-
Sehemu ya 1 Mambo Yenye Mukristo AnaaminiTengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
-
-
MAULIZO KWA AJILI YA WALE WENYE KUPENDA KUBATIZWA
Sehemu ya 1 Mambo Yenye Mukristo Anaamini
Kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova kumekusaidia ujue kweli. Bila shaka, mambo yenye umejifunza imekusaidia ukuwe na urafiki wa muzuri pamoya na Mungu, na imekupatia tumaini ya kuishi ku dunia paradiso yenye itatawaliwa na Ufalme wa Mungu. Umeamini kabisa kama Biblia ni Neno ya Mungu, na tayari uko napata baraka mingi juu umeingia mu kutaniko ya Kikristo. Umefurahia kuona namna Yehova iko natendea watumishi wake leo.—Zek. 8:23.
Juu sasa uko najitayarisha kwa ajili ya ubatizo, itakuwa muzuri wazee wa kutaniko warudilie pamoya na weye mafundisho ya musingi ya Wakristo. (Ebr. 6:1-3) Yehova aendelee basi kubariki bidii yako ya kupenda kumujua, na akupatie zawadi yenye ametuahidi.—Yoh. 17:3.
1. Juu ya nini unapenda kubatizwa?
2. Yehova ni nani?
• “Yehova ndiye Mungu wa kweli juu mbinguni na chini duniani. Hakuna mwingine.”—Kum. 4:39.
• “Wewe, mwenye jina lako ni Yehova, wewe peke yako ndiye Mwenye Kuwa Juu Zaidi, juu ya dunia yote.”—Zb. 83:18.
3. Juu ya nini ni muzuri ukuwe natumia jina ya pekee ya Mungu?
• “Basi ninyi munapaswa kusali hivi: ‘Baba yetu mwenye kuwa mbinguni, jina lako litakaswe.’”—Mt. 6:9.
• “Kila mutu mwenye anaitia jina la Yehova ataokolewa.”—Ro. 10:13.
4. Biblia inatumia maneno gani juu ya kuzungumuzia Yehova?
• “Yehova, Muumbaji wa miisho ya dunia, ni Mungu kwa umilele wote.”—Isa. 40:28.
• “Baba yetu mwenye kuwa mbinguni.”—Mt. 6:9.
• “Mungu ni upendo.”—1 Yo. 4:8.
5. Ni mambo gani yenye unaweza kumupatia Yehova Mungu?
• “Unapaswa kumupenda Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote na kwa nguvu zako zote.”—Mk. 12:30.
• “Yehova Mungu wako ndiye unapaswa kuabudu, na yeye peke yake ndiye unapaswa kutolea utumishi mutakatifu.”—Lu. 4:8.
6. Juu ya nini unapenda kuwa muaminifu kwa Yehova?
• “Ukuwe na hekima, mwana wangu, na ufurahishe moyo wangu, ili niweze kumujibu ule mwenye ananichokoza.”—Mez. 27:11.
7. Ni nani njo unaombaka, na unaombaka mu jina ya nani?
• “Kwa kweli kabisa [mimi Yesu] ninawaambia ninyi, kama munamuomba Baba jambo lolote, atawapatia ninyi katika jina langu.”—Yoh. 16:23.
8. Unaweza kusali juu ya mambo gani?
• “Basi ninyi munapaswa kusali hivi: ‘Baba yetu mwenye kuwa mbinguni, jina lako litakaswe. Ufalme wako ukuje. Mapenzi yako yafanyike duniani kama mbinguni. Utupatie leo mukate wetu kwa ajili ya siku hii; na utusamehe madeni yetu, kama vile sisi pia tumesamehe wenye kuwa na madeni yetu. Na usituingize katika jaribu, lakini utukomboe na ule muovu.’”—Mt. 6:9-13.
• “Huu ndio uhakika wenye tuko nao kwake, kwamba hata kama tunaomba nini kulingana na mapenzi yake, yeye anatusikia.”—1 Yo. 5:14.
9. Nini inaweza kufanya Yehova asisikilize sala ya mutu?
• “Watamuita Yehova awasaidie, lakini hatawajibu . . . kwa sababu ya matendo yao maovu.”—Mik. 3:4.
• “Macho ya Yehova yako juu ya wenye haki, na masikio yake yanasikiliza sala yao ya kumulilia Mungu, lakini uso wa Yehova unapinga wale wenye kutenda mambo ya mubaya.”—1 Pe. 3:12.
10. Yesu Kristo ni nani?
• “Simoni Petro akajibu: ‘Wewe ndiye Kristo, Mwana wa Mungu mwenye kuishi.’”—Mt. 16:16.
11. Juu ya nini Yesu alikuya ku dunia?
• “Mwana wa binadamu hakukuja ili watu wamutumikie, lakini ili yeye atumikie wengine na atoe uzima wake kuwa bei ya ukombozi pa nafasi ya wengi.”—Mt. 20:28.
• “[Mimi Yesu] ni lazima pia nitangaze habari njema ya Ufalme wa Mungu katika miji ingine, kwa sababu nilitumwa ili kufanya vile.”—Lu. 4:43.
12. Unaweza kufanya nini ili kuonyesha shukrani yako juu ya zabihu ya Yesu?
• “Alikufa kwa ajili ya watu wote ili wale wenye wanaishi wasiishi tena kwa ajili yao wenyewe, lakini kwa ajili ya ule mwenye alikufa kwa ajili yao na akafufuliwa.”—2 Ko. 5:15.
13. Yesu iko na mamlaka gani?
• “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.”—Mt. 28:18.
• “Mungu alimuinua kwenye cheo cha juu zaidi na kumupatia kwa fazili jina lenye kuwa juu zaidi ya kila jina lingine.”—Flp. 2:9.
14. Unaamini kama Baraza Yenye Kuongoza ya Mashahidi wa Yehova njo “mutumwa muaminifu na mwenye busara” mwenye Yesu aliweka?
• “Ni nani kwa kweli mutumwa muaminifu na mwenye busara mwenye bwana wake ameweka juu ya watumishi wake wa nyumbani, ili kuwapatia chakula chao kwa wakati wenye kufaa?”—Mt. 24:45.
15. Roho takatifu ni mutu?
• “Malaika akamujibu: ‘Roho takatifu itakuja juu yako, na nguvu za Mwenye Kuwa Juu Zaidi zitakufunika kwa kivuli. Na kwa hiyo ule mwenye atazaliwa ataitwa mutakatifu, Mwana wa Mungu.’”—Lu. 1:35.
• “Kwa hiyo, ikiwa ninyi, hata kama muko waovu, munajua kupatia watoto wenu zawadi za muzuri, Baba yenu wa mbinguni atawapatia hata zaidi roho yake takatifu wale wenye kumuomba!”—Lu. 11:13.
16. Yehova anatumiaka namna gani roho takatifu?
• “Kwa neno la Yehova mbingu zilifanywa, na kwa roho ya kinywa chake kila kitu chenye kuwa katika mbingu kilifanywa.”—Zb. 33:6.
• “Mutapokea nguvu wakati roho takatifu itakuja juu yenu, na mutakuwa mashahidi wangu . . . mupaka kwenye sehemu ya mbali zaidi ya dunia.”—Mdo. 1:8.
• “Hakuna unabii wa Andiko wenye unatokana na mawazo yoyote ya mutu. Kwa maana unabii haukuletwa wakati wowote kwa mapenzi ya mwanadamu, lakini wanadamu walisema yenye yalitoka kwa Mungu wakiongozwa na roho takatifu.”—2 Pe. 1:20, 21.
17. Ufalme wa Mungu ni nini?
• “Mungu wa mbinguni atasimamisha ufalme wenye hautaharibiwa hata siku moya. Na ufalme huo hautapewa watu wengine wowote. Utaponda na kumaliza falme hizi zote, na ufalme huo peke yake utasimama milele.”—Da. 2:44.
18. Ufalme wa Mungu utakuletea baraka gani?
• “Atapanguza kila chozi katika macho yao, na kifo hakitakuwa tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu havitakuwa tena. Mambo ya zamani yamepita kabisa.”—Ufu. 21:4.
19. Nini inafanya ujue kama baraka za Ufalme zitafika hivi karibuni?
• “Wanafunzi wakamukaribia akiwa peke yake, na kusema: ‘Tuambie, mambo haya yatakuwa wakati gani, na ni nini itakuwa alama ya kuwapo kwako na ya umalizio wa mupangilio wa mambo?’ Yesu akawajibu na kuwaambia: ‘. . . Taifa litasimama kupigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme, na kutakuwa upungufu wa chakula na matetemeko ya inchi mahali pamoja kisha pengine. Na hii habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote yenye kuikaliwa na watu ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote, na kisha ule mwisho utakuja.’”—Mt. 24:3, 4, 7, 14.
• “Katika siku za mwisho kutakuwa nyakati za hatari zenye kuwa ngumu kuvumilia. Kwa maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda feza, wenye kujisifu, wenye kujivuna, wenye kumutukana Mungu, wenye hawatii wazazi, wenye hawana shukrani, wenye hawana ushikamanifu, wenye hawana upendo wa asili, wenye hawataki makubaliano yoyote, wachongezi, wenye hawajizuie, wakali, wenye hawapendi wema, wasaliti, wenye vichwa vigumu, wenye kujivuna kwa kiburi, wenye kupenda raha kuliko kumupenda Mungu, wenye kwa inje wanaonekana kuwa na ushikamanifu kwa Mungu lakini wanakana nguvu za ushikamanifu huo.”—2 Ti. 3:1-5.
20. Unafanyaka nini ili kuonyesha kama Ufalme ni jambo ya maana kwako?
• “Basi, muendelee kutafuta kwanza Ufalme na haki yake.”—Mt. 6:33.
• “Yesu akaambia wanafunzi wake: ‘Kama mutu yeyote anataka kunifuata, lazima ajikane mwenyewe, achukue muti wake wa mateso na aendelee kunifuata.’”—Mt. 16:24
21. Shetani na pepo wachafu ni nani?
• “Ninyi mumetoka kwa baba yenu Ibilisi . . . Huyo alikuwa muuaji wakati alianza.”—Yoh. 8:44.
• “Ule nyoka mukubwa akatupwa chini, ule nyoka wa zamani, mwenye kuitwa Ibilisi na Shetani, mwenye anapotosha dunia yote yenye kuikaliwa na watu; akatupwa chini katika dunia, na malaika wake wakatupwa chini pamoja naye.”—Ufu. 12:9.
22. Shetani alimusingizia Yehova nini na wale wenye wanamuabudu?
• “Mwanamuke akamuambia nyoka: ‘Tunaweza kula matunda ya miti ya bustani. Lakini kuhusu matunda ya muti wenye kuwa katikati ya bustani Mungu amesema: “Hamupaswe kuyakula, hapana, hamupaswe kuyagusa; mukifanya vile mutakufa.”’ Kwa hiyo nyoka akamuambia mwanamuke: ‘Hakika hamutakufa. Kwa sababu Mungu anajua kwamba siku ileile yenye mutakula matunda ya muti huo, macho yenu yatafunguliwa na mutakuwa kama Mungu; mukijua mema na mabaya.’”—Mwa. 3:2-5.
• “Shetani akamujibu Yehova: ‘Ngozi kwa ngozi. Mutu atatoa kila kitu chenye iko nacho ili aokoe uzima wake.’”—Yob. 2:4.
23. Unaweza kufanya nini ili kuonyesha kama Shetani alidanganya?
• “Umutumikie [Mungu] kwa moyo kamili.”—1 Ny. 28:9.
• “Mupaka wakati nitakufa, sitaacha uaminifu-mushikamanifu wangu!”—Yob. 27:5.
24. Juu ya nini watu wanakufaka?
• “Kupitia mutu mumoja zambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia zambi, na ni vile kifo kilienea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya zambi.”—Ro. 5:12.
25. Wafu wako mu hali gani?
• “Wazima wanajua kwamba watakufa, lakini wafu hawajue kitu chochote.”—Muh. 9:5.
26. Kuko tumaini gani juu ya wenye washakakufa?
• “Kutakuwa ufufuo wa wenye haki na wenye hawako wenye haki.”—Mdo. 24:15.
27. Ni watu ngapi njo wataenda mbinguni ili kutawala na Yesu?
• “Angalia! Mwana-Kondoo amesimama juu ya Mulima Sayuni, na pamoja naye watu elfu mia moja makumi ine na ine (144 000) wenye kuwa na jina lake na jina la Baba yake likiwa limeandikwa kwenye mapaji ya nyuso zao.”—Ufu. 14:1.
-
-
Sehemu ya 2 Maisha ya MukristoTengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
-
-
MAULIZO KWA AJILI YA WALE WENYE KUPENDA KUBATIZWA
Sehemu ya 2 Maisha ya Mukristo
Kujifunza Biblia, kumekusaidia ujue mambo yenye Yehova anapenda ufanye na namna ya kutumikisha kanuni zake za haki mu maisha yako. Pengine mambo yenye umejifunza, imekuchochea kubadilisha mwenendo yako mu njia fulani na namna yako ya kuona uzima. Kwa kuwa sasa umeamua kutii kanuni za haki za Yehova mu maisha yako, unastahili kuwa muhubiri wa habari njema na kumutolea Yehova utumishi wenye atakubali. Kurudilia maulizo yenye kufuata kutakusaidia kuweka muzuri mu akili yako kanuni za haki za Yehova, na kutakukumbusha mambo fulani yenye unaweza kufanya juu ukuwe kati ya watumishi wenye Yehova anakubali. Hii sehemu, itakusaidia uelewe juu ya nini ni lazima sana kufanya mambo yote na uko na zamiri safi na ili kumuletea Yehova heshima.—2 Ko. 1:12; 1 Ti. 1:19; 1 Pe. 3:16, 21. Bila shaka hii hatua yenye umefikia mu funzo yako, inaonyesha wazi kama uko na hamu sana ya kutii muongozo wa Yehova na kuwa sehemu ya tengenezo yake. Maulizo na Maandiko yenye kutajwa mu hii sehemu, itakusaidia ujichunguze ili kuona kama ulishaelewa kabisa maana ya kutii mupango wenye Yehova ameweka, ikuwe mu kutaniko, mu familia, ao juu ya serikali za hii mupangilio wa mambo. Utakuwa mwenye shukrani sana juu ya mipango yenye Yehova amekamata ili kufundisha watu wake na kufanya wakuwe nguvu kiroho. Ile inatia ndani mikutano ya kutaniko, yenye unapenda kukuwa naendaako na kutoa majibu kulingana na hali zako. Tena, hii sehemu itazungumuzia faida ya kuhubiri Ufalme kwa ukawaida ili kusaidia watu wengi wamujue Yehova na mambo yenye iko nafanyia wanadamu. (Mt. 24:14; 28:19, 20) Na ku mwisho, itakusaidia uweke mu akili yako kama kujitoa kwa Yehova na kubatizwa ni mambo yenye unapaswa kukamata kwa uzito. Ukuwe hakika kama Yehova anafurahi kuona vile unakubali fazili zake zenye hazistahiliwe.
1. Wakristo wanafuata kanuni gani juu ya ndoa? Ni sababu gani moya tu ya Maandiko yenye inaweza kufanya ndoa ivunjike?
• “Je, hamukusoma kama ule mwenye aliwaumba tangu mwanzo aliwafanya mwanaume na mwanamuke na alisema: ‘Kwa sababu hiyo mwanaume atamuacha baba yake na mama yake na atashikamana na bibi yake, na hao wawili watakuwa mwili mumoja’? Na hivyo hawako wawili tena, lakini mwili mumoja. Kwa hiyo, kile chenye Mungu ameunganisha, mutu yeyote asikitenganishe. . . . Kila mutu mwenye anavunja ndoa na bibi yake, kama haiko tu kwa sababu ya uasherati, na kumuoa mwingine anafanya uzinifu.”—Mt. 19:4-6, 9.
2. Juu ya nini watu wenye wanaishi pamoya sawa bibi na bwana wanapaswa kuoana kulingana na sheria? Kama umeoa ao kuolewa, uko hakika ndoa yako imeandikishwa kisheria na serikali?
• “Endelea kuwakumbusha wajitiishe na kutii serikali na mamlaka.”—Tit. 3:1.
• “Ndoa iheshimiwe kati ya watu wote, na kitanda cha ndoa kikuwe bila uchafu, kwa maana Mungu atahukumu waasherati na wazinifu.”—Ebr. 13:4.
3. Uko na daraka gani mu familia?
• “Mwana wangu, sikiliza nizamu ya baba yako, na usiache mafundisho ya mama yako.”—Mez. 1:8.
• “Bwana ni kichwa cha bibi yake kama vile Kristo ni kichwa cha kutaniko . . . Bwana, muendelee kupenda bibi zenu, kama vile Kristo pia alipenda kutaniko.”—Efe. 5:23, 25.
• “Baba, musikuwe munakasirisha watoto wenu, lakini muendelee kuwalea katika nizamu na maonyo ya Yehova.”—Efe. 6:4.
• “Ninyi watoto, mutii wazazi wenu katika kila jambo, kwa maana hilo linamupendeza Bwana.”—Kol. 3:20.
• “Ninyi bibi, mujitiishe kwa bwana zenu.”—1 Pe. 3:1.
4. Juu ya nini tunapaswa kuheshimia uzima?
• “[Mungu] anapatia watu wote uzima na pumuzi na vitu vyote. . . . Kupitia kwake tuko na uzima na tunatembea na tuko.”—Mdo. 17:25, 28.
5. Juu ya nini hatupaswe kuua mutu yeyote, kutia ndani mutoto mwenye hayazaliwa?
• ‘Kama watu wanapigana na wanamuumiza mwanamuke mwenye mimba, na kifo kinatokea, basi unapaswa kutoa uzima kwa uzima.’—Kut. 21:22, 23.
• “Macho yako hata yaliniona wakati nilikuwa kiini-tete; sehemu zake zote ziliandikwa katika kitabu chako kuhusiana . . . [na] siku zenye sehemu hizo ziliumbwa, mbele sehemu yoyote kati ya hizo ikuwe.”—Zb. 139:16.
• “Yehova anachukia . . . mikono yenye kumwanga damu yenye haina kosa.”—Mez. 6:16, 17.
6. Sheria ya Mungu inasema nini juu ya damu?
• “[Muendelee] kujiepusha . . . na damu na vitu vyenye vilinyongwa.”—Mdo. 15:29.
7. Juu ya nini tunapaswa kupenda ndugu na dada zetu Wakristo?
• “Ninawapatia ninyi amri mupya, kwamba mupendane; kama vile nimewapenda ninyi, ninyi pia mupendane vilevile. Kwa jambo hili wote watajua kama ninyi ni wanafunzi wangu—kama muko na upendo kati yenu.”—Yoh. 13:34, 35.
8. Juu ya kuepuka kusambaza ugonjwa hatari wenye kuambukiza: (a) Juu ya nini mutu mwenye iko na ugonjwa ya vile hapaswe kukumbatia ao kubusu wengine? (b) Juu ya nini hapaswe kukasirika kama watu fulani wanaamua kutomualika kwao? (c) Juu ya nini mutu mwenye pengine ameambukizwa na ugonjwa ya vile anapaswa enda kupima damu yake mbele ya kuanzisha uchumba? (d) Juu ya nini mutu mwenye iko na ugonjwa ya kuambukiza anapaswa kujulisha muratibu wa baraza ya wazee mbele ya kubatizwa?
• “Musikuwe na deni lolote kwa mutu yeyote isipokuwa kupendana. . . . ‘Unapaswa kumupenda jirani yako kama wewe mwenyewe.’ Upendo haumufanyie jirani mambo ya mubaya.”—Ro. 13:8-10.
• “Mukiendelea kuangalia, hapana faida zenu ninyi wenyewe tu, lakini pia faida za wengine.”—Flp. 2:4.
9. Juu ya nini Yehova anataka tusamehe wengine?
• “Muendelee kuvumiliana na kusameheana kwa kupenda hata kama mutu yeyote iko na sababu ya kulalamika juu ya mwingine. Kama vile Yehova aliwasamehe ninyi kwa kupenda, ninyi pia munapaswa kufanya vilevile.”—Kol. 3:13.
10. Unapaswa kufanya nini kama ndugu ao dada anakusemea uongo ao anakuiba mu mayele?
• “Kama ndugu yako anatenda zambi, uende ufunue kosa lake kati yako na yeye peke yake. Kama anakusikiliza, umemupata ndugu yako. Lakini kama hasikilize, chukua pamoja na wewe mutu mumoja ao wawili zaidi, ili kila jambo lihakikishwe kwa ushuhuda wa mashahidi wawili ao watatu (3). Kama hawasikilize hao, uambie kutaniko. Kama hasikilize hata kutaniko, acha akuwe kwako kama mutu wa mataifa na kama mukusanya-kodi.”—Mt. 18:15-17.
11. Yehova anaona namna gani zambi zenye kufuata?
▪ Uasherati
▪ Kutumia sanamu mu ibada
▪ Ngono ya mwanaume na mwanaume na mwanamuke na mwanamuke
▪ Kuiba
▪ Michezo ya makuta
▪ Kulewa
• “Musidanganywe. Waasherati, waabudu-sanamu, wazinifu, wanaume wenye wanakubali matendo ya kulalwa na wanaume wenzao, wanaume wenye kulala na wanaume wenzao, wezi, watu wenye kuwa na pupa, walevi, watukanaji, wanyanganyi hawatariti Ufalme wa Mungu.”—1 Ko. 6:9, 10.
12. Umeazimia kufanya nini juu ya uasherati, ni kusema, matendo mbalimbali ya ngono inje ya ndoa?
• “Mukimbie uasherati!”—1 Ko. 6:18.
13. Juu ya nini tunapaswa kuepuka kutumia dawa za kulewesha ao za kuvuruga akili zenye munganga hakutuandikia?
• “Mutoe miili yenu ikuwe zabihu yenye uzima, takatifu, na yenye kukubalika kwa Mungu, utumishi mutakatifu pamoja na nguvu zenu za kufikiri. Na muache kufinyangwa na mupangilio huu wa mambo, lakini mugeuzwe kwa kufanya upya akili yenu, ili mujihakikishie ninyi wenyewe mapenzi ya Mungu yenye kuwa mema na yenye kukubalika na makamilifu.”—Ro. 12:1, 2.
14. Ni mazoea gani ya kuzungumuza na pepo wachafu yenye Mungu anakataza?
• “Asipatikane katikati yako . . . mutu yeyote mwenye kufanya uaguzi, mutu yeyote mwenye kufanya uchawi, mutu yeyote mwenye kutafuta alama za mambo yenye yatatokea, mulozi, mutu yeyote mwenye anafunga wengine kwa uchawi, mutu yeyote mwenye anatafuta shauri kwa mutu mwenye kupashana habari na pepo wachafu ao mutu mwenye kutabiri matukio, ao mutu yeyote mwenye kuuliza habari kwa wafu.”—Kum. 18:10, 11.
15. Kama mutu anafanya zambi nzito na anataka arudilie tena urafiki wake pamoya na Yehova, anapaswa kufanya nini bila kuchelewa?
• “Niliungama zambi yangu kwako; sikufunika kosa langu. Nilisema: ‘Nitaungama makosa yangu kwa Yehova.’”—Zb. 32:5.
• “Kuko mutu yeyote mwenye kuwa mugonjwa kati yenu? Aite wazee wa kutaniko, na wasali kwa ajili yake, wakimupakaa mafuta katika jina la Yehova. Na sala ya imani itaponyesha ule mugonjwa, na Yehova atamuinua. Pia, kama amefanya zambi, atasamehewa.”—Yak. 5:14, 15.
16. Ukijua kama Mukristo mwenzako amefanya zambi nzito, unapaswa kufanya nini?
• “Kama mutu anafanya zambi kwa sababu amesikia mwito wa waziwazi wa kutoa ushahidi naye ni shahidi ao amejionea ao amepata kujua kuhusu jambo hilo, lakini hatoe habari, basi atajibu kwa sababu ya kosa lake.”—Law. 5:1.
17. Kama tunasikia tangazo yenye inasema mutu fulani haiko tena Shahidi wa Yehova, tunapaswa kumutendea namna gani?
• “Muache kushirikiana na mutu yeyote mwenye kuitwa ndugu mwenye kuwa mwasherati ao mutu mwenye kuwa na pupa ao muabudu-sanamu ao mutukanaji ao mulevi ao munyanganyi, hata musikule chakula pamoja na mutu wa namna hiyo.”—1 Ko. 5:11.
• “Kama mutu anakuja kwenu na halete fundisho hili, musimupokee katika nyumba zenu wala kumusalimia.”—2 Yoh. 10.
18. Juu ya nini marafiki wako wa karibu wanapaswa kuwa wenye wanamupenda Yehova?
• “Mwenye anatembea na wenye hekima atakuwa na hekima, lakini mwenye kufanya urafiki na wajinga ataumia.”—Mez. 13:20.
• “Musidanganywe. Mashirika ya mubaya yanaharibu tabia za muzuri.”—1 Ko. 15:33.
19. Juu ya nini Mashahidi wa Yehova hawaungake mukono upande wowote?
• “Wao hawako sehemu ya ulimwengu, kama vile mimi siko sehemu ya ulimwengu.”—Yoh. 17:16.
20. Juu ya nini unapaswa kutii serikali?
• “Kila mutu ajitiishe kwa mamlaka zenye kuwa kubwa, kwa maana hakuna mamlaka isipokuwa kwa ruhusa ya Mungu; mamlaka zenye ziko zimewekwa na Mungu katika vyeo vyao vya kadiri.”—Ro. 13:1.
21. Kama sheria ya mwanadamu inapingana na sheria ya Mungu, unapaswa kufanya nini?
• “Tunapaswa kumutii Mungu kuwa mutawala kuliko wanadamu.”—Mdo. 5:29.
22. Wakati uko nachagua kazi, ni Maandiko gani inaweza kukusaidia usijiingize mu mambo ya ulimwengu?
• “Taifa halitainua upanga juu ya taifa, wala hawatajifunza vita tena.”—Mik. 4:3.
• “Mutoke kwake [Babiloni Mukubwa], watu wangu, kama hamutaki kushiriki pamoja naye katika zambi zake, na kama hamutaki kupokea sehemu ya mapigo yake.”—Ufu. 18:4.
23. Ni mambo gani ya kujifurahisha yenye inafaa na yenye haifae?
• “Yehova . . . anachukia mutu yeyote mwenye kupenda jeuri.”—Zb. 11:5.
• “Muchukie sana mambo maovu; mushikamane na mambo mema.”—Ro. 12:9.
• “Mambo yoyote yenye kuwa ya kweli, mambo yoyote yenye kuwa ya hangaiko nzito, mambo yoyote ya haki, mambo yoyote yenye kuwa safi, mambo yoyote yenye kustahili kupendwa, mambo yoyote yenye kusemwa muzuri, tabia zozote za muzuri, na mambo yoyote yenye kustahili sifa, muendelee kufikiria mambo hayo.”—Flp. 4:8.
24. Juu ya nini Mashahidi wa Yehova hawachangake ibada yao na ya madini ingine?
• “Hamuwezi kuwa munashiriki ‘meza ya Yehova’ na meza ya pepo wachafu.”—1 Ko. 10:21.
• “‘Mujitenge,’ ni vile Yehova anasema, ‘na muache kugusa kitu kichafu’; ‘na mimi nitawakaribisha ninyi ndani.’”—2 Ko. 6:17.
25. Ni kanuni gani zitakusaidia kuamua kufanya sikukuu fulani ao hapana?
• “Walichangamana na mataifa hayo na kukubali njia zao. Waliendelea kutumikia sanamu zao, na hizo zikakuwa mutego kwao.”—Zb. 106:35, 36.
• “Wafu hawajue kitu chochote.”—Muh. 9:5.
• “Hawako sehemu ya ulimwengu, kama vile mimi siko sehemu ya ulimwengu.”—Yoh. 17:16.
• “Wakati wenye ulipita uliwatosha ninyi kufanya mapenzi ya mataifa wakati mulifanya matendo ya mwenendo mupotovu wa bila haya, tamaa kali yenye haiwezi kuzuiwa, kunywa kupita kiasi, karamu za kupitisha mipaka, mashindano ya kunywa, na ibada za sanamu zenye kuchukiza.”—1 Pe. 4:3.
26. Habari fulani zenye kuwa mu Biblia zinaweza kukusaidia namna gani kuamua kama utakubali kufanya sikukuu za kuzaliwa?
• “Siku ya tatu (3) ilikuwa sikukuu ya kuzaliwa kwa Farao, na alifanya karamu kwa ajili ya watumishi wake wote, na akatosha katika gereza mukubwa wa wanyweshaji . . . Lakini akamutundika mukubwa wa watengenezaji wa mikate.”—Mwa. 40:20-22.
• “Wakati wa karamu ya sikukuu ya kuzaliwa kwa Herode, binti ya Herodia alicheza dansi kwenye karamu hiyo na kufurahisha sana Herode mupaka akaahidi kwa kiapo kumupatia kila kitu chenye ataomba. Halafu binti huyo, kwa sababu alichochewa na mama yake, akasema: ‘Unipatie hapa kwenye sahani kichwa cha Yohana Mubatizaji.’ Basi Herode akatuma watu katika gereza ili wamukate Yohana kichwa.”—Mt. 14:6-8, 10.
27. Juu ya nini unaona ni muzuri kufuata muongozo wa wazee?
• “Mutii wale wenye wanaongoza kati yenu na munyenyekee, kwa maana wanaendelea kuwalinda ninyi kama wale wenye watatoa hesabu, ili wafanye vile kwa furaha, hapana kwa kusumbuka, kwa maana jambo hilo lingewaumiza ninyi.”—Ebr. 13:17.
28. Juu ya nini ni jambo ya lazima weye na familia yako mukuwe na wakati ya kusoma na kujifunza Biblia kwa ukawaida?
• “Anapendezwa na sheria ya Yehova, na anasoma sheria Yake kwa sauti ya chini muchana na usiku. Atakuwa kama muti wenye kupandwa pembeni ya mito midogo ya maji, muti wenye unazaa matunda katika wakati wake, na majani yake hayakauke. Na kila jambo lenye anafanya litafanikiwa.”—Zb. 1:2, 3.
29. Juu ya nini unapendaka kuenda ku mikutano na kutoa majibu?
• “Nitatangaza jina lako kwa ndugu zangu; katikati ya kutaniko nitakusifu.”—Zb. 22:22.
• “Na tufikiriane ili kuchocheana katika upendo na matendo ya muzuri, bila kuacha kukutana pamoja, kama vile wengine wako na desturi, lakini tutiane moyo, na kufanya vile zaidi sana kwa kadiri munaona siku ile kuwa inakaribia.”—Ebr. 10:24, 25.
30. Ni kazi gani ya maana sana yenye Yesu alitupatia?
• “Kwa hiyo, muende, na mufanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, na muwabatize . . . , muwafundishe kushika mambo yote yenye nimewaamuru ninyi.”—Mt. 28:19, 20.
31. Wakati tunatoa michango ili kutegemeza kazi ya Ufalme ao ili kusaidia ndugu na dada zetu, tunapaswa kufanya vile na roho ya namna gani juu Yehova afurahi?
• “Umuheshimie Yehova kupitia vitu vyako vyenye samani.”—Mez. 3:9.
• “Kila mumoja afanye kama vile alikusudia katika moyo wake, haiko kwa kutokupenda wala kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu anapenda mutu mwenye anatoa kwa furaha.”—2 Ko. 9:7.
32. Wakristo wanatazamia kupata magumu gani?
• “Wenye furaha ni wale wenye wameteswa kwa sababu ya haki, kwa maana Ufalme wa mbinguni ni wao. Wenye furaha ni ninyi wakati watu wanawalaumu na kuwatesa na kuwasingizia kila namna ya uovu kwa sababu yangu. Mushangilie na kufurahi sana, kwa sababu zawabu yenu ni kubwa mbinguni, kwa maana ni vile walitesa manabii wenye waliwatangulia.”—Mt. 5:10-12.
33. Mwenye anabatizwa ili kuwa Shahidi wa Yehova, iko na pendeleo gani ya pekee?
• “Neno lako lilikuwa kwangu furaha na shangwe ya moyo wangu, kwa maana jina lako liliitwa juu yangu, Ee Yehova.”—Yer. 15:16.
-
-
Mazungumuzo ya Kumalizia Pamoya na Wale Wenye WatabatizwaTengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
-
-
MAULIZO KWA AJILI YA WALE WENYE KUPENDA KUBATIZWA
Mazungumuzo ya Kumalizia Pamoya na Wale Wenye Watabatizwa
Kwa kawaida, ubatizo unafanywaka ku mikusanyiko ya Mashahidi wa Yehova. Mu maneno ya kumalizia hotuba ya ubatizo, musemaji ataomba wale wenye watabatizwa wasimame na wajibu kwa sauti maulizo mbili yenye kuwa hapa chini:
1. Ulishatubu zambi zako, ulishajitoa kwa Yehova katika sala, na unakubali wokovu wenye anatoa kupitia Yesu Kristo?
2. Unaelewa kama wakati unabatizwa unakuwa Shahidi wa Yehova na unaingia sasa mu tengenezo yake?
Wakati wale wenye watabatizwa wanajibu ndiyo ku hii maulizo, ‘wanatangaza mbele ya watu wote’ kama wanaamini bei ya ukombozi na kama walishajitoa kabisa kwa Yehova katika sala. (Ro. 10:9, 10) Wale wenye watabatizwa wanapaswa kufikiria sana ile maulizo katika sala mbele ya wakati ili waweze kujibu kulingana na mambo yenye wanaamini kabisa.
Ulishajitoa kwa Yehova katika sala, kwa kumutolea ahadi ya kama ni yeye tu njo utaabudu na kama kitu ya lazima sana mu maisha yako itakuwa kufanya mapenzi yake?
Sasa uko hakika kabisa kama unastahili kubatizwa?
Ni manguo gani yenye kustahili yenye mutu anapaswa kuvala wakati ya kubatizwa? (1 Ti. 2:9, 10; Yoh. 15:19; Flp. 1:10)
Tunapaswa kujipamba “kwa kiasi na akili ya muzuri” ili kuonyesha kama ‘tunashikamana na Mungu.’ Kwa hiyo, wale wenye watabatizwa hawapaswe kuvala manguo yenye kuonyesha sehemu za siri za mwili ao manguo yenye kuwa na maandishi. Kuliko kufanya vile, wanapaswa kuvala manguo yenye kuwa na mupangilio muzuri, yenye kuwa safi na yenye kustahili ile tukio.
Ni mambo gani mutu hapaswe kufanya wakati ya ubatizo? (Lu. 3:21, 22)
Leo, Wakristo wanaweza kuiga namna Yesu alijiendesha wakati alibatizwa. Alijua kama ubatizo ni hatua ya maana sana, na alionyesha vile kupitia mawazo na matendo yake. Kwa hiyo, wakati ya ubatizo, haiko saa ya kuchekesha-chekesha, kucheza, kuogelea, ao kufanya mambo ingine yenye inaweza kushushia heshima ile tukio. Zaidi ya ile, mwenye anatoka tu kubatizwa, hapaswe kufanya alama fulani sawa ile mutu anafanyaka wakati anapata ushindi mukubwa. Hata kama wakati ya ubatizo ni saa ya furaha, inaomba kufurahi kwa heshima.
Juu ya nini kukusanyika kwa ukawaida na ndugu na dada kunaweza kukusaidia utimize ahadi yenye ulimutolea Yehova?
Kisha kubatizwa, juu ya nini inaomba ukuwe unahubiri kwa ukawaida na kuwa na programu ya muzuri ya funzo ya pekee?
-