Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w22 Mwezi wa 12 uku. 28-30
  • Uko Najitayarisha Ili ‘Kuriti Dunia’?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Uko Najitayarisha Ili ‘Kuriti Dunia’?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • UJITAYARISHE ILI KUGEUZA DUNIA KUWA PARADISO
  • UJITAYARISHE ILI KUHANGAIKIA WALE WENYE WATAFUFULIWA
  • UJITAYARISHE ILI KUFUNDISHA WALE WENYE WATAFUFULIWA
  • Kutakuwa Ufufuo!
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Sehemu ya 10
    Umusikilize Mungu
  • Ufufuo Ni Nini?
    Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Ufufuo Unaonyesha Kama Mungu Iko na Upendo, Hekima, na Uvumilivu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
w22 Mwezi wa 12 uku. 28-30
Watu wako nageuza dunia ili ikuwe paradiso. Wamoya wako natosha uchafu, wengine wako najenga nyumba na wengine wako nalima bustani.

Uko Najitayarisha ili ‘Kuriti Dunia’?

SIYE wote tunachunga kwa hamu wakati hii ahadi ya Yesu itatimia: “Wenye furaha ni wale wenye tabia ya upole, kwa sababu watariti dunia.” (Mt. 5:5) Watiwa-mafuta watariti dunia wakati watatawala pamoya na Yesu mbinguni. (Ufu. 5:10; 20:6) Wakristo wengi wa kweli leo wanatazamia kuishi milele mu dunia. Watakuwa wakamilifu, wataishi kwa amani na furaha. Lakini, juu ile iwezekane kabisa, watakuwa na kazi mingi ya kufanya. Tuzungumuzie mambo tatu yenye watafanya: Kugeuza dunia ikuwe Paradiso, kuhangaikia wenye watafufuliwa, na kufundisha wenye watafufuliwa. Fikiria namna unaweza kujitayarisha tangu sasa ili kuonyesha kama unapenda kufanya ile mambo mu dunia mupya.

UJITAYARISHE ILI KUGEUZA DUNIA KUWA PARADISO

Wakati Yehova aliambia wanadamu ‘wajaze dunia na kuitawala,’ alionyesha kama alipenda dunia yote ifikie kuwa Paradiso. (Mwa. 1:28) Wale wenye wataishi milele ku dunia, itawaomba pia kutii ileile amri ya kutawala dunia, ni kusema, kugeuza dunia ikuwe Paradiso. Ku mwanzo, dunia haitakuwa Paradiso juu bustani ya Edeni haiko tena. Kisha tu Armagedoni, kutakuwa kazi mingi ya kufanya ili kusafisha maeneo ya dunia yenye imeharibiwa. Ile itakuwa kazi ya mingi kabisa!

Ile inatukumbusha kazi yenye Waisraeli walipaswa kufanya kisha kutoka Babiloni. Inchi yao haikuikaliwa kwa miaka 70. Lakini, Isaya alitabiri kama Yehova angewasaidia wafanye inchi yao ikuwe tena mu hali ya muzuri. Isaya alisema hivi: “Atafanya jangwa lake kuwa kama Edeni na jangwa lake tambarare kama bustani ya Yehova.” (Isa. 51:3) Yehova alisaidia Waisraeli wafanye vile. Vilevile, Yehova atasaidia wale wenye watariti dunia waifanye kuwa Paradiso. Na tangu sasa unaweza kujitayarisha ili kufanya vile.

Jambo moya yenye unaweza kufanya ni kujikaza kadiri unaweza ili nyumba yako ikuwe safi. Unapaswa kufanya vile, hata kama majirani wako hawahangaikie mambo ya usafi. Unaweza pia kusaidia kusafisha na kutunza Jumba yenu ya Ufalme na Jumba ya Mukusanyiko. Kama hali yako inaruhusu, unaweza pia kujaza ombi ili kusaidia wakati kunatokea musiba. Ile itaonyesha kama uko tayari kusaidia. Ujiulize hivi: ‘Ninaweza kujifunza ufundi fulani wenye nitatumikisha kama ninakuwa kati ya wale wenye watariti dunia?’

Ndugu na dada wako nasafisha na kutunza Jumba ya Ufalme.

