Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
    • Somo ya 31. Yesu, Mufalme wa Ufalme wa Mungu, iko mbele ya utukufu wa Yehova.

      SOMO YA 31

      Ufalme wa Mungu Ni Nini?

      Ufalme wa Mungu njo habari ya maana sana yenye Biblia inazungumuzia. Yehova atatumia Ufalme wake juu ya kufanya dunia ikuwe tena paradiso. Ufalme wa Mungu ni nini? Nini njo inaonyesha kama Ufalme wa Mungu uko natawala sasa. Ufalme wa Mungu ulishafanya nini? Na utafanya nini mu siku zenye ziko nakuya? Tutapata majibu ya ile maulizo mu hii somo na mu somo mbili zenye kufuata.

      1. Ufalme wa Mungu ni nini, na nani njoMufalme wa ule Ufalme?

      Ufalme wa Mungu ni serikali ao guvernema yenye Yehova Mungu ameweka. Yesu Kristo njo Mufalme wa Ufalme wa Mungu, na iko anatawala kule mbinguni. (Matayo 4:17; Yohana 18:36) Biblia inasema hivi juu ya Yesu: “Atatawala akiwa Mufalme . . . milele.” (Luka 1:32, 33) Yesu, Mufalme wa Ufalme wa Mungu, atatawala kila mutu ku dunia.

      2. Ni nani njo watatawala na Yesu?

      Yesu hatatawala peke yake. Watu wa kutoka mu “kila kabila na luga na watu na taifa . . . watatawala wakiwa wafalme juu ya dunia.” (Ufunuo 5:9, 10) Ni watu ngapi njo watatawala na Yesu? Tangu Yesu akuye ku dunia, watu wengi sana wamekuwa wanafunzi wake. Wote watatawala naye? Hapana. Ni watu 144000 tu njo wataenda mbinguni juu watawale na Yesu. (Soma Ufunuo 14:1-4.) Wakristo wengine wote wataishi ku dunia na watatawaliwa na Ufalme wa Mungu.​—Zaburi 37:29.

      3. Juu ya nini Ufalme wa Mungu unapita guvernema zote za wanadamu?

      Viongozi fulani wa guvernema za wanadamu wanapendaka kufanya mambo ya muzuri. Lakini, hawana nguvu. Kisha wakati fulani, viongozi wengine wanakamataka nafasi yao, na pengine wale viongozi hawana nia ya kusaidia watu. Lakini, hakuna mutu mwenye atakamataka nafasi ya Yesu, Mufalme wa Ufalme wa Mungu. Mungu “atasimamisha ufalme wenye hautaharibiwa hata siku moja.” (Danieli 2:44) Yesu atatawala dunia yote, na hataonyesha upendeleo. Anapenda watu, ni mupole, mwenye haki, na atafundisha watu kufuata mufano wake, ni kusema kutendeana kwa upendo, kwa upole, na kwa haki.​—Soma Isaya 11:9.

      TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

      Tuone mambo yenye inaonyesha kama Ufalme wa Mungu unapita guvernema zote za wanadamu.

      Yesu iko natawala dunia akiwa kwenye kiti yake ya ufalme mbinguni. Watawala wenzake wameikala nyuma yake. Utukufu wa Yehova unaangazia nyuma yao.

      4. Guvernema yenye nguvu sana itatawala dunia yote

      Yesu Kristo iko na nguvu kupita watawala wote wa guvernema za wanadamu. Musome Matayo 28:18, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

      • Kuko tofauti gani kati ya mamlaka ya Yesu na mamlaka ya watawala wanadamu?

      Guvernema za wanadamu zinabadilikaka-badilikaka, na kila mutawala anatawalaka tu eneo fulani mu dunia. Halafu Ufalme wa Mungu? Musome Danieli 7:14, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

      • Ufalme wa Mungu “hautaharibiwa.” Ile itakuwa na faida gani?

      • Ufalme wa Mungu utatawala dunia yote. Ile itakuwa na faida gani?

      5. Guvernema za wanadamu zinapaswa kuharibiwa

      Juu ya nini Ufalme wa Mungu unapaswa kukamata nafasi ya guvernema za wanadamu? Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

      VIDEO: Ufalme wa Mungu Ni Nini?​—Sehemu (1:41)

      • Guvernema za wanadamu zimeletea watu magumu gani?

      Musome Muhubiri 8:9, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

      • Unawaza kama Ufalme wa Mungu unapaswa kukamata nafasi ya guvernema za wanadamu? Juu ya nini?

      6. Watawala wa Ufalme wa Mungu wanatujua muzuri

      Yesu, Mufalme wetu, aliishi hapa ku dunia. Njo maana anaweza “kusikilia uzaifu wetu huruma.” (Waebrania 4:15) Wanaume na wanamuke 144000 wenye Yehova amechagula juu watawale na Yesu wanatoka “katika kila kabila na luga na watu na taifa.”​—Ufunuo 5:9.

      • Yesu na watawala wenzake wanajua magumu yetu na namna tunajisikiaka. Kujua vile, kunakutia moyo? Juu ya nini?

      Wanaume na wanamuke watiwa-mafuta wa wakati mbalimbali na desturi mbalimbali.

      Yehova amechagula wanaume na wanamuke wa hali zote juu watawale na Yesu

      7. Sheria za Ufalme wa Mungu ni za muzuri kupita sheria za guvernema za wanadamu

      Guvernema za wanadamu zinawekaka sheria juu ya kusaidia na kulinda watu. Ufalme wa Mungu nao uko na sheria zenye watu wanapaswa kufuata. Musome 1 Wakorinto 6:9-11, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

      • Unawaza dunia itakuwa namna gani wakati watu wote watafuata sheria za Mungu?a

      • Unawaza Yehova iko na haki ya kuomba watu wenye Ufalme wake utatawala wafuate sheria zake? Juu ya nini?

      • Nini njo inaonyesha kama watu wenye hawako nafuata sheria za Mungu wanaweza kubadilika?​—Ona mustari wa 11.

      Polisi anasimamisha gari. Watu wa miaka mbalimbali wanavuka barabara.

      Guvernema zinawekaka sheria juu ya kulinda na kusaidia watu. Ufalme wa Mungu nao uko na sheria za kulinda na kusaidia watu. Lakini sheria za Ufalme wa Mungu zinapita sheria za guvernema za wanadamu

      KAMA MUTU ANAULIZA: “Ufalme wa Mungu ni nini?”

      • Utamujibia nini?

      KWA KIFUPI

      Ufalme wa Mungu ni guvernema ya kweli kabisa yenye iko mbinguni, na itatawala dunia yote.

      Maulizo ya kujikumbusha

      • Nani njo Mufalme wa Ufalme wa Mungu, na atatawala na nani?

      • Juu ya nini Ufalme wa Mungu unapita guvernema zote za wanadamu?

      • Yehova anaomba watu wenye Ufalme wake utatawala wafanye nini?

      Pima kufanya hivi

      HABARI ZINGINE

      Ufalme wa Mungu uko wapi? Ona mambo yenye Yesu alifundisha.

      “Ufalme wa Mungu Uko mu Moyo Wako?” (Inapatikana ku Enternete)

      Juu ya nini Mashahidi wa Yehova wanaona kama wanapaswa kwanza kuwa washikamanifu kwa Ufalme wa Mungu kuliko kwa guvernema za wanadamu?

      Tunashikamana na Ufalme wa Mungu (1:43)

      Ona mambo yenye Biblia inasema juu ya wale 144000 wenye Yehova amechagula juu watawale na Yesu.

      “Nani Njo Wataenda Mbinguni?” (Inapatikana ku Enternete)

      Nini njo ilifanya mwanamuke fulani mwenye alikuwa mu gereza akuwe hakika kama Mungu tu njo anaweza kuleta haki ku dunia?

      “Nilifikia Kujua Mwenye Anaweza Kuleta Haki ku Dunia” (Amuka!, Mwezi wa 11, 2011)

      a Tutazungumuzia sheria fulani za Mungu mu Sehemu ya 3.

  • Ufalme wa Mungu Uko Natawala!
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
    • Somo ya 32. Yesu Kristo, Mufalme wa mbinguni, iko na fimbo ya ufalme na iko natawala dunia.

      SOMO YA 32

      Ufalme wa Mungu Uko Natawala!

      Ufalme wa Mungu ulianza kutawala mbinguni mu mwaka wa 1914. Na ni mu ile mwaka njo siku za mwisho za utawala wa wanadamu zilianza. Nini njo inatusaidia kujua vile? Tuchunguze unabii fulani wa Biblia, hali zenye ziko mu dunia tangu mwaka wa 1914, na tabia zenye watu wengi wako nazo tangu ile mwaka.

      1. Unabii wa Biblia unaonyesha nini?

      Kitabu ya Danieli ilionyesha kama Ufalme wa Mungu ungeanza kutawala ku mwisho wa kipindi yenye Biblia inaita “nyakati saba.” (Danieli 4:16, 17) Miaka mingi kisha pale, Yesu aliita ile kipindi “nyakati zenye ziliwekwa za mataifa,” na alifundisha kama ile kipindi ilikuwa haiyamalizika. (Luka 21:24) Sawa vile tutaona, zile nyakati saba zilimalizika mu mwaka wa 1914.

      2. Tangu mwaka wa 1914, hali za dunia zimekuwa namna gani, na watu wamekuwa na tabia gani?

      Wanafunzi wa Yesu walimuuliza hivi: “Ni nini itakuwa alama ya kuwapo kwako na ya umalizio wa mupangilio wa mambo?” (Matayo 24:3) Wakati Yesu aliwajibia, aliwaambia mambo yenye ingetokea wakati angeanza kutawala mbinguni. Alisema kama mu dunia mutakuwa mambo sawa vile vita, njala, na matetemeko ya inchi. (Soma Matayo 24:7.) Tena Biblia ilisema kama tabia zenye watu wangekuwa nazo mu “siku za mwisho” zingefanya maisha ikuwe nguvu kuvumilia. (2 Timoteo 3:1-5) Ile mambo yote iko naonekana sana tangu mwaka wa 1914.

      3. Juu ya nini mambo imeharibika sana ku dunia tangu Ufalme wa Mungu uanze kutawala?

      Kisha tu Yesu kuwa Mufalme wa Ufalme wa Mungu, alipigana vita na Shetani na pepo wake wachafu kule mbinguni. Alimushinda Shetani. Biblia inasema kama Shetani ‘alitupwa chini katika dunia, na malaika wake wakatupwa chini pamoja naye.’ (Ufunuo 12:9, 10, 12) Shetani iko na kasirani sana juu anajua kama ataharibiwa. Njo maana iko naletea wanadamu mateso mu dunia yote. Ile inatusaidia kuelewa juu ya nini mambo imekuwa mubaya sana ku dunia! Lakini, Ufalme wa Mungu utamaliza mambo yote ya mubaya.

      TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

      Tuone nini njo inatusaidia kujua kama Ufalme wa Mungu ulianza kutawala mu mwaka wa 1914, na tuone kujua vile kunatuchochea kufanya nini.

      4. Unabii wa Biblia unaonyesha kama Ufalme wa Mungu ulianza kutawala mu mwaka wa 1914

      Muangalie VIDEO.

      VIDEO: Ufalme wa Mungu Ulianza Kutawala mu 1914 (5:02)

      Mungu alifanya Nebukadneza, mufalme wa Babiloni ya zamani, alote ndoto yenye ilionyesha mambo yenye ingetokea. Wakati tunasoma ile ndoto na namna Danieli aliifasiria, tunaona wazi kama inazungumuzia utawala wa Nebukadneza na inazungumuzia pia Ufalme wa Mungu.​—Musome Danieli 4:17.a

      Musome Danieli 4:20-26, na kisha mutumie muchoro juu ya kujibia maulizo yenye kufuata:

      • (A) Nebukadneza aliona nini mu ndoto yake?​—Ona mustari wa 20 na 21.

      • (B) Nini njo ingefikia ile muti?​—Ona mustari wa 23.

      • (C) Nini njo ingetokea ku mwisho wa “nyakati saba”?​—Ona mustari wa 26.

      Uhusiano Kati ya Ndoto ya Nebukadneza na Ufalme wa Mungu

      UNABII (Danieli 4:20-36)

      Utawala

      (A) Muti mukubwa

      Muti ya murefu sana.

      Utawala unakatizwa

      (B) “Mukate muti huu” mupaka “nyakati saba zipite juu yake”

      Kisiki ya muti inafungwa kwa chuma na shaba.

      Utawala unarudishwa

      (C) “Ufalme wako, utakuwa wako tena”

      Muti ya murefu sana.

      Mu utimizo wa kwanza wa huu unabii . . .

      • (D) Muti ilifananisha nani? ​—Ona mustari wa 22.

      • (E) Utawala wa Nebukadneza ulikatizwa wakati gani?​—Musome Danieli 4:29-33.

      • (F) Ni mambo gani ilimufikia Nebukadneza ku mwisho wa “nyakati saba”? ​—Musome Danieli 4:34-36.

      UTIMIZO WA KWANZA

      Utawala

      (D) Nebukadneza, mufalme wa Babiloni

      Mufalme Nebukadneza anasimama kwa majivuno.

      Utawala unakatizwa

      (E) Kisha mwaka wa 606 M.K.Y., Nebukadneza anapoteza akili na haweze tena kutawala kwa miaka saba

      Nebukadneza analala chini na iko nakula majani sawa vile munyama.

      Utawala unarudishwa

      (F) Akili ya Nebukadneza inamurudilia na anaanza tena kutawala

      Mufalme Nebukadneza anainua mikono na iko naangalia juu.

      Mu utimizo wa pili wa huu unabii . . .

      • (G) Muti ilifananisha nani? ​—Musome 1 Mambo ya Nyakati 29:23.

      • (H) Utawala wao ulikatizwa wakati gani? Nini njo inatusaidia kujua kama utawala wao ulikuwa ungali unakatizwa wakati Yesu alikuwa ku dunia? ​—Musome Luka 21:24.

      • (I) Ule utawala ulirudishwa wakati gani na wapi?

      UTIMIZO WA PILI

      Utawala

      (G) Wafalme Waisraeli wenye waliwakilisha utawala wa Mungu

      Mufuatano wa wafalme wa Israeli ku kiti ya ufalme. Mwangaza uko naangaza juu yao.

      Utawala unakatizwa

      (H) Yerusalemu inaharibiwa, na kwa miaka 2520 hakuna mufalme yeyote mu Israeli mwenye anatawala

       Moto unalunguza Yerusalemu ya zamani mu mwaka wa 607 M.K.Y. Kisha pale, kunapita miaka 2,520.

      Utawala unarudishwa

      (I) Yesu anakuwa Mufalme wa Ufalme wa Mungu, na anaanza kutawala kule mbinguni

      Yesu iko mbinguni na iko natawala dunia tangu mwaka wa 1914 K.K.Y. Mwangaza uko natoka kwake.

      Nyakati saba ziko na urefu gani?

      Sehemu fulani za Biblia zinatusaidiaka kuelewa sehemu zingine. Kwa mufano, kitabu ya Ufunuo inasema kama nyakati tatu na nusu ni siku 1260. (Ufunuo 12:6, 14) Ni kusema, nyakati saba ni siku 1260 mara mbili ao siku 2520. Wakati fulani, Biblia inatumiaka neno “siku” juu ya kumaanisha mwaka. (Ezekieli 4:6) Ni vile pia kuhusu nyakati saba zenye kitabu ya Danieli inazungumuzia, ziko na urefu wa miaka 2520.

      5. Dunia imebadilika tangu mwaka wa 1914

      Muangalie VIDEO.

      VIDEO: Dunia Imebadilika Tangu 1914 (1:10)

      Yesu alionyesha mambo yenye ingetokea mu dunia wakati angeanza kutawala. Musome Luka 21:9-11, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

      • Kati ya ile mambo, kuko yenye ulishajionea ao kusikia?

      Mutume Paulo alionyesha tabia zenye watu wengi wangekuwa nazo mu siku za mwisho za utawala wa wanadamu. Musome 2 Timoteo 3:1-5, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

      • Kati ya zile tabia, kuko yenye unaona watu wako nayo leo?

       Picha: Hali mbalimbali zenye ziko mu dunia mu siku za mwisho. 1. Kiongozi wa jeshi iko ku jukwaa na iko nasema kwa sauti na anainua mikono juu. 2. Majengo imeanguka kisha tetemeko ya inchi. 3. Ndege za vita. 4. Watu wengi wenye kuvala maske wako natembea. 5. Majengo mbili ya murefu kule New York iko nalungula kisha kushambuliwa na wateroriste. 6. Mwanaume iko natumia dawa za kulewesha. 7. Bwana alishapiga bibi yake na iko namufokea. 8. Dawa za kulewesha na pombe. 9. Wanamuke wawili wenye kuvala nguo na vitu vya kujipamba vya bei wako najikamata selfi. 10. DJ iko nafurahisha watu ku concert. 11. Mutu mwenye kuwa kati ya watu wenye kuleta fujo anatupa kitu fulani yenye kutosha moto.

      6. Kujua kama Ufalme wa Mungu uko natawala kunapaswa kutuchochea kufanya jambo fulani

      Musome Matayo 24:3, 14, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

      • Ni kazi gani ya maana yenye inaonyesha kama Ufalme wa Mungu uko natawala?

      • Unaweza kufanya nini juu ya kusaidia ku ile kazi?

      Ufalme wa Mungu uko natawala, na siku yenye utaanza kutawala dunia yote iko karibu. Musome Waebrania 10:24, 25, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

      • Kadiri “tunaona siku ile kuwa inakaribia,” tunapaswa kufanya nini?

      Picha: 1. Mwanafunzi wa Biblia iko ku mukutano wa Mashahidi wa Yehova. 2. Uleule mwanafunzi anahubiria mutu fulani mwenye anajua.

      Kama unajua jambo fulani yenye inaweza kusaidia na kuokoa wengine, utafanya nini?

      KAMA MUTU ANAULIZA: “Juu ya nini Mashahidi wa Yehova wanazungumuziaka sana mwaka wa 1914?”

      • Utamujibia nini?

      KWA KIFUPI

      Unabii wa Biblia, na hali zenye ziko mu dunia, zinaonyesha kama Ufalme wa Mungu uko natawala. Tunaonyesha kama tunaamini vile, wakati tunajikaza kuhubiria watu na kufika ku mikutano.

      Maulizo ya kujikumbusha

      • Nini njo ilitokeaka ku mwisho wa nyakati saba zenye kitabu ya Danieli inazungumuzia?

      • Juu ya nini unaamini kama Ufalme wa Mungu ulianza kutawala mu mwaka wa 1914?

      • Unaweza kufanya nini juu ya kuonyesha kama unaamini kama Ufalme wa Mungu uko natawala?

      Pima kufanya hivi

      HABARI ZINGINE

      Ona mambo yenye watu wenye kujifunza historia na watu wengine wamesema juu ya mabadiliko yenye ilitokea mu dunia tangu mwaka wa 1914.

      “Wakati Tabia za Watu Ziliharibika Kabisa” (Amuka!, Mwezi wa 4, 2007)

      Ona namna unabii wenye kuwa mu Matayo 24:14 ulibadilisha maisha ya mwanaume fulani.

      Nilipenda Besiboli Kuliko Kitu Kingine!” (Munara wa Mulinzi Na. 3 2017)

      Nini njo inatusaidia kujua kama unabii wenye kuwa mu Danieli sura ya 4 unazungumuzia pia Ufalme wa Mungu?

      “Ufalme wa Mungu Ulianza Kutawala Wakati Gani? (Sehemu ya 1)” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 10, 2014)

      Nini njo inaonyesha kama “nyakati saba” zenye Danieli sura ya 4 inazungumuzia zilimalizika mu mwaka wa 1914?

      “Ufalme wa Mungu Ulianza Kutawala Wakati Gani? (Sehemu ya 2)” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 11, 2014)

      a Ona habari mbili za mwisho-mwisho zenye kuwa mu sehemu Habari Zingine mu hii somo.

  • Ufalme wa Mungu Utafanya Nini?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
    • Somo ya 33. Watu wako wanaishi mu dunia paradiso.

      SOMO YA 33

      Ufalme wa Mungu Utafanya Nini?

      Ufalme wa Mungu ulishaanza kutawala. Mu siku zenye ziko nakuya, utabadilisha mambo ku dunia. Tuone mambo fulani ya muzuri yenye Ufalme wa Mungu utafanya.

      1. Ufalme wa Mungu utafanya nini juu ya kurudisha amani na haki ku dunia?

      Yesu, Mufalme wa Ufalme wa Mungu, ataharibu watu wabaya na guvernema zote za wanadamu ku vita ya Armagedoni. (Ufunuo 16:14, 16) Ile wakati, hii maneno ya Biblia itakuwa imetimia kabisa: “Kunabakia wakati kidogo tu, waovu hawatakuwa tena.” (Zaburi 37:10) Yesu atatumia Ufalme wa Mungu juu ya kurudisha amani na haki mu dunia yote.​—Soma Isaya 11:4.

      2. Maisha itakuwa namna gani wakati mapenzi ya Mungu itafanyika ku dunia?

      Wakati Ufalme wa Mungu utatawala dunia, “wenye haki watariti dunia, na wataishi milele juu yake.” (Zaburi 37:29) Wazia unaishi mu dunia yenye hamuna watu wabaya, lakini watu wote wanamupenda Yehova na wanapendana! Hakuna mutu mwenye atagonjwa, na kila mutu ataishi milele.

      3. Ufalme wa Mungu utafanya nini kisha watu wabaya kuharibiwa?

      Kisha watu wabaya kuharibiwa, Yesu atatawala kwa miaka 1000. Mu ile miaka, yeye na watawala wenzake 144000 watasaidia wanadamu wafikie kuwa wakamilifu. Ku mwisho wa ile miaka 1000, dunia yote itakuwa paradiso ya muzuri. Na watu wote watakuwa na furaha juu watakuwa wanatii sheria za Yehova. Kisha, Yesu atarudishia Baba yake Ufalme. Jina ya Yehova ‘itatakaswa’ mu namna yenye haiyakuwaka. (Matayo 6:9, 10) Itakuwa imeonekana wazi kabisa kama Yehova ni Mutawala muzuri mwenye anahangaikia watu wake. Kisha Yehova ataharibu Shetani, pepo wake wachafu, na wengine wote wenye watakatala utawala wake. (Ufunuo 20:7-10) Mambo ya muzuri yenye Ufalme wa Mungu utafanya itaendelea milele.

      TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

      Tuone juu ya nini tunaweza kuamini kama Mungu atatumia Ufalme wake juu ya kutimiza ahadi zake.

      4. Ufalme wa Mungu utaharibu guvernema za wanadamu

      “Mwanadamu anatawala mwanadamu mwenzake ili kumuumiza.” (Muhubiri 8:9) Yehova atatumia Ufalme wake juu ya kumaliza ukosefu wa haki ku dunia.

      Musome Danieli 2:44 na 2 Watesalonike 1:6-8, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

      • Yehova na Yesu, Mwana wake, watafanya nini guvernema za wanadamu na watu wenye kuziunga mukono?

      • Umejifunza mambo gani juu ya Yehova na Yesu yenye inakufanya ukuwe hakika kama watatendea watu kwa haki?

      Yesu, Mufalme wa Ufalme wa Mungu, iko natawala Dunia paradiso.

      5. Yesu ni Mufalme muzuri sana

      Yesu, Mufalme wa Ufalme wa Mungu, atafanya mambo mingi sana juu ya kusaidia watu ku dunia. Muangalie VIDEO juu ya kuona mambo yenye Yesu alishafanya yenye inaonyesha kama iko na nia ya kusaidia watu, na kama Mungu amemupatia nguvu ya kufanya vile.

      VIDEO: Yesu Alionyesha Mambo Yenye Ufalme wa Mungu Utafanya (1:13)

      Mambo yenye Yesu alifanya wakati alikuwa ku dunia, ilionyesha mambo yenye Ufalme wa Mungu utafanya. Hapa chini kuko baraka zenye Ufalme wa Mungu utaletea wanadamu. Ni baraka gani njo unangoya kwa hamu? Musome maandiko yenye inazungumuzia zile baraka.

      WAKATI YESU ALIKUWA KU DUNIA . . .

      NA IKO MBINGUNI, YESU . . .

      • alikuwa na mamlaka juu ya hali ya hewa.​—Marko 4:36-41.

      • atafanya dunia ikuwe tena fasi ya muzuri.​—Isaya 35:1, 2.

      • alikulisha watu wengi sana. ​—Matayo 14:17-21.

      • atamaliza njala mu dunia. ​—Zaburi 72:16.

      • aliponyesha wagonjwa. ​—Luka 18:35-43.

      • atasaidia watu wote wakuwe na afya ya muzuri.​—Isaya 33:24.

      • alifufua wafu. ​—Luka 8:49-55.

      • atafufua wafu na kumaliza kifo. ​—Ufunuo 21:3, 4.

      6. Ufalme wa Mungu utafanya maisha ikuwe muzuri sana ku dunia

      Ufalme wa Mungu utarudishia wanadamu maisha yenye Yehova alipendaka wakuwe nayo. Wataishi milele ku dunia paradiso. Muangalie VIDEO juu ya kuona namna Yehova atatumia Yesu, Mwana wake, juu ya kusaidia wanadamu wakuwe na maisha yenye alipendaka wakuwe nayo.

      VIDEO: Maisha ya Muzuri Yenye Iko Natuchunga (4:38)

      Musome Zaburi 145:16, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

      • Yehova ‘atatimiza tamaa ya kila kitu chenye uzima.’ Kujua vile kunafanya ujisikie namna gani?

      WATU FULANI WANASEMAKA: “Kama tunaungana mukono, tunaweza kumaliza magumu mu dunia.”

      • Ufalme wa Mungu utamaliza magumu gani yenye guvernema za wanadamu haziwezi kumaliza?

      KWA KIFUPI

      Ufalme wa Mungu utafanya mambo yenye Mungu anapenda. Utafanya dunia yote kuwa paradiso, na watu wote mu dunia watamuabudu Yehova milele.

      Maulizo ya kujikumbusha

      • Ufalme wa Mungu utafanya nini juu ya kutakasa jina ya Yehova?

      • Nini njo inatusaidia tuamini kama Ufalme wa Mungu utafanya mambo yote yenye Biblia inasema?

      • Kati ya mambo yote yenye Ufalme wa Mungu utafanya, ya wapi njo uko nangoya kwa hamu?

      Pima kufanya hivi

      HABARI ZINGINE

      Armagedoni ni nini?

      “Vita ya Armagedoni Ni Nini?” (Inapatikana ku Enternete)

      Ona mambo yenye itafanyika mu kipindi yenye Yesu aliita “taabu kubwa.”​—Matayo 24:21

      “Taabu Kubwa Ni Nini?” (Inapatikana ku Enternete)

      Ona namna watu wanaweza kufikiri pamoja mu familia juu ya baraka zenye Ufalme wa Mungu utaleta.

      Ujiwazie mu Paradiso (1:50)

      Mu habari “Maulizo Mingi Sana Ilikuwa Nanihangaisha,” ona namna mutu mwenye alikuwa napinga serikali alipata mambo yenye alikuwa natafuta.

      “Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 1, 2012)

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine