Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha
© 2023 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
TAREHE 4-10/9
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | ESTA 1-2
“Ujikaze Kuwa Mwenye Kiasi Kama Esta”
Unaweza Kuendelea Kuwa Mwenye Kiasi Wakati wa Majaribu
11 Inaweza pia kuwa vigumu kwetu kuonyesha sifa ya kiasi watu wanapoturai au kutusifu kupita kiasi. Fikiria mwenendo mzuri wa Esta maisha yake yalipobadilika ghafula. Alikuwa mrembo sana na alitendewa kwa njia ya pekee kwa mwaka mzima. Kila siku, alishirikiana na wanawake wengi vijana kutoka milki yote ya Uajemi ambao walikuwa wakijitahidi kupata kibali cha mfalme. Hata hivyo, aliendelea kuwa mwenye heshima na mtulivu. Hakuanza kuwa na kiburi au kukosa sifa ya kiasi, hata baada ya mfalme kumchagua awe malkia wake.—Esta 2:9, 12, 15, 17.
Alihatarisha Uzima Wake ili Kulinda Watu wa Mungu
15 Siku inapofika ili Esta apelekwe kwa mufalme, anapewa nafasi ya kuchagua kitu chochote ambacho anafikiri kuwa ni cha lazima kwake, labda ili ajifanye kuwa muzuri zaidi. Lakini, anajionyesha kuwa mwenye kiasi na haombe kitu chochote zaidi ya vitu ambavyo Hegai anamutolea. (Esta 2:15) Ameelewa kabisa kwamba uzuri wa sura hautoshe ili kuvutia moyo wa mufalme; anajua kwamba sifa ya kiasi na unyenyekevu ambayo wengi wanakosewa nayo katika nyumba ya mufalme itavutia zaidi. Je, ana haki ya kufikiri hivyo?
Unaweza Kuendelea Kuwa Mwenye Kiasi Wakati wa Majaribu
12 Ikiwa tuko wenye kiasi, muvalio na mwenendo wetu vitaonyesha kama tunajiheshimia sisi wenyewe na wengine pia. Kuliko kuwa na majivuno ao kujaribu kushangaza watu, tunajikaza kuwa na “roho ya utulivu na ya upole.” (Soma 1 Petro 3:3, 4; Yeremia 9:23, 24) Namna tunajiona sisi wenyewe itafikia kuonekana katika maneno na matendo yetu. Kwa mufano, tunaweza kujaribu kufanya watu wafikiri kuwa tuko wa hali ya juu kuliko wengine kwa sababu ya mambo yenye tunafanya, mambo yenye tunajua, ao watu wenye tunajua. Ao tunaweza kujaribu kuonyesha kuwa tulifanya jambo fulani la maana kwa uwezo wetu wenyewe, hata kama wengine walitusaidia kufanya jambo hilo. Lakini fikiria mufano wa Yesu. Angeweza kushangaza sana watu na hekima nyingi yenye alikuwa nayo. Lakini, Yesu alikuwa anataja kila mara maneno ya Neno la Mungu. Hakupenda watu wamutukuze yeye. Sikuzote, alipenda utukufu umuendee Yehova.—Yohana 8:28.
Mali ya Kiroho
Ulijua?
Walipata bamba yenye maandishi ya Waajemi yenye ilikuwa na jina ya mwanaume mwenye kuitwa Marduka (mu Kiswahili Mordekai). Alikuwa mufanyakazi wa serikali. Pengine kazi yake ilikuwa kufanya hesabu ya mali ya mufalme katika Shushani. Wakati ile bamba ilivumbuliwa, Arthur Ungnad, mutu mwenye elimu ya historia ya Mashariki, alisema kama “zaidi ya Biblia na ile bamba tu, hakuna kitu ingine yenye ilizungumuzia Mordekai” ile wakati.
Tangu Ungnad aseme vile, watu wenye elimu wametafsiri maandishi yenye kupatikana ku maelfu ya mabamba ingine ya Waajemi. Kati ya ile mabamba, kuko mabamba ya Persépolis yenye ilivumbuliwa mu mabomoko ya Nyumba ya Hazina karibu na kuta za muji. Ile mabamba iliandikwa wakati wa utawala wa Mufalme Artashasta wa Kwanza. Iliandikwa mu luga ya Waelamu, na iko na majina mingi yenye inapatikana mu kitabu ya Esta.
Mabamba mbalimbali ya Persépolis inataya jina Marduka, mwenye alikuwa mwandishi kwenye makao ya mufalme katika Shushani wakati ya utawala wa Artashasta wa Kwanza. Bamba moya inasema kama Marduka alikuwa mutafsiri. Ile inapatana na mambo yenye Biblia inasema juu ya Mordekai. Alikuwa ofisa kwenye makao ya mufalme Ahasuero (Artashasta wa Kwanza) na alikuwa nazungumuza karibu luga mbili. Mara mingi Mordekai aliikala ku mulango mukubwa wa makao ya mufalme katika Shushani. (Est. 2:19, 21; 3:3) Mulango mukubwa wa makao ya mufalme ulikuwa jengo kubwa kwenye maofisa wa nyumba ya mufalme walikuwa natumikia.
Kuko mambo mingi yenye kufanana kati ya Marduka mwenye ile mabamba inazungumuzia na Mordekai mwenye Biblia inazungumuzia. Waliishi wakati ileile, fasi ileile, walitumikia cheo ileile, na walitumikia fasi ileile. Wakati tunatia ile mambo yote pamoya, tunaona kama mambo yenye wale wenye kuvumbula vitu vya zamani walivumbula inapatana na Mordekai mwenye kuzungumuziwa mu kitabu ya Esta.
Hotuba: Musaada Kutoka kwa Yesu na Malaika
Ukuwe Hodari—Yehova Ni Musaidizi Wako
3 Paulo alikuwa na lazima ya musaada. Mu mwaka wa 56 hivi kisha kuzaliwa kwa Yesu, kikundi cha watu walimupeleka inje ya hekalu katika Yerusalemu, na walijaribu kumuua. Siku yenye ilifuata, wakati Paulo alipelekwa mbele ya Sanhedrini, maadui wake walikuwa karibu kumupasua vipande-vipande. (Mdo. 21:30-32; 22:30; 23:6-10) Ile wakati pengine Paulo alijiuliza hivi: ‘Nitaendelea kuteseka hivi mupaka wakati gani?’
4 Paulo alipata musaada gani? Kisha Paulo kufungwa, “Bwana,” ni kusema Yesu, alisimama pembeni yake usiku na kumuambia hivi: “Usiogope! Kwa maana kama vile umekuwa ukitoa ushahidi kamili juu yangu katika Yerusalemu, ni vile unapaswa kutoa ushahidi katika Roma pia.” (Mdo. 23:11) Ile maneno ilimutia moyo kabisa. Yesu alimupongeza juu alikuwa ametoa ushahidi katika Yerusalemu. Na alimuahidi kama atafika Roma akiwa salama na kama atatoa ushahidi kule pia. Bila shaka ile maneno ilimufanya Paulo ajisikie salama kama vile mutoto anajisikiaka wakati iko mu mikono ya baba yake.
5 Paulo alipata magumu gani ingine? Miaka mbili hivi kisha mambo yenye ilimufikia Yerusalemu, Paulo alisafiri kuenda Italia. Wakati alikuwa mu mashua, kulitokea zoruba kali yenye ilifanya wafanyakazi wa mu ile mashua na watu wenye walikuwa wanasafiri mu ile mashua wawaze kama watakufa. Lakini Paulo hakuogopa. Juu ya nini? Aliambia watu wenye walikuwa mu mashua hivi: “Usiku huu malaika wa Mungu mwenye mimi ni mali yake na mwenye ninatolea utumishi mutakatifu alisimama karibu yangu na akasema: ‘Usiogope, Paulo. Unapaswa kusimama mbele ya Kaisari, na angalia! Mungu amekupatia wale wote wenye wanasafiri pamoja na wewe.’” Yehova alitumia malaika ili amuhakikishie Paulo mambo yenye Yesu alikuwa amemuambia. Na kwa kweli, Paulo alifika Roma.—Mdo. 27:20-25; 28:16.
6 Tunapata musaada gani? Yesu atatutegemeza kama vile alimutegemeza Paulo. Kwa mufano, Yesu alitolea wafuasi wake wote ahadi hii: “Niko pamoja na ninyi sikuzote mupaka umalizio wa mupangilio wa mambo.” (Mt. 28:20) Maneno ya Yesu inaweza kututia nguvu. Juu ya nini? Juu wakati fulani, tunapataka magumu yenye iko nguvu kuvumilia. Kwa mufano, tunahuzunikaka sana wakati mutu mwenye tulikuwa tunapenda anakufa. Na ile huzuni haikuwake ya siku kidogo tu, inaweza kufanya miaka mingi. Wengine wako wanapata magumu kwa sababu ya uzee, na wengine wako wanapata magumu kwa sababu wakati fulani wanakuwaka wenye kushuka moyo. Hata hali yetu ikuwe namna gani, tunapata nguvu ya kuvumilia kwa sababu tunajua kama Yesu iko pamoja na sisi “sikuzote,” hata wakati tunapata matatizo ya nguvu sana mu maisha yetu.—Mt. 11:28-30.
7 Neno la Mungu linatuhakikishia kama, Yehova anatusaidia kupitia malaika wake. (Ebr. 1:7, 14) Kwa mufano, malaika wanatutegemeza na kutuongoza wakati tuko tunahubiri “habari njema ya Ufalme” kwa watu wa “kila taifa na kabila na luga.”—Mt. 24:13, 14; soma Ufunuo 14:6.
TAREHE 11-17/9
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | ESTA 3-5
“Saidia Wengine Watumikishe Uwezo Wao Wote”
it-2-F uku. 345 fu. 5
Mordekai
Anakatala Kumuinamia Hamani. Mbele ya pale, Mufalme Ahasuero alimuweka Hamani Mwagagi kuwa waziri mukubwa na aliamuru watu wote wenye kuwa ku mulango mukubwa wa mufalme wamuinamie Hamani, juu ya cheo yake ya mupya. Mordekai alikatala kabisa kufanya vile na alisema kama ni kwa sababu alikuwa Muyahudi. (Est 3:1-4) Juu Mordekai alisema kama ile njo ilikuwa sababu, ile inaonyesha kama kufanya vile kungekuwa na matokeo juu ya uhusiano wake pamoya na Yehova, akiwa Muyahudi mwenye kujitoa kwa Mungu. Alijua kama kumuinamia Hamani kulimaanisha mambo mingi zaidi, haikukuwa tu kuinamia mutu mwenye mamlaka, kama vile Waisraeli walifanyaka zamani, ili kuonyesha heshima kwa sababu ya cheo yake. (2Sa 14:4; 18:28; 1Fa 1:16) Kuhusu Hamani, Mordekai alikuwa na sababu ya muzuri ya kukatala kumuinamia. Pengine Hamani alikuwa Mwamaleki na Yehova alisema kama atapigana na Waamaleki “kizazi mupaka kizazi.” (Kut 17:16; ona HAMANI.) Mordekai alikatala kufanya vile kwa sababu alipenda kuwa mushikamanifu kwa Mungu hapana kwa sababu za kipolitike.
it-2-F uku. 345 fu. 7
Mordekai
Alitumiwa ili Kukomboa Waisraeli. Kuhusu sheria yenye iliamuru kuua Wayahudi wote wenye walikuwa mu ule utawala, Mordekai aliamini kama Esta alipewa mamlaka ya kifalme mu ile wakati juu ya kukomboa Wayahudi. Alimuonyesha Esta daraka nzito yenye alikuwa nayo na alimuambia aende kuona mufalme ili awaonyeshe wema na awasaidie. Hata kama kufanya vile kungetia uzima wake mu hatari, Esta aliitika kuenda.—Est 4:7–5:2.
iAlihatarisha Uzima Wake ili Kulinda Watu wa Mungu
22 Bila shaka, Esta ni mwenye wasiwasi anapopata ujumbe wa Mordekai. Anapatwa na jaribu kubwa la imani. Namna anavyomujibia Mordekai inaonyesha kwamba anaogopa. Esta anamukumbusha Mordekai sheria ya mufalme. Mutu yeyote anayeingia kwa mufalme bila kuitwa anapaswa kuuawa. Mutu anaweza kupona ikiwa tu mufalme anamunyooshea fimbo yake ya kifalme ya zahabu. Je, Esta ana sababu yoyote ya kumufanya afikiri kwamba hatauawa, zaidi sana anapokumbuka jambo lililomufikia Vashti kwa sababu ya kukataa amri ya mufalme ya kuja mbele yake alipoitwa? Esta anamujibia Mordekai kwamba tangu siku 30 mufalme hajamuita ili aingie kumuona! Kwa kuwa hakuitwa kwa siku nyingi, Esta hajue ikiwa mufalme amebadilisha mawazo yake na kwamba hapendezwe naye tena.—Esta 4:9-11.
23 Mordekai anamujibia Esta kwa uhakika ili kutia nguvu imani yake. Anamuhakikishia kwamba akinyamaza, wokovu wa Wayahudi utakuja katika njia nyingine. Lakini, je, yeye ataponyoka kweli wakati Wayahudi wataanza kuuawa? Mordekai anaonyesha hapa kwamba ana imani yenye nguvu katika Yehova, ambaye hawezi kamwe kuacha watu wake waangamizwe na ahadi zake zikose kutimizwa. (Yos. 23:14) Kwa hiyo, Mordekai anamuuliza Esta hivi: “Ni nani anayejua ikiwa si kwa ajili ya wakati kama huu kwamba umefikia heshima ya kifalme?” (Esta 4:12-14) Hauone kwamba Mordekai anastahili kuigwa? Anamutumainia kabisa Yehova, Mungu wake. Je, sisi pia tunafanya hivyo?—Met. 3:5, 6.
Mali ya Kiroho
Kupigania Uhuru wa Kuabudu
14 Kama Esta na Mordekai wa hapo zamani, watu wa Yehova leo wanapigania uhuru wa kumuabudu Yehova kama vile ameamuru. (Esta 4:13-16) Unaweza pia kuwaunga mukono? Ndiyo. Unaweza kuendelea kusali kwa ajili ya ndugu na dada ambao wanateseka leo kwa sababu wanatendewa isivyo haki kisheria. Sala kama hizo zinaweza kusaidia sana ndugu na dada zetu ambao wanapambana na hali ngumu na ambao wanateseka kwa sababu ya imani yao. (Soma Yakobo 5:16.) Yehova anajibu sala hizo? Ushindi mbalimbali ambao tumepata kwenye tribinali unashuhudia jambo hilo!—Ebr. 13:18, 19.
TAREHE 18-24/9
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | ESTA 6-8
“Mufano Muzuri Juu ya Namna ya Kuzungumuza”
Alitenda kwa Hekima, Ujasiri na kwa Kujinyima
15 Kwa sababu Esta alikuwa muvumilivu kungojea siku moja zaidi ili kutoa ombi lake kwa mufalme, hilo lilimupatia Hamani wakati wa kufanya mambo yaliyoongoza kwenye kuanguka kwake. Na inawezekana ni Yehova aliyefanya mufalme huyo akose usingizi, sivyo? (Met. 21:1) Haishangaze ikiwa Neno la Mungu linatutia moyo tuwe katika hali ya ‘kungojea’! (Soma Mika 7:7.) Tunapomutumainia Mungu na kumungojea atende, tunaweza kufikia kutambua kwamba njia yake ya kutatua matatizo ndio nzuri zaidi kuliko njia zetu.
Anasema kwa Ujasiri
16 Esta hapaswe kuendelea kumuacha mufalme katika wasiwasi kuhusu kile anachotaka; kwenye karamu anayotayarisha siku ya pili anapaswa kumuambia mambo yote. Lakini, ni wakati gani kaitbisa atamuambia? Bila kutazamia, mufalme anamuuliza tena ikiwa ombi lake ni nini, naye Esta anatumia nafasi hiyo ili kujieleza. (Esta 7:2) Sasa ‘wakati wa Esta wa kusema’ umefika.
Alitenda kwa Hekima, Ujasiri na kwa Kujinyima
17 Unaweza kuwazia namna Esta anavyofanya sala fupi kwa Mungu wake mbele ya kusema maneno haya: ‘Ikiwa nimepata kibali machoni pako, Ee mufalme, na mufalme akiona vema, na nipewe nafsi yangu mwenyewe kuwa ombi langu na watu wangu kuwa haja yangu.’ (Esta 7:3) Katika maneno hayo, unaona kwamba anamuheshimu mufalme, anamuhakikishia kwamba ataheshimu uamuzi wake kadiri anavyoona kuwa ni hivyo. Esta anatofautiana kabisa na Vashti ambaye alimupatisha bwana yake haya kimakusudi! (Esta 1:10-12) Tena, Esta hamuseme mufalme vibaya kwa sababu ya tendo lake la upumbavu la kumuaminia Hamani. Kuliko kufanya hivyo, anamulilia mufalme amulinde na hali inayohatarisha uzima wake.
Alitenda kwa Hekima, Ujasiri na kwa Kujinyima
18 Bila shaka, mufalme anashangazwa na anaguswa moyo na ombi hilo. Ni nani huyo anayetaka kuhatarisha maisha ya malkia wake? Esta anamujibu: ‘Tumeuzishwa, mimi na watu wangu, tuangamizwe, tuuawe na kuharibiwa. Basi ikiwa tungaliuzishwa tuwe watumwa na wajakazi, ningalinyamaza kimya. Lakini taabu hii haifae ikiwa inamuletea mufalme hasara.’ (Esta 7:4) Unaona kwamba Esta ameonyesha tatizo waziwazi, hata hivyo, anaongeza kwamba ingekuwa ni jambo tu la kuuzishwa kuwa watumwa hangesema lolote. Lakini, kwa kuwa mauaji hayo makubwa yangemuletea mufalme mwenyewe hasara kubwa, kwa hiyo hawezi kubaki kimya.
19 Mufano wa Esta unatufundisha mambo mengi kuhusu ufundi wa kumufanya mutu akubali yale unayomuambia. Ikiwa una tatizo nzito na ni lazima umuambie mutu unayemupenda ao mutu fulani mwenye mamlaka tatizo hilo, ili kumusadikisha ni vizuri kuwa na uvumilivu, heshima na kusema tatizo hilo waziwazi.—Met. 16:21, 23.
Mali ya Kiroho
w06-SW 1/3 uku. 11 fu. 1
Neno la Yehova Liko Hai Mambo Makuu Katika Kitabu cha Esta
7:4—Kuangamizwa kwa Wayahudi kungemleteaje “mfalme hasara”? Kwa kutaja kwa busara uwezekano wa kuwauza Wayahudi kama watumwa, Esta alimwonyesha mfalme hasara ambayo ingesababishwa ikiwa Wayahudi wangeangamizwa. Vipande 10,000 vya fedha ambavyo Hamani alikuwa ameahidi havingeleta faida kubwa katika hazina ya mfalme kuliko utajiri ambao ungepatikana ikiwa Hamani angepanga njama ya kuwauza Wayahudi utumwani. Ikiwa njama hiyo ingetekelezwa, malkia pia angeangamizwa.
Hotuba: Ufundishe Muzuri Kama Yakobo—Fundisha kwa Njia ya Mwepesi
Ujifunze Kupitia Ndugu Moja Mudogo wa Yesu
8 Yakobo hakusoma masomo mingi ya ulimwengu yenye kuvutia. Viongozi wa dini wa wakati wake walimuona kama vile waliona mutume Petro na Yohana, ni kusema, kama “watu wenye hawana elimu na watu wa kawaida.” (Mdo. 4:13) Lakini Yakobo alijifunza kuwa mwalimu muzuri, kama vile inaonyeshwa wakati tunasoma kitabu yenye kuwa na jina yake. Kama Yakobo, tunaweza kuwa hatukusoma masomo mingi ya ulimwengu. Hata vile, kwa musaada wa roho ya Yehova na mazoezi mbalimbali yenye tengenezo yake inatutolea, siye pia tunaweza kuwa walimu wazuri. Tuzungumuzie basi mufano wenye Yakobo alituachia akiwa mwalimu na tuone somo fulani zenye tunaweza kujifunza.
9 Yakobo hakutumia maneno ya nguvu ao mafasirio yenye haieleweke. Ile ilisaidia wasikilizaji wake wajue mambo yenye walipaswa kufanya na namna walipaswa kuifanya. Kwa mufano, mu njia ya mwepesi Yakobo alifundisha kama Wakristo wanapaswa kuwa tayari kuteseka bila kuweka kinyongo. Aliandika hivi: “Tunaona wale wenye wamevumilia kuwa wenye furaha. Mumesikia juu ya uvumilivu wa Yobu na mumeona matokeo yenye Yehova alileta, kwamba Yehova ni mwenye upendo mwingi sana na mwenye rehema.” (Yak. 5:11) Kumbuka kama mambo yenye Yakobo alikuwa anafundisha ndugu zake ilitegemea Maandiko. Alitumia Neno ya Mungu ili kusaidia wasikilizaji wake waone kama siku zote Yehova anabariki wale wenye kuwa washikamanifu kwake, kama Yobu. Yakobo alifundisha ile somo wakati alitumia maneno ya mwepesi na yenye kuwa wazi. Mu ile njia, hakupenda watu wamukazie yeye uangalifu, lakini wakazie Yehova uangalifu.
10 Somo: Tumia habari ya mwepesi, na utumie Neno ya Mungu ili kufundisha. Wakati tuko nafundisha wengine, kusudi yetu haipaswe kuwa kuwaonyesha namna tunajua mambo mingi, lakini tunapaswa kuwaonyesha namna Yehova anajua mambo mingi na namna anawahangaikia. (Ro. 11:33) Tunaweza kufikia kufanya vile kwa kuacha kila mara mambo yenye tunasema itegemee Maandiko. Kwa mufano, kuliko kuambia wanafunzi wetu wa Biblia mambo yenye tungefanya ku fasi yao, tunapaswa kuwasaidia kufikiri kuhusu mifano ya Biblia na kuwasaidia waelewe mawazo ya Yehova na namna anajisikia. Kisha watatumikisha mambo yenye wanajifunza juu wanapenda kumufurahisha Yehova, hapana siye.
