Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w20 Mwezi wa 5 uku. 8-11
  • Wafalme Wenye Kushindana Katika Wakati wa Mwisho

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Wafalme Wenye Kushindana Katika Wakati wa Mwisho
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Habari za Kufanana na Zile
  • “Mufalme wa Kaskazini” Katika Wakati wa Mwisho
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Yehova Anafunua Mambo Ambayo “Lazima Yatendeke Upesi”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Ni Nani “Mufalme wa Kaskazini” Leo?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Kitabu ya Ufunuo—Iko na Maana Gani kwa Maadui wa Mungu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
w20 Mwezi wa 5 uku. 8-11

Wafalme Wenye Kushindana Katika Wakati wa Mwisho

Unabii fulani wenye kuonyeshwa katika muchoro huu unazungumuzia matukio yenye ilitokea wakati uleule. Unabii huo wote unaonyesha kama tunaishi “wakati wa mwisho.”​—Da. 12:4.

Muchoro wenye kuonyesha unabii mbalimbali juu ya mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini na namna walitambuliwa kuanzia mwaka wa 1870 mupaka leo.
  • Muchoro wa 1 katika ya michoro 4, unaonyesha unabii mbalimbali wenye ulitimia kwa wakati uleule katika wakati wa mwisho na kuanzia mwaka 1870 hivi mupaka 1918. Wakati wa mwisho unaanzia mu mwaka 1914 na kuendelea. Unabii wa 1: Munyama wa pori mwenye vichwa saba anatokea wa kwanza katika mufuatano wa matukio kwenye muchoro. Wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, kichwa cha saba cha munyama huyo kinaumizwa. Kuanzia mwaka wa 1917, kichwa cha saba kinapona na ule munyama wa pori anakuwa na nguvu tena. Unabii wa 2: Kunakuwa uwezekano wa kutambua mufalme wa kaskazini na mufalme wa kusini mu mwaka wa 1870. Mufalme wa kaskazini anatokea tena mu mwaka wa 1871, akiwa Ujerumani. Mufalme wa kusini anatambuliwa kwanza kuwa Uingereza, lakini mu mwaka wa 1917 Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika inakamata ile nafasi. Unabii wa 3: Kuanzia 1870, Charles Russell na wenzake wanatambuliwa kuwa ule ‘mujumbe.’ Kuanzia 1881 gazeti ‘Le Phare de la Tour de Sion’ linatia moyo wasomaji wake wahubiri habari njema. Unabii wa 4: Kuanzia 1914, mavuno. Magugu inatenganishwa na ngano. Unabii wa 5: Kuanzia 1917, vikanyangio vya chuma na udongo vinatokea. Muchoro unaonyesha pia: Matukio ya ulimwengu kuanzia 1914 mupaka 1918, Vita ya Kwanza ya Ulimwengu. Matukio yenye iligusa watu wa Yehova: Kuanzia 1914 mupaka 1918, wanafunzi wa Biblia katika Uingereza na Ujerumani wanafungwa. Katika mwaka wa 1918, ndugu wa makao makubwa mu Inchi ya Amerika wanafungwa.
    Unabii wa 1.

    Maandiko Ufu. 11:7; 12:13, 17; 13:1-8, 12

    Unabii “Munyama wa pori” ametawala dunia kwa maelfu ya miaka. Katika wakati wa mwisho, kichwa chake cha saba kinaumizwa. Kisha, kichwa chake kinapona na “dunia yote” inafuata ule munyama. Shetani anatumia ule munyama ili “kupigana vita na wale wenye kubakia.”

    Utimizo Kisha Garika, serikali zenye kumupinga Yehova zinatokea. Kisha miaka mingi, wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, serikali ya Uingereza inakuwa zaifu sana. Inapata nguvu tena wakati inajiunga na Inchi ya Amerika. Zaidi sana wakati wa mwisho, Shetani anatumia serikali zote za dunia ili kutesa watu wa Mungu.

  • Unabii wa 2.

    Maandiko Da. 11:25-45

    Unabii Mufalme wa kaskazini na mufalme na kusini wanapigania mamlaka wakati wa mwisho.

    Utimizo Ujerumani inapigana na Uingereza na Amerika. Mu mwaka wa 1945, Muungano wa Sovieti na inchi zenye kuunga mukono muungano huo zinakuwa mufalme wa kaskazini. Mu mwaka wa 1991, Muungano wa Sovieti unaanguka, na kisha, serikali ya Urusi na inchi zenye kuiunga mukono zinakuwa mufalme wa kaskazini.

  • Unabii wa 3.

    Maandiko Isa. 61:1; Mal. 3:1; Lu. 4:18

    Unabii Yehova anatuma “mujumbe” wake ili ‘afungue njia’ mbele Ufalme wa Kimasiya usimamishwe. Ule “mujumbe” anaanza ‘kutangazia wapole habari njema.’

    Utimizo Kuanzia mwaka wa 1870, Russell na wenzake wanatumika kwa bidii ili kufasiria watu kweli za Biblia. Katika miaka ya 1880, wanaanza kukazia kama watumishi wa Mungu wanapaswa kuhubiri. Wanachapisha habari kama vile “Wahubiri 1 000 Wanahitajiwa” na “Mumetiwa Mafuta ili Kuhubiri.”

  • Unabii wa 4.

    Maandiko Mt. 13:24-30, 36-43

    Unabii Mutu fulani anapanda ngano mu shamba. Kisha, adui fulani anapanda magugu mu shamba hilo. Magugu inakomaa na kufunika ngano. Wakati wa mavuno, magugu inatenganishwa na ngano.

    Utimizo Kuanzia mwaka wa 1870, tofauti kati ya Wakristo wa kweli na Wakristo wa uongo inaanza kuonekana wazi zaidi na zaidi. Katika wakati wa mwisho, Wakristo wa kweli wanakusanywa na kutenganishwa na Wakristo wa uongo.

  • Unabii wa 5.

    Maandiko Da. 2:31-33, 41-43

    Unabii Vikanyangio vya chuma na udongo vya sanamu ya munyama yenye kutengenezwa na metali mbalimbali.

    Utimizo Udongo unafananisha watu wa kawaida, wenye Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika inatawala, wenye wanapinga serikali hiyo. Watu hao wanafanya serikali hiyo ikuwe zaifu na ishindwe kutawala kwa mamlaka yenye kuwa nguvu kama chuma.

  • Muchoro wa 2 na wa 4, unaonyesha unabii wenye ulitokea kwa wakati uleule katika wakati wa mwisho na katika kipindi kuanzia 1919 hivi mupaka 1945. Mufalme wa kaskazini anatambuliwa kuwa Ujerumani mupaka 1945. Mufalme wa kusini anatambuliwa kuwa Serikali Kubwa ya Uingereza na Amerika. Unabii wa 6: Katika mwaka 1919, Wakristo watiwa-mafuta wanakusanywa katika kutaniko lenye kusafishwa. Kuanzia 1919, kazi ya kuhubiri inafanywa zaidi na zaidi na inaendelea. Unabii wa 7: Katika mwaka wa 1920, Ushirika wa Mataifa unaanzishwa mupaka mwanzo wa Vita ya Pili ya Ulimwengu. Muchoro unaonyesha pia: Unabii wa 1, munyama wa pori mwenye vichwa saba, anaendelea. Unabii wa 5, vikanyangio vya chuma na udongo, vinaendelea. Matukio ya ulimwengu kuanzia 1939 mupaka 1945, Vita ya Pili ya Ulimwengu. Matukio yenye iligusa watu wa Yehova: Katika inchi ya Ujerumani kuanzia 1939 mupaka 1945, Mashahidi zaidi ya 11 000 wanafungwa. Katika inchi ya Uingereza kuanzia 1939 mupaka 1945, Mashahidi karibu 1 600 wanafungwa. Katika Inchi ya Amerika kuanzia 1940 mupaka 1944, vikundi vya watu wenye jeuri vinashambulia Mashahidi mara zaidi ya 2 500.
    Unabii wa 6.

    Maandiko Mt. 13:30; 24:14, 45; 28:19, 20

    Unabii “Ngano” inakusanywa mu “depo” na “mutumwa muaminifu na mwenye busara” anawekwa juu ya “watumishi wa nyumbani.” Kazi ya kuhubiri “habari njema ya Ufalme” inaanza kufanywa katika “dunia yote yenye kuikaliwa na watu.”

    Utimizo Mu mwaka wa 1919, mutumwa muaminifu anawekwa ili asimamie watu wa Mungu. Kuanzia wakati huo, Wanafunzi wa Biblia wanahubiri kwa bidii sana. Leo, Mashahidi wa Yehova wanahubiri mu inchi zaidi ya 200 na wanachapisha vichapo vyenye kutegemea Biblia mu luga zaidi ya 1 000.

  • Unabii wa 7.

    Maandiko Da. 12:11; Ufu. 13:11, 14, 15

    Unabii Munyama wa pori mwenye pembe mbili anaambia watu wafanye “sanamu ya munyama wa pori,” na anapatia “pumuzi ile sanamu.”

    Utimizo Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika inaanzisha Ushirika wa Mataifa. Mataifa ingine inaunga mukono ushirika huo. Kisha, mufalme wa kaskazini anajiunga pia na Ushirika wa Mataifa, lakini ni kuanzia tu mwaka wa 1926 mupaka mwaka wa 1933. Watu waliamini kama Ushirika wa Mataifa njo utaleta amani mu dunia, jambo lenye Ufalme wa Mungu tu njo unaweza kufanya. Na wanaamini vile pia kuhusu Umoja wa Mataifa wenye ulianzishwa kisha.

  • Muchoro wa 3 kati ya michoro 4, unaonyesha unabii wenye ulitokea kwa wakati uleule katika wakati wa mwisho na kuanzia 1945 mupaka 1991. Mufalme wa kaskazini anatambuliwa kuwa Muungano wa Sovieti na serikali zenye kuunga mukono muungano huo mupaka 1991, na kisha pale mufalme wa kaskazini anatambuliwa kuwa serikali ya Urusi pamoja na serikali zenye kumuunga mukono. Mufalme wa kusini anatambuliwa kuwa Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika. Unabii wa 8: Moshi wenye kutokezwa na bombe ya atomu, unaonyesha kama Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika ilileta uharibifu mukubwa sana. Unabii wa 9: Umoja wa Mataifa unaanzishwa mu mwaka wa 1945, unakamata nafasi ya Ushirika wa Mataifa. Muchoro unaonyesha pia: Unabii wa 1, munyama wa pori mwenye vichwa saba, anaendelea. Unabii wa 5, vikanyangio vya chuma na udongo, vinaendelea. Unabii wa 6, katika mwaka wa 1945 kulikuwa wahubiri zaidi ya 156 000. Katika mwaka wa 1991, kulikuwa wahubiri zaidi ya 4 278 000. Matukio yenye iligusa watu wa Yehova: Katika Muungano wa Sovieti kuanzia 1945 mupaka miaka ya 1950, maelfu ya Mashahidi walipelekwa Siberia.
    Unabii wa 8.

    Maandiko Da. 8:23, 24

    Unabii Mufalme mwenye kuonekana kuwa mukali analeta “uharibifu kwa njia ya ajabu.”

    Utimizo Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika imeua watu wengi na kuleta uharibifu mukubwa. Kwa mufano, wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu, Inchi ya Amerika ilileta uharibifu mukubwa sana kuliko uharibifu wowote wenye ulikuwa umekwisha kutokea wakati iliangusha bombe mbili za atomu juu ya taifa lenye lilikuwa adui wa Uingereza na Amerika.

  • Unabii wa 9.

    Maandiko Da. 11:31; Ufu. 17:3, 7-11

    Unabii Munyama “mwenye rangi nyekundu yenye kungaa” mwenye kuwa na pembe kumi anatoka mu abiso na yeye njo mufalme wa munane. Kitabu cha Danieli kinaita ule mufalme kuwa “chukizo lenye linaleta uharibifu.”

    Utimizo Ushirika wa Mataifa unaacha kufanya kazi wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu. Kisha vita hiyo, Umoja wa Mataifa ‘unasimamishwa’ ao unaundwa. Watu waliamini kama Umoja wa Mataifa njo utaleta amani mu dunia, jambo lenye Ufalme wa Mungu njo unaweza kufanya. Ni vile pia waliamini kuhusu Ushirika wa Mataifa wenye ulikuwa mbele yake. Umoja wa Mataifa utashambulia dini.

  • Muchoro wa 4 kati ya michoro 4, unaonyesha unabii wenye ulitokea kwa wakati uleule katika wakati wa mwisho na siku za leo mupaka Armagedoni. Mufalme wa kaskazini anatambuliwa kuwa Urusi na serikali zenye kuiunga mukono. Mufalme wa kusini anatambuliwa kuwa Serikali Kubwa Ulimwengu ya Uingereza na Amerika. Unabii wa 10: Viongozi wa ulimwengu wanatangaza ‘amani na usalama.’ Kisha pale, taabu kubwa inaanza. Unabii wa 11: Mataifa inashambulia matengenezo ya dini za uongo. Unabii wa 12: Serikali za ulimwengu zinashambulia watu wa Mungu. Mabaki ya watiwa-mafuta wanapelekwa mbinguni. Unabii wa 13: Armagedoni. Ule mwenye kukaa juu ya farasi mweupe anakamilisha ushindi wake. Munyama wa pori mwenye vichwa saba anaharibiwa; sanamu kubwa inapondwa-pondwa kwenye vikanyangio vyake vya chuma na udongo. Muchoro unaonyesha pia: Unabii wa 1, munyama wa pori mwenye vichwa saba, anaendelea mupaka Armagedoni. Unabii wa 5, vikanyangio vya chuma na udongo, vinaendelea mupaka Armagedoni. Unabii wa 6, leo kuko wahubiri zaidi ya 8 580 000. Matukio yenye inagusa watu wa Yehova: Katika mwaka wa 2017, wakubwa wa serikali ya Urusi wanafunga Mashahidi wa Yehova na wananyanganya majengo ya tawi.
    Unabii wa 10 na wa 11.

    Maandiko 1 Te. 5:3; Ufu. 17:16

    Unabii Mataifa inatangaza “amani na usalama,” na “zile pembe kumi” na “ule munyama wa pori” wanashambulia “ule kahaba” na kumuharibu. Kisha, mataifa yote inaharibiwa.

    Utimizo Mataifa itasema kama imeleta amani na usalama mu dunia. Kisha, mataifa yenye kuunga mukono Umoja wa Mataifa itaharibu matengenezo ya dini za uongo. Tukio hilo litakuwa mwanzo wa taabu kubwa. Ile taabu itamalizika wakati Yesu ataharibu ulimwengu wote wa Shetani ku Armagedoni.

  • Unabii wa 12.

    Maandiko Eze. 38:11, 14-17; Mt. 24:31

    Unabii Gogu anashambulia inchi ya watu wa Mungu. Kisha, malaika wanakusanya wale “wenye kuchaguliwa.”

    Utimizo Mufalme wa kaskazini na serikali zingine za dunia, wanashambulia watu wa Mungu. Wakati fulani kisha shambulizi hilo kuanza, mabaki ya watiwa-mafuta wanapelekwa mbinguni.

  • Unabii wa 13.

    Maandiko Eze. 38:18-23; Da. 2:34, 35, 44, 45; Ufu. 6:2; 16:14, 16; 17:14; 19:20

    Unabii “Ule mwenye kukaa” juu ya “farasi mweupe” anakamilisha “ushindi wake” kwa kuharibu Gogu na jeshi lake. “Ule munyama wa pori” ‘anatupwa ndani ya ziwa la moto,’ na ile sanamu kubwa inapondwa-pondwa.

    Utimizo Yesu, Mufalme mwenye kutawala Ufalme wa Mungu, anakuja kuokoa watu wa Mungu. Yeye na watawala wenzake 144 000 na majeshi yake ya malaika, wanaharibu muungano wa mataifa. Huo utakuwa mwisho wa ulimwengu wa Shetani.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine