Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g22 na. 1 uku. 4-6
  • 1 | Ulinde Afya Yako

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • 1 | Ulinde Afya Yako
  • Amuka!—2022
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • JUU YA NINI NI JAMBO YA MAANA?
  • Mambo Yenye Unapaswa Kujua
  • Mambo Yenye Unaweza Kufanya Sasa
  • Mambo ya Kufanya ili Afya Yako Ikuwe Muzuri
    Amuka!—2015
  • Afya ya Kimwili
    Amuka!—2019
  • Namna ya Kupambana na Mukazo
    Amuka!—2020
  • Usamini Zawadi ya Mungu ya Uzima
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
Amuka!—2022
g22 na. 1 uku. 4-6
Chakula mbalimbali yenye kujenga iko ku meza.

MAGUMU INAYALA MU DUNIA

1 | Ulinde Afya Yako

JUU YA NINI NI JAMBO YA MAANA?

Ukilinda afya yako, inaweza kuwa mwepesi kwako kuvumilia magumu ya nguvu sana. Musiba wa asili ao jambo ingine ya mubaya inaweza kuwa na matokeo ya mubaya juu ya afya yetu mu njia mbalimbali.

  • Wakati jambo fulani ya mubaya inatokea, ile inaweza kuhangaisha watu. Na kama mahangaiko inaendelea kwa wakati murefu, ile inaweza kufanya watu wagonjwe.

  • Wakati ya misiba, hopitale zinakuwaka na watu wengi wa kuhangaikia. Ile inaweza kufanya ikuwe nguvu kupata matunzo ao kupata dawa.

  • Wakati ya misiba, inaweza kuwa nguvu kupata makuta. Juu ya ile, watu wanaweza kushindwa kuuza vitu vyenye wako navyo lazima, sawa vile chakula na dawa.

Mambo Yenye Unapaswa Kujua

  • Magonjwa ya nguvu na mahangaiko ya akili inaweza kufanya ukamate maamuzi ya mubaya na ufikie kukosa kuhangaikia afya yako. Na ile inaweza kufanya ugonjwe zaidi.

  • Kama uko mugonjwa na hautafute matunzo, magonjwa inaweza kuongezeka sana. Na ile inaweza kufanya uzima wako ukuwe mu hatari.

  • Kama uko na afya ya muzuri, itakuwa mwepesi kwako kukamata maamuzi ya muzuri ikiwa jambo fulani ya mubaya inatokea.

  • Ikuwe uko na makuta mingi ao hapana, kuko mambo yenye unaweza kufanya juu ya kulinda afya yako.

Mambo Yenye Unaweza Kufanya Sasa

Kila mara wakati inawezekana, mutu mwenye kuwa na hekima anafikiriaka hatari fulani zenye zinaweza kutokea, kisha anafanya mambo fulani juu ya kuziepuka. Ni vile pia juu ya afya. Kama uko safi na unafanya nyumba yako ikuwe safi, ile inaweza kukuepusha na magonjwa. Banasemaka: Ni muzuri kuzuia ugonjwa kuliko kuuponyesha.

“Wakati tuko safi na fasi kwenye tunaishi kuko safi, ile inatusaidia miye na bibi yangu tusitumikishe makuta mingi juu ya kuenda ku hopitale ao juu ya kuuza dawa.”​—Andreas.a

a Majina fulani mu hii gazeti imebadilishwa.

MAMBO YA KUFANYA​—Mashauri Yenye Inaweza Kusaidia

Wakati jambo fulani ya mubaya inatokea, ufanye hii mambo juu ya kulinda afya yako

UKUWE MUSAFI

Mwanaume fulani iko ananawa mikono na maji na sabuni.

Ukuwe musafi

Biblia inasema hivi: “Mutu mwerevu anaona hatari na kujificha.” (Mezali 22:3) Ujikaze kujua mambo yenye inaweza kutia uzima wako mu hatari na uiepuke.

  • Unawe mikono kila mara kwa kutumia sabuni na maji, zaidi sana mbele ya kugusa chakula ao wakati unatoka ku choo (ao wc).

  • Ukuwe na kawaida ya kusafisha nyumba yako na kuondoa mikrobe, zaidi sana ku fasi na vitu vyenye watu wanagusaka mara mingi.

  • Kama inawezekana, uepuke kuwa karibu na watu wenye wako na ugonjwa wa kuambukiza.

UKULE MUZURI

Chakula mbalimbali yenye kujenga iko ku meza.

Ukule muzuri

Biblia inasema hivi: “Hakuna mutu mwenye anachukia mwili wake; lakini anaukulisha na kuutunza kwa upendo.” (Waefeso 5:29) Juu tuonyeshe kama tunapenda mwili wetu, tunapaswa kuwa waangalifu juu ya vitu vyenye tunakula na kunywa.

  • Ukunywe maji mingi.

  • Ukule matunda na mboga za majani za aina mbalimbali.

  • Uepuke kutumia mafuta mingi, chumvi mingi, na sukari mingi.

  • Usivute tumbako, uepuke kunywa pombe kupita kiasi, uepuke dawa za kulewesha, na usitumie dawa mu njia yenye haifae.

“Juu ya kuepuka magonjwa, miye na bibi yangu tunajikazaka kukula muzuri; juu kama hatufanye vile, makuta kidogo yenye tunapataka inaweza kuishia mu matunzo. Njo maana tunaonaka kama ni muzuri tutumie makuta yetu juu ya kuuza chakula yenye itasaidia tukuwe na afya ya muzuri.”​—Carlos.

UFANYE MAZOEZI NA UPUMUZIKE VYA KUTOSHA

Mwanaume mumoja iko anafanya mazoezi ya kukimbia mu barabara.

Ufanye mazoezi

Biblia inasema hivi: “Mukono mumoja wa pumuziko ni muzuri zaidi kuliko mikono mbili ya kazi ya nguvu na kufuatilia upepo.” (Muhubiri 4:6) Kazi ni ya maana, lakini kupumuzika vya kutosha nayo ni ya maana pia.

  • Ukuwe unafanya mazoezi kwa ukawaida. Unaweza kuanza kwa kufanya mazoezi ya kutembea. Mazoezi inaweza kukusaidia ukuwe na afya ya muzuri hata kama ulishazeeka, uko na ulemavu, ao uko na uzaifu fulani juu ya ugonjwa wa wakati murefu.

  • Mwanamuke mumoja iko analala.

    Ulale vya kutosha

    Ukuwe unapumuzika vya kutosha. Kukosa kupumuzika vya kutosha kunaweza kufanya ukuwe na mahangaiko na kunaweza kupunguza uwezo wako wa kukaza akili. Na kama unaendelea vile kwa wakati murefu, unaweza kupata matatizo makubwa ya afya.

  • Upange wakati ya kukuwa nalala na uheshimie ile wakati. Ukuwe unalala na kulamuka saa ileile kila siku.

  • Uepuke kuangalia televizyo ao vyombo vingine vya kielektroniki wakati uko ku kitanda.

  • Kama utakula chakula mbele ya kulala, ikuwe chakula ya mwepesi. Uepuke pia kutumia caféine na pombe mbele ya kulala.

“Naonaka kama usingizi unakuwaka na matokeo juu ya afya yangu. Kama silale vya kutosha, wakati fulani nasikiaka kichwa inaniluma na sijisikiake tu muzuri mu mwili. Lakini wakati nalala vya kutosha, nasikiaka sawa vile ninaweza kunyangula hii dunia! Nakuwaka na nguvu mingi na sigonjwake sana.”​—Justin.

Picha ya video “Magonjwa ya Kuambukiza​—Mambo Yenye Unaweza Kufanya.” Mwanamuke mumoja anafungula mulango na mikrobe inaingia.

UJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI. Uangalie video Magonjwa ya Kuambukiza​—Mambo Yenye Unaweza Kufanya. Usome pia habari “Mambo ya Kufanya ili Afya Yako Ikuwe Muzuri.”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine