Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w15 1/10 uku. 3
  • Sababu Gani Watu Wanasali?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Sababu Gani Watu Wanasali?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Kumukaribia Mungu Karibu Katika Sala
    Mungu Anataka Nini Kwetu?
  • Sala Ni Zawadi Kutoka kwa Mungu
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Go Rapela Modimo go Nyoko go Šutetsa Thina Naye
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Unaweza Kusali Namna Gani Juu Mungu Akusikie?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2021
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 1/10 uku. 3

HABARI KUBWA | KUSALI KUNALETA FAIDA FULANI?

Sababu Gani Watu Wanasali?

“Nilikuwa mutumwa wa michezo ya feza. Nilikuwa ninasali ili nipate ushindi wa utajiri mwingi. Lakini jambo hilo halikutokea hata siku moja.”—Samuel,a inchi ya Kenya.

“Kwenye masomo tulipaswa tu kurudilia sala zenye ­tulikuwa tumefundishwa na kuweka katika akili.”—Teresa, inchi ya Ufilipino.

“Ninasali wakati niko na magumu. Ninasali ili kuomba musamaha wa zambi na ili nikuwe Mukristo muzuri.”—Magdalene, inchi ya Ghana.

1. Mwanaume anasali kwenye meza ya michezo yenye kuzunguka; 2. Mutoto mwanamuke anasali kwenye masomo; 3. Mwanamuke anasali

Maneno ya Samuel, Teresa, na Magdalene, yanaonyesha kama kuko sababu nyingi zenye zinafanya watu wasali, sababu fulani ni za muzuri kupita zingine. Sala za watu fulani zinatoka moyoni na zingine hazitoke moyoni kabisa. Hata hivyo, iwe watu fulani wanasali ili kuweza mashindano (examen) kwenye masomo, ao kusali ili kikundi cha muchezo chenye wanapenda kipate ushindi, ili wapate muongozo wa Mungu katika maisha yao ya familia ao kwa sababu zingine nyingi, mamilioni ya watu wanaona kuwa ni lazima kusali. Kwa kweli, uchunguzi mbalimbali unaonyesha kama hata watu fulani wenye hawana dini yoyote wanasali kwa ukawaida.

Unasali wakati fulani? Ikiwa jibu ni ndiyo, unasali kwa ajili ya mambo gani? Iwe uko na tabia ya kusali ao hapana, unaweza kujiuliza hivi: ‘Kusali kunaleta faida fulani? Kuko mutu fulani mwenye kusikiliza sala?’ Muandikaji mumoja alionyesha kama sala ni “aina fulani ya matunzo . . . kama vile kuzungumuza na samaki-rafiki.” Waganga fulani wako pia na mawazo kama hayo, wanaita sala kuwa “aina ingine ya matunzo.” Watu wenye kusali wanafanya zoezi fulani lenye halina maana, ao wanapata tu matunzo fulani kupitia zoezi hilo?

Hapana. Biblia inaonyesha kuwa sala iko na faida nyingi, haiko tu aina fulani ya matunzo. Tena, Biblia inatuonyesha kama kuko mutu mwenye anasikiliza sala zenye kutolewa kwa njia ya muzuri na kwa ajili ya mambo yenye kufaa. Jambo hilo ni kweli? Tuone mambo yenye kuhakikisha hilo.

a Majina fulani yamebadilishwa.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine