Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g 6/14 uku. 10-11
  • Joseph Priestley

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Joseph Priestley
  • Amuka!—2014
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ANATAFUTA KWELI KATIKA SAYANSI
  • ANATAFUTA KWELI KATIKA DINI
  • Habari Zilizo Ndani
    Amuka!—2014
  • Alikuwa Baba Muzuri wa Familia, na Mwanaume Mwaminifu
    Tuige Imani Yao
  • “Mimi Niko Mahali pa Mungu?”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Aliilinda Familia Yake, Akawaandalia, na Akavumilia
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2014
g 6/14 uku. 10-11
Sanamu ya Joseph Priestley

MAMBO YENYE HISTORIA INATUFUNDISHA

Joseph Priestley

“Uwezo wake mbalimbali, bidii yake, mambo aliyofanya na kuwahangaikia watu; tamaa yake kubwa ya kutafuta kujua mambo kuhusu ulimwengu, mwenendo, ao watu; nafasi yake katika sayansi, teolojia, filozofia, na siasa ao politike; mambo aliyofanya katika Mapinduzi [ya Ufaransa], na habari yenye kuhuzunisha ya mateso aliyopata ambayo hakustahili, yanaweza kumufanya awe mutu wa maana sana katika kipindi cha kuanzia mwaka wa 1701 mupaka mwaka wa 1800.”—Mwanafilozofia Frederic Harrison.

JOSEPH PRIESTLEY alifanya mambo gani ya maana sana? Mambo aliyovumbua na kuandika yalibadili mawazo ya watu juu ya serikali, Mungu, na hewa tunayopumua.

Katika mambo aliyoandika juu ya sayansi na dini, Priestley alikataa mawazo na desturi za watu ili atetee kweli. Tuone alifanya hivyo namna gani.

ANATAFUTA KWELI KATIKA SAYANSI

Kisha kukutana na mwanasayansi Muamerika Benjamin Franklin katika mwaka wa 1765, Joseph Priestley, ambaye alikuwa ameanza kupitisha wakati mwingi katika mambo ya sayansi, alianza kufanya utafiti katika mambo ya umeme. Mwaka uliofuata, wanasayansi wenzake walishangazwa sana na mambo aliyovumbua na hivyo walimufanya kuwa mushiriki wa shirika linalojulikana sana la Royal Society of London.

Kisha, Priestley alianza kufanya utafiti katika elimu ya kemia (Chimie). Kwa muda muchache, alivumbua gaze nyingi, kama vile amonia na oksidi nitrasi (gaze inayowafanya watu wacheke). Na hata alichanganya maji na kaboni dioksidi, na hivyo akatengeneza maji yenye kuwa na kaboni.

Katika mwaka wa 1774, alipokuwa akifanya utafiti kusini mwa Uingereza, Priestley alivumbua gaze ya pekee inayofanya mishumaa iangaze sana. Kisha aliweka mililita 60 za gaze hiyo ndani ya kilauri pamoja na panya. Panya huyo hakukufa lakini aliendelea kuishi kama vile tu ambavyo angekuwa katika kilauri chenye kuwa na hewa ya kawaida. Priestley mwenyewe alipumua gaze hiyo, na alisema kuwa “baadaye ilikuwa vyepesi zaidi kupumua.”

Joseph Priestley alikuwa amevumbua oksijeni.a Lakini aliita gaze hiyo hewa inayofanya vitu viwake moto, alionyesha kwamba alikuwa amevumbua hewa ya kawaida ambayo haikuwa na flojistoni, ni kusema, kitu ambacho watu wanafikiri kinazuia vitu visiwake moto. Mawazo ya Priestley yalikuwa ya uongo, lakini watu wengi leo wanaona uvumbuzi huo kuwa “uvumbuzi mukubwa sana katika kazi alizofanya.”

ANATAFUTA KWELI KATIKA DINI

Priestley aliamini kwamba mawazo ambayo hayakuchunguzwa yalizuia watu kujua ukweli wa sayansi, kwa hiyo aliona kwamba desturi na mafundisho ambayo watu wanakubali bila kuchunguza yalificha ukweli wa dini. Inashangaza kwamba wakati wote aliotumia ili kutafuta kweli katika dini, Priestley alikubali mafundisho fulani ambayo yalipingana kabisa na Biblia. Kwa mufano, wakati fulani hakuamini kwamba Biblia iliongozwa na roho ya Mungu. Tena, alipinga fundisho la Biblia la kwamba Yesu aliishi mbinguni mbele ya kuja katika dunia.

“Ikiwa kusudi la sayansi ni kutafuta kweli, basi Priestley alikuwa mwanasayansi wa kweli.”—Mwanabiolojia Katherine Cullen

Kwa upande mwengine, Priestley alifunua waziwazi mafundisho ya uongo ya wakati huo, ambayo yanaendelea kukubaliwa leo na makanisa mengi makubwa. Aliandika kwamba mafundisho ya kweli ambayo Yesu na wafuasi wake walifundisha yaliharibishwa baadaye na mafundisho ambayo Biblia inapinga kabisa kama vile Utatu, kutokufa kwa nafsi, na kuabudu sanamu.

Mawazo ya Priestley juu ya dini na namna alivyounga mukono Mapinduzi ya Amerika na Ufaransa yalikasirisha washiriki wenzake wa Uingereza. Katika mwaka wa 1791, kikundi fulani cha watu kiliharibu nyumba yake na chumba chake cha kufanyia utafiti, na mwishowe Priestley alikimbilia Amerika. Hata kama watu wanamukumbuka zaidi sana kwa sababu alivumbua mambo mengi katika sayansi, Joseph Priestley aliamini kwamba kujifunza juu ya Mungu na kusudi Lake lilikuwa “jambo la maana sana.”

a Hapo mbele, mwanakemia wa Uswisi Carl Scheele alivumbua oksijeni, lakini alishindwa kutangaza uvumbuzi wake. Kisha, mwanakemia Mufaransa Antoine-Laurent Lavoisier ndiye aliipatia gaze hiyo jina la oksijeni.

MAELEZO MAFUPI

  • Joseph Priestley alizaliwa katika mwaka wa 1733 karibu na muji wa Leeds, katika Uingereza..

  • Katika mambo ya sayansi, inasemekana ni yeye alivumbua gaze nyingi.

  • Katika mambo ya siasa, alitetea uhuru wa kusema, kuabudu, na elimu.

  • Katika mambo ya dini, alikataa mafundisho mengi ya dini kama vile Utatu na kutokufa kwa nafsi.

  • Katika mwaka wa 1794, Priestley alikimbilia Amerika, na akakufia huko kisha karibu miaka kumi.

NI KWELI AO NI MAPOKEO?

watu wenye hasira waliharibu nyumba ya Priestley na chumba chake cha kufanyia

Katika mwaka wa 1791, watu wenye hasira waliharibu nyumba ya Priestley na chumba chake cha kufanyia utafiti

Priestley alivumbua kwamba mapokeo ao mafundisho mengi ya zamani ya dini yalipingana na mambo ambayo Biblia inafundisha. Fikiria mifano fulani:

  • Pokeo: Yesu iko sawa na Mungu.

    Kweli ya Biblia: Yesu Kristo alisema hivi: ‘Baba ni mukubwa kuliko mimi.’—Yohana 14:28.

  • Pokeo: Nafsi haiwezi kufa.

    Kweli ya Biblia: ‘Nafsi inayotenda zambi—hiyo yenyewe itakufa.’—Ezekieli 18:4.

  • Pokeo: Tunaweza kutumia sanamu ili kumuabudu Mungu.

    Kweli ya Biblia: ‘Mimi ni Yehova. Hilo ni jina langu; na mimi sitamupa mwingine yeyote utukufu wangu mwenyewe, wala sitazipa sanamu za kuchongwa sifa yangu.’—Isaya 42:8.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine