Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g19 na. 3 uku. 12-13
  • Hali ya Kiroho

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Hali ya Kiroho
  • Amuka!—2019
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • UKUWE NA TUMAINI
  • MAJIBU YA MAULIZO YA MAANA SANA JUU YA MAISHA
  • KANUNI ZINGINE ZA BIBLIA
  • Tunaweza Kupata Wapi Majibu ya Maulizo ya Maana Sana Juu ya Maisha?
    Tunaweza Kupata Wapi Majibu ya Maulizo ya Maana Sana Juu ya Maisha?
  • Musaada Zaidi Kwa Ajili Ya Familia
    Amuka!—2018
  • Musaada Zaidi kwa Ajili ya Wazazi
    Amuka!—2019
  • Endelea Kukomaa Kiroho!
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2019
g19 na. 3 uku. 12-13
Mwanamuke mumoja anakaa ku kiti chenye kuwa mu bustani na anafikiri

Hali ya Kiroho

Kama vile habari ya kwanza ya gazeti hili ilionyesha, watu mingi wanaona Biblia kuwa kitabu kitakatifu. Wanaona kuwa wakati wanasoma na kutumia mashauri ya Biblia, wanajisikia kuwa karibu zaidi na Mungu na wanafikia kuelewa kusudi lao katika maisha.

Biblia inatumia maneno “hali ya muzuri ya kiroho” ili kumaanisha mutazamo ao maoni fulani yenye mutu iko nayo kuelekea maisha. (Yuda 18, 19) Tofauti na mutu mwenye anakazia tu mambo ya kimwili, ni kusema, mutu mwenye anakazia sana faida zake mwenyewe, watu wenye kuwa na hali ya muzuri ya kiroho wanapenda kanuni za Mungu.​—Waefeso 5:1.

UKUWE NA TUMAINI

KANUNI YA BIBLIA: “Kama unavunjika moyo nyakati za taabu, nguvu zako zitakuwa kidogo.”​—Mezali 24:10, maelezo ya chini.

ILE INAMAANISHA NINI? Kuvunjika moyo kunaweza kutufanya tukose nguvu yenye tuko nayo lazima ili kupambana na magumu ya maisha. Kwa upande mwingine, kuwa na tumaini kunaweza kutupatia nguvu yenye tuko nayo lazima ili tuendelee kuvumilia. Kujua kama magumu yenye tunapambana nayo ni ya wakati kidogo, kunaweza kututia moyo; kwa kweli, tunaweza kutazamia kupata jambo ao kitu fulani cha muzuri kisha ile magumu.

KILE UNAWEZA KUFANYA: Fikiria mambo ya muzuri ya wakati wenye kuja. Kuliko kuhangaika juu ya kile kinaweza kutokea ao kungojea tu wakati wenye mambo itakuwa muzuri kabisa, utende kulingana na miradi yako. Ni kweli kwamba, “matukio yenye hayatazamiwe” inaweza kutokea. (Muhubiri 9:11) Lakini, kusema kweli, mara mingi mambo inabadilikaka na kuwa ya muzuri zaidi kuliko vile tunaweza kutazamia. Kwa hiyo, kwa kutumia usemi wa mufano wa mupandaji, Biblia inasema hivi: “Panda mbegu zako asubui na usiache mukono wako upumuzike mupaka mangaribi; kwa maana haujue ni ya wapi itafanikiwa, kama ni hii ao ile, ao kama zote mbili zitakuwa muzuri.”​—Muhubiri 11:6.

MAJIBU YA MAULIZO YA MAANA SANA JUU YA MAISHA

KANUNI YA BIBLIA: “Unipatie uelewaji . . . Neno lako ni kweli.”​—Zaburi 119:144, 160.

ILE INAMAANISHA NINI? Biblia inatoa majibu ya maulizo yenye karibu kila mutu anajiulizaka. Kwa mufano, inajibia maulizo kama vile

  • Tulitoka wapi?

  • Juu ya nini tuko ku dunia?

  • Ni nini inatupata wakati tunakufa?

  • Maisha itabakiaka tu hivi?

Mamilioni ya watu mu dunia yote wamefanya maisha yao ikuwe ya muzuri zaidi kwa kuchunguza majibu ya Biblia ya ile maulizo na ya maulizo ingine.

KILE UNAWEZA KUFANYA: Uchunguze wewe mwenyewe mambo yenye Biblia inafundisha. Omba Shahidi wa Yehova akusaidie kuelewa Biblia. Fungua site yetu ya Enternete jw.org, ao ukuje ku mikutano yetu. Mikutano yetu ni ya bure na watu wote wanakaribishwa.

KANUNI ZINGINE ZA BIBLIA

Mwanamuke mumoja anaangalia video Sababu Gani Ujifunze Biblia? yenye kuwa ku jw.org

Angalia video Sababu Gani Ujifunze Biblia? kwenye jw.org. Inapatikana mu luga zaidi ya 880

UTAMBUE UHITAJI WAKO WA KIROHO.

“Wenye furaha ni wale wenye wanatambua uhitaji wao wa kiroho.”​—MATAYO 5:3.

UJIFUNZE MINGI ZAIDI KUMUHUSU MUNGU MWENYE KUZUNGUMUZIWA MU BIBLIA.

‘Umutafute Mungu . . . na kwa kweli utamupata . . . Haiko mbali sana na kila mumoja wetu.’​—MATENDO 17:27.

USOME NA UFIKIRI SANA JUU YA UJUMBE WA BIBLIA.

“Anapendezwa na sheria ya Yehova,a na anafikiri sana juu ya sheria Yake muchana na usiku. . . . Kila jambo lenye anafanya litafanikiwa.”​—ZABURI 1:2, 3, maelezo ya chini.

a Yehova ni jina la Mungu kama vile inaonyeshwa mu Biblia.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine