Inchi Na Watu | Brazili
Kutembelea Inchi ya Brazili
Chakula kitamu kinachoitwa feijoada, ni chakula cha asili cha watu wa Brazili
Ndege anayeitwa toucan
ZAMANI inchi ya Brazili ilikaliwa na wawindaji na walimaji. Wagunduzi wa inchi ya Ureno (Portugal) walileta dini ya Katoliki, na baadaye, makanisa mengi na makanisa madogo-madogo yalijengwa, mengine yalipambwa na sanamu za mbao zenye kufunikwa na zahabu.
Kuanzia mwaka wa 1550 mupaka mwaka wa 1850, mashua za kusafirisha watumwa zilibeba Waafrika milioni ine hivi Brazili ili kutumika katika mashamba. Watumwa hao walipeleka desturi zao, ambazo zilitokeza dini za Wabrazili zenye asili ya Afrika kama vile dini inayoitwa makumba na dini ya Candomblé. Pia, uvutano wa Waafrika unaonekana wazi katika muziki, dansi, na chakula cha Wabrazili.
Chakula cha asili kinachoitwa feijoada, ambacho kiliigwa kwa Wareno, ni muchuzi unaofanywa kwa kuchanganya nyama na maharagwe meusi, watu wanakula chakula hicho pamoja na wali na mboga za majani. Tangu mwaka wa 1801 na kuendelea, mamilioni ya watu walihama kutoka Japani, Ulaya (zaidi sana Ujerumani, Italia, Polandi, na Hispania), na sehemu zingine za dunia na wakaenda kuishi Brazili.
Leo, katika inchi yote ya Brazili kuna Mashahidi wa Yehova zaidi ya 750 000 walio katika makutaniko zaidi ya 11 000. Wanajifunza Biblia na watu zaidi ya 800 000. Ili kupata nafasi za kufanyia mikutano, vikundi 31 vya wajenzi wenye kusafiri katika inchi yote vinatumika pamoja na Mashahidi wa Yehova wa mahali hapo ili kujenga na kurekebisha Majumba ya Ufalme karibu 250 mupaka 300 kila mwaka. Tangu Mwezi wa 3, 2000, Majumba ya Ufalme 3 647 yamejengwa ao kurekebishwa.
Bonde la Muto Amazone ndilo lenye pori yenye kuwa na mvua nyingi zaidi duniani
JE, ULIJUA?
Muto Amazone unamwanga maji mengi zaidi katika bahari kuliko muto mwengine wowote na una urefu wa kilometa karibu 6400