TAREHE 25/9–1/10
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | ESTA 9-10
“Alitumia Mamlaka Yake kwa Ajili ya Wengine”
it-2-F uku. 346 fu. 1
Mordekai
Mordekai aliwekwa kuwa waziri mukubwa pa nafasi ya Hamani na mufalme alimupatia pete yake ya kutia muhuri dokima za inchi. Mufalme alimupatia Esta nyumba ya Hamani na Esta aliipatia Mordekai ili aisimamie. Kwa ruhusa ya mufalme, Mordekai alitoa amri yenye ilipatia Wayahudi haki ya kujipigania. Ile ilikuwa furaha kubwa sana kwa Wayahudi na iliwapatia tumaini ya kukombolewa. Watu wengi mu Utawala wa Waajemi walijiunga na Wayahudi, na wakati tarehe 13, ya Mwezi wa Adari ilifika, siku yenye zile sheria zilipaswa kutumika, Wayahudi walikuwa tayari. Maofisa walitegemeza Wayahudi kwa sababu ya cheo ya juu ya Mordekai. Mu Shushani pigano iliendelea mupaka siku yenye kufuata. Zaidi ya maadui 75000 wa Wayahudi waliuawa mu Utawala wa Waajemi, kutia ndani watoto kumi wa Hamani. (Est 8:1–9:18) Kisha kukubaliana na Esta, Mordekai aliamuru Wayahudi wakuwe wanasherehekea tarehe ya 14 na 15 ya Mwezi wa Adari, kuwa “siku za Purimu,” ili kufurahi, kufanya karamu, kupatiana zawadi, na kusaidia maskini. Wayahudi walikubali na waliifanya kuwa amri kwa wazao wao na wote wenye kujiunga nao. Juu Mordekai alikuwa mutu wa pili mu utawala, aliheshimiwa na watu wote wa Mungu, ni kusema Wayahudi, na aliendelea kutumika kwa faida yao.—Est 9:19-22, 27-32; 10:2, 3.
it-2-F uku. 627 fu. 8
Purimu
Kusudi. Hata kama watu fulani wanasema kama sherehe ya Purimu yenye Wayahudi wanafanya leo inatia ndani zaidi sana mambo ya kimwili kuliko mambo ya kidini na wakati fulani watu wanafanya ku ile sherehe mambo yenye kupita mipaka, mambo haikukuwa vile wakati ile karamu ilianzishwa. Mordekai na Esta walikuwa waabudu wa Mungu wa kweli, Yehova. Na ile sherehe ilianzishwa ili kumutukuza Yehova. Na tunaweza kusema kama Yehova njo alikomboa Wayahudi ile wakati, juu tatizo ilianza wakati Mordekai aliazimia kumuabudu Yehova tu na kubakia mushikamanifu kwake. Inawezekana Hamani alikuwa Mwamaleki, taifa yenye Yehova alilaani na kuamuru iharibiwe. Mordekai aliheshemia amri ya Mungu na alikatala kumuinamia Hamani. (Est 3:2, 5; Kut 17:14-16) Pia, maneno yenye Mordekai alimuambia Esta (Est 4:14) inaonyesha kama alitumainia mutu mwenye kuwa na mamlaka ya juu zaidi ili akomboe Wayahudi. Na kwa sababu Esta alifunga mbele ya kuenda kuonana na mufalme na kumutolea ombi yake ya kwanza ya kumualika ku karamu, ile ilionyesha kama alitafuta musaada wa Mungu.—Est 4:16.
cl-SW uku. 101-102 fu. 12-13
“Iweni Waigaji wa Mungu” Mnapotumia Uwezo
12 Yehova ameweka waangalizi wa kuongoza kutaniko la Kikristo. (Waebrania 13:17) Wanaume hao wenye sifa za kustahili wanapaswa kutumia mamlaka waliyopewa na Mungu kutoa msaada unaohitajiwa na kulisaidia kutaniko likue kiroho. Je, wazee wana haki ya kupiga ubwana juu ya waamini wenzao kwa sababu ya wadhifa wao? La hasha! Wazee wanahitaji kuwa na usawaziko na unyenyekevu wanapotimiza daraka lao kutanikoni. (1 Petro 5:2, 3) Biblia inawaambia hivi waangalizi: ‘Lichungeni kutaniko la Mungu, ambalo alilinunua kwa damu ya Mwana wake mwenyewe.’ (Matendo 20:28) Kwa sababu hiyo, wazee wanapaswa kumtendea kila mshiriki wa kutaniko kwa fadhili.
13 Mfano ufuatao unaonyesha jambo hilo: Rafiki yako mpendwa anakuomba umtunzie mali fulani yenye thamani kubwa. Wajua kwamba mali hiyo ilimgharimu pesa nyingi sana. Je, hutaitunza kwa tahadhari na uangalifu mkubwa mno ili isiharibike? Vivyo hivyo, Mungu amewakabidhi wazee wajibu wa kutunza mali yenye thamani kubwa sana: kutaniko, ambalo washiriki wake wanalinganishwa na kondoo. (Yohana 21:16, 17) Yehova anapenda sana kondoo wake—anawapenda kiasi cha kwamba aliwanunua kwa damu yenye thamani ya Mwana wake mzaliwa-pekee, Yesu Kristo. Yehova aliwanunua kondoo wake kwa bei ya juu sana. Wazee wanyenyekevu hukumbuka jambo hilo na kuwatendea kondoo wa Yehova kwa njia inayofaa.
Mali ya Kiroho
w06-SW 1/3 uku. 11 fu. 4
Neno la Yehova Liko Hai Mambo Makuu Katika Kitabu cha Esta
9:10, 15, 16—Ingawa amri iliidhinisha kupora nyara, kwa nini Wayahudi hawakuzichukua? Kutochukua kulionyesha wazi kwamba kusudi lao hasa lilikuwa kuwaokoa watu wao wala si kujitajirisha.
TAREHE 2-8/10
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | YOBU 1-3
“Endelea Kuonyesha Kama Unamupenda Yehova Sana”
Uige Imani na Utii wa Noa, Danieli, na Ayubu
16 Magumu yenye Ayubu alipambana nayo. Ayubu alipatwa na mabadiliko makubwa katika maisha yake. Mbele apate majaribu, alikuwa ‘mukubwa kuliko watu wote wa Mashariki.’ (Ayu. 1:3) Alikuwa tajiri, alijulikana sana, na watu walimuheshimia sana. (Ayu. 29:7-16) Lakini, hata kama alikuwa na mambo hayo yote, Ayubu hakuanza kuwa na kiburi ao kuona kama hakukuwa na lazima ya Mungu. Kwa kweli, Yehova alimuita, ‘mutumishi wangu,’ na aliongezea hivi: ‘Mutu asiye na lawama na munyoofu [ao, muaminifu], mwenye kumuogopa Mungu na kujiepusha na ubaya.’—Ayu. 1:8.
17 Kwa muda mufupi sana, maisha ya Ayubu yalibadilika kabisa. Alipoteza mali yake yote na akashuka moyo sana. Tunajua kwamba mambo hayo yalimupata kwa sababu, Shetani muchongezi, alimushitaki Ayubu mambo ya uwongo kwamba anamuabudu Mungu kwa sababu ya faida fulani. (Soma Ayubu 1:9, 10.) Yehova alichukua mashitaka hayo kwa uzito. Alimupatia Ayubu nafasi ya kuonyesha ushikamanifu wake, ili kuonyesha kama alikuwa anamuabudu Mungu kwa moyo muzuri, haiko kwa sababu ya faida fulani.
Endelea Kuwa Muaminifu-Mushikamanifu!
10 Shetani anashitaki kila mumoja wetu mambo ileile yenye alimushitaki Yobu. Ile mashitaka inakuhusu namna gani? Kwa kweli, anasema kama haumupendi kabisa Yehova Mungu, kama utaacha kumutumikia ili kuokoa uzima wako, na kama uaminifu-mushikamanifu wako ni wa uongo! (Yob. 2:4, 5; Ufu. 12:10) Ile maneno inakufanya ujisikie namna gani? Inakuumiza, haiko vile? Lakini, fikiria jambo hili: Yehova anakutumainia kabisa, njo maana amekupatia nafasi ya muzuri sana. Yehova anamuruhusu Shetani ajaribu uaminifu-mushikamanifu wako. Yehova iko hakika kama unaweza kuendelea kuwa muaminifu-mushikamanifu na kusaidia kuonyesha kama Shetani ni musema-uongo. Na anaahidi kama atakusaidia kufanya vile. (Ebr. 13:6) Ni pendeleo kubwa sana kutumainiwa na Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi katika ulimwengu wote! Unaona ni juu ya nini uaminifu-mushikamanifu ni wa maana sana? Unatusaidia kupinga uongo wa Shetani na kutetea jina la muzuri la Baba yetu na kuunga mukono namna yake ya kutawala. Tunaweza kufanya nini ili tuendelee kuonyesha ile sifa ya maana sana?
Hotuba: Ufundishe Muzuri Kama Yakobo—Ona Mambo vile Iko na Ukuwe Munyenyekevu
Ujifunze Kupitia Ndugu Moja Mudogo wa Yesu
11 Yakobo aliona mambo vile ilikuwa. Mu barua yake, ni wazi kama Yakobo alijua magumu yenye waamini wenzake walikutana nayo, na aliwatolea muongozo juu ya namna ya kupambana nayo. Kwa mufano, Wakristo fulani hawakutumikisha ile shauri palepale. (Yak. 1:22) Wengine walipendelea matajiri. (Yak. 2:1-3) Tena, ilikuwa nguvu kwa wengine kuzuia kutumia mubaya ulimi wao. (Yak. 3:8-10) Wale Wakristo walikuwa na magumu ya nguvu sana, lakini Yakobo aliamini kama wangebadilika. Alitoa shauri yake mu njia ya muzuri lakini pia mu njia ya moja kwa moja, na alitia moyo wale wenye walikuwa na magumu kiroho watafute musaada ingine kwa wazee.—Soma Yakobo 5:13-15.
12 Somo: Ona mambo vile iko, lakini pia uendelee kuwa na maoni yenye kufaa juu ya wengine. Inaweza kuwa nguvu kwa watu wengi wenye tunajifunzaka nao Biblia kutumikisha mashauri yenye kuwa ndani yake. (Yak. 4:1-4) Inaweza kuchukua wakati fulani juu waache tabia zao za mubaya na kuwa na sifa za Kikristo. Juu ya kuiga Yakobo, tunapaswa kuwa na uhodari wa kuambia wanafunzi wetu ni wapi wanapaswa kufanya mabadiliko. Tuko pia na lazima ya kuwa na maoni yenye kufaa, kutumainia kama Yehova atavuta watu wanyenyekevu kwake na atawapatia nguvu ya kufanya mabadiliko mu maisha yao.—Yak. 4:10.
13 Yakobo aliendelea kuwa na maoni ya muzuri juu yake mwenyewe. Yakobo hakuwaza kama alikuwa wa maana zaidi kuliko Wakristo wengine juu alikuwa ndugu ya Yesu ao juu ya mapendeleo ya utumishi yenye alikuwa nayo. Aliita Wakristo wengine kuwa “ndugu zangu wapendwa.” (Yak. 1:16, 19; 2:5) Hakuonyesha kama alikuwa mukamilifu. Lakini, alijitia pia ndani wakati alisema hii maneno yenye kufuata: “Sisi wote tunafanya makosa mara nyingi.”—Soma Yakobo 3:2 na maelezo ya chini.
14 Somo: Usisahau kama siye wote tuko watenda-zambi. Hatupaswe kuwaza kama tunapita wale wenye tunafundishaka. Juu ya nini tunasema vile? Kama tunafanya mwanafunzi wetu awaze kama hatufanyake makosa, anaweza kuwaza kama hawezi kutimiza kabisa mambo yenye Mungu anatuomba kufanya. Lakini, kama tunamuambia waziwazi kama haikuwake pia mwepesi kwetu kufuata kanuni za Maandiko na kama tunamufasiria namna Yehova alitusaidia kushinda magumu yetu, ile itasaidia mwanafunzi wetu aone kama yeye pia anaweza kumutumikia Yehova.
Mali ya Kiroho
Maneno ya Mwisho ya Yesu Inaweza Kutufundisha Nini?
9 Yesu alisema nini? Wakati kidogo mbele akufe, Yesu alisema hivi kwa sauti kubwa: “Mungu wangu, Mungu wangu, sababu gani umeniacha?” (Mt. 27:46) Biblia haionyeshe waziwazi juu ya nini Yesu alisema vile. Lakini, ona mambo yenye ile maneno inaweza kutufundisha. Jambo la kwanza lenye tunajifunza ni hili: Kwa kusema ile maneno, Yesu alikuwa anatimiza unabii wa Zaburi 22:1. Tena, ile maneno inaonyesha waziwazi kama, Yehova hakutia “ukuta wa ulinzi kumuzunguka” Mwana wake. (Yob. 1:10) Yesu alielewa kama Baba yake aliruhusu wale wenye walikuwa wanamuchukia wajaribu imani yake kabisa mupaka kufikia kifo. Hakuna mwanadamu mwenye alishakajaribiwa sawa vile Yesu. Zaidi ya ile, ile maneno ilihakikisha kama Yesu hakufanya kitu fulani yenye ingefanya astahili kifo.
TAREHE 9-15/10
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | YOBU 4-5
“Epuka Habari za Uongo”
it-1-F uku. 725 fu. 17
Elifazi
2. Mumoja kati ya marafiki tatu wa Yobu. (Yob 2:11) Alikuwa Mutemani, pengine alikuwa muzao wa muzaliwa wa kwanza wa Esau. Kwa hiyo alikuwa mu uzao wa Abrahamu na alikuwa wa mu jamaa ya Yobu lakini hapana ndugu wa karibu-karibu. Yeye na wazao wake walijivunia hekima yao. (Yer 49:7) Kati ya “wafariji” watatu wa Yobu, Elifazi alionekana kuwa wa maana zaidi na mwenye uvutano zaidi. Ile inaweza kuonyesha kama pengine yeye njo alikuwa mukubwa zaidi kati ya wale wafariji. Mu sehemu zote tatu za mazungumuzo, yeye njo alisema wa kwanza na alisema mingi.
w05 15/9 uku. 26 fu. 2
Kataa Mawazo Yasiyofaa!
Elifazi alisema hivi kuhusu maono yasiyo ya kibinadamu aliyoona: “Roho fulani ikapita juu ya uso wangu; nywele za mwili wangu zikaanza kusimama. Ikaanza kusimama tuli, lakini sikuitambua sura yake; umbo fulani lilikuwa mbele ya macho yangu; kulikuwa na utulivu, na sasa nikasikia sauti.” (Ayubu 4:15, 16) Ni roho ya aina gani iliyoathiri kufikiri kwa Elifazi? Maneno yenye kushutumu yaliyosemwa yalionyesha kwamba kwa hakika roho hiyo haikuwa mmoja wa malaika waadilifu wa Mungu. (Ayubu 4:17, 18) Ilikuwa roho mwovu. Kama sivyo, kwa nini Yehova alimkaripia Elifazi na wenzake wawili kwa kuwa walisema uwongo? (Ayubu 42:7) Naam, Elifazi aliathiriwa na roho mwovu. Maneno yake yalidhihirisha kwamba fikira zake hazikuwa kama za Mungu
w10-SW 15/2 uku. 19 fu. 5-6
Kataa Kabisa Uwongo wa Shetani!
Shetani alimtumia Elifazi, mmoja kati ya marafiki watatu waliomtembelea Ayubu, kudai kwamba wanadamu ni dhaifu sana hivi kwamba hawawezi kuendelea kuwa waaminifu. Elifazi alisema kwamba wanadamu ‘wanakaa katika nyumba za udongo,’ kisha akamwambia Ayubu hivi: “Msingi wao umo mavumbini! Mtu huwaponda upesi kuliko nondo. Kuanzia asubuhi mpaka jioni wao hupondwa vipande-vipande; wao huangamia milele bila yeyote kutia hilo moyoni.”—Ayu. 4:19, 20.
Maandiko mengine yanasema sisi ni kama “vyombo vya udongo,” vyungu vya udongo wa mfinyanzi vinavyovunjika kwa urahisi. (2 Kor. 4:7) Sisi ni dhaifu kwa sababu tumerithi dhambi na hali ya kutokamilika. (Rom. 5:12) Hatuwezi kushinda mashambulizi ya Shetani kwa uwezo wetu wenyewe. Lakini tukiwa Wakristo, Yehova anaweza kutusaidia. Hata ingawa tuna udhaifu mbalimbali, sisi ni wenye thamani machoni pa Mungu. (Isa. 43:4) Kwa kuongezea, Yehova anawapa roho takatifu wale wanaomwomba. (Luka 11:13) Roho yake inaweza kututia “nguvu zinazopita zile za kawaida,” na kutuwezesha kuvumilia hali yoyote ngumu ambayo Shetani anatuletea. (2 Kor. 4:7; Flp. 4:13) Tukimpinga Ibilisi huku ‘tukiwa imara katika imani,’ Mungu atatuimarisha na kutufanya tuwe wenye nguvu. (1 Pet. 5:8-10) Kwa hiyo, hatuna sababu ya kumwogopa Shetani Ibilisi.
mrt 32 fu. 13-17
Ujilinde na Habari za Uongo
● Tafuta kujua kwenye habari inatoka na inazungumuzia nini
Mambo yenye Biblia inasema: “Muchunguze mambo yote.”—1 Watesalonike 5:21.
Mbele ya kuamini ao kutumia wengine habari, hata habari yenye kuenea sana ao yenye kuzungumuziwa sana mu vyombo vya habari, chunguza ikiwa ni ya kweli. Utafanya vile namna gani?
Chunguza ikiwa habari ilitoka fasi yenye kutumainika. Vyombo vya kutoa habari na kompanyi zingine zinaweza kubadilisha habari ili kujitafutia faida za kibiashara ao za kipolitike. Linganisha habari yenye umepata fasi fulani na habari zenye kutolewa fasi zingine. Wakati fulani bila kujua marafiki wanaweza kukutumia habari kupitia email ao site za kupashana habari. Kwa hiyo, usiaminie zile habari mbele ya kuchunguza kwenye zilitoka.
Uchunguze ikiwa mambo yenye kuzungumuziwa ni ya sasa na ni ya kweli. Angalia tarehe, mambo yenye inaweza kuchunguzwa, na ushuhuda wenye kuhakikisha kabisa mambo yenye inasemwa. Ukuwe muangalifu zaidi sana ikiwa habari nzito zinaonekana kuwa mwepesi sana ao ikwa habari imetayarishwa ili ikuchochee ujisikie mu njia fulani.
Mali ya Kiroho
w03-SW 15/5 uku. 22 fu. 5-6
Uwe Imara, na Ushinde Shindano la Mbio la Kupata Uhai
Kuwa katika tengenezo la ulimwenguni pote la waabudu wa kweli kunaweza kutusaidia tuwe thabiti sana. Ni baraka iliyoje kushirikiana na ndugu wenye upendo wa ulimwenguni pote! (1 Petro 2:17) Nasi tunaweza kuwasaidia waamini wenzetu wawe thabiti.
Fikiria jinsi Ayubu mwadilifu alivyowasaidia wengine. Hata Elifazi mfariji bandia alilazimika kukiri hivi: “Maneno yako yamemtegemeza huyo aliyekuwa anaanguka, nawe umeyaimarisha magoti manyonge.” (Ayubu 4:4) Je, sisi huwasaidia wengine? Sote tuna daraka la kuwasaidia ndugu na dada zetu wa kiroho waendelee kumtumikia Mungu. Tunapokuwa pamoja na ndugu na dada zetu, tunaweza kutenda kulingana na maneno haya: “Itieni nguvu mikono iliyo dhaifu, yafanyeni imara magoti yaliyolegea.” (Isaya 35:3) Kwa hiyo, mbona usiazimie kuwaimarisha na kuwatia moyo Wakristo wenzako unapokutana nao? (Waebrania 10:24, 25) Kwa kuwatia moyo, kuwapongeza, na kuwashukuru kwa jitihada zao za kumpendeza Yehova, unaweza kuwasaidia sana waendelee kuwa imara, wakiwa na taraja la kushinda shindano la mbio la kupata uhai.
TAREHE 16-22/10
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | YOBU 6-7
“Wakati Maisha Inakuwa Nguvu Sana Kuvumilia”
w06-SW 15/3 uku. 14 fu. 10
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Ayubu
7:1; 14:14—Kazi ya lazima” au ‘kazi ya kulazimishwa’ inamaanisha nini? Ayubu alitaabika sana hivi kwamba akakata kauli kuwa maisha yalikuwa magumu kama kazi ngumu ya lazima. (Ayubu 10:17) Ayubu alilinganisha kazi ya kulazimishwa na kipindi ambacho mtu hulazimika kukaa Sheoli, yaani, tangu wakati wa kifo hadi ufufuo.
“Yehova . . . Anaokoa Wale Wenye Kuvunjika Moyo”
WAKATI fulani, tunaweza kufikiria namna maisha ni ya mufupi na ‘yenye kujaa taabu.’ (Yob. 14:1) Ile inaweza kufanya tuvunjike moyo wakati fulani. Watumishi fulani wa Yehova wa zamani walijisikiaka pia kuwa wenye kuvunjika moyo. Wamoja kati yao walipendaka hata wakufe. (1 Fa. 19:2-4; Yob. 3:1-3, 11; 7:15, 16) Lakini kila mara, Yehova alikuwa anawatia moyo na kuwatia nguvu kwa sababu walimutumainia. Habari yao iliandikwa katika Biblia ili itufariji na itufundishe.—Ro. 15:4.
g-SW 1/12 uku. 16-17
Unapohisi Kwamba Hutaki Kuendelea Kuishi
Hata ingawa huenda hali yako ikaonekana kuwa mbaya, kumbuka kwamba si wewe peke yako unayekabili hali hiyo na kwamba kwa kusikitisha, karibu kila mtu leo anakumbwa na tatizo fulani. Biblia inasema hivi: “Uumbaji wote unaendelea kuugua pamoja na kuwa katika maumivu pamoja.” (Waroma 8:22) Ingawa huenda kwa sasa ikaonekana kwamba tatizo lako haliwezi kusuluhishwa, mara nyingi mambo hubadilika kadiri wakati unavyopita. Kwa sasa, ni nini kinachoweza kukusaidia?
Mweleze rafiki mkomavu, unayemwamini hisia zako. Biblia inasema: “Rafiki wa kweli anapenda nyakati zote, naye ni ndugu aliyezaliwa kwa ajili ya wakati wa taabu.” (Methali 17:17) Mwanamume mwadilifu Ayubu, anayetajwa katika Biblia, aliwaeleza wengine jinsi alivyohisi alipokuwa akikabili hali ngumu. Alipohisi kwamba ‘anachukizwa na uhai wake,’ alisema hivi: “Nitaonyesha hangaiko langu kujihusu mwenyewe. Nitasema kwa uchungu wa nafsi yangu!” (Ayubu 10:1) Kuwaeleza wengine jinsi unavyohisi kunaweza kupunguza uzito wa hisia zako, na hilo linaweza kukusaidia ubadili maoni yako kuhusu matatizo unayokabili.
Mmiminie Mungu moyo wako katika sala. Wengine hufikiri kwamba sala ni njia tu ya kutuliza hisia, lakini Biblia inaonyesha jambo tofauti. Zaburi 65:2 inasema kwamba Yehova ni “msikiaji wa sala,” na 1 Petro 5:7 inasema: “Yeye anawajali ninyi.” Biblia inakazia mara nyingi umuhimu wa kumtegemea Mungu. Kwa mfano:
“Mtegemee Yehova kwa moyo wako wote wala usitegemee uelewaji wako mwenyewe. Mtambue yeye katika njia zako zote, naye atanyoosha mapito yako.”—METHALI 3:5, 6.
“[Yehova] atawatimizia wale wanaomwogopa tamaa yao, naye atakisikia kilio chao cha kuomba msaada, naye atawaokoa.”—ZABURI 145:19.
“Huu ndio uhakika ambao tunao kwake, kwamba, hata tukiomba nini kulingana na mapenzi yake, yeye hutusikia.”—1 YOHANA 5:14.
“Yehova yuko mbali sana na waovu, lakini huisikia sala ya waadilifu.”—METHALI 15:29.
Ukimweleza Mungu matatizo unayokabili, atakupa msaada. Biblia ina sababu nzuri inapokutia moyo ‘umtegemee nyakati zote. Mimina moyo wako mbele zake.’—Zaburi 62:8.
Mali ya Kiroho
Usikilize Wengine, Uwajue Muzuri, na Uwasikilie Huruma
10 Tunaweza kumuiga Yehova kwa kujikaza kuelewa ndugu na dada zetu. Ujikaze kujua muzuri ndugu na dada zako. Uzungumuze nao mbele na kisha mikutano, uhubiri pamoja nao, na kama inawezekana uwaalike ili mukule pamoja nao. Wakati unafanya vile, unaweza kujua kama dada mwenye anaonekana kuwa mwenye kujitenga na wengine kwa kweli iko mwenye haya, ndugu mwenye pengine unawazia kuwa anapenda vitu vya kimwili ni mwenye kuonyesha ukaribishaji-wageni, ao watu wa familia fulani wenye wanafika nyuma kila mara ku mikutano wanavumilia upinzani. (Yob. 6:29) Kwa kweli, hatupaswe ‘kujiingiza katika mambo ya watu wengine.’ (1 Ti. 5:13) Lakini, ni muzuri kujua jambo fulani juu ya ndugu na dada zetu na hali zenye kuwafanya wakuwe na utu fulani.
Hotuba: Ufundishe Muzuri Kama Yakobo—Tumia Mifano Yenye Kugusa Moyo
Ujifunze Kupitia Ndugu Moja Mudogo wa Yesu
15 Yakobo alitumia mifano yenye kugusa moyo. Bila shaka roho takatifu ilimusaidia, lakini inaonekana pia kama alijifunza mambo mingi kuhusu namna ya kufundisha kwa kuchunguza mifano yenye ndugu yake mukubwa Yesu alitumia. Mifano yenye Yakobo alitumia mu barua yake iko mwepesi na somo iko wazi.—Soma Yakobo 3:2-6, 10-12.
16 Somo: Tumia mifano yenye kufaa. Wakati uko natumia mifano yenye kufaa, ile inasaidia wasikilizaji wako wasisikie tu mufano lakini pia wakuwe na wazo fulani mu akili yao juu ya mambo yenye unawafundisha. Ile mufano inasaidia wasikilizaji wako wakumbuke kweli za maana zenye kuwa mu Biblia. Yesu alikuwa fundi wa kutumia mifano yenye kufaa, na ndugu yake Yakobo alifuata mufano wake. Tuzungumuzie basi moja kati ya mifano ya Yakobo na tuone juu ya nini ni yenye kufaa sana.
17 Soma Yakobo 1:22-25. Mufano wa Yakobo wa kioo ni wenye kufaa juu ya sababu fulani. Alikuwa anafundisha kwa kutumia mufano fulani, ni kusema, jambo yenye inaweza kutusaidia kufaidika na Neno ya Mungu. Zaidi ya kusoma Biblia, tunapaswa pia kutumikisha mambo yenye tunasoma. Yakobo alichagula mufano wenye wasikilizaji wake wangeweza kuelewa haraka, ni kusema, mufano wa mutu mwenye kujiangalia kwenye kioo. Alipenda kufundisha somo gani? Inaweza kuwa ujinga kama mutu anajiangalia kwenye kioo na kuona kasoro fulani yenye anaweza kurekebisha, lakini hafanye jambo yoyote juu ya ile. Vilevile, inaweza kuwa ujinga kama tunasoma Neno ya Mungu na kuona jambo fulani yenye tunapaswa kufanyia mabadiliko kuhusu utu wetu, lakini hatufanye jambo yoyote juu ya ile
18 Wakati uko unatumia mufano, unaweza kuiga mufano wa Yakobo kwa kufanya hii mambo tatu: (1) Hakikisha kama mufano wako ni wenye kufaa kupatana na mambo yenye uko unazungumuzia. (2) Tumia mufano wenye musikilizaji wako anaweza kuelewa kwa wepesi. (3) Fasiria waziwazi somo ya ile mufano. Kama ni nguvu kwako kufikiria mifano yenye kufaa, ona Index des publications des Témoins de Jéhovah. Chini ya kichwa “Exemples,” utapata mifano mingi yenye unaweza kutumia. Kumbuka kama mikro inasaidiaka kupandisha sauti. Mifano nayo iko sawa vile micro. Inasaidia somo fulani yenye uko unafundisha ikuwe wazi. Kwa hiyo, hakikisha kama unatumia mufano wenye kufasiria wazo kubwa yenye unapenda kufundisha. Kusema kweli, kwetu jambo ya maana zaidi yenye inaweza kutusaidia kukomalisha ufundi wetu wa kufundisha haiko kukaza uangalifu juu yetu siye wenyewe, lakini ni kusaidia watu wengi, kadiri inawezekana, wakuwe mu familia ya Yehova yenye furaha.
TAREHE 23-29/10
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | YOBU 8-10
“Upendo Mushikamanifu wa Mungu Unatulinda ili Shetani Asitudanganye”
Tunaweza Kabisa Kumufurahisha Mungu?
Ayubu alipata magumu mengi, na ilionekana hakustahili kupata magumu hayo. Alianza kuwa na mawazo mabaya. Aliwaza kama Mungu hahangaike ikiwa iko na imani kwake ao hapana. (Ayubu 9:20-22) Ayubu alikuwa hakika kabisa kuwa yeye ni mwenye haki, na watu wengine waliona kuwa alikuwa anajitangaza kuwa mwenye haki kuliko Mungu.—Ayubu 32:1, 2; 35:1, 2.
Upendo Mushikamanifu wa Yehova Uko na Faida Gani Kwako?
14 Upendo mushikamanifu wa Mungu unatulinda kiroho Daudi alimuambia Yehova hivi mu sala: “Wewe ni mahali pangu pa kujificha; utanilinda nisipatwe na taabu. Utanizunguka kwa vigelegele vya shangwe ya ukombozi. . . . Mwenye kumutegemea Yehova amezungukwa na upendo wake mushikamanifu.” (Zb. 32:7, 10) Sawa vile zamani kuta zenye zilizunguka muji zilikuwa zinalinda wakaaji wake, vilevile matendo ya Yehova ya upendo mushikamanifu inatuzunguka sawa vile ukuta, ni kusema, inatulinda na mambo yote yenye inaweza kufanya tusiendelee kuwa waaminifu. Zaidi ya ile, upendo mushikamanifu wa Yehova, unamusukuma atuvute kwake.—Yer. 31:3.
Mali ya Kiroho
w10-SW 15/10 uku. 6-7 fu. 19-20
“Ni Nani Ameijua Akili ya Yehova?”
19 Tumejifunza nini kuhusu “akili ya Yehova”? Tunapaswa kuruhusu Neno la Mungu litufinyange ili tuelewe akili ya Yehova. Hatupaswi kamwe kumwekea Yehova mipaka yetu na kumhukumu kulingana na viwango na fikira zetu. Ayubu alisema hivi: “[Mungu] si mwanadamu kama mimi ndipo nimjibu, kwamba tuje pamoja katika hukumu.” (Ayu. 9:32) Kama Ayubu, tunapoanza kuelewa akili ya Yehova, tunachochewa kusema hivi: “Tazama! Hizo ndizo kingo za njia zake, nao ni mnong’ono ulioje wa jambo lililosikiwa juu yake! Lakini kuhusu mngurumo wake wenye nguvu ni nani anayeweza kuonyesha uelewaji?”—Ayu. 26:14.
20 Tunaposoma Maandiko, tunapaswa kufanya nini tunapopata sehemu fulani ambayo ni vigumu kuelewa, hasa inayohusu jinsi Yehova anavyofikiri? Ikiwa bado hatuelewi kabisa sehemu hiyo hata baada ya kufanya utafiti, tunaweza kuona hilo kuwa jaribu la kuonyesha kwamba tunamtegemea Yehova. Kumbuka kwamba nyakati nyingine, maneno fulani katika Biblia yanatupatia nafasi ya kuonyesha imani yetu katika sifa za Yehova. Acheni tukubali kwa unyenyekevu kwamba hatuelewi kila jambo analofanya. (Mhu. 11:5) Hivyo tutachochewa kukubaliana na maneno haya ya mtume Paulo: “Lo! Jinsi kilivyo kina cha utajiri wa Mungu na hekima na ujuzi! Jinsi hukumu zake zisivyochunguzika na njia zake zisivyotafutika! Kwa maana ‘ni nani amekuja kuijua akili ya Yehova, au ni nani amekuwa mshauri wake?’ Au, ‘Ni nani amempa yeye kwanza, hivi kwamba iwe lazima arudishiwe?’ Kwa sababu vitu vyote ni kutoka kwake na kwa yeye na kwa ajili yake. Kwake yeye na kuwe na utukufu milele. Amina.”—Rom. 11:33-36.
TAREHE 30/10–5/11
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | YOBU 11-12
“Njia Tatu za Kupata Hekima na Kufaidika Nayo”
w09-SW 15/4 uku. 6 fu. 17
Ayubu Alilitukuza Jina la Yehova
17 Ni nini kilichomsaidia Ayubu kudumisha utimilifu wake? Ni wazi kwamba kabla ya kupatwa na misiba hiyo, alikuwa tayari amesitawisha uhusiano wa karibu pamoja na Yehova. Ingawa hatuna uthibitisho wa kwamba alijua kwamba Shetani alikuwa ametoa mashtaka fulani kumhusu Yehova, Ayubu aliazimia kubaki mshikamanifu. Alisema hivi: “Mpaka nitakapokata pumzi, sitajiondolea utimilifu wangu!” (Ayu. 27:5) Ayubu alidumisha jinsi gani uhusiano huo wa karibu pamoja na Mungu? Bila shaka, alithamini yale aliyosikia kuhusu jinsi Mungu alivyoshughulika na Abrahamu, Isaka, na Yakobo, ambao walikuwa watu wake wa ukoo. Na kwa kuchunguza uumbaji, Ayubu angeweza kutambua sifa nyingi za Yehova.—Soma Ayubu 12:7-9, 13, 16.
Hauko Peke Yako Juu Sikuzote Yehova Iko na Weye
10 Ufanye urafiki pamoja na Wakristo waaminifu. Tafuta marafiki mu kutaniko wenye unaweza kujifunza mambo fulani kutoka kwao, ikuwe wanakupita miaka ao hapana, na hata kama wako na desturi tofauti na yako. Biblia inatukumbusha kama “wazee ndio wenye kuwa na hekima.” (Yob. 12:12) Lakini, watu wakubwa wanaweza pia kujifunza mambo mingi kwa vijana waaminifu. Hata kama Daudi alikuwa mudogo kwa Yonatani, ile haikuwazuia wasikuwe marafiki wa karibu sana. (1 Sa. 18:1) Daudi na Yonatani walisaidiana ili kumutumikia Yehova hata wakati walikuwa na magumu mingi. (1 Sa. 23:16-18) Irina, dada mumoja mwenye watu wa familia yake hawako Mashaidi wa Yehova, anasema hivi: “Ndugu na dada zetu wanaweza kabisa kufikia kuwa sawa vile wazazi wetu wa kiroho ao watu wa familia yetu. Yehova anaweza kuwatumikisha juu wakuwe familia yenye tuko nayo lazima.”
11 Haiko mwepesi kufanya urafiki na watu wengine zaidi sana kama uko mutu wa haya. Ratna, dada mumoja mwenye kuwa na haya mwenye alijifunza kweli ijapokuwa upinzani, anasema hivi: “Nilipaswa kukubali kama niko na lazima ya musaada wa ndugu na dada mu kutaniko.” Inaweza kuwa nguvu kuambia mutu mwengine namna uko unajisikia. Lakini wakati unafanya vile, ule mutu anaweza kufikia kuwa rafiki yako wa karibu. Marafiki wenye uko nao wanapenda kukutia moyo na kukutegemeza. Njo maana unapaswa kuwaambia vile unajisikia juu wajue namna wanaweza kukusaidia.
12 Moja kati ya njia ya muzuri zaidi ya kupata marafiki, ni kuhubiri nao. Carol, mwenye tulishataja, anasema hivi: “Nilipata marafiki wazuri sana saa nilipitisha wakati pamoja na dada mu mahubiri na mu mambo ingine ya kiroho. Yehova amenitegemeza kwa miaka mingi kupitia wale marafiki.” Kila mara inakuwaka muzuri sana wakati tunafanya urafiki na Wakristo waaminifu. Yehova anatumia wale marafiki juu ya kutusaidia tupiganishe mawazo yenye kutuhangaisha, sawa vile kujisikia kuwa peke yetu.—Mez. 17:17.
it-2-F uku. 850 fu. 7
Hekima
Hekima Kutoka kwa Mungu. Yehova Mungu njo mwenye iko na hekima kamilifu na yenye haina mipaka. Yeye “peke yake ni mwenye hekima” mu ile njia. (Ro 16:27; Ufu 7:12) Ujuzi ni kujua mambo fulani. Na juu Yehova njo Muumbaji mwenye iko “tangu milele mupaka milele” (Zb 90:1, 2), anajua mambo yote kuhusu ulimwengu. Anajua mambo yenye kuifanyiza, mambo yenye kuwa ndani, na historia yake mupaka leo. Ni yeye njo alifanya sheria, mizunguko, na kanuni za asili zenye wanadamu wanategemea ili kufanya uchunguzi na kutengeneza vitu. Bila ile mambo hawangeweza kufanya kitu. (Yob 38:34-38; Zb 104:24; Mez 3:19; Yer 10:12, 13) Kwa hiyo, ni wazi kama kanuni zake za mwenendo ni za maana hata zaidi juu mutu aishi muzuri, akamate maamuzi ya muzuri, na akuwe na furaha mu maisha. (Kum 32:4-6; ona YEHOVA [Mungu wa kanuni za mwenendo].) Hakuna kitu yenye inapita uelewaji wake. (Isa 40:13, 14) Hata kama anaweza kuruhusu mambo yenye haipatane na kanuni zake za haki itokee na hata iendelee kwa wakati fulani, yeye njo wa kuamua namna wakati wenye kuja utakuwa na kuhakikisha kama unapatana na mapenzi yake. Na mambo yenye anasema, ‘hakika itafanikiwa.’—Isa 55:8-11; 46:9-11.
Mali ya Kiroho
w08-SW 1/8 uku. 11 fu. 5
Siri ya Furaha ya Familia Kuwasiliana na Vijana Wanaobalehe
▪ ‘Je, ninatambua hisia zinazochochea maneno yake?’ Andiko la Ayubu 12:11 linasema: “Je, sikio halipimi maneno kama kaakaa linavyoonja chakula?” Katika kipindi hiki kuliko wakati mwingine wowote, unahitaji ‘kupima’ kile ambacho mwana au binti yako anasema. Mara nyingi, vijana wanazungumzia mambo kana kwamba yanafanyika hivyo kila wakati. Kwa mfano, mwana au binti yako anaweza kusema, “Sikuzote wewe unanitendea kana kwamba mimi ni mtoto!” au “Hunisikilizi kamwe!” Badala ya kukazia maneno “sikuzote” na “kamwe,” tambua kwamba mtoto wako hayachukulii kwa uhalisi. Kwa mfano, maneno “Sikuzote wewe unanitendea kana kwamba mimi ni mtoto!” yanaweza kumaanisha “Ninahisi kwamba huniamini,” na maneno “Hunisikilizi kamwe!” huenda yakamaanisha “Ninataka kukuambia jinsi ninavyohisi kikweli.” Jaribu kutambua hisia zinazochochea maneno yake.