Kujikumbusha Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maulizo yanayofuata yatatumiwa kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi katika juma tokea tarehe 27, mwezi wa 12, 2010. Kwa muda wa dakika 20 mwangalizi wa shule ataongoza kujikumbusha kunakotegemea habari zilizozungumziwa tokea tarehe 1 mwezi wa 11 mpaka tarehe 27 mwezi wa 12, 2010.
1. Tunaweza kujifunza nini kutokana na maneno ya sifa yaliyoimbwa na Walawi yaliyo kwenye 1 Mambo ya Nyakati 16:34? [w02 1/15 uku. 11 fu. 6-7]
2. Je, andiko la 1 Mambo ya Nyakati 22:8 linaonyesha kwamba vita ambavyo Mfalme Daudi alipigana vilikuwa visivyofaa, kwa kuwa Yehova hakutaka yeye ajenge nyumba Yake? Eleza. [it-2-F uku. 869 fu. 10]
3. Mfalme Daudi alitaka mwana wake Sulemani awe na maoni gani kumhusu Mungu? (1 Nya. 28:9) [w08 10/15 uku. 7 fu. 18]
4. Kwa nini lilikuwa jambo lenye kufaa kutumia mfano wa ng’ombe-dume katika ujenzi wa sehemu ya chini ya bahari ya kuyeyushwa? (2 Nya. 4:2-4) [w05 12/1 uku. 19 fu. 3; w98 6/15 uku. 16 fu. 17]
5. Je, sanduku la agano lilikuwa tu na yale mabamba mawili ya mawe, ao lilikuwa pia na vitu vingine? (2 Nya. 5:10) [w06 1/15 uku. 31]
6. Sulemani alimaanisha nini alipomwomba Yehova asikilize maombi ya kila mutu ambaye angeweza “kusali kuelekea nyumba hii”? (2 Nya. 6:21, 32, 33) [it-1-F uku. 36 fu. 5]
7. Usemi “agano la chumvi” kwenye 2 Mambo ya Nyakati 13:5 unamaanisha nini? [w05 12/1 uku. 20 fu. 2; it-2-F uku. 921 fu. 5]
8. Namna gani 2 Mambo ya Nyakati 17:9, 10 inaweza kutumiwa kuhusiana na kanuni yetu ya kuhubiri? [w09 6/15 uku. 12 fu. 7]
9. Namna gani watu wa Mungu watatenda kulingana na 2 Mambo ya Nyakati 20:17? [w03 6/1 uku. 21-22 fu. 14-17]
10. Tunaweza kujifunza nini kutokana na habari ya kiburi cha Mfalme Uzia? (2 Nya. 26:15-21) [w99 12/1 uku. 26 fu. 1-2]