Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp21 na. 1 uku. 5-7
  • Mungu Anasikiaka Sala Zetu?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mungu Anasikiaka Sala Zetu?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2021
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MUNGU ANASIKILIZAKA SALA.
  • MUNGU ANAPENDA USALI KWAKE.
  • MUNGU ANAKUHANGAIKIA KABISA.
  • “NINAMUPENDA YEHOVA KWA SABABU ANASIKIA SAUTI YANGU”
  • Namna ya Kumukaribia Mungu Katika Sala
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Sala Ni Zawadi Kutoka kwa Mungu
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Utangulizi
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2021
  • Go Rapela Modimo go Nyoko go Šutetsa Thina Naye
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2021
wp21 na. 1 uku. 5-7
Kijana mwanamuke anaonyesha sura ya furaha.

“Mumukaribie Mungu, naye atawakaribia ninyi.”​—Yakobo 4:8

Mungu Anasikiaka Sala Zetu?

Ulishakajiuliza ikiwa Mungu anasikilizaka zako? Kama ni vile, hauko peke yako. Watu wengi walishakasali kwa Mungu kuhusu magumu fulani, lakini ile magumu inaendelea. Ile inamaanisha kama Mungu haangaikiake sala zetu? Hapana! Biblia inatuhakikishia kama Mungu anatusikilizaka wakati tunasali kwa njia yenye kufaa. Tuone mambo yenye Biblia inasema.

MUNGU ANASIKILIZAKA SALA.

“Ee Musikiaji wa sala, watu wa namna zote watakuendea.”​—Zaburi 65:2.

Watu fulani wanasema kama, sala inawasaidiaka wajisikie muzuri, ijapokuwa hawaamini kabisa kama kuko mwenye anawasikilizaka. Lakini, hatusalake tu juu tujisikie muzuri ili tuweze kuvumilia magumu. Biblia inatuhakikishia kama “Yehovaa iko karibu na wale wote wenye kumuitia, wote wenye kumuitia katika ukweli. . . . Anasikia kilio chao cha kuomba musaada.”​—Zaburi 145:18, 19.

Kwa hiyo, tunaweza kuwa hakika kama, Yehova Mungu anasikilizaka sala za wale wenye kumuabudu. Kwa upendo anasema hivi: “Mutaniita na kuja na kusali kwangu, na nitawasikiliza.”​—Yeremia 29:12.

MUNGU ANAPENDA USALI KWAKE.

Baba mumoja anakaa pembeni ya mutoto wake mwanamuke wakati iko anacheza na kamotokari.

“Mudumu katika sala.”​—Waroma 12:12.

Biblia inatutia moyo “kusali bila kuacha” na ‘kuendelea kusali kila wakati.’ Ni wazi kuwa, Yehova Mungu anapenda tusali kwake.​—Matayo 26:41; Waefeso 6:18.

Juu ya nini Mungu anapenda tusali kwake? Fikiri kidogo: Ni muzazi gani hawezi kufurahi wakati mutoto wake anamuambia, “Baba unaweza kunisaidia”? Kwa kawaida, tayari muzazi anaweza kuwa anajua mambo yenye mutoto yake iko nayo lazima ao namna anajisikia. Lakini wakati anasikia ile maneno, ile inaonyesha kama mutoto wake anamutumainia na anamupenda. Vilevile, wakati tunasali kwa Yehova Mungu, tunaonyesha kama tunamutumainia na kama tunapenda kumukaribia.​—Mezali 15:8; Yakobo 4:8.

MUNGU ANAKUHANGAIKIA KABISA.

Mufanyabiashara mwenye kuwa na mahangaiko anakaa ku ngazi ya nyumba. Pembeni yake kuko karto yenye kuwa na vitu ya mu biro.

“Mumutupie mahangaiko yenu yote, kwa sababu yeye anawahangaikia ninyi.” ​—1 Petro 5:7.

Mungu anapenda tusali kwake juu anatupenda na anatuhangaikia. Anajua muzuri mahangaiko yetu na magumu yetu, na anapenda kutusaidia.

Mu maisha yake yote, Mufalme Daudi alikuwa anasali kwa Yehova Mungu ili kumuomba musaada na alikuwa anamuambia mawazo yake na namna alikuwa anajisikia. (Zaburi 23:1-6) Mungu aliona Daudi namna gani? Mungu alimupenda Daudi na alisikiliza sala mingi zenye alitoa. (Matendo 13:22) Vilevile, Mungu anasikilizaka sala zetu juu anatuhangaikia.

“NINAMUPENDA YEHOVA KWA SABABU ANASIKIA SAUTI YANGU”

Ile maneno yenye kuwa mu Biblia ni ya muandikaji mumoja wa zaburi. Alikuwa hakika kama Yehova alikuwa anasikiliza sala zake, na ile ilimusaidia sana. Alijisikia kuwa karibu sana na Mungu na alipata nguvu ya kupambana na taabu na huzuni.​—Zaburi 116:1-9.

Wakati tuko hakika kama Mungu anasikilizaka sala zetu, tutaendelea kusali kwake. Tufikirie mufano wa Pedro, mwenye anaishi kaskazini mwa Uhispania. Mutoto wake mwanaume wa miaka 19 alikufa mu aksidenti ya mu barabara. Wakati wa ile huzuni, Pedro alimufungulia Mungu moyo wake na alisali mara mingi ili kumuomba Mungu amufariji na kumusaidia. Ni nini ilitokea? Pedro anasema hivi: “Yehova alijibia sala zangu kwa kutumia Wakristo wenzetu ili watufariji mimi na bibi yangu na kutusaidia.”

Mwanaume mwenye huzuni anakamata picha wakati marafiki wake fulani wako wanamufariji.

Mara mingi Mungu anajibiaka sala zetu kwa kutumia marafiki wenye wanatupenda ili kutufariji na kutusaidia

Hata kama sala hazikumurudishia mutoto wake, zilimusaidia sana Pedro na familia yake. Bibi yake María Carmen, anakumbuka hivi: “Sala zilinisaidia nivumilie huzuni yangu. Nilijua kama Yehova alisikiliza sala zangu juu wakati nilisali kwake, nilijisikia kuwa na amani na utulivu.”

Biblia na mambo mingi yenye watu walijionea mu maisha yao, inaonyesha waziwazi kama Mungu anasikilizaka sala. Lakini, Mungu hasikilizake sala zote. Juu ya nini Mungu anasikilizaka sala fulani na zingine hapana?

a Yehova ni jina la pekee la Mungu.​—Zaburi 83:18.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine