WIMBO 90
Tutiane Moyo
Maandishi
1. Kama tunatiana moyo
Kumutumikia Mungu,
Upendo unakuwa nguvu,
Tunakuwa na umoja.
Upendo wetu unafanya
Tuvumilie magumu.
Mu kutaniko ya Kikristo
Tunapata usalama.
2. Tunapendaka kusikia
Maneno yenye kujenga,
Yenye ndugu na dada zetu
Wanasema kwa upendo.
Kutumika pamoja nao
Kunafurahisha sana!
Tunatiana nguvu sana
Na tunasaidiana.
3. Sasa ile siku ya Mungu
Inakaribia sana,
Tusiache kukusanyika
Ili tukuwe tayari.
Tutatumikia Yehova
Milele na kwa umoja.
Basi, na tutiane moyo;
Tukuwe waaminifu.
(Ona pia Lu. 22:32; Mdo. 14:21, 22; Gal. 6:2; 1 Te. 5:14.)