HABAKUKI
1 Tangazo lenye nabii Habakuki* alipokea katika maono:
2 Ee Yehova, nililie musaada mupaka wakati gani, lakini wewe hausikie?+
Nitakuomba musaada kwa sababu ya jeuri mupaka wakati gani, lakini wewe hauingilie kati?*+
3 Sababu gani unanifanya nione matendo mabaya?
Na sababu gani unaachilia ukandamizaji?
Sababu gani uharibifu na jeuri viko mbele yangu?
Na sababu gani ugomvi na vita vinaongezeka?
4 Sheria haitumike,
Na haki haifuatwe hata kidogo.
Kwa sababu muovu amemuzunguka mwenye haki;
Ndiyo sababu haki imepotoshwa.+
5 “Muangalie kati ya mataifa, na mukaze uangalifu!
Mushangae na kustaajabu;
Kwa maana jambo fulani litatokea katika siku zenu
Lenye hata mukiambiwa hamutaliamini.+
6 Kwa maana, angalia, ninasimamisha Wakaldayo,+
Taifa lenye halina huruma na lenye kutenda haraka bila kufikiri,
Wanaenda haraka katika maeneo mengi ya dunia
Ili kunyanganya makao yenye hayako yao.+
7 Ni wenye kutisha na wenye kuogopesha.
Wanajiwekea haki na mamlaka* yao wenyewe.+
Farasi wao wa vita wanakimbia kuenda mbele;
Farasi wao wanatoka mbali.
Wanashuka mbio sana kama tai mwenye kuenda kula.+
9 Wote wanakuja kutenda jeuri.+
Wakati nyuso zao zinakusanywa, ni kama upepo wa mashariki,+
Na wanakusanya watu wenye walikamatwa mateka kama muchanga.
Wanachekelea kila mahali kwenye ngome;+
Wanarundika udongo na kukamata mateka mahali pale.
12 Je, wewe hauko wa tangu milele, Ee Yehova?+
Ee Mungu wangu, Mutakatifu wangu, wewe hauwezi kufa.*+
Lakini sababu gani unavumilia wadanganyifu+
Na kunyamaza wakati muovu anameza mutu mwenye haki kuliko yeye?+
14 Sababu gani unafanya mwanadamu kuwa kama samaki wa bahari,
Kama viumbe vyenye kutambaa vyenye havina mutawala?
15 Yeye* ameinua hao wote kwa ndoano.
Anawakamata kwa wavu wake wa* kukokotwa,
Na anawakusanya katika wavu wake wa kuvua samaki.
Ndiyo sababu anashangilia sana.+
16 Ndiyo sababu anatolea wavu wake wa* kukokotwa zabihu
Na anatolea wavu wake wa kuvua samaki zabihu;*
Kwa maana kupitia hizo fungu lake ni kubwa,*
Na chakula chake ni kizuri.
17 Je, ataendelea kuondoa vyote vyenye kuwa katika wavu wake wa* kukokotwa?*
Je, ataendelea kuchinja mataifa bila huruma?+
Nitaendelea kuwa macho ili nione atasema nini kupitia mimi
Na jambo lenye nitajibu wakati nitakaripiwa.
2 Kisha Yehova akanijibu:
“Andika maono haya, na uyaandike waziwazi kwenye mabamba,+
3 Kwa maana maono haya ni ya wakati wenye uliwekwa,
Na yanaenda haraka kufikia mwisho* wake, hayatasema uongo.
Hata yakikawia,* endelea kuyangojea!*+
Kwa maana hayatakosa kutimia.
Hayatachelewa!
Lakini mwenye haki ataishi kwa uaminifu wake.*+
5 Kwa kweli, kwa sababu divai ni yenye udanganyifu,
Mutu mwenye kiburi hatafikia muradi wake.
Anaendelea kukusanya mataifa yote
Na kujikusanyia vikundi vyote vya watu.+
6 Je, hao wote hawatasema mezali, fumbo, na vitendawili juu yake?+
Watasema:
‘Ole wake mutu mwenye kujirundikia vitu vyenye haviko vyake
—Mupaka wakati gani?—
Na mwenye kuongeza deni lake mwenyewe!
7 Je, watu wenye walikukopesha hawatakuja bila kutazamia?
Wataamuka na kukutikisa kwa jeuri,
Na utakuwa kwao kitu chenye wao watanyanganya.+
8 Kwa sababu ulinyanganya vitu vya mataifa mengi,
Watu wote wenye kubakia wa vikundi vya watu watanyanganya vitu vyako,+
Kwa sababu ulimwanga damu ya wanadamu
Na kwa sababu ya jeuri yenye ulitendea dunia,
Miji na wakaaji wake.+
9 Ole wake mutu mwenye kutafutia nyumba yake faida ya uovu,
Ili kujenga chicha yake* katika nafasi ya juu,
Kusudi aepuke kushikwa na musiba!
10 Umeletea familia yako haya kwa sababu ya mipango yako,
11 Kwa maana jiwe litalilia kwenye ukuta,
Na kipande cha muti chenye kuwa juu ya nyumba kitalijibu.
12 Ole wake mutu mwenye kujenga muji kupitia umwangaji wa damu,
Na mwenye kujenga muji kupitia ukosefu wa haki!
13 Angalia! Je, haiko Yehova wa majeshi ndiye anaagiza kwamba vikundi vya watu vifanye kazi ya nguvu yenye itakulisha moto,
Na kwamba mataifa yajichokeshe bure?+
15 Ole wake mutu mwenye kupatia wenzake kinywaji,
Mwenye kuongeza kwenye kinywaji hicho kasirani kali na hasira, ili kuwalewesha,
Kusudi aangalie uchi wao!
16 Utajaa haya pa nafasi ya utukufu.
Wewe pia—kunywa na ufunue hali yako ya kukosa kutahiriwa.*
Kikombe chenye kuwa katika mukono wa kuume wa Yehova kitakufikia,+
Na haya itafunika utukufu wako;
17 Kwa sababu jeuri yenye ulitendea Lebanoni itakufunika,
Na uharibifu wenye uliogopesha sana wanyama utakuja juu yako,
Kwa sababu ulimwanga damu ya wanadamu
Na kwa sababu ya jeuri yenye ulitendea dunia,
Miji na wakaaji wake.+
18 Sanamu ya kuchongwa iko na faida gani
Wakati mwenye aliifanya ameichonga?
Sanamu ya metali* na mwalimu wa uongo wako na faida gani,
Hata kama mwenye aliitengeneza anaitegemea,
Kwa kutengeneza miungu yenye haina mafaa yoyote na yenye haiwezi kusema?+
19 Ole wake mutu mwenye kuambia kipande cha muti: “Amuka!”
Ao mwenye kuambia jiwe lenye haliwezi kusema: “Amuka! Utufundishe”!
20 Lakini Yehova iko* katika hekalu lake takatifu.+
Kaa kimya mbele yake, dunia yote!’”+
3 Sala ya nabii Habakuki, katika nyimbo za huzuni:*
2 Ee Yehova, nimesikia habari juu yako.
Nimeogopa matendo yako, Ee Yehova.
Uyafanye tena katikati ya miaka!*
Uyafanye yajulikane katikati ya miaka.*
Ukumbuke kuonyesha rehema wakati wa muvurugo.+
Utukufu wake ulifunika mbingu;+
Na dunia ilijaa sifa yake.
4 Kungaa kwake kulikuwa kama vile mwangaza.+
Miali mbili ilitoka kwenye mukono wake,
Kwenye nguvu yake ilifichwa.
6 Alisimama wima na kutikisa dunia.+
Aliangalia, na jambo hilo lilifanya mataifa yaruke.+
Milima ya milele ilivunjwa-vunjwa,
Na vilima vya zamani viliinama.+
Njia zake ni za tangu zamani sana.
7 Niliona taabu katika mahema ya Kushani.
Vitambaa vya hema vya inchi ya Midiani vilitetemeka.+
8 Ee Yehova, je, ni juu ya mito,
Je, kasirani yako imewaka juu ya mito?
Ao je, kasirani yako kali iko juu ya bahari?+
9 Upinde wako haufunikwe na uko tayari.
Fimbo zako zimewekwa* kwa kiapo.* (Sela)
Unapasua dunia kwa mito.
10 Milima ilisumbuka katika maumivu wakati ilikuona.+
Mafuriko ya maji yalipita.
Mahali kwenye maji yenye kuenda chini sana kulinguruma.+
Kuliinua mikono yake juu.
11 Jua na mwezi vilisimama kwenye makao yake ya juu.+
Mishale yako ilienda mbio kama mwangaza.+
Mungao wa mukuki wako ulingaa sana.
12 Ulipita katikati ya dunia ukiwa mwenye kasirani kali.
Ukakanyanga* mataifa kwa hasira.
13 Ulitoka ili kuokoa watu wako, kuokoa mutiwa-mafuta wako.
Uliponda kiongozi wa* nyumba ya waovu.
Iliachwa wazi kuanzia kwenye musingi mupaka juu.* (Sela)
14 Ulitoboa kichwa cha wapiganaji-vita wake kwa silaha zake mwenyewe*
Wakati walinishambulia ili wanisambaze.
Walifurahia sana kumeza kwa uficho mutu mwenye kuteseka.
15 Ulipita katika bahari kwa farasi zako,
Ulipita katika mawimbi makubwa ya bahari.
Mifupa yangu ilianza kuoza;+
Miguu yangu chini ilikuwa inatetemeka.
Lakini ninangojea kimya-kimya siku ya taabu,+
Kwa sababu inakuja juu ya watu wenye kutushambulia.
17 Hata kama muti wa tini hautoe maua,
Na mizabibu ikose matunda;
Hata kama mizeituni haizae matunda,
Na mashamba* hayatoe chakula chochote;
Hata kama kundi linaweza kukosekana katika zizi,*
Na kusikuwe ngombe katika vibanda;
18 Lakini mimi, nitafurahi katika Yehova;
Nitashangilia katika Mungu wa wokovu wangu.+
19 Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova ndiye nguvu zangu;+
Atafanya miguu yangu ikuwe kama ile ya paa
Na atanifanya nikanyange mahali pa juu.+
Kwa kiongozi;
utaimbwa kwa vyombo vya kamba.
Pengine jina hili linamaanisha “Kumbatio Changamufu.”
Ao “hauokoe.”
Ao “heshima.”
Ao pengine, “nguvu zao ni mungu wao.”
Ao pengine, “sisi hatutakufa.”
Ao “ili uwakaripie.”
Ni kusema, adui Mukaldayo.
Ao “makila yake ya.”
Ao “makila yake ya.”
Ao “anachoma zabihu ili zitoe moshi kwa ajili ya wavu wake wa kuvua samaki.”
Tnn., “limetiwa mafuta muzuri.”
Ao “makila yake ya.”
Ao pengine, “Je, ataendelea kuchomoa upanga wake?”
Ao “bila kusita-sita.”
Ao “utimizo.”
Ao “Kama inaonekana kwamba yanakawia.”
Ao “kuyangojea kwa hamu!”
Ao “Angalia! Nafsi yake imevimba.”
Ao pengine, “imani yake.”
Ao “nafsi yake.”
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
Ao “Eko.”
Ao “nyumba yake; kiota chake.”
Ao “umetendea nafsi yako.”
Ao pengine, “na uyumbe-yumbe.”
Ao “sanamu ya kuyeyushwa.”
Ao “eko.”
Ao “nyimbo za maombolezo.”
Ao pengine, “wakati wetu!”
Ao pengine, “wakati wetu.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “yalikuwa wokovu.”
Ao pengine, “Mishale yako imewekwa.”
Ao pengine, “Viapo vya makabila vimesemwa.”
Ao “Ukapiga.”
Tnn., “kichwa cha.”
Tnn., “kwenye shingo.”
Tnn., “fimbo zake.”
Tnn., “na tumbo langu likatetemeka.”
Ao “matuta.”
Zizi ni lupango ya kuchungia wanyama.