UJITAYARISHE ILI KUHANGAIKIA WALE WENYE WATAFUFULIWA

Wakati fulani tu kisha kufufua mutoto mwanamuke wa Yairo, Yesu alisema wapatie ule mutoto chakula. (Mk. 5:42, 43) Pengine haikukuwa kazi ya nguvu sana kupatia chakula ule mutoto mwanamuke wa miaka 12. Lakini, fikiria mambo yenye itaomba kufanya wakati Yesu atatimiza ahadi yake ya kama “wale wote wenye kuwa katika makaburi ya ukumbusho watasikia sauti yake na watatoka.” (Yoh. 5:28, 29) Kusema kweli, Biblia haituambie mambo mingi juu ya ile. Lakini, kama unafikiri sana, utaona kama wale wenye watafufuliwa watakuwa na lazima ya chakula, fasi ya kuishi, na nguo. Unaweza kufanya nini tangu sasa ili kuonyesha kama unapenda kusaidia wale wenye watafufuliwa? Ona maulizo fulani yenye unaweza kujiuliza.

Unaweza kufanya nini leo ili kuonyesha kama uko najitayarisha kuriti dunia?

Ndugu na dada wenye furaha wako ku aéroport ili kukaribisha ndugu na dada wenye walikuya ku mukusanyiko wa kimataifa mu Paris.

Kwa mufano, wakati munatangaziwa kama mwangalizi wa muzunguko atatembelea kutaniko yenu, unapangaka kumualika ili kukula pamoya naye? Wakati watumishi wa pekee wa wakati yote wanatoka ku Beteli na wanatumwa mu kutaniko yenu, ao wakati mwangalizi wa muzunguko hataendelea tena na kazi ya kutembelea makutaniko, unaweza kuwasaidia wapate fasi ya kuishi? Kama mukusanyiko wa eneo ao wa pekee utafanywa mu eneo yenu, unaweza kujitolea ili kusaidia ku kazi mbalimbali mbele na kisha mukusanyiko ao kusaidia kukaribisha ndugu na dada wenye walitoka mbali ili kuhuzuria mukusanyiko?

UJITAYARISHE ILI KUFUNDISHA WALE WENYE WATAFUFULIWA

Sawa vile Matendo 24:15 inaonyesha, tunatazamia kama mamiliare ya watu watafufuliwa. Wengi kati yao hawakupata nafasi ya kumujua Yehova mbele wakufe. Watakuwa sasa na nafasi ya kujifunza juu ya Yehova kisha kufufuliwa.a Watumishi wa Yehova waaminifu na wenye uzoefu watafanya ile kazi ya kuwafundisha. (Isa. 11:9) Charlotte, mwenye amehubiri mu inchi za Ulaya, Amerika ya Kusini, na Afrika, anachunga kwa hamu kufanya ile kazi. Anasema hivi: “Ninachunga kwa hamu kufundisha watu wakati watafufuliwa. Mara mingi kama ninasoma habari kuhusu mutu fulani mwenye aliishi zamani, ninajiambiaka hivi: ‘Huyu mutu angemujuaka Yehova, maisha yake haingekuwaka vile.’ Ninachunga kwa hamu kufundisha wale wenye watafufuliwa na kuwaambia mambo yenye hawakujuaka.”

Hata watumishi wa Yehova waaminifu wenye waliishi mbele Yesu akuye ku dunia watakuwa na mambo mingi ya kujifunza. Fikiria furaha na pendeleo yenye tutakuwa nayo ya kumufasiria Danieli namna maunabii yenye aliandika lakini hakuelewa, ilitimia. (Da. 12:8) Itakuwa pendeleo kumusaidia Rutu na Naomi wajue kama Masiya alitokea mu kizazi yao. Itakuwa furaha kufanya ile kazi kubwa ya kufundisha mu dunia yote, na hakutakuwa magumu na mambo yenye kukengeusha yenye tuko naona mu hii dunia leo!

Dada iko napatia trakte mwanamuke mwenye anatumikaka fasi ya kufulia manguo.

Unaweza kufanya nini sasa ili kuonyesha kama uko tayari kufundisha wale wenye watafufuliwa? Jambo moya yenye unaweza kufanya ni kujikaza ili ukuwe mwalimu muzuri na kuhubiri kwa ukawaida. (Mt. 24:14) Hata kama kwa sasa hauwezi kuhubiri sana vile ungependa juu ya miaka ao juu ya sababu zingine, unaweza kuonyesha kama unapenda kufundisha wale wenye watafufuliwa kwa kuhubiri kulingana na uwezo wako.

Maulizo ya maana ya kujiuliza ni hii: Uko na hamu kabisa ya kuriti dunia? Unapenda kabisa kufanya dunia ikuwe Paradiso, kuhangaikia na kufundisha wale wenye watafufuliwa? Unaweza kujitayarisha sasa kwa kufanya kazi mbalimbali zenye zinafanana na zile zenye utafanya wakati utariti dunia!

a Ona habari ‘Kuleta Watu Wengi Kwenye Haki’ mu Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 9, 2022.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine