Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lv uku. 218-uku. 219 fu. 1
  • Namna ya Kushinda Tabia ya Kupiga Punyeto

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna ya Kushinda Tabia ya Kupiga Punyeto
  • Mubaki “Katika Upendo wa Mungu”
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tunaweza Kufanya Nini Juu Tukuwe Safi mu Macho ya Mungu?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • ‘Kimbia Uasherati’
    Mubaki “Katika Upendo wa Mungu”
  • ‘Kimbia Uasherati!’
    Namna ya Kubakia Katika Upendo wa Mungu
Mubaki “Katika Upendo wa Mungu”
lv uku. 218-uku. 219 fu. 1

NYONGEZA

Namna ya Kushinda Tabia ya Kupiga Punyeto

Kupiga punyeto ni zoea ao tabia chafu inayomuchukiza Mungu; tabia hiyo inamufanya mutu afikirie kujitosheleza yeye mwenyewe, na inaharibu akili ya mutu.a Mutu huyo anaweza pia kufikia kuwaona watu wengine kuwa ni vyombo tu vilivyofanywa ili kutosheleza tamaa ya ngono. Yeye haone ngono kuwa alama ya upendo kati ya watu wawili, lakini anaiona kuwa njia ya kujipatia raha haraka na kutuliza tamaa zake za ngono. Lakini kitulizo hicho ni cha muda tu. Kwa kweli, kuliko kuua viungo vya mwili ‘kwa habari ya uasherati, uchafu, na hamu isiyofaa ya ngono,’ kupiga punyeto kunaviamusha.—Wakolosai 3:5.

Mutume Paulo aliandika: ‘Wapendwa, kwa kuwa tuna ahadi hizi, acheni tujisafishe wenyewe kila unajisi [ao uchafu] wa mwili na roho, tukiukamilisha utakatifu katika kumuogopa Mungu.’ (2 Wakorintho 7:1) Ikiwa una magumu ya kutii maneno hayo, usikate tumaini. Kila siku, Yehova iko “tayari kusamehe” na kusaidia. (Zaburi 86:5; Luka 11:9-13) Kwa kweli, kwa kuwa moyo wako unakuhukumu na kwa sababu unafanya nguvu ili kuachana na zoea hilo, hata ikiwa unaanguka mara mojamoja, hizo ni alama zinazoonyesha kwamba una mawazo mazuri. Kumbuka pia kwamba, ‘Mungu ni mukubwa kuliko mioyo yetu naye anajua mambo yote.’ (1 Yohana 3:20) Mungu haone tu zambi zetu; anaona namna tulivyo kwelikweli. Kwa kuwa anajua kila jambo kutuhusu, hilo linamufanya asikilize kwa huruma sala zetu tunapomuomba atusamehe. Kwa hiyo, usichoke kuzungumuza na Mungu katika sala kwa unyenyekevu na kwa moyo wote, kama vile mutoto anavyomuendea baba yake anapokuwa katika shida. Yehova atakupatia zamiri safi. (Zaburi 51:1-12, 17; Isaya 1:18) Ndiyo, unapaswa kutenda kulingana na sala yako. Kwa mufano, unapaswa kuepuka kuangalia aina zote za ponografia (picha ao habari za ngono) na pia kuepuka kushirikiana na marafiki wabaya.b

Ikiwa tatizo lako la kupiga punyeto linaendelea, tafazali zungumuza jambo hilo na muzazi fulani Mukristo ao rafiki yako fulani anayejulikana kuwa mutu mwenye kukomaa kiroho.c—Methali 1:8, 9; 1 Wathesalonike 5:14; Tito 2:3-5.

a Kupiga punyeto ni kugusa-gusa ao kupapasa-papasa viungo vya uzazi ili kuingia katika raha ya ngono na kuitosheleza.

b Ili ordinatere ya familia isiwe mutego, familia nyingi zinaiweka mahali ambapo kila mutu anaweza kuona mambo unayotazama. Familia zingine zimenunua programu ya ordinatere inayochuja mambo yasiyofaa. Hata hivyo, jua kwamba hakuna programu ya ordinatere inayoweza kutumainiwa kabisa.

c Ili kupata habari zaidi kuhusu namna ya kushinda zoea la kupiga punyeto, soma habari “Vijana Huuliza . . . Ninaweza Kushindaje Zoea Hili?” katika Amkeni! ya Mwezi wa 11, 2006, na katika Buku la 1, la kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, ukurasa wa 178-182.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine