WIMBO 105
“Mungu Ni Upendo”
Maandishi
1. Vile Mungu ni upendo,
Na siye tupendane.
Tukipenda majirani
Tutawasaidia.
Kama hatuna upendo
Tuko watu wa bure.
Tupendane kama Kristo.
Upendo haushindwe.
2. Tupendane kwa matendo,
Hapana tu maneno.
Na hata tukikosea
Tusivunjike moyo.
Upendo hauna wivu
Na unavumilia.
Tupende ndugu na dada
Ili tubarikiwe.
3. Upendo wetu ukuwe
Wa kutoka mu moyo.
Tutumainie Mungu
Ili atuongoze.
Basi tumupende sana,
Tupende na jirani.
Hakuna mambo ingine
zaidi ya upendo.
(Ona pia Mk. 12:30, 31; 1 Ko. 12:31–13:8; 1 Yoh. 3:23.)