Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 58
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Isaya—Yaliyomo

      • Kufunga kwa kweli na kwa uwongo (1-12)

      • Kushika Sabato kwa furaha (13, 14)

Isaya 58:1

Marejeo

  • +Isa 1:2; 31:6; 59:13

Isaya 58:2

Marejeo

  • +Isa 29:13; Eze 33:32
  • +Isa 1:14, 15

Isaya 58:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “tunapozitesa nafsi zetu?”

  • *

    Au “mambo mnayofurahia.”

Marejeo

  • +Mal 3:14
  • +Law 16:29
  • +Yer 34:15, 16; Mik 3:2-4

Isaya 58:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kuitesa nafsi yake.”

Isaya 58:6

Marejeo

  • +Yer 34:8, 9
  • +Met 28:27

Isaya 58:7

Marejeo

  • +Zb 41:1; 112:9; Met 19:17; 22:9
  • +Eze 18:7, 8; Yak 2:15, 16; 1Yo 3:17

Isaya 58:8

Marejeo

  • +Met 4:18
  • +Kut 14:19; Isa 52:12

Isaya 58:9

Marejeo

  • +Isa 32:6; 59:3

Isaya 58:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “tamaa za nafsi yako.”

  • *

    Au “kuzishibisha nafsi zinazoteseka.”

Marejeo

  • +Kum 15:7, 8
  • +Zb 37:5, 6

Isaya 58:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kuishibisha nafsi yako.”

Marejeo

  • +Isa 49:10
  • +Isa 61:11; Yer 31:12

Isaya 58:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “wa mashimo yaliyo katika ukuta.”

Marejeo

  • +Ne 2:5; Yer 31:38
  • +Isa 61:4
  • +Ne 6:1; Amo 9:11, 14

Isaya 58:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “unaugeuza mguu wako usifuatilie.”

  • *

    Au “mambo unayofurahia.”

Marejeo

  • +Ne 13:15; Isa 56:2; Yer 17:21
  • +Kum 5:12-14

Isaya 58:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “ufurahie.”

Marejeo

  • +Kum 32:13
  • +Zb 105:10, 11; Yer 3:18

Jumla

Isa. 58:1Isa 1:2; 31:6; 59:13
Isa. 58:2Isa 29:13; Eze 33:32
Isa. 58:2Isa 1:14, 15
Isa. 58:3Mal 3:14
Isa. 58:3Law 16:29
Isa. 58:3Yer 34:15, 16; Mik 3:2-4
Isa. 58:6Yer 34:8, 9
Isa. 58:6Met 28:27
Isa. 58:7Zb 41:1; 112:9; Met 19:17; 22:9
Isa. 58:7Eze 18:7, 8; Yak 2:15, 16; 1Yo 3:17
Isa. 58:8Met 4:18
Isa. 58:8Kut 14:19; Isa 52:12
Isa. 58:9Isa 32:6; 59:3
Isa. 58:10Kum 15:7, 8
Isa. 58:10Zb 37:5, 6
Isa. 58:11Isa 49:10
Isa. 58:11Isa 61:11; Yer 31:12
Isa. 58:12Ne 2:5; Yer 31:38
Isa. 58:12Isa 61:4
Isa. 58:12Ne 6:1; Amo 9:11, 14
Isa. 58:13Ne 13:15; Isa 56:2; Yer 17:21
Isa. 58:13Kum 5:12-14
Isa. 58:14Kum 32:13
Isa. 58:14Zb 105:10, 11; Yer 3:18
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Isaya 58:1-14

Isaya

58 “Ita kwa sauti yote kutoka kooni; usijizuie!

Paza sauti yako kama pembe.

Watangazie watu wangu uasi wao,+

Na nyumba ya Yakobo dhambi zao.

 2 Wananitafuta siku baada ya siku,

Nao wanafurahia kuzijua njia zangu,

Kana kwamba walikuwa taifa lililotenda uadilifu

Na ambalo halikuacha haki ya Mungu wao.+

Wananiomba hukumu za uadilifu,

Wakifurahia kumkaribia Mungu:+

 3 ‘Kwa nini huoni, tunapofunga?+

Na kwa nini hutambui tunapojitesa?’*+

Kwa sababu siku mnayofunga mnafuatia mapendezi yenu wenyewe,*

Nanyi mnawakandamiza wafanyakazi wenu.+

 4 Kufunga kwenu huishia kwenye ugomvi na vita,

Nanyi mnashambulia kwa ngumi ya uovu.

Hamwezi kufunga kama mnavyofanya leo na sauti yenu isikiwe mbinguni.

 5 Je, kufunga ambako ninachagua kunapaswa kuwa hivi,

Siku ya mtu kujitesa,*

Kuinamisha chini kichwa chake kama utete,

Na kufanya nguo za magunia na majivu yawe kitanda chake?

Je, huko ndiko unakoita kufunga na siku inayompendeza Yehova?

 6 Hapana, huku ndiko kufunga ambako ninachagua:

Kuondoa pingu za uovu,

Kufungua vifungo vya nira,+

Kuwaachilia huru waliokandamizwa,+

Na kuivunja kila nira mara mbili;

 7 Ni kumgawia aliye na njaa mkate wako,+

Kuwaleta maskini na wasio na makao nyumbani mwako,

Kumvisha aliye uchi unapokutana naye,+

Na kutowageuzia mgongo watu wako wa ukoo.

 8 Ndipo nuru yako itakapochomoza kama mapambazuko,+

Na uponyaji wako utatokea upesi.

Uadilifu wako utakutangulia,

Na utukufu wa Yehova utakuwa ulinzi nyuma yako.+

 9 Kisha utaita, na Yehova atakujibu;

Utalilia msaada, naye atasema, ‘Mimi hapa!’

Ukiiondoa nira kati yako

Ukiacha kunyoosha kidole chako na kuacha kuongea mambo yanayodhuru,+

10 Ukimpa mwenye njaa kile ambacho wewe mwenyewe unatamani*+

Na kuwashibisha wale wanaoteseka,*

Ndipo nuru yako itakapong’aa hata gizani,

Na giza lako litakuwa kama adhuhuri.+

11 Yehova atakuongoza daima

Na kukushibisha* hata katika nchi iliyokauka;+

Ataitia nguvu mifupa yako,

Nawe utakuwa kama bustani iliyonyweshwa maji vizuri,+

Kama chemchemi ambayo maji yake hayakauki kamwe.

12 Watajenga upya magofu ya kale kwa sababu yako,+

Nawe utairudisha misingi ya vizazi vilivyopita.+

Utaitwa mrekebishaji wa kuta zilizobomoka,*+

Mrekebishaji wa barabara zinazopita kwenye makao.

13 Ikiwa kwa sababu ya Sabato unaacha kufuatilia* mapendezi yako mwenyewe* katika siku yangu takatifu+

Nawe uiite Sabato kuwa ni furaha tele, siku takatifu ya Yehova, siku ya kutukuzwa,+

Nawe uitukuze badala ya kufuatilia mapendezi yako mwenyewe na kusema maneno ya upuuzi,

14 Ndipo utakapopata furaha tele katika Yehova,

Nami nitakufanya upande sehemu za juu za dunia.+

Nitakufanya ule kutokana na* urithi wa Yakobo babu yako,+

Kwa maana kinywa cha Yehova kimesema hivyo.”

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki