Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w11 1/5 uku. 5
  • 2. Njala

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • 2. Njala
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
w11 1/5 uku. 5

2. Njala

“Kutakuwa upungufu wa chakula.”​—MARKO 13:8.

● Mwanaume mumoja anafika mu kijiji ya Quaratadji, mu inchi ya Niger. Ndugu zake, dada zake, na watu wengine fulani wa jamaa yake wametoka pia mu eneo ya mbali juu ya kukimbia njala. Lakini ule mwanaume analala yeye peke ku murago. Juu ya nini iko yeye peke? Sidi, mukubwa wa kile kijiji anasema hivi: “Hana uwezo wa kulisha [familia yake] na anashindwa kuendelea kuona vile wako wanateseka.”

USHUHUDA UNAONYESHA NINI? Mu dunia yote karibu mutu 1 kati ya watu 7 hapate chakula yenye iko nayo lazima kila siku. Hali iko mubaya zaidi mu inchi zenye kuwa kusini ya jangwa (désert) ya Sahara, kwenye mutu 1 kati ya watu 3 anashindwaka kabisa kupata chakula ya kuenea. Juu ya kuelewa muzuri ile jambo, fikiria familia yenye iko na baba, mama, na mutoto. Kama kuko chakula ya kuenea tu watu wawili, nani njo atabakia na njala? Baba? Mama? Ao mutoto? Ule ni uamuzi wenye familia fulani zinalazimika kukamata kila siku.

WATU FULANI WANASEMA NINI? Dunia inatoshaka chakula ya kuenea kila mutu. Inaomba tu kuigawanya muzuri.

ILE NI KWELI? Ni kweli kama leo watu wenye kufanya kazi ya kulima wako wanavuna chakula mingi na kuisafirisha sana kuliko zamani. Na serikali za wanadamu zinapaswa kugawanya muzuri ile chakula juu ya kumaliza njala. Lakini, hata kama zimejikaza kufanya vile kwa miaka mingi, zimeshindwa.

UNAWAZA NINI? Marko 13:8 iko inatimia? Hata kama teknolojia inaendelea sana, watu wako wanateseka kwa sababu ya njala mu dunia yote?

Mara mingi, matetemeko ya inchi na njala vinaletaka tatizo ingine yenye nayo ni alama ya siku za mwisho.

[Wazo la fungu kwenye ukurasa wa 5]

“Mutoto 1 hivi kati ya watoto 3 wenye wanakufaka kwa sababu ya ugonjwa wa pneumonie, ugonjwa wa kuhara, na magonjwa ingine angepona kama angekuwa anakula muzuri.”​—ANN M. VENEMAN, MWENYE ALIKUWA MUMOJA WA WASIMAMIZI WA UNICEF.

[Kwenye Picha Zilitoka ukurasa wa 5]

© Paul Lowe​/Panos Pictures

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine