SOMO YA 44
Mungu Anakubali Sikukuu Zote?
Yehova anapenda tufurahie maisha, na anapenda tujifurahishe wakati fulani. Lakini Mungu anakubali sikukuu zote? Kuhusu mambo ya sikukuu, tunaweza kufanya nini juu ya kuonyesha kama tunamupenda Yehova?
1. Juu ya nini Yehova hakubali sikukuu za mingi?
Unaweza kushangala kujifunza kama sikukuu za mingi, hazitegemee mafundisho ya Biblia ao zilianzishwa na wapagani. Zile sikukuu zinatokana na dini ya uongo. Zinaweza kuwa na uhusiano na mambo ya uchawi ao kutegemea fundisho yenye inaonyesha kama nafsi haikufake. Sikukuu fulani zinatokana na ushirikina ao kuaminia bahati. (Isaya 65:11) Yehova anashauria waabudu wake hivi: “Mujitenge . . . na muache kugusa kitu kichafu.”—2 Wakorinto 6:17.a
2. Yehova anaona namna gani sikukuu zenye zinatukuza wanadamu?
Yehova anatushauria tusiangukie mu mutego wa ‘kutegemea wanadamu bure.’ (Soma Yeremia 17:5.) Sikukuu fulani zinafanywa juu ya kutukuza watawala ao maaskari. Zingine zinafanywa juu ya kutukuza alama fulani za inchi ao juu ya kukumbuka siku yenye inchi fulani ilipata uhuru. (1 Yohana 5:21) Na zingine zinafanywa juu ya kutukuza matengenezo ya politike ao matengenezo ingine ya kusaidia watu. Yehova anaweza kujisikia namna gani kama tunatukuza mutu ao tengenezo yenye inatetea zaidi sana mawazo yenye haipatane na mapenzi yake?
3. Ni matendo gani inaweza kufanya Mungu asikubali sikukuu fulani?
Biblia inakataza “kunywa kupita kiasi, karamu za kupitisha mipaka, [na] mashindano ya kunywa.” (1 Petro 4:3) Ku sikukuu fulani, watu hawajizuiake na wanafanyaka mambo ya mubaya. Juu tuendelee kuwa marafiki wa Yehova, tunapaswa kuepuka kabisa ile matendo ya mubaya.
TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI
Tuone namna unaweza kumufurahisha Yehova kwa kukamata maamuzi ya muzuri juu ya sikukuu.
4. Epuka sikukuu zenye Yehova hakubali
Musome Waefeso 5:10, na kisha muzungumuzie hii maulizo:
Tunapaswa kujihakikishia nini wakati tuko naamua ikiwa tutafanya sikukuu fulani ao hapana?
Fasi kwenye unaishi, watu wanazoea kufanya sikukuu gani?
Unawaza Yehova anakubali zile sikukuu?
Kwa mufano, ulishakajiuliza Mungu anaonaka namna gani sikukuu za kuzaliwa? Hakuna fasi kwenye Biblia inaonyesha kama mutumishi fulani wa Yehova alifanyaka sikukuu ya kuzaliwa. Biblia inazungumuzia sikukuu mbili za kuzaliwa, na wenye walizifanyaka hawakukuwa namutumikia Yehova. Musome Mwanzo 40:20-22 na Matayo 14:6-10. Kisha muzungumuzie hii maulizo:
Ni jambo gani yenye inafanana mu zile sikukuu mbili za kuzaliwa?
Wakati unachunguza zile habari, unawaza Yehova anaona namna gani sikukuu za kuzaliwa?
Lakini, unaweza kujiuliza, ‘Yehova anaweza kuhuzunika kabisa kama ninafanya sikukuu ya kuzaliwa ao sikukuu ingine yenye haipatane na Biblia?’ Musome Kutoka 32:1-8. Kisha, muangalie VIDEO na muzungumuzie maulizo yenye kufuata.
Juu ya nini ni lazima tujue mambo yenye Yehova anakubali?
Tunaweza kufanya vile namna gani?
Maulizo ya kukusaidia kujua ikiwa Yehova anakubali sikukuu fulani
Inategemea mafundisho ya uongo? Juu ujue, chunguza namna ile sikukuu ilianzaka.
Inatukuza wanadamu, matengenezo ya wanadamu ao alama za inchi? Yehova njo tunapaswa kwanza kutukuza na tunaamini kama yeye njo atamaliza magumu yote yenye iko ku dunia.
Desturi na mambo yenye inafanywa wakati wa ile sikukuu inapingana na kanuni za Biblia? Tunapaswa kuendelea kuwa na mwenendo muzuri.
5. Saidia wengine waheshimie mambo yenye unaamini
Inaweza kuwa nguvu kukatala wakati wengine wanatukaza tufanye sikukuu yenye Yehova hakubali. Uwafasirie kwa uvumilivu na kwa heshima juu ya nini haufanyake sikukuu fulani. Juu ya kuona namna unaweza kufanya vile, muangalie VIDEO.
Musome Matayo 7:12, na kisha muzungumuzie hii maulizo:
Vile unasikia mu ile andiko, unapaswa kukataza watu wa familia yako wenye hawako Mashahidi kufanya sikukuu fulani?
Unaweza kufanya nini juu ya kuonyesha watu wa familia yako kama unawapenda na kuwaona kuwa wa maana hata kama haufanye sikukuu fulani pamoja nao?
6. Yehova anapenda tufurahie maisha
Yehova anapenda tukuwe najifurahisha pamoja na watu wa familia yetu na marafiki wetu. Musome Muhubiri 8:15, na kisha muzungumuzie hii ulizo:
Ni maneno gani iko mu ile andiko yenye inaonyesha kama Yehova anapenda tukuwe na furaha?
Yehova anapenda watu wake wafurahie maisha na wapitishe wakati muzuri pamoja na wengine. Muangalie VIDEO juu ya kuona namna watumishi wa Yehova wanafanyaka vile ku mikusanyiko ya kimataifa.
Musome Wagalatia 6:10, na kisha muzungumuzie hii maulizo:
Ni lazima tu tufanye sikukuu zenye watu wengi wanapenda, juu tuweze kufanyia wengine “mambo ya muzuri”?
Nini njo inaweza kukuletea furaha zaidi, kupatia wengine juu tu ni sikukuu fulani ao juu unapenda kuwapatia?
Wakati fulani, Mashahidi wengi wa Yehova wanapangaka kujifurahisha pamoja na watoto wao na hata kuwapatia zawadi. Kama uko na watoto, unaweza kuwafanyia nini juu ya kuwafurahisha?
WATU FULANI WANASEMAKA: “Namna sikukuu fulani ilianzaka, haiko njo jambo ya lazima. Ya lazima ni kufurahi pamoja na watu wa familia na marafiki.”
Na weye unawaza nini?
KWA KIFUPI
Yehova anapenda tufurahi pamoja na watu wa familia na marafiki. Lakini, anapenda pia tuepuke sikukuu zenye hakubali.
Maulizo ya kujikumbusha
Ni maulizo gani inaweza kukusaidia kujua ikiwa Yehova anakubali ao hakubali sikukuu fulani?
Unaweza kufanya nini juu ya kusaidia watu wa familia na marafiki waelewe juu ya nini haufanyake sikukuu fulani?
Nini njo inakusaidia kujua kama Yehova anapenda tufurahie maisha?
HABARI ZINGINE
Ona sikukuu fulani zenye Wakristo hawafanyake.
“Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Hawafanyake Sikukuu Fulani?” (Inapatikana ku Enternete)
Ona sababu ine zenye zinatufanya tuamini kama Mungu hakubali sikukuu za kuzaliwa.
“Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Hawafanyake Sikukuu za Kuzaliwa?” (Inapatikana ku Enternete)
Ona namna watoto wanaweza kumufurahisha Yehova wakati wengine wakonafanya sikukuu.
Wakristo wengi sana wameamua kama hawatakuwa nafanya sikukuu ya Noeli. Wanaona namna gani uamuzi wao?
“Walipata Jambo Nzuri Zaidi Kuliko Noeli” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 12, 2012)
a Ona Mafasirio Ingine ya 5 juu uone unaweza kufanya nini wakati watu wako nafanya sikukuu fulani.