Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g 9/13 uku. 14-15
  • Zheng He

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Zheng He
  • Amuka!—2013
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MAMLAKA, BIASHARA, NA USHURU
  • Habari Zilizo Ndani
    Amuka!—2013
Amuka!—2013
g 9/13 uku. 14-15

MAMBO TUNAYOJIFUNZA KUTOKANA NA HISTORIA

Zheng He

“Tumesafiri umbali wa zaidi ya lia 100 000 juu ya maji mengi sana na tumeona mawimbi makubwa yaliyo kama milima yakiinuka juu sana na tuliona kwa mbali maeneo ya washenzi . . . wakati matanga ya mashua zetu yalijifungua kama vile mawingu ya usiku na muchana yanavyoendelea kutembea (haraka kama vile) mushale, tulipita mawimbi hayo makali kana kwamba tulikuwa wenye kusafiri katika barabara kubwa.”​—Maandishi ya kati ya mwaka wa 1401 na 1500 katika muji wa Changle, Jimbo la Fujian, huko China, yanayosemwa kuwa yaliandikwa na Zheng He.

CHINA ni inchi ya mambo makubwa. Inchi hiyo ina wakaaji wengi sana na ni moja kati ya inchi kubwa zaidi za dunia. Wakaaji wa inchi hiyo walijenga Ukuta Mukubwa, ukuta huo ni moja kati ya majengo makubwa zaidi katika historia ya wanadamu. Kikundi cha mashua kubwa zilizotengenezwa na Watawala wa China wa ukoo wa kifalme wa Ming, Yongle na Xuande, kilikuwa kikubwa sana kuliko kikundi kingine chochote cha mashua ambacho kilitengenezwa katika kipindi cha miaka 500 iliyofuata. Kiongozi wa kikundi hicho cha wanamaji alikuwa Mwislamu mumoja wa kusini-mangaribi mwa China anayeitwa Zheng He.

MAMLAKA, BIASHARA, NA USHURU

Kulingana na maandishi yaliyotajwa kwa sehemu mwanzoni mwa habari hii, kusudi la safari za Zheng He lilikuwa “kuwatendea watu wa mbali sana kwa wema na kuonyesha kwamba wale ambao wangejitiisha kwa utawala wa ukoo wa kifalme wa Ming wangekuwa na maisha mazuri.” Kulingana na maandishi hayo, matokeo ya safari hizo ni kwamba, “inchi za mbali sana na inchi za mwisho wa dunia zote zimejitiisha chini [ya inchi ya China] . . . Washenzi kutoka ngambo ya bahari . . . wamekuja [kwenye uwanja wa mutawala] wakileta vitu vya maana sana na zawadi.”

Watu wamebishana sana juu ya kusudi lililowachochea watawala wa ukoo wa kifalme wa Ming kufanya safari hizo. Watu fulani wanamuona Zheng He kuwa balozi ao ambasadere aliyependa mambo ya asili na aliyekuwa na nia nzuri, ambaye alitaka taifa lake liwe lenye nguvu lakini lenye kufanya amani. Wengine wanaona kwamba kusudi lake la kufanya safari hizo lilikuwa kushambulia mataifa mengine kwa njia ya kisiasa ili kuyatawala. Kwa kweli, Zheng He alitoa zawadi nzuri sana na aliwasaidia kwa njia ya kisiasa watawala ambao walimukaribisha, lakini wale ambao walikataa kumutii kabisa na kutoa ushuru kwa mutawala Ming, aliwaondoa kwenye mamlaka watawala hao na akawafanya kuwa wafungwa. Matokeo ya safari hizo kubwa sana za Zheng He ni kwamba watawala wengi kutoka maeneo ya Bahari ya Hindi walituma mabalozi huko China ili kumutolea heshima mutawala Ming.

Hata iwe kusudi la safari hizo lilikuwa gani, mashua za Ming zilibeba vitu kama vile vanishi, kauri (udongo mweupe unaongaa ambao unatumiwa kutengeneza vyombo vya udongo), na hariri (nyuzi laini na nyembamba), vitu hivyo vilitengenezwa na mafundi wa hali ya juu wa Ming ili kufanya biashara katika bandari za mbali. Mashua hizo zilirudi zikiwa na vitu vya maana sana, pembe za tembo, vikolezo, mbao za kitropiki, na vitu vingine vya starehe vinavyopendwa na Wachina. Mashua hizo zilileta hata munyama mwenye shingo ndefu anayeitwa twiga, ambaye inasemekana kwamba alisababisha musisimuko mukubwa katika inchi ya China. Kupitia kubadilishana vitu na mawazo, watu wa inchi zingine walionyeshwa mbele ya wakati maendeleo yenye kuvutia ya inchi ya China katika miaka kati ya 1401 na 1500.

Safari hizo kubwa sana hazikuendelea. Kisha tu makumi ya miaka kisha safari za Zheng He, inchi ya China iliacha kufanya biashara na pia mahusiano na inchi zingine. Kwa kuwa aliona kwamba inchi ya China haina lazima ya kuendelea kuwa na mahusiano na inchi zingine, mutawala mupya pamoja na washauri wake ambao walikuwa na mawazo ya Conficius walijaribu kuzuia uvutano wa inchi zingine usiingie katika inchi ya China. Waliachana kabisa na vitu vyote vya maana sana ambavyo mashua hizo zilileta, inaonekana waliharibu maandishi yote ya safari hizo kubwa sana na hata waliharibu mashua zenyewe. Ni katika miaka ya hivi karibuni tu ndipo watu wa inchi ya China na wa inchi zingine walijua kuhusu wakati huo wa pekee ambapo kikundi kikubwa cha mashua za Zheng He kilifanya safari katika bahari mbalimbali.

[Maelezo ya chini]

a Li ni kipimo cha Wachina, urefu wake ulitofautiana kwa muda wa mamia ya miaka. Watu wanafikiri kwamba wakati wa Zheng He, li moja ilikuwa karibu nusu ya kilometa.

MAELEZO MAFUPI

  • Kikundi cha mashua zinazoitwa kwa jina la Ming kilichoongozwa na Zheng He kilifanya safari saba kubwa kati ya mwaka wa 1405 na 1433.

  • Labda kikundi hicho kilikuwa na mashua 200 ao zaidi, ni kusema, mashua za vita, mashua za chakula, mashua zenye matangi ya maji, mashua zilizobeba farasi, na kazalika. Mashua hizo zilikuwa zinabeba wanamaji zaidi ya 27 000, wakubwa wa serikali, maaskari-jeshi, wafanyabiashara, wafanyakazi wa kutunza mashua hizo na watu wengine.

  • Kufikia Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, hakuna taifa lingine ambalo lilikuwa na kikundi cha mashua kama kile cha Zheng He. Mashua hizo zilienda kwenye bandari (port) za Mashariki ya Mbali na Bahari ya Hindi, zilifikia mbali sana mupaka Afrika ya Mashariki.

  • Watu watatu kati ya watu waliokuwa chini ya uongozi wa Zheng He waliandika kila mumoja habari ambazo walijionea wao wenyewe; habari hizo zinatujulisha mambo mengi kuhusu safari za Zheng He.

Mashua za Zheng He Zilizobeba Vitu vya Maana​—Zilikuwa Kubwa Kadiri Gani na Zilikuwa Ngapi?

Maandishi ya kihistoria ya ukoo wa kifalme wa Ming yanasema kwamba Mashua za Zheng He zilizobeba vitu vya maana zilikuwa kubwa sana, ni kusema, zilikuwa na urefu wa meta 136 na upana wa meta 56. Watu wenye elimu hawana uhakika na vipimo hivyo na wanaona kwamba ni vigumu kuvihakikisha, kulingana nao, mashua zilizotengenezwa kwa mbao ambazo zina urefu wa meta zaidi ya 90 zinaweza kuvunjika kwa vyepesi.

Habari moja inasema hivi juu ya jambo hilo: “Ni wazi kwamba maelezo yote yanayotolewa kuhusu ukubwa wa mashua hizo ni habari tu zilizotiwa chumvi. Mashua iliyo na urefu wa meta 60-75 ni yenye kufaa zaidi kuliko mashua iliyo na urefu wa meta 135.” Kwa vyovyote vile, kati ya mwaka wa 1401 na 1500, mashua zilizokuwa na urefu wa meta 60 zilikuwa za pekee sana, na kati ya mashua za Zheng He kulikuwa mashua 62 zenye urefu huo!

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine