Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp21 na. 1 uku. 3-4
  • Mambo Yenye Watu Wanasemaka Juu ya Sala

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mambo Yenye Watu Wanasemaka Juu ya Sala
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2021
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Namna ya Kumukaribia Mungu Katika Sala
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Sala Ni Zawadi Kutoka kwa Mungu
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Go Rapela Modimo go Nyoko go Šutetsa Thina Naye
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Mungu Anasikiaka Sala Zetu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2021
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2021
wp21 na. 1 uku. 3-4
Watu wa fasi mbalimbali za dunia, wako wanasali ili kumuomba Mungu muongozo.

Mambo Yenye Watu Wanasemaka Juu ya Sala

“Wakati ninasali, ninajisikia kama Mungu iko pembeni yangu. Ninajisikia kama ananikamata mukono na kuniongoza wakati ninajisikia kuwa nimepotea.”​—MARÍA.

“Bibi yangu alikufa kisha kupigana na ugonjwa wa kansere kwa miaka 13. Ninakumbuka wakati nilikuwa ninasali kila siku kwa Mungu na kujisikia kuwa alikuwa anasikia sala yangu mu ile wakati wa maumivu. Ile ilifanya nikuwe mwenye kutulia.”​—RAÚL.

“Sala ni zawadi ya muzuri sana yenye Mungu amepatia wanadamu.”​—ARNE.

María, Raúl, Arne, na wengine wengi, wanaona sala kuwa zawadi ya pekee. Wanaona kama sala inawasaidia kuzungumuza na Mungu, kumushukuru na kumuomba musaada. Wanaamini kabisa kama mambo yenye Biblia inasema juu ya sala ni ya kweli. Biblia inasema hivi: “Huu ndio uhakika wenye tuko nao kwake, kwamba hata kama tunaomba nini kulingana na mapenzi yake, yeye anatusikia.”​—1 Yohana 5:14.

Lakini watu wengi wanaona kama ni nguvu kukubali mambo yenye Biblia inasema juu ya sala. Steve anasema mawazo yenye alikuwa nayo juu ya sala. Anasema hivi: “Wakati nilikuwa na miaka 17, marafiki wangu watatu walikufa mu aksidenti mbili tofauti. Mumoja alikufa mu aksidenti ya gari na wengine wawili walizama mu bahari.” Steve alifanya nini? “Nilisali na kumuuliza Mungu ni juu ya nini ile mambo yote ilitokea, lakini sikupata jibu. Kwa hiyo nilijiuliza, ‘Sala iko na faida gani?’” Watu wengi wanaona kama Mungu hajibiake sala zao na ile inafanya waone kama hakuna faida ya kuendelea kusali.

Kuko pia sababu zingine zenye zinafanya watu waone kuwa sala haiko ya maana. Watu fulani wanasema kama Mungu anajua mambo yote. Tayari anajua mambo yenye tuko nayo lazima ao magumu yetu. Kwa hiyo, haiko lazima tumuambie ile mambo.

Wengine wanaamini kama Mungu anakataa kusikiliza sala zao juu ya makosa yenye walifanya zamani. Jenny anasema hivi: “Ninajiona kuwa wa bure, na ile njo tatizo kubwa lenye niko nalo. Nilifanya mambo yenye inafanya nihuzunike, kwa hiyo ninajiambia kama Mungu hawezi kusikia sala zangu juu ninajiona kuwa sistahili.”

Mu kanisa, mwanamuke mumoja anaangalia juu wakati iko anasali, na wengine wanainamisha vichwa wakati wako wanasali.

Uko na mawazo gani juu ya sala? Kama unajisikiaka sawa watu wenye tumetoka kuzungumuzia ao uko na mashaka juu ya sala, unaweza kutiwa moyo na majibu yenye kuwa wazi yenye Biblia inatoa. Biblia iko na majibu ya kweli juu ya sala;a inaweza kukusaidia kupata majibu ya maulizo kama vile:

  • Mungu anasikiaka kabisa sala zetu?

  • Juu ya nini Mungu hajibiake sala fulani?

  • Unaweza kusali namna gani juu Mungu akusikie?

  • Kusali kunaweza kukuletea faida gani?

a Mu Biblia muko sala za watumishi wengi wa Mungu, kutia ndani sala za Yesu Kristo. Maandiko ya Kiebrania, yenye watu wengi wanaita Agano la Kale, iko na sala zaidi ya 150.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine