Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w11 1/5 uku. 9
  • 6. Kazi ya kuhubiri mu dunia yote

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • 6. Kazi ya kuhubiri mu dunia yote
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ‘Muende Mufanye Wanafunzi Kutoka kwa Watu wa Mataifa Yote’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Ni Nani Wanaohubiri Habari Njema?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Habari Njema Iko Nahubiriwa Namna Gani?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Sababu gani Mashahidi wa Yehova wanahubiri nyumba kwa nyumba?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
w11 1/5 uku. 9

6. Kazi ya kuhubiri mu dunia yote

“Hii habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote yenye kuikaliwa na watu.”​—MATAYO 24:14.

● Vaiatea anaishi mu kisiwa kidogo yenye kuwa mbali sana mu Bahari ya Pasifike na watu kidogo njo wanaishi kule. Hata vile, Mashahidi wa Yehova wametembelea Vaiatea na majirani wake. Juu ya nini? Juu Mashahidi wa Yehova wanapenda kuhubiria watu wote habari njema ya Ufalme wa Mungu, hata ikuwe wanaishi wapi.

USHUHUDA UNAONYESHA NINI? Mashahidi wa Yehova wako wanahubiri habari ya Ufalme wa Mungu mu dunia yote. Mu mwaka wa 2010 tu, walipitisha saa miliare 1.6 mu kazi ya kuhubiri, na walifanya vile mu inchi 236. Kwa kukadiria, kila Shahidi alihubiri dakika 30 kila siku. Mu miaka kumi yenye ilipita, walitoa na kugawanya vichapo miliare 20 vya kusaidia watu wajifunze Biblia.

WATU FULANI WANASEMA NINI? Habari yenye iko mu Biblia inahubiriwaka tangu zamani.

ILE NI KWELI? Ni kweli kwamba watu wengi wamehubiri habari fulani zenye kuwa mu Biblia. Lakini wengi wamefanya vile mu wakati kidogo tu na mu eneo ya kidogo. Tofauti na wale watu, Mashahidi wa Yehova wanahubiri mu dunia yote kwa njia yenye kupangwa muzuri, na wameweza kuhubiria mamilioni ya watu. Matengenezo yenye nguvu na yenye haina huruma imewapinga sana, hata vile wameendelea kuhubiri. (Marko 13:13) Zaidi ya ile, Mashahidi wa Yehova hawalipwe juu ya kuhubiri. Lakini wanatoa wakati wao juu ya kuhubiri, na wanapatia watu vichapo bila kuwaomba feza. Michango ya kujipendea njo inasaidia kazi yao iendelee.

UNAWAZA NINI? “Habari njema ya Ufalme” iko inahubiriwa mu dunia yote? Kutimia kwa ule unabii kunaonyesha kama mambo ya muzuri iko karibu kutokea?

[Wazo la fungu kwenye ukurasa wa 9]

“Tutaendelea kuhubiri habari njema ya Ufalme kwa bidii, na kufanya yetu yote ili kuhubiria watu mupaka wakati Yehova atasema tuache sasa.”​—KITABU CHA MWAKA CHA MASHAHIDI WA YEHOVA CHA 2010.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine