Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lff somo 38
  • Uheshimie Uzima

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Uheshimie Uzima
  • Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI
  • KWA KIFUPI
  • HABARI ZINGINE
  • Biblia Inasema Nini Juu ya Kutosha Mimba?
    Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Kutosha Mimba
    Amuka!—2017
  • Unaona Uzima Kama Vile Mungu Anauona?
    Namna ya Kubakia Katika Upendo wa Mungu
  • Mungu Anapenda Tukuwe na Maisha ya Namna Gani?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
Ona Habari Zaidi
Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
lff somo 38
Somo ya 38. Bibi na bwana wanabeba mutoto wao.

SOMO YA 38

Uheshimie Uzima

Maandishi
Maandishi
Maandishi

Wakati mutu iko muzima, kuko mambo mingi yenye anaweza kufanya na kufurahia. Hata kama tuko na magumu, kuko mambo fulani yenye inaweza tu kutuletea furaha mu maisha. Tunaweza kufanya nini juu ya kuonyesha kama tunaheshimia uzima? Na juu ya nini tunapaswa kufanya vile?

1. Juu ya nini tunapaswa kuheshimia uzima?

Tunapaswa kuheshimia uzima, juu ni zawadi yenye Yehova, Baba yetu mwenye upendo anatupatia. Yeye njo “Chemchemi ya uzima,” ni kusema yeye njo aliumba vitu vyote vyenye uzima. (Zaburi 36:9) “Yeye mwenyewe anapatia watu wote uzima na pumuzi na vitu vyote.” (Matendo 17:25, 28) Yehova anatupatiaka mambo yote yenye tuko nayo lazima juu tuendelee kuishi. Na tena, anatusaidia tufurahie maisha.​—Soma Matendo 14:17.

2. Tunaweza kufanya nini juu ya kuonyesha kama tunaheshimia uzima?

Tangu wakati ulikuwa mu tumbo ya uzazi ya mama yako, Yehova alikuhangaikia. Mu Biblia, mutumishi fulani wa Yehova mwenye kuitwa Daudi, alisema hivi: “Macho yako hata yaliniona wakati nilikuwa kiini-tete.” (Zaburi 139:16) Yehova anaona uzima wako kuwa wa maana sana. (Soma Matayo 10:29-31.) Yehova anahuzunikaka sana wakati mutu anaua mwingine kimakusudi, ao wakati mutu anajiua kimakusudi.a (Kutoka 20:13) Tena, Yehova hawezi kufurahi wakati tunatia uzima wetu mu hatari ao tunatia uzima wa wengine mu hatari juu ya kukosa kuwa waangalifu. Wakati tunahangaikia uzima wetu na tunaheshimia uzima wa wengine, tunaonyesha kama tunaona uzima wenye Mungu alitupatia kuwa wa maana.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone mambo fulani yenye tunaweza kufanya juu ya kuonyesha kama tunaheshimia uzima.

3. Hangaikia afya yako

Juu tulishajitoa kwa Yehova, tunatumia maisha yetu yote juu ya kumutumikia. Ni sawa vile tunamutolea Yehova miili yetu kuwa zabihu. Musome Waroma 12:1, 2 na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Juu ya nini unapaswa kuhangaikia sana afya yako?

  • Unaweza kufanya mambo gani juu ya kuhangaikia afya yako?

Mwanamuke mwenye iko na mimba iko nazungumuza na munganga.

4. Ukuwe muangalifu juu mutu asiumie ao kufa

Biblia inatutia moyo tuepuke tabia zenye zinaweza kutia maisha mu hatari. Muangalie VIDEO juu uone mambo fulani yenye unaweza kufanya juu uepuke hatari.

VIDEO: Uhangaikie Usalama (8:34)

Musome Mezali 22:3, na kisha muzungumuzie namna weye na wengine munaweza kuhangaikia usalama . . .

  • ku nyumba.

  • ku kazi.

  • wakati muko nacheza michezo.

  • wakati muko natumia vyombo vya kusafiri, ikuwe nyie njo muko natembeza ao hapana.

Mwanaume iko najifunga mukaba wenye uko ku kiti ya gari.

5. Heshimia uzima wa mutoto mwenye hayazaliwa

Mwanamuke mwenye mimba iko nagusa-gusa tumbo yake.

Daudi alionyesha kama Yehova anaangaliaka mambo yote yenye inapitikanaka wakati mutoto iko nakomala mu tumbo ya mama yake. Musome Zaburi 139:13-17, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Yehova anaonaka kama uzima wa mutu unaanzaka wakati mama anakuwa na mimba ao wakati mutoto anazaliwa?

Sheria yenye Yehova alipatia Waisraeli wa zamani ililinda mama na mutoto wake mwenye hayazaliwa. Musome Kutoka 21:22, 23, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Yehova aliona namna gani mutu mwenye aliua bila kukusudia mutoto mwenye hayazaliwa?

  • Yehova anaweza kujisikia namna gani wakati mutu anaua kimakusudi mutoto mwenye hayazaliwa?b

  • Unaona namna gani mawazo ya Mungu juu ya ile jambo?

Muangalie VIDEO.

VIDEO: Uone Uzima Kuwa wa Maana Kama Vile Mungu Anauona (5:00)

Wakati fulani, hata mwanamuke mwenye anaheshimia uzima, anaweza kuona kama ni lazima tu atoshe mimba. Musome Isaya 41:10, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Kama mwanamuke iko nachochewa sana kutosha mimba, anapaswa kutafuta musaada kwa nani? Juu ya nini?

WATU FULANI WANASEMAKA: “Mwanamuke iko na haki ya kuamua kama atatosha mimba ao hapana, ni mwili yake.”

  • Nini njo inakuhakikishia kama Yehova anaona uzima wa mama na wa mutoto mwenye hayazaliwa kuwa wa maana?

KWA KIFUPI

Biblia inatufundisha kama tunapaswa kupenda, kuheshimia, na kulinda uzima wenye Yehova ametupatia. Ni kusema uzima wetu na uzima wa wengine.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Juu ya nini Yehova anaona uzima wetu kuwa wa maana?

  • Yehova anajisikia namna gani wakati mutu anaua mwanadamu mwenzake kimakusudi?

  • Juu ya nini na weye unaona uzima kuwa wa maana?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Tunaweza kufanya nini ili kumushukuru Yehova juu ya uzima wenye ametupatia?

Wimbo 141​—Uzima Ni Muujiza (2:41)

Ona ikiwa Mungu anaweza kusamehe mwanamuke mwenye alishakatosha mimba?

“Biblia Inasema Nini Juu ya Kutosha Mimba?” (Inapatikana ku Enternete)

Ona namna kuwa na mawazo sawa ya Mungu juu ya uzima kunaweza kutusaidia tuepuke mambo ya kujifurahisha yenye inaweza kutia uzima mu hatari.

“Inafaa Kabisa Kucheza ‘Michezo Hatari?’” (Amuka!, 8 Mwezi wa 10, 2000)

Mutu anaweza kufanya nini kama iko na mawazo ya kujiua? Ona namna Biblia inaweza kusaidia.

“Ninapenda Kufa​—Biblia Inaweza Kunisaidia Wakati Niko na Mawazo ya Kujiua?” (Inapatikana ku Enternete)

a Yehova anahangaikiaka sana watu wenye kuvunjika moyo. (Zaburi 34:18) Anaelewa kama huzuni ya mingi inaweza kufanya mutu akuwe na mawazo ya kujiua. Njo maana iko tayari kusaidia. Juu ya kuona namna Yehova anaweza kupatia mutu nguvu ya kupiganisha mawazo ya kujiua, soma habari yenye kichwa “Ninapenda Kufa​—Biblia Inaweza Kunisaidia Wakati Niko na Mawazo ya Kujiua?” yenye inapatikana mu sehemu Habari Zingine mu hii somo.

b Wale wenye walishakatosha mimba hawapaswe kuendelea kujihukumu, juu Yehova anaweza kuwasamehe. Juu ujue mambo mingi zaidi, ona habari yenye kichwa “Biblia Inasema Nini Juu ya Kutosha Mimba?” yenye inapatikana mu sehemu Habari Zingine mu hii somo.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine