Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w17 Mwezi wa 5 uku. 31-32
  • “Mioyo Yetu Ilijaa Bidii na Upendo Kuliko Wakati Mwingine Wowote”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Mioyo Yetu Ilijaa Bidii na Upendo Kuliko Wakati Mwingine Wowote”
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
w17 Mwezi wa 5 uku. 31-32

VITU VYA MAANA SANA VYA HISTORIA YETU

Jumba lenye kujaa watu kwenye mukusanyiko katika Cedar Point, Ohio, mwaka wa 1922

“Mioyo Yetu Ilijaa Bidii na Upendo Kuliko Wakati Mwingine Wowote”

JOTO ilikuwa imeanza kuongezeka siku hiyo ya Tano asubuhi Mwezi wa 9, 1922 wakati watu 8000 walikusanyika katika jumba moja. Musimamizi wa mukutano alitangaza kwamba kwenye programu hiyo ya pekee, mutu yeyote angeweza kuondoka ikiwa anapenda, lakini hakuna mutu mwenye angeruhusiwa kurudia tena katika jumba hilo.

Nyimbo ziliimbwa wakati wa “Kipindi cha Kutoa Sifa,” kisha Ndugu Joseph Rutherford alisimama kwenye kinara cha musemaji. Wasikilizaji wengi walingojea kwa hamu mambo yenye atasema. Wahuzuriaji fulani walitembea-tembea katika jumba kwa sababu ya joto. Musemaji aliwaomba kwa upole wakae na kusikiliza. Wakati alianza kutoa hotuba, mutu yeyote aliona nguo kubwa yenye kukunjwa muzuri yenye ilifungiwa juu katika jumba hilo?

Ndugu Rutherford alizungumuzia hotuba yenye kichwa “Ufalme wa mbinguni uko karibu.” Kwa saa moja na nusu, sauti yake yenye nguvu ilisikika kabisa katika jumba hilo wakati alikuwa anazungumuzia namna manabii wa zamani walitangaza bila woga kuja kwa Ufalme. Wakati alifikia mwisho wa hotuba yake, aliuliza hivi: “Je! Munaamini kwamba Mufalme wa utukufu ameanza kutawala?” Wahuzuriaji walijibia hivi kwa sauti kubwa: “Ndiyo!”

Ndugu Rutherford alisema hivi kwa sauti kubwa: “Basi murudie katika shamba, ninyi wana wa Mungu aliye juu zaidi! Mutazame, Mufalme anatawala! Ninyi ndio mawakili wake. Kwa hiyo, mutangaze, mutangaze, mutangaze.”

Wakati huo, nguo yenye ilifungiwa juu katika jumba hilo, ilifunguliwa muzuri na kuonyesha maneno haya mafupi: “Tangazeni Mufalme na Ufalme.”

Ray Bopp alikumbuka hivi: “Wahuzuriaji walifurahi sana.” Anna Gardner alieleza namna “nguzo za jumba hilo zilitikisika kwa sababu ya kupiga mikono sana.” Fred Twarosh alisema hivi; “Wahuzuriaji wote walisimama mara moja.” Evangelos Scouffas alisema hivi: “Ilikuwa kama vile nguvu fulani ya ajabu ilitusimamisha kutoka kwenye viti vyetu, na tukasimama na macho yetu yalikuwa yenye kujaa machozi.”

Wengi kwenye mukusanyiko huo walikuwa tayari wanahubiri kwa bidii habari njema ya Ufalme. Lakini sasa walijisikia kuwa wamechochewa upya kufanya kazi ya kuhubiri. Ethel Bennecoff alieleza kuwa Wanafunzi wa Biblia walisonga mbele na “mioyo [yao] ilijaa bidii na upendo mwingi kuliko wakati mwingine wowote.” Odessa Tuck, alikuwa na miaka 18 wakati huo, na wakati alitoka kwenye mukusanyiko huo alikuwa ameazimia kujibia ombi hili: “Nani ataenda?” Alisema hivi: “Sikujua mahali pa kuhubiri, namna ya kufanya hivyo, ao mambo ya kuhubiri. Jambo moja lenye nilijua ni kwamba nilipenda kuwa kama Isaya, mwenye alisema hivi: ‘Mimi hapa! Nitume mimi!’” (Isaya 6:8) Ralph Leffler alisema hivi: “Siku hiyo yenye kujulikana sana, ilikuwa mwanzo wa kampanye ya kutangaza Ufalme yenye imeenea katika dunia yote leo.”

Ndiyo sababu mukusanyiko wenye ulifanywa mwaka wa 1922 katika Cedar Point, Ohio, unaendelea kuwa tukio la maana sana katika utendaji wa kiteokrasi! George Gangas alisema hivi: “Mukusanyiko huo ulinichochea nisikose hata kidogo mukusanyiko hata mumoja.” Kwa kadiri angeweza kukumbuka, hakukosa mukusanyiko hata mumoja. Julia Wilcox aliandika hivi: “Ninashindwa kueleza kabisa furaha yenye ninapata kila wakati mukusanyiko wa mwaka wa 1922 katika Cedar Point unazungumuziwa katika vichapo vyetu. Sikuzote ninasema hivi, ‘Asante Yehova, kwa kuniruhusu nikuwe hapo.’”

Vilevile, kama vile ndugu na dada hao, wengi kati yetu tunakumbuka pia mambo ya maana ya mukusanyiko mumoja wenye ulifurahisha kabisa mioyo yetu, na kuongeza bidii na upendo wetu kwa Mungu wetu mukubwa na kwa Mufalme wake. Wakati tunaendelea kufikiria mambo hayo, sisi pia tunachochewa kusema hivi: “Asante Yehova, kwa kuniruhusu nikuwe hapo.”

Alama Hizo Zilikuwa Fumbo

Herufi “ADV” zilipatikana kila mahali, kwenye miti, kwenye majengo, na hata kwenye programu ya mukusanyiko! Watu wenye walikuwa wamekuja kuhuzuria mukusanyiko huo, walikuwa na hamu sana ya kujua maana ya alama hizo.a

“Kwenye kila nguzo, na mulango kulikuwa karte za mweupe na herufi kubwa ADV zilikuwa zimechapwa kwa rangi nyeusi kwenye karte hizo. Tuliuliza ikiwa herufi hizo zinamaanisha nini, lakini ilionekana kuwa hakuna mwenye alijua, ao ikiwa kuko mwenye alijua, hangetuambia.”—Edith Brenisen.

a Alama hizo zingali fumbo. Mupaka leo, hakuna picha za alama hizo zenye zimepatikana katika vitu vya maana vya historia yetu.

Sala Inajibiwa Mahali Kwenye Hakuonekane

Arthur na Nellie Claus walifika mbele ya wakati ili wapate nafasi za muzuri za kukaa. Arthur alisema hivi: “Nilikuwa ninasikiliza kwa uangalifu kila neno.” Mara moja tumbo yake ikaanza kuuma. Bila kupenda, alitoka katika jumba na alijua kama hangeweza kurudia tena. Mukaribishaji mumoja alimuuliza hivi: “Namna gani unaweza kutoka wakati kama huu?” Arthur alijua kama alipaswa kutoka.

Wakati alirudia, Arthur alisikia watu wanapiga sana mikono katika jumba. Wakati alikuwa anatafuta nafasi kwenye angeweza kusikiliza mambo yenye yalikuwa yanasemwa katika jumba hilo, akavumbua nafasi moja kwenye anaweza kupanda ili aingie kwenye sehemu ya juu ya jumba hilo yenye ilikuwa kwenye urefu wa metre karibu 5. Kisha akajielekeza kwenye sehemu ya kuingiza mwangaza katika jumba hilo yenye ilikuwa na madirisha yenye kufunguliwa.

Hapo, Arthur alikutana ndugu fulani wenye kuwa na wasiwasi, wenye kuangalia musemaji mwenye alikuwa chini yao. Walikuwa wamepewa maagizo ya kukata kwa wakati mumoja kamba mbalimbali ili kuachilia nguo yenye ilikuwa na maandishi. Lakini ili wakate kwa wakati mumoja kamba hizo zote, walikuwa na lazima ya kisu kingine. Arthur alikuwa na kisu ya makali katika mufuko wake? Walifurahi sana kuona kuwa alikuwa na kisu hiyo. Arthur na wale wengine kila mumoja alibakia upande wake na kungojea wakati wenye waliambiwa kuwa walipaswa kutenda. Wakati Ndugu Rutherford alisema kwa mara ya pili “Mutangaze!” walipaswa kukata kamba hizo.

Watu wenye walijionea jambo hilo, walieleza namna nguo hiyo yenye ilikuwa na maandishi yenye rangi tatu ilishuka muzuri. Nguo hiyo ilikuwa na picha ya Yesu katikati.

Kisha hapo, ndugu hao walimuambia Arthur kama walitumia ngazi ili kupanda kwenye sehemu ya juu ya jumba na kisha ngazi hiyo ilikuwa imechukuliwa. Kwa sababu hawangeenda kutafuta musaada, walisali ili Yehova atume ndugu mwenye kuwa na kisu. Ndugu hao walikuwa hakika kuwa Yehova alijibia sala yao kwa njia yenye kufurahisha zaidi.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine