Zaburi
71 Nimekukimbilia wewe, Ee Yehova.
Usiache niaibishwe kamwe.+
2 Niokoe na kuninusuru kwa uadilifu wako.
Nitegee sikio lako* na uniokoe.+
3 Uwe ngome ya mwamba kwangu
Ambamo ninaweza kuingia sikuzote.
Toa amri ya kuniokoa,
Kwa maana wewe ni jabali langu na ngome yangu.+
4 Ee Mungu wangu, niokoe kutoka mikononi mwa mwovu,+
Kutoka katika makucha ya mkandamizaji asiyetenda haki.
5 Kwa maana wewe ni tumaini langu, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova;
6 Nimekutegemea tangu nilipozaliwa;
Wewe ndiye uliyenitoa tumboni mwa mama yangu.+
Ninakusifu daima.
7 Nimekuwa kama muujiza kwa watu wengi,
Lakini wewe ni kimbilio langu imara.
8 Kinywa changu kimejaa sifa zako;+
Mchana kutwa ninasimulia kuhusu fahari yako.
10 Maadui wangu wanasema mambo mabaya kunihusu,
Na wale wanaotaka kuniua* wanapanga njama pamoja,+
11 Wakisema: “Mungu amemwacha.
Mkimbizeni na kumkamata, kwa maana hakuna yeyote wa kumwokoa.”+
12 Ee Mungu, usiendelee kukaa mbali nami.
Ee Mungu wangu, njoo haraka unisaidie.+
13 Wale wanaonipinga
Na waaibishwe na kuangamia.+
Wale wanaonitakia msiba
Na wafunikwe na aibu na fedheha.+
14 Lakini mimi, nitaendelea kungoja;
Nitakusifu hata zaidi.
15 Kinywa changu kitasimulia uadilifu wako,+
Mchana kutwa kitasimulia matendo yako ya wokovu,
16 Nitakuja na kutangaza matendo yako yenye nguvu,
Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova;
Nitatangaza uadilifu wako, wako peke yako.
17 Ee Mungu, umenifundisha tangu nilipokuwa kijana,+
Na mpaka sasa ninaendelea kutangaza kazi zako zinazostaajabisha.+
18 Ee Mungu, hata nikizeeka na kuwa na mvi, usiniache.+
19 Uadilifu wako, Ee Mungu, unafika vileleni;+
Umetenda mambo makuu;
Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?+
20 Ingawa umenifanya nipate taabu nyingi na misiba mingi,+
Nihuishe tena;
21 Ongeza ukuu wangu
Nizunguke na kunifariji.
22 Kisha nitakusifu kwa zeze
Kwa sababu ya uaminifu wako, Ee Mungu wangu.+
Nitaimba sifa zako* kwa kinubi,
Ee Mtakatifu wa Israeli.