Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Maandamano Ya Kupinga Serikali Yanasaidia Kumaliza Magumu Ya Wanadamu?
    Amuka!—2013 | Mwezi wa 7
    • [Picha katika ukurasa wa 6]

      KICHWA

      Maandamano Ya Kupinga Serikali Yanasaidia Kumaliza Magumu Ya Wanadamu?

      Mashahidi wa Yehova, wachapishaji wa gazeti hili, hawajiingize katika mambo ya siasa. (Yohana 17:16; 18:36) Kwa hiyo, ijapokuwa habari inayofuata inazungumuzia zaidi sana mifano ya muvurugo wa kiraia, haitukuze taifa moja juu ya taifa lingine na haiunge mukono upande wowote wa siasa.

      TAREHE 17 Mwezi wa 12, 2010, Mohamed Bouazizi alifikia mwisho wa uvumilivu wake. Kijana huyo wa miaka 26 aliyekuwa anauzisha vitu kwenye barabara huko Tunisia, alikuwa amevunjika moyo kwa sababu hakuweza kupata kazi nzuri. Pia alijua matendo mabaya ya wenye mamlaka ya kuomba rushwa. Asubuhi moja, wakuu wa polisi walimunyanganya biashara yake ya matunda kama vile ndizi na matunda mengine. Walipochukua mizani ao vipimo vyake, alikataa; na watu fulani walioona tukio hilo wanasema kwamba polisi mumoja mwanamuke alimupiga kofi.

      Kwa sababu alijisikia kuwa amezarauliwa, Mohamed alikasirika sana na hivyo akaenda kwenye biro ya serikali iliyokuwa karibu ili kutoa malalamiko yake lakini hakuna mutu aliyemusikiliza huko. Akiwa mbele ya jengo hilo la serikali, alisema kwa sauti kubwa hivi: “Munataka nifanye nini ili niishi?” Kisha kujimwangia petroli, alijiwashia kibiriti. Alikufa kutokana na vidonda hivyo baada ya majuma matatu.

      Tendo lenye kuhuzunisha la Mohamed Bouazizi lilisikitisha sana watu wa inchi ya Tunisia na wa inchi zingine. Watu wengi wanaona kwamba matendo yake ndiyo yaliwasha moto wa muvurugo wa kiraia ambao ulisababisha kuanguka kwa utawala wa inchi ya Tunisia na maandamano ya kupinga serikali ambayo yalienea pia haraka katika inchi zingine za Kiarabu. Bunge ao baraza la wasimamizi wa Muungano wa Inchi za Ulaya lilimupatia Bouazizi na watu wengine ine Tuzo ao Zawadi ya Kutetea Uhuru wa Kusema iliyoitwa Sakharov ya 2011, na gazeti fulani la Londres (The Times) lilimuita Bouazizi kuwa mutu aliyejulikana sana wa mwaka wa 2011.

      Kama mufano huo unavyoonyesha, maandamano ya kupinga serikali yanaweza kuchochea kabisa kuwe na mabadiliko. Lakini ni nini kinafanya kuwe na ongezeko kubwa la maandamano ulimwenguni siku hizi? Na je, kuna njia nyingine yoyote ya kumaliza matatizo ya wanadamu?

      Sababu Gani Kumekuwa Ongezeko Kubwa la Maandamano ya Kupinga Serikali?

      Maandamano mengi ya kupinga serikali yanasababishwa na mambo yanayofuata:

      • Kukosa kutosheka na nanma serikali inavyoendesha mambo. Watu wakiona kwamba uchumi na serikali ya inchi yao vinawatimizia mahitaji yao, hawawezi kuwa na nia ya kufanya maandamano ya kupinga serikali yao, watu wanatumika kwa bidii pamoja na serikali ili kutatua magumu yao. Lakini, watu wakiona kwamba serikali yao inajaa uovu na mambo ya rushwa, na haitende kwa haki, na inafaidisha watu wachache tu, watu wako tayari kufanya maandamano ya kupinga serikali hiyo.

      • Jambo linalochochea maandamano. Mara nyingi, tukio fulani linachochea watu kutenda, kukosa kuwa watiifu kwa serikali na kuamini kwamba wanapaswa kufanya kitu fulani ili mambo yabadilike. Kwa mufano, tendo la Mohamed Bouazizi lilichochea maandamano makubwa ya kiraia ya kupinga serikali huko Tunisia. Katika inchi ya India, watu walikataa kula chakula ili kupinga mambo ya rushwa wakichochewa na Anna Hazare, ambaye ni muteteaji wa mabadiliko. Watu wengi waliunga mukono jambo hilo katika miji na majiji 450.

      Kama vile Biblia ilivyosema zamani sana, tunaishi katika “ulimwengu ambamo watu fulani wana mamlaka na wengine wanateseka chini ya mamlaka yao.” (Mhubiri 8:9, Good News Translation) Rushwa na ukosefu wa haki vimeenea sana leo kuliko ilivyokuwa zamani. Kwa kweli, kuliko wakati mwengine wowote, leo watu wanatambua zaidi namna mipango ya kisiasa na kiuchumi ulimwenguni imeshindwa kuwatimizia mambo ambayo walitazamia. Simu ao telefone za hali ya juu sana, Internete, habari za ulimwengu zinazotangazwa usiku na muchana kwenye vyombo vya habari, zinafanya sasa matukio ambayo yanatendeka hata katika sehemu za mbali za mashambani yachochee watu kufanya maandamano katika sehemu nyingi zaidi za ulimwengu.

      Maandamano ya kupinga serikali yametimiza mambo gani?

      Watu wanaounga mukono muvurugo wa kiraia wanadai kwamba maandamano hayo yalitimiza mambo yanayofuata:

      • Yalileta kitulizo kwa watu masikini. Maandamano ya fujo na uharibifu wa mali za watu yalifanywa ili kupinga kupanda kwa garama za kulipia nyumba katika muji wa Chicago, Illinois, huko Amerika wakati wa Matatizo Makubwa ya Feza Ulimwenguni kati ya mwaka wa 1930 na 1940. Kwa sababu ya maandamano hayo, wenye mamlaka wa muji huo walisimamisha mupango huo wa kufukuza watu mahali walipoishi na wakafanya mupango wa kuwapatia kazi watu fulani kati ya wale waliofanya maandamano. Maandamano kama hayo katika muji wa New York City yaliwezesha familia 77 000 ambazo zilikuwa zimefukuzwa zirudishwe tena katika nyumba zao.

      • Yalirekebisha ukosefu wa haki. Mwishowe, katika miaka ya 1955/1956, waendeshaji wa mabisi ya kubeba watu walipokataa kufanya kazi katika muji wa Montgomery, Alabama, Amerika, hilo lilifanya sheria za ubaguzi wa rangi ndani ya mabisi kuhusu viti vya kukalia ziondolewe.

      • Yalisimamisha mipango ya ujenzi. Mwezi wa 12, 2011, makumi ya maelfu ya watu waliandamana ili kupinga ujenzi wa kiwanda cha kutoa moto wa umeme kutokana na makaa ya mawe karibu na Hong Kong kwa kuogopa uchafuzi wa hewa, hivyo mupango huo ulisimamishwa.

      [Picha katika ukurasa wa 7]

      Hata ikiwa watu fulani wanaoandamana wanaweza kupata mambo ambayo wanataka, Ufalme wa Mungu ndio utamaliza kabisa magumu ya wanadamu

      Bila shaka, watu wenye kufanya maandamano hawapate sikuzote mambo wanayotaka. Kwa mufano, viongozi wanaweza kuamua kuazibu watu wanaoandamana kuliko kuwapatia mambo wanayoomba. Hivi karibuni, raisi wa inchi moja ya Mashariki ya Kati alisema hivi kuhusu watu waliokuwa wakiandamana: “Maandamano hayo yanapaswa kuvunjwa-vunjwa kwa fimbo ya chuma,” na maelfu ya watu walikufa katika muvurugo huo.

      Hata wakati watu wanaoandamana wanapata kitu ambacho wanataka, mambo yanayofuata baada ya maandamano yanaleta matatizo mengine. Mwanaume mumoja aliyesaidia kupindua kiongozi wa inchi moja ya Afrika aliliambia hivi gazeti moja (Time) kuhusu utawala mupya: “Ilikuwa ndoto kwa sababu kisha tu kupinduliwa kwa serikali hiyo inchi iliingia katika muvurugo mukubwa.”

      Kuna njia nyingine iliyo nzuri zaidi ya kumaliza matatizo ya wanadamu?

      Watu wengi wenye kujulikana sana wanaamini kwamba wanadamu wana daraka la kupinga serikali zenye kukandamiza watu. Kwa mufano, Václav Havel, raisi wa zamani wa inchi ya Cheki ambaye amekwisha kufa na aliyepitisha miaka mingi katika kifungo kwa sababu ya kutetea haki za wanadamu, aliandika hivi katika mwaka wa 1985: “[Mupinzani] hana kitu kingine cha kutoa isipokuwa tu uzima wake, anatoa uzima wake kwa sababu hana njia nyingine ya kusadikisha watu mambo ya kweli ambayo anatetea.”

      Maneno ya Havel yalionyesha mbele ya wakati matendo yenye kuhuzunisha ya Mohamed Bouazizi na wengine. Katika inchi moja ya Asia, watu 12 walijiua kwa kujichoma kwa moto hivi karibuni ili kupinga kuonewa na wanadini na wanasiasa. Akieleza sababu gani walifanya matendo makali kama hayo, mwanaume fulani aliliambia gazeti moja (Newsweek) hivi: “Hatuna bunduki. Hatutaki kuwaumiza wanadamu wengine. Tunaweza kufanya jambo gani lingine?”

      Biblia inaonyesha namna Mungu atamaliza ukosefu wa haki, rushwa, na matendo ya kuonea wengine. Inazungumuza juu ya serikali ambayo Mungu amesimamisha huko mbinguni ili kuchukua mahali pa serikali za kisiasa na mipango ya kiuchumi ambayo imeshindwa kumaliza magumu ya wanadamu na hivyo kuwafanya waandamane ili kupinga mipango hiyo. Unabii mumoja unaohusu Mutawala wa serikali hiyo ya Mungu unasema hivi: ‘Kwa maana atamukomboa masikini anayelilia musaada, pia mwenye kuteseka na yeyote ambaye hana musaidizi. Ataikomboa nafsi yao kutoka katika ukandamizaji na katika jeuri.’​—Zaburi 72:12, 14.

      Mashahidi wa Yehova wanaamini kwamba Ufalme wa Mungu ndilo tumaini pekee la kweli la kuletea wanadamu amani duniani. (Mathayo 6:9, 10) Kwa hiyo, Mashahidi wa Yehova hawafanye maandamano ili kupinga serikali. Je, wazo la kwamba serikali ya Mungu itaondoa mambo yanayowachochea watu wafanye maandamano ya kupinga serikali ni wazo lisilowezekana? Linaweza kuonekana kuwa wazo lisilowezekana. Hata hivyo, watu wengi wamesadiki kabisa kwamba utawala wa Mungu utamaliza matatizo ya wanadamu. Unaweza kuchunguza wewe mwenyewe ikiwa jambo hilo ni la kweli.

  • Niliona Ukosefu wa Haki Kila Mahali Nilipoangalia
    Amuka!—2013 | Mwezi wa 7
    • Niliona Ukosefu wa Haki Kila Mahali Nilipoangalia

      Patrick O’Kane anaeleza maisha yake

      [Picha katika ukurasa wa 8]

      NILIZALIWA mwaka wa 1965 katika familia masikini huko Kaskazini mwa Irelandi. Nilikomalia katika muji wa County Derry wakati wa “Misukosuko,” ni kusema, mapigano makali yaliyokuwa kati ya Wakatoliki na Waprotestanti ambayo yalidumu miaka zaidi ya 30. Wakatoliki ambao walikuwa wachache walijisikia kuwa wanabaguliwa na Waprotestanti ambao ndio ilikuwa dini kubwa. Wakatoliki waliwashitaki Waprotestanti kuwa wanafanya matendo ya ukosefu wa haki kuhusiana na uchaguzi, uongozi, kazi, na makao.

      Kila mahali nilipoangalia, niliona ukosefu wa haki na kutotendea watu kwa usawa. Mara nyingi nilipigwa, nilisukumwa ndani ya motokari ya polisi nikiwa mwenye kuelekezwa bunduki, na niliulizwa maulizo na kupekuliwa-pekuliwa na polisi ao waaskari. Nilijisikia kuwa ninateswa sana na nikafikiri, ‘Ninaweza kukubali matendo haya, ao kuyapinga kabisa!’

      Nilishiriki katika maandamano ambamo watu wengi waliuawa katika mwaka wa 1972. Maandamano hayo yalifanywa ili kukumbuka watu 14 ambao walikufa kwa kupigwa risasi na waaskari wa Uingereza. Nilishiriki pia katika maandamano ya kukataa kula chakula yaliyofanywa ili kukumbuka wafungwa waliokataa kula chakula mupaka wakakufa mwaka wa 1981 kwa sababu ya kupinga utawala wa Uingereza. Nilipandisha bendera za inchi ya Irelandi ambazo zilikatazwa na niliandika mahali popote kwenye kuta maneno yenye kupinga utawala wa Uingereza. Kila siku ilionekana kulikuwa na Mukatoliki aliyeuawa na iliomba kupinga uuaji huo. Jambo ambalo lilianza kama maandamano ya watu wachache tu, mara nyingi lilifikia kuwa muvurugo mukubwa wa uharibifu wa mali za watu.

      Nilipokuwa kwenye masomo ya juu, nilijiunga katika maandamano ya wanafunzi ya kupinga uharibifu wa mazingira. Kisha, nilihamia huko Londres, na nikiwa huko nilishiriki katika maandamano ya Wasoshalisti ya kupinga namna serikali ilivyokuwa ikiendesha mambo, namna ambayo ilionekana kuwa inafaidi watu wa hali ya juu tu na kuwakandamiza watu masikini. Nilijiunga na wafanyakazi wakati waliamua kuacha kufanya kazi kwa sababu ya kupunguzwa kwa mushahara wao, na katika mwaka wa 1990 nilishiriki katika maandamano ya kupinga kulipa kodi iliyoombwa ili kuwa na haki ya kushiriki katika uchaguzi. Maandamano hayo yalitokeza uharibifu mukubwa sana wa uwanja wa watu wote unaoitwa Trafalgar Square.

      Hata hivyo, mwishowe nilivunjika moyo. Kuliko kutimiza miradi yetu, mara nyingi maandamano yalifanya chuki iongezeke zaidi.

      Hata kama wana nia nzuri, wanadamu hawawezi kuleta haki na kufanya watu wote watendewe kwa usawa

      Ni wakati huo nilikutana na rafiki mumoja aliyenifanya nijuane na Mashahidi wa Yehova. Walinifundisha kupitia Biblia kwamba Mungu anahangaika juu ya mateso yetu na kwamba ataondoa mambo yote mabaya ambayo yamefanywa na wanadamu. (Isaya 65:17; Ufunuo 21:3, 4) Hata kama wana nia nzuri, wanadamu hawawezi kuleta haki na kufanya watu wote watendewe kwa usawa. Tunahitaji muongozo wa Mungu na pia nguvu zake ili kushinda uvutano wa mashetani ambao unatokeza matatizo mengi katika ulimwengu.​—Yeremia 10:23; Waefeso 6:12.

      Sasa ninaelewa kwamba bidii niliyofanya ili kupinga ukosefu wa haki ilikuwa kama kupiga hewa tu. Nimetulizwa sana kujua kwamba wakati utakuja ambapo ukosefu wa haki hautakuwa tena duniani, na wakati huo watu wote watatendewa kwa usawa kabisa.

      Biblia inafundisha kwamba Yehova Mungu ni ‘mupenda-haki.’ (Zaburi 37:28) Hiyo ni sababu moja inayoweza kutufanya tuwe na uhakika wa kwamba Mungu ataleta haki katika njia ambayo serikali za wanadamu haziwezi kufanya. (Danieli 2:44) Ikiwa unataka kujua mengi zaidi, zungumuza na Mashahidi wa Yehova wa eneo lenu ao ufungue adresi yetu ya Internete, www.jw.org.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine