Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w14 1/5 uku. 3-32
  • Matabiri Fulani Yametimia, Mengine Mengi Hayakutimia

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Matabiri Fulani Yametimia, Mengine Mengi Hayakutimia
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Kuna mutu Anayeweza Kujua wakati Unaokuja?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Mwisho wa Hii Dunia Uko Karibu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2021
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 1/5 uku. 3-32
Mama na watoto wake wawili wanatembea katika barabara kuelekea mahali ambapo hawaone

KICHWA | KUNA MUTU ANAYEWEZA KUJUA WAKATI UNAOKUJA?

Matabiri Fulani Yametimia, Mengine Mengi Hayakutimia

Ungependa kujua wakati wako unaokuja? Wazo la kutafuta kujua wakati unaokuja linavutia watu wengi. Kuna watu wengi wanaotabiri matukio ya wakati unaokuja, na wanapata matokeo mbalimbali. Chunguza mambo yanayofuata:

  • WANASAYANSI wanatumia vifaa vya hali ya juu na feza nyingi sana ili kutabiri mambo mbalimbali, kwa mufano matokeo ya kuchafuka kwa hewa juu ya dunia na ikiwa mvua itanyesha kesho katika eneo lenu.

  • WACHUNGUZI WA HALI YA JUU wanatabiri mabadiliko katika biashara na siasa. Warren Buffett, mumoja kati ya matajiri sana wa duniani, aliweza kutabiri bila kukosea mabadiliko katika biashara na hivyo watu fulani walimuita nabii. Nate Silver, muchunguzi mwengine, alifasiria hesabu fulani zilizomusaidia kutabiri juu ya kila kitu kuanzia siasa za inchi ya Amerika mupaka zawadi za sinema za Hollywood.

  • MAANDISHI YA ZAMANI yameelezwa kuwa unabii. Watu fulani wanaona kuwa maandishi yasiyo wazi ya Michel de Notredame (Nostradamus) ya kati ya mwaka wa 1501 na 1600 yanatimizwa leo. Kalenda ya Wamaya iliisha tarehe 21 Mwezi wa 12, 2012; watu fulani walieleza kwamba tarehe hiyo kutakuwa matukio ya uharibifu mukubwa duniani.

  • VIONGOZI WA DINI wakati fulani wanatabiri kwamba kutakuwa matukio mabaya sana duniani pote ili kuonya watu na kupata wafuasi. Harold Camping, nabii aliyetabiri maangamizi tu pamoja na wafuasi wake walitangaza sana kwamba dunia ingeharibiwa katika mwaka wa 2011. Lakini dunia ingali mupaka leo.

  • WACHAWI FULANI wanasema kwamba wana uwezo wa pekee wa kutabiri mambo ya wakati unaokuja. Edgar Cayce na Jeane Dixon wote wawili walitabiri bila kukosea mambo fulani juu ya matukio kati ya mwaka wa 1901 na 2000. Kila mumoja wao alitabiri pia mambo mengi yenye hayakutimia. Kwa mufano, Dixon alitabiri kwamba Vita ya Tatu ya Ulimwengu ingetokea katika mwaka wa 1958, na Cayce alitabiri kwamba muji wa New York ungezama ndani ya bahari katika mwaka wa 1975 hivi.

Kuna njia yoyote yenye kutegemeka ya kujua wakati unaokuja? Ulizo hilo ni lenye kufaa. Ikiwa ungekuwa na uwezo wa kuona mbele ya wakati matukio ya wakati unaokuja, maisha yako yangekuwa tofauti.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine