaona “mema” ambayo inaweza kutufurahisha, iwe watu wanakubali ujumbe wetu ao hapana. Tunashiriki katika kulitakasa jina la Yehova. (Isa. 43:10-12; Mt. 6:9) Tuna pendeleo la kutumika pamoja na Mungu. (1 Kor. 3:9) Na “tunda la midomo” yetu linamufurahisha Yehova.—Ebr. 13:15, 16.
4 Tena, tujue kama kazi yetu ngumu inaweza kuendelea kuwa na matokeo mazuri ambayo hatuone. Inawezekana watu fulani waliosikiliza mafundisho ya Yesu walifikia kuwa wanafunzi wake kisha yeye kumaliza huduma yake duniani. Vilevile, mbegu tunazopanda zinaweza kuota na kukomaa katika moyo wa mutu baada ya muda, na mutu huyo anaweza kuikubali kweli bila sisi kujua. Kwa kweli, kazi yetu ya kuhubiri inatimiza mambo mengi mema. Kwa hiyo, acheni ‘tuendelee kuzaa matunda mengi’ na kujionyesha kuwa wanafunzi wa Yesu.—Yoh. 15:8.
TAREHE 7-13/8
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | NEHEMIA 5-7
“Nehemia Alipenda Kutumikia Wengine, Hapana Wengine Wamutumikie”
w02-SW 1/11 uku. 27 fu. 3
Watu Waliounga Mkono Ibada ya Kweli Zamani za Kale na Leo
Nehemia hakutumia tu wakati na ustadi wake wa kupanga mambo. Alitumia pia mali zake ili kuendeleza ibada ya kweli. Alitumia fedha zake kuwatoa ndugu zake Wayahudi utumwani. Alikopesha fedha bila faida. Hakuwawekea Wayahudi mzigo “mzito” kwa kudai posho lake kama liwali, jambo ambalo lilikuwa haki yake. Badala yake, alikuwa mkarimu, akawalisha “watu mia na hamsini, zaidi ya wale waliotujia kutoka makafiri waliotuzunguka.” Kila siku aliwaandalia wageni wake ‘ng’ombe mmoja, na kondoo wazuri sita; tena kuku.’ Isitoshe, kila baada ya siku kumi aliwapa “akiba ya mvinyo ya namna zote.” Naye ndiye aliyelipa gharama za vitu hivyo.—Nehemia 5:8, 10, 14-18.
Usiache ‘Mikono Yako Iregee’
16 Kupitia musaada wa Yehova, Nehemia na Wayahudi wenzake walitia nguvu mikono yao. Walimaliza kujenga kuta za Yerusalemu katika siku 52 tu! (Nehemia 2:18; 6:15, 16) Nehemia hakuangalia tu wengine wakati walikuwa wanafanya kazi hiyo. Yeye pia alisaidia kujenga kuta za Yerusalemu. (Nehemia 5:16) Vilevile, wazee wengi wa kutaniko wanaiga mufano wa Nehemia wakati wanasaidia katika mipango ya ujenzi ao kusafisha na kutengeneza Jumba la Ufalme. Pia, wanaume hao wenye upendo wanatia nguvu ndugu na dada wenye ‘wanahangaika moyoni’ wakati wanawatembelea na wakati wanahubiri pamoja nao.—Soma Isaya 35:3, 4.
w00-SW 1/2 uku. 32
Yehova Atakukumbukaje?
Biblia huonyesha daima kwamba Mungu ‘hukumbuka’ kwa kuchukua hatua. Kwa mfano, baada ya dunia kugharikishwa kwa siku 150, “Mungu akamkumbuka Nuhu . . . , Mungu akavumisha upepo juu ya nchi, maji yakapungua.” (Mwanzo 8:1) Karne kadhaa baadaye, Samsoni, akiwa amepofushwa na kufungwa kwa minyororo na Wafilisti, alisali hivi: “MUNGU, unikumbuke, nakuomba, ukanitie nguvu, nakuomba, mara hii tu.” Yehova alimkumbuka Samsoni kwa kumpa nguvu zipitazo za kibinadamu ili aweze kujilipizia kisasi dhidi ya adui za Mungu. (Waamuzi 16:28-30) Kwa habari ya Nehemia, Yehova alibariki jitihada zake, na ibada ya kweli ikarudishwa Yerusalemu.
Mali ya Kiroho
w07-SW 1/7 uku. 30 fu. 15
“Endelea Kuushinda Uovu Kwa Wema”
15 Tatu, maadui wa Nehemia walitumia msaliti, Mwisraeli aliyeitwa Shemaya, ili wajaribu kumfanya Nehemia avunje Sheria ya Mungu. Shemaya alimwambia hivi Nehemia: “Tukutane kwa mapatano katika nyumba ya Mungu wa kweli, ndani ya hekalu, halafu tufunge milango ya hekalu; kwa maana wanakuja kukuua.” Shemaya alisema kwamba Nehemia angeuawa lakini angeweza kuokoa uhai wake kwa kujificha hekaluni. Lakini, Nehemia hakuwa kuhani. Angetenda dhambi kwa kujificha katika nyumba ya Mungu. Je, angevunja Sheria ya Mungu akijaribu kuokoa uhai wake? Nehemia alimjibu hivi: “Ni nani kama mimi anayeweza kuingia hekaluni kisha akaishi? Sitaingia!” Kwa nini Nehemia hakunaswa na mtego ambao aliwekewa? Kwa sababu alijua kwamba ingawa Shemaya alikuwa Mwisraeli mwenzake, “si Mungu aliyemtuma.” Kwa vyovyote vile, nabii wa kweli hangeweza kamwe kumshauri avunje Sheria ya Mungu. Tena, Nehemia hakujiruhusu ashindwe na wapinzani waovu. Muda mfupi baadaye aliripoti hivi: “Mwishowe ukuta ukakamilika siku ya 25 ya mwezi wa Eluli, katika muda wa siku 52.”—Nehemia 6:10-15; Hesabu 1:51; 18:7.
Hotuba: Waeneza-Injili Wazuri Wanasaidiana
Timiza Daraka Lako la Mweneza-injili
17 Yesu alituma wanafunzi wake katika kazi ya kuhubiri wakiwa wawili-wawili. (Mk. 6:7; Lu. 10:1) Baadaye, mutume Paulo alizungumuzia ‘wafanyakazi wenzake waliokazana pamoja naye katika habari njema.’ (Flp. 4:3) Kwa kuiga wahubiri hao wa wakati wa mitume, katika mwaka wa 1953, Mashahidi wa Yehova, walianzisha programe ya kuwazoeza wengine katika mahubiri.
18 Unapomusindikiza muhubiri mwenzako katika mahubiri, namna gani munaweza kuungana mukono? (Soma 1 Wakorintho 3:6-9.) Muhubiri mwenzako anaposoma maandiko fulani, wewe pia uyatafute katika Biblia yako. Sikiliza vizuri yale ambayo muhubiri mwenzako ao musikilizaji anasema. Kufuata mazungumuzo kwa uangalifu kutakusaidia kujua wakati gani unaweza kumusaidia muhubiri mwenzako kujibu ulizo fulani ngumu ao kushinda tatizo lingine. (Mhu. 4:12) Lakini angalisho: Epuka kumukatiza-katiza muhubiri mwenzako anapojaribu kufikiri vizuri pamoja na musikilizaji. Ukimukatiza-katiza, hilo linaweza kumuvunja moyo na kuvuruga musikilizaji. Wakati mwengine, inaweza kuwa vizuri kushiriki katika mazungumuzo. Lakini, ukipenda kusema jambo fulani, toa maelezo mafupi mara moja ao mara mbili. Kisha umuache muhubiri mwenzako aendelee na mazungumuzo.
19 Namna gani munaweza kusaidiana munapotoka kwenye mulango mumoja mupaka mulango mwengine? Munaweza kutumia wakati huo ili kuzungumuzia namna ya kufanya utangulizi wenu uwe muzuri zaidi. Muwe waangalifu ili mazungumuzo yenu kuhusu watu wa eneo lenu yasiwe yenye kuvunja moyo. Pia, muepuke kuongea-ongea juu ya uzaifu wa wahubiri wengine. (Met. 18:24) Ni vizuri tukumbuke kwamba sisi ni vyombo vya udongo. Yehova ametuonyesha wema mukubwa kwa kututolea hazina ya kuhubiri habari njema. (Soma 2 Wakorintho 4:1, 7.) Kwa hiyo, acheni sote tupendezwe sana na hazina hiyo kwa kufanya yote tunayoweza ili kutimiza daraka letu la kueneza injili.
TAREHE 14-20/8
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | NEHEMIA 8-9
“Shangwe ya Yehova Ni Ngome Yenu”
Sala Iliyotayarishwa Vizuri Inatufundisha Nini?
2 Mwezi mumoja mbele ya mukusanyiko huo, Wayahudi walikuwa wamemaliza kujenga upya kuta za Yerusalemu. (Neh. 6:15) Watu wa Mungu walimaliza kazi hiyo katika siku 52 tu, na kisha walianza kufikiria sana mahitaji yao ya kiroho. Kwa hiyo, siku ya kwanza ya mwezi uliofuata, unaoitwa Tishri, walikusanyika pamoja kwenye kiwanja cha watu wote ili kumusikiliza Ezra, na Walawi wengine, wakisoma kwa sauti na kufasiria Sheria ya Mungu. Familia nzima, kutia ndani “wote wenye akili ya kutosha kuweza kusikiliza,” walisimama na kusikiliza ‘kuanzia mapambazuko [asubuhi sana] mupaka katikati ya muchana.’ Huo ni mufano muzuri kwa wengi kati yetu leo tunaohuzuria mikutano katika Majumba mazuri ya Ufalme! Lakini, je, wakati fulani akili yetu inaanza kutangatanga na tunaanza kufikiria mambo yasiyo ya maana tunapokuwa kwenye mikutano? Ikiwa ndiyo, tufikirie tena mufano wa Waisraeli wa zamani ambao hawakusikiliza tu lakini pia waliguswa moyo na mambo waliyosikia, na hilo liliwafanya waanze kulia walipotambua kwamba taifa lao lilikuwa limeshindwa kutii Sheria ya Mungu.—Neh. 8:1-9.
w07-SW 15/7 uku. 22 fu. 9-10
Je, ‘Utaendelea Kutembea Kwa Roho’?
9 Shangwe ni hali ya kuwa na furaha kubwa. Yehova ni “Mungu mwenye furaha.” (1 Timotheo 1:11; Zaburi 104:31) Mwana wake anafurahia kufanya mapenzi ya Baba yake. (Zaburi 40:8; Waebrania 10:7-9) Na “shangwe ya Yehova ndiyo ngome [yetu].”—Nehemia 8:10.
10 Shangwe inayotoka kwa Mungu inatuletea uradhi mkubwa tunapofanya mapenzi ya Mungu hata katika nyakati za magumu, huzuni, au mateso. “Kumjua Mungu” kunatuletea furaha kama nini! (Methali 2:1-5) Uhusiano wetu wenye shangwe pamoja na Mungu unategemea ujuzi sahihi na imani katika yeye na katika dhabihu ya fidia ya Yesu. (1 Yohana 2:1, 2) Kuwa sehemu ya undugu wa pekee wa kweli wa ulimwenguni pote ni jambo lingine linalotuletea shangwe. (Sefania 3:9; Hagai 2:7) Tumaini letu la Ufalme na pendeleo kubwa ajabu la kutangaza habari njema linatuletea shangwe. (Mathayo 6:9, 10; 24:14) Pia, tarajio la uzima wa milele linatuletea shangwe. (Yohana 17:3) Kwa kuwa tuna tumaini hilo zuri ajabu, tunapaswa kuwa na “shangwe kwelikweli.”—Kumbukumbu la Torati 16:15.
Mali ya Kiroho
it-1-F uku. 151 fu. 7
Kiaramu
Miaka mingi kisha Wayahudi kutoka mu uhamisho mu Babiloni, Ezra kuhani alisomea Wayahudi wenye walikusanyika Yerusalemu kitabu ya Sheria. Na Walawi mbalimbali walifasiria watu mambo yenye ilikuwa nasomwa. Nehemia 8:8 inasema: “Wakaendelea kusoma kwa sauti kubwa katika kile kitabu, katika Sheria ya Mungu wa kweli, wakaifasiria waziwazi na kueleza maana yake; kwa hiyo wakasaidia watu kuelewa mambo yenye yalikuwa yanasomwa.” Neno kufasiria yenye inatajwa hapa inaweza kutia ndani kutosha maandishi mu Kiebrania na kuifasiria mu Kiaramu. Na inawezekana Waebrania walianza kutumia Kiaramu wakati walikuwa mu uhamisho Babiloni. Bila shaka, kufasiria kulitia pia ndani kueleza mambo waziwazi. Hata kama Wayahudi walikuwa naelewa Kiebrania, ile ingewasaidia waelewe muzuri maana ya mambo yenye ilikuwa nasomwa.
TAREHE 21-27/8
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | NEHEMIA 10-11
“Walijiima na Kujitoa Wenyewe kwa Ajili ya Yehova”
w98-SW 15/10 uku. 22 fu. 13
Yerusalemu Lililo Kama Vile Jina Lake Limaanishavyo
13 “Agano la hakika” lililotiwa muhuri siku ya Nehemia liliwatayarisha watu wa kale wa Mungu kwa ajili ya siku ya mzinduo wa ukuta wa Yerusalemu. Lakini jambo jingine lenye uharaka lilihitaji kushughulikiwa. Likiwa limezungukwa na ukuta mkubwa wenye malango 12, Yerusalemu lilihitaji idadi kubwa zaidi ya watu. Ingawa Waisraeli fulani waliishi humo, “mji ulikuwa na nafasi nyingi, tena mkubwa; lakini watu waliomo walikuwa haba.” (Nehemia 7:4) Ili kutatua tatizo hilo, watu ‘walipiga kura, ili katika watu kumi kumleta mmoja akae ndani ya Yerusalemu mji mtakatifu.’ Itikio lenye utayari kwa mpango huo lilisukuma watu ‘wajitoe kwa hiari ili wakae Yerusalemu.’ (Nehemia 11:1, 2) Ni kielelezo kizuri kama nini kwa waabudu wa kweli leo ambao hali zao zinawaruhusu kuhamia mahali ambapo pana uhitaji mkubwa wa msaada wa Wakristo wakomavu!
w86 15/2 uku. 26
Ibada ya Kweli Inapata Ushindi
Kuacha uriti wote na kuhamia Yerusalemu ingeleta garama na matokeo fulani yenye haiko ya muzuri. Pia, wale wenye kuishi mu ile muji wangepambana na hatari mbalimbali. Njo maana wengine waliona kama wale wenye walijitolea walistahili kusifiwa, na bila shaka walisali ili Yehova awabariki.
Tunakubaliwa na Mungu Ikiwa Tunabakia Waaminifu Kwake
15 Wakati tulitoa maisha yetu kwa Yehova, tulimuahidi kwamba tutafanya mapenzi yake hata kutokee nini. Tulijua kwamba wakati fulani itakuwa vigumu kutimiza ahadi hiyo. Lakini, tunatenda namna gani wakati tunaombwa kufanya jambo fulani lenye hatupendi? Tutaonyesha kwamba tuko waaminifu kwa ahadi yetu ikiwa tunatenda bila kuogopa na kuwa tayari kumutii Mungu. Pengine inaweza kuwa vigumu kwetu kutoa zabihu fulani, lakini baraka za Yehova ni kubwa sikuzote. (Malaki 3:10) Tuseme nini juu ya binti ya Yeftha? Alitenda namna gani kulingana na ahadi ya baba yake?
Mali ya Kiroho
w06-SW 1/2 uku. 11 fu. 1
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Nehemia
10:34—Kwa nini watu walipaswa kutoa kuni? Matoleo ya kuni hayakuamuriwa katika Sheria ya Musa. Takwa hilo lilitokana na uhitaji. Kuni nyingi zilihitajiwa ili kuteketeza dhabihu kwenye madhabahu. Yaelekea Wanethini, ambao walikuwa watumwa wa hekaluni wasio Waisraeli, walikuwa wachache. Hivyo, watu walipiga kura ili kuhakikisha kwamba kuni zilikuwapo kwa ukawaida.
Hotuba: Zabihu Zenye Kumufurahisha Mu-
ngu Leo
w11-SW 15/2 uku. 15-16 fu. 12-15
Kukubaliwa na Mungu Kunaongoza Kwenye Uzima wa Milele
12 Mtume Paulo aliandika hivi katika barua yake kwa Waroma: “Mtoe miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, yenye kukubalika kwa Mungu, utumishi mtakatifu pamoja na nguvu zenu za kufikiri.” (Rom. 12:1) Ili kupata kibali cha Mungu mtu anahitaji kuhakikisha kwamba mwili wake unakubaliwa na Mungu. Ikiwa mtu angejichafua kwa kuvuta sigara, kutafuna miraa, kutumia dawa za kulevya, au kunywa pombe kupita kiasi, dhabihu hiyo haingekuwa na thamani. (2 Kor. 7:1) Zaidi ya hayo, kwa kuwa yule “aliye na mazoea ya kufanya uasherati anautendea dhambi mwili wake mwenyewe,” mwenendo mpotovu wa aina yoyote unafanya dhabihu yake kuwa chukizo kwa Yehova. (1 Kor. 6:18) Ili kumpendeza Mungu, mtu anapaswa ‘kuwa mtakatifu katika mwenendo wake wote.’—1 Pet. 1:14-16.
13 Dhabihu nyingine ambayo Yehova anapendezwa nayo ni nguvu yetu ya usemi. Wale wanaompenda Yehova wanasema sikuzote mambo mazuri kumhusu mbele ya watu wote na katika nyumba zao. (Soma Zaburi 34:1-3.) Soma Zaburi ya 148-150, na uone ni mara ngapi zaburi hizo tatu zinatutia moyo kumsifu Yehova. Kwa kweli, “sifa ni jambo linalofaa kwa wanyoofu.” (Zab. 33:1) Na Kielelezo chetu, Yesu Kristo, alikazia umuhimu wa kumsifu Mungu kwa kuhubiri habari njema.—Luka 4:18, 43, 44.
14 Tunapohubiri kwa bidii tunaonyesha kwamba tunampenda Yehova na tunatamani kupata kibali chake. Kwa mfano, fikiria jinsi nabii Hosea alivyowahimiza Waisraeli waliofuata ibada ya uwongo na hivyo wakapoteza kibali cha Mungu. (Hos. 13:1-3) Hosea aliwaambia wasihi hivi: “[Yehova] samehe kosa letu; na ukubali lililo jema, nasi tutatoa ng’ombe-dume wachanga wa midomo yetu.”—Hos. 14:1, 2.
15 Ng’ombe-dume alikuwa mnyama wa bei ghali zaidi ambaye Mwisraeli angemtolea Yehova. Kwa hiyo, “ng’ombe-dume wachanga wa midomo yetu” ni maneno manyoofu, yaliyofikiriwa vizuri ambayo yalisemwa ili kumsifu Mungu wa kweli. Yehova aliwajibu jinsi gani wale waliotoa dhabihu kama hizo? Alisema: “Nitawapenda kwa kupenda kwangu mwenyewe.” (Hos. 14:4) Yehova aliwasamehe wale waliotoa dhabihu kama hizo za sifa, akawakubali, naye akawa rafiki yao.
TAREHE 28/8–3/9
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | NEHEMIA 12-13
“Ukuwe Mushikamanifu kwa Yehova Wakati” Unachagua Marafiki”
it-1-F uku. 100 fu. 8
Waamoni
Kisha Tobia kufukuzwa katika uwanja wa hekalu, sheria ya Mungu yenye kuwa mu Kumbukumbu la Torati 23:3-6 yenye ilisema kama Waamoni na Wamoabu hawapaswe kuingia katika kutaniko ya Israeli ilisomwa na kutumikishwa. (Ne 13:1-3) Ile sheria ilitolewa miaka 1 000 hivi mbele ya pale kwa sababu Waamoni na Wamoabu walikatala kusaidia Waisraeli wakati walikaribia Inchi ya Ahadi. Kwa ujumla ile sheria inaeleweka kama inamaanisha kuwa, wakiwa kikundi, kisheria hawangekuwa sehemu ya taifa ya Israeli. Na kwa hiyo, hawangekuwa na haki na mapendeleo yenye ile ingewaletea. Lakini ile haikumaanisha kama, kipekee, Muamoni ao Mumoabu hangeweza kushirikiana na Waisraeli ao kuishi kati ya Waisraeli, na kufaidika na baraka zenye Mungu alipatia watu wake. Tunajua vile juu Zeleki mwenye tulishazungumuzia, alikuwa kati ya wapiganaji wenye nguvu wa Daudi; na habari kuhusu Rutu mumoabu inaonyesha pia vile.—Ru 1:4, 16-18.
Tumetakaswa
5 Soma Nehemia 13:4-9. Si rahisi kwetu kubaki watakatifu kwa sababu tunazungukwa na watu wabaya. Tufikirie mufano wa Eliashibu na Tobia. Eliashibu alikuwa kuhani mukubwa, na Tobia alikuwa Mwamoni na labda alikuwa wa cheo cha chini katika utawala wa Waperse huko Yudea. Tobia na marafiki wake walipinga jitihada za Nehemia za kujenga upya kuta za Yerusalemu. (Neh. 2:10) Waamoni walikatazwa kuingia katika viwanja vya hekalu. (Kum. 23:3) Namna gani basi kuhani mukubwa angemupatia mutu kama Tobia nafasi katika chumba kimoja cha kulia chakula cha hekalu?
6 Tobia alikuwa rafiki wa karibu wa Eliashibu. Tobia na mwana wake Yehohanani walioa wanawake Wayahudi, na Wayahudi wengi walimusifu sana Tobia. (Neh. 6:17-19) Mumoja wa wajukuu wa Eliashibu alioa binti wa Sanbalati, aliyekuwa gavana wa Samaria, ambaye alikuwa mumoja wa marafiki wa karibu wa Tobia. (Neh. 13:28) Uhusiano huo unaweza kutusaidia kuelewa kwa nini Kuhani Mukubwa Eliashibu alijiacha achochewe na mutu asiyeamini na mupinzani kama huyo. Lakini Nehemia alionyesha ushikamanifu kwa Yehova kwa kutupa inje vitu vyote vya Tobia.
w96-SW 15/3 uku. 16 fu. 6
Kukabili Mtihani wa Uaminifu-Mshikamanifu
6 Tukiwa waaminifu-washikamanifu kwa Yehova Mungu, tutaepuka kufanya urafiki na wale wote ambao ni adui zake. Hiyo ndiyo sababu mwanafunzi Yakobo aliandika: “Enyi wazinzi, hamjui ya kwamba kuwa rafiki wa dunia ni kuwa adui wa Mungu? basi kila atakaye kuwa rafiki wa dunia hujifanya kuwa adui wa Mungu.” (Yakobo 4:4) Tunataka kuwa na uaminifu-mshikamanifu ambao Mfalme Daudi alionyesha aliposema hivi: “Je! BWANA nisiwachukie wanaokuchukia? Nisikirihike nao wakuasio? Nawachukia kwa ukomo wa chuki, wamekuwa adui kwangu.” (Zaburi 139:21, 22) Hatutaki kuchangamana na watu wowote watendao dhambi kimakusudi, kwa kuwa hakuna jambo la kutushirikisha nao. Je, uaminifu-mshikamanifu kwa Mungu hautatuzuia kuchangamana na maadui wowote wa Yehova kama hao, wawe ni watu au iwe ni televisheni?
Mali ya Kiroho
it-2-F uku. 359 fu. 8
Muziki
Ku hekalu kuimba ilionwa kuwa jambo ya maana sana. Tunajua vile juu maandiko mingi inazungumuzia waimbaji, na pia juu “hawakupangwa kufanya kazi” zenye Walawi wengine walikuwa wanafanya ili kutimiza utumishi wao kwa ukamili. (1Ny 9:33) Jambo yenye inakazia kama waliendelea kuwa kikundi ya pekee ya Walawi ni kwamba, wakati walirudia Babiloni walitajwa mu kikundi tofauti na Walawi wengine. (Ezr 2:40, 41) Na hata Artashasta mufalme wa Uajemi, aliwatendea kwa njia ya pekee kwa kuamuru wasilipe ‘kodi, ushuru, na malipo,’ pamoja na vikundi vingine vya pekee. (Ezr 7:24) Kisha, mufalme aliamuru kama ‘kukuwe mupango fulani kwa ajili ya mahitaji ya kila siku ya waimbaji.’ Hata kama Biblia inasema kama Artashasta njo mwenye alitoa ile amri, inawezekana ni Ezra njo alitoa ile amri kwa mamlaka yenye Artashasta alimupatia. (Ne 11:23; Ezr 7:18-26) Kwa hiyo, tunaelewa juu ya nini hata kama waimbaji wote walikuwa Walawi, Biblia inawataya mu kikundi tofauti kwa kusema “waimbaji, na Walawi.”—Ne 7:1; 13:10.