Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w13 1/7 uku. 16
  • Maulizo juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maulizo juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Bei ya Ukombozi: Zawadi Kubwa Zaidi Kutoka kwa Mungu
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Yesu Kristo Ni Nani?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Yesu Kristo Ni Nani?
    Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
  • Zabihu ya Ukombozi Ndiyo Zawadi ya Mungu Iliyo Nzuri Kuliko Zote
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 1/7 uku. 16

MAULIZO JUU YA HABARI ZA BIBLIA YANAJIBIWA

Je, inawezekana kuishi milele?

Ni nini kinachoweza kutukomboa kutokana na kifo?

Adamu, mwanaume wa kwanza, aliishi mamia ya miaka. Lakini mwishowe, alizeeka na kufa. Tangu wakati huo, watu wamejaribu njia nyingi ili waepuke kuzeeka. Hata hivyo, hakuna mutu ambaye ameweza kuepuka kifo. Sababu gani? Adamu alizeeka na kufa kwa sababu alifanya zambi kwa kukosa kumutii Mungu. Tunazeeka kwa sababu tumeriti zambi kutoka kwa Adamu na kifo ambacho ni azabu inayotokana na zambi.​—Soma Mwanzo 5:5; Waroma 5:12.

Ili tupate uzima wa milele, tulihitaji mutu fulani alipe zabihu ya ukombozi kwa ajili yetu. (Ayubu 33:24, 25) Zabihu ya ukombozi ni bei inayolipwa ili kumuweka huru mutu aliyekuwa amefungwa, na kwa upande wetu, tulihitaji kufunguliwa kutokana na kifo. (Kutoka 21:29, 30) Yesu alilipa bei hiyo wakati alikufa kwa ajili yetu.​—Soma Yohana 3:16.

Tunaweza kufanya nini ili tupate uzima wa milele?

Si watu wote ambao watakombolewa kutokana na ugonjwa na uzee. Kwa kweli, watu ambao hawamutii Mungu kama Adamu hawatapata pendeleo la kuishi milele. Ni watu tu ambao wanasamehewa zambi zao ndio watapata uzima wa milele.​—Soma Isaya 33:24; 35:3-6.

Ili tusamehewe zambi zetu, tunapaswa kufanya jambo fulani. Ni lazima tumujue Mungu kwa kujifunza Biblia, Neno lake. Biblia inatufundisha namna nzuri ya kuishi na pia namna ya kukubaliwa na Mungu na kupata uzima wa milele.​—Soma Yohana 17:3; Matendo 3:19.

Ili kupata habari zingine, soma sura ya 3 ya kitabu hiki: Biblia Inafundisha Kabisa Nini?, